Kuna rafik yangu alinihadithia kitu kilimuuma sana. Ofisini kwao kuna mfanya usafi,maofisini na chooni na mazingira yote.
Kuna siku, jamaa alimkuta chooni anafanya usafi, akamsalimia, yule mfanya usafi,hakujibu na hata hakumtazama. Yule rafiki, akaona dharau na kuweka kinyongo. Kuna siku mfanya usafi alimkuta rafiki ananunua na kula matunda muda wa lunch hapo nje. Akamuongelesha boss, naona unapata matunda, Jamaa alimjibu SHIT sana hadi sio poa. Lakin kesho yake, ktk mazungumzo na wafanyakaz wenzie,aliwahadithia jamaa yule mnasemag ana dharau alishoboka, nikampa makavu, mmoja wa wafanyakaz akasema, Bro yule hana dharau hasikiii vizuri. Yaan ukimuongelesha, hadi akuone midomo ndio atakuelewa, mchizi ilimuuma sana, ika bidi akaenda kumuomba msamaha.
Alichojibiw ndio kilimuuma zaidi, akasema Bro, sasa mm nitaweza kweli kumtangazia kila mtu madhaifu yangu,ofisi yote kubwa hivi. Anasema kuna muda najikuta hata nimesukumwa, kumbe mtu tu alisema OYAA NAOMBA KUPITA, AU SOGEA KIDOGO. nisipo sikia unakuta nimesukumw huko, ila mwisho wa siku naelewa huyu itakuwa kanisemesha sija msikia, so nimeipokea hali yangu boss,kuwa na amani.
Kukoroma, ishu ya viooo unakuta mwingine anashida za kifua, sauti mwingine ndo mshamba wa maisha hana mazoea na hivo so inabid aenjoy muacheni, au asikiii vizuri. Sasa anatafta Decoy ya kupata atakacho.
Tuvumiliane tu, kuna yasio vumilika, kama ulevi, uchafu, kubebeshw majukum yasiyokuhusu nk.