Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,733
- 5,490
Bata:
Kujivutavuta, hufanya kazi polepole na kuendekeza uvivu mpaka mambo ya kikundi yanazorota au kufa kabisa.
Bundi:
Mtu anayefikiria ana akili kuliko wote kwenye kikundi- hutumia lugha ngumu na haeleweki
Chura:
Hurudiarudia kitu kile kile mpaka anawachosha wenzake kundini
Kenge:
Hatumii akili sawasawa, ujinga mwingi na hufanya maamuzi ya ovyo yenye kuwakatisha tamaa wenzake
Kiboko:
Hulala lala na kupiga miayo. Wakati wenzake wanachacharika yeye ni kukaa tu, hafanyi kazi.
Kifaru:
Yeye hushambulia wengine kwenye kikundi bila sababu
Kinyonga:
Kigeugeu, akiwa kwa mwanakikundi huyu anasema hili na akiwa kwa mwingine anasema tofauti
Kobe:
Hujitoa akiudhiwa, hana uvumilivu kwenye changamoto zinazokabili kikundi.
Kuku:
Kuvuruga palipotengenezwa, huenda tofauti na maono ya kikundi kwa kujali na kuzingatia mambo ya muda mfupi tu.
Mbuni:
Huficha kichwa na hufikiri hakuna shida kwenye kikundi hata kama zipo shida nyingi
Nyati:
Kujihami tu kwa sababu ya woga. Hakosolewi, ukimgusa tu anaazisha vita vya maneno au kupigana
Nyoka:
Anajificha huku akiuma bila kusema. Mchonganishi
Nyumbu:
Mwoga na hatumii akili kabisa.
Paka:
Yeye hutaka ahurumiwe tu na wenzake, hana mchango wowote kwenye kikundi.
Panya:
Hachangii chochote yeye hujificha tu na kujitokeza wakati wa neema.
Popo:
Hana msimamo. Kwa wanaokubali hoja yupo na kwa wanaopinga hoja yupo! Haeleweki.
Punda:
Mgumu kubadilika. Hata umuelimishe vipi, misimamo yake ni ile ile ya zamani.
Samaki:
Hachangii hoja, kazi tu, kukwepa na kutoweka na huonekana hali ikitulia na kuwa shwari.
Simba:
Hupigana kama mawazo yake hakubaliwi na wanakikundi wengine.
Sungura:
Hukimbia kama kuna dalili za hatari na kwenda kinyume na makubaliano ya kikundi
Tausi:
Yeye huringa kwa mambo mazuri aliyonayo ambayo wanakikundi wenzake hawana.
Tembo:
Hufunga njia bila sababu watu wasipite. Huzuia mawazo na maamuzi ya kikundi yasifanikiwe bila sababu.
Tumbili:
Mizaha mizaha tu wakati wote hayuko makini hata kwa mambo muhimu ya kikundi.
Kujivutavuta, hufanya kazi polepole na kuendekeza uvivu mpaka mambo ya kikundi yanazorota au kufa kabisa.
Bundi:
Mtu anayefikiria ana akili kuliko wote kwenye kikundi- hutumia lugha ngumu na haeleweki
Chura:
Hurudiarudia kitu kile kile mpaka anawachosha wenzake kundini
Kenge:
Hatumii akili sawasawa, ujinga mwingi na hufanya maamuzi ya ovyo yenye kuwakatisha tamaa wenzake
Kiboko:
Hulala lala na kupiga miayo. Wakati wenzake wanachacharika yeye ni kukaa tu, hafanyi kazi.
Kifaru:
Yeye hushambulia wengine kwenye kikundi bila sababu
Kinyonga:
Kigeugeu, akiwa kwa mwanakikundi huyu anasema hili na akiwa kwa mwingine anasema tofauti
Kobe:
Hujitoa akiudhiwa, hana uvumilivu kwenye changamoto zinazokabili kikundi.
Kuku:
Kuvuruga palipotengenezwa, huenda tofauti na maono ya kikundi kwa kujali na kuzingatia mambo ya muda mfupi tu.
Mbuni:
Huficha kichwa na hufikiri hakuna shida kwenye kikundi hata kama zipo shida nyingi
Nyati:
Kujihami tu kwa sababu ya woga. Hakosolewi, ukimgusa tu anaazisha vita vya maneno au kupigana
Nyoka:
Anajificha huku akiuma bila kusema. Mchonganishi
Nyumbu:
Mwoga na hatumii akili kabisa.
Paka:
Yeye hutaka ahurumiwe tu na wenzake, hana mchango wowote kwenye kikundi.
Panya:
Hachangii chochote yeye hujificha tu na kujitokeza wakati wa neema.
Popo:
Hana msimamo. Kwa wanaokubali hoja yupo na kwa wanaopinga hoja yupo! Haeleweki.
Punda:
Mgumu kubadilika. Hata umuelimishe vipi, misimamo yake ni ile ile ya zamani.
Samaki:
Hachangii hoja, kazi tu, kukwepa na kutoweka na huonekana hali ikitulia na kuwa shwari.
Simba:
Hupigana kama mawazo yake hakubaliwi na wanakikundi wengine.
Sungura:
Hukimbia kama kuna dalili za hatari na kwenda kinyume na makubaliano ya kikundi
Tausi:
Yeye huringa kwa mambo mazuri aliyonayo ambayo wanakikundi wenzake hawana.
Tembo:
Hufunga njia bila sababu watu wasipite. Huzuia mawazo na maamuzi ya kikundi yasifanikiwe bila sababu.
Tumbili:
Mizaha mizaha tu wakati wote hayuko makini hata kwa mambo muhimu ya kikundi.
KILA MDAU AJITAFAKARI INAWEZEKANA KUNA MAHALI AMEGUSWA.