Nitoe mfano wa mwanangu
.mtundu kupitiliza.
Kila siku kesi za kuwabonda wenzie haziishi.
Ukishika kiboko lazima ajikojolee kwa uoga, ukimaliza kumtia viboko hapati shida kurudia kosa lile lile.
Anaongea kuliko kasuku.
Ni mbabe hadi ananunua kesi za wenzie.
Ana mwandiko kama dakitari.
Darasani namba moja kama mwalimu akimbana..ukimuachia yeye ni michezo.
Hajijali...anaweza enda dukani uchi, kuoga mbinde na kufua.
Alishawahi kukataliwa shule akiwa darasa la kwanza kwa utundu.
Ukimuacha sehemu yoyote ngeni ndani ya dakika kumi atakuwa ndie kiongozi wa wenyeji.
Kazi yoyote ya mikono labda utumie rungu ndio atafanya! Ni mvivu ile mbaya!
Good thing anapenda sana kufundisha wenzie na ana uwezo wa kushawishi