barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,405
- 29,807
ABIRIA:I wish angetokea konda hapa naye akaeleza kero zake kuhusu abiria. Kuna abiria wanakera jamani mweh!
Aaah mimi usintanie kabisa natoa kipochi nakaa unless otherwise niheshimu umri.ABIRIA: Unakuta umepigania daladala hapo kitu darajani ubungo kwenda Gomz, ile kuingia tu unakuta eti abiria anadai kawahi siti huku kaweka kipochi au liboksi lake ktk siti kupitia dirishani, ukikaa anazusha!!
- Abiria anapanda huku anajua ana hela pungufu, baadae ukianza kudai nauli yako anakupa hela pungufu, ukimmaind abiria wanaanza ooh hiyo mia tu si uachane naye, ukiwaambia wamlipie wanakaa kimya.
- Abiria unamwomba nauli anakwambia ntakupa nimekaa vibaya, umekaa vibaya kivipi? Leta nauli niende kudai wengine, ukijifanya kumsahau unamwona anataka kuondoka bila kulipa.
- Tabia ya abiria kuwapa makonda noti mbovu, ukiikataa anakwambia eti sina nyingine, na hapo mmeshafika mbali, jamani noti mbovu pelekeni benki
- Tabia ya mtu kupandia Kimara anakwambia eti nashukia Manzese ambapo nauli ni 400 (hapo kama route ya Posta ni sh 500), mkifika Manzese hashuki, ukianza kumdai nauli mpya anajifanya ooh sina, au nimebadili maamuzi nashukia Posta, sasa mbona hukunijulisha mpaka nimekukumbuka mimi?
- Tatizo la abiria kuingia kwenye gari ukimwambia sogea nyuma wenzio wapande anamaind, kama vipi tafuteni usafiri wenu.
- Harafu kuna hawa jamaa ambao wengi watakuwa ni member wa JF, kila akiingia kwenye gari anajifanya kupiga simu eti anaongea na fundi wake kuhusu gari lake lililoko garage ili aonekane matawi kwenye dala dala.
- Abiria analala gari inampitisha kituo, anaanza kulalamika eti konda hakuita vituo, ni jukumu lako kujua unashukia wapi, kama ni mgeni niambie mapema kwamba wewe ni mgeni.
ha ha ha ha ha lengo la konda hapo inakuwa ni kumuaibisha anayedai mia yake au?
Hayo ni matokeo ya kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya konda abiria.mara nyingi sana kwenye daldala naona jinsi abiria wanavyosumbua makonda. mwingine unaona kabisa anatafuta ugomvi kitu kidogo tu matusi. kazi ya ukonda ngumu sana!
ha ha ha ha ha lengo la konda hapo inakuwa ni kumuaibisha anayedai mia yake au?
pwagu nimetoa mada pwaguzi ukachangia.
Ukisema makonda ni wachafu nitakuunga mkono. Lakini hili la chenchi linawahusu abiria na kondakta ambao lazima tuwasemee maana muda wa kuingia humu hawana. Ni asubuhi abia wanne wanatoa noti za sh. Kumi 10 sawa na sh 40, 000 wkt nauli ni sh 500?
Umenena vyema mkuu,baadhi wanasema eti unatoaje shilingi elfu kumi asubuhi.Sasa mimi nisipande gari asubuhi kwakuwa tu sina pesa ndogo? au nianze kuamsha majirani kuomba chenji? hapana ,hii mimi siikubali hata kidogo.Konda anatakiwa awe na float ebo!! ajiandae kabisa , si anajua biashara yake ni machenji chenji au? Ni kiasi tu cha kujiongeza . hapo wa kulaumiwa ni konda tu , kama unamtazamo wa mbali.