Tabia za kishamba za mabasi ya mikoani

Tabia za kishamba za mabasi ya mikoani

Bila kusahau wale kina mama wanaosafiri na watoto wawili huku wamekata seat moja

Nilishawahi kujikuta dada msaidizi wa mtoto mwanzo hadi mwisho wa safari,yaaani kale kadogo nimekashikilia mimi,kale kengine kadada mtu kameshikwa na mama yake

Mbaya zaidi kale katoto kalinipenda na kunizoea mapema sana,kila muda dada hivi dada vile mara kanilishe vitu kanavyopewa na mama yake

Sio kwa ubaya,lakini ni usumbufu...kama una watoto wadogo wawili jitahidi kuweka seat mbili aseee

Siku hizi namuagiza anayenikatia ticket ahakikishe nakaa na mkaka
Unasafiri lini tena
 
mimi kwenye Bus hua napenda kukaa seat moja na mdada alafu anilalie begani, kero zingine zote ulizotaja navumilia
 
Kuna Wale wanaotapika tapika hovyo

Kuna mdada Aliwahi nitapikia kwenye Paja kidgo tuu, Likawa linasema Sorry Sorry mdogo wangu huku ananifuta...Yani nilitamani nimpige kichwaa
Yakaisha tukaongea ongea likanipa Namba , Mpaka Leo nimemsave Vomit hahah

NB, Sijaomba mzigo
Ahaaaahaaaahaaa

Madame Vomit
 
Bila kusahau wale kina mama wanaosafiri na watoto wawili huku wamekata seat moja

Nilishawahi kujikuta dada msaidizi wa mtoto mwanzo hadi mwisho wa safari,yaaani kale kadogo nimekashikilia mimi,kale kengine kadada mtu kameshikwa na mama yake

Mbaya zaidi kale katoto kalinipenda na kunizoea mapema sana,kila muda dada hivi dada vile mara kanilishe vitu kanavyopewa na mama yake

Sio kwa ubaya,lakini ni usumbufu...kama una watoto wadogo wawili jitahidi kuweka seat mbili aseee

Siku hizi namuagiza anayenikatia ticket ahakikishe nakaa na mkaka

Umeandika kwa hekima sana,I like that!
 
Mimi nikiwa na safiri iwe ndege au basi lazima nilale sema huwa sikoromi na siegemei mtu nikifunga mkanda..

Siongei na mtu hadi nafika ..


Sema sipendi

1. Kukaa na mtu anakulakula.mavyakula

2. Kina mama wenye watoto wadogo

3. Wenye simu ya nokia unakuta anawasha radio au mziki wakati kwenye gari kuna mziki

4. Wapambe wa safari mara dereva ongeza mwendo etc

5.. waxhimba dawa maarufu... kila kituo anachimab dawa na mara nyingine anasimamisha basi achimbe dawa..


Niliwahi safiri kwenda tanga na simba mtoto ya jioni.. nilijuta
 
Mimi nishawah panda bus siti yangu pemben kulikua na mmama pamoja na mtoto wa kama miez Saba HIV
Sasa yule mtoto kwanza alinikaribisha kwa kilio kikali Kama kile Cha watoto wa nguru, tulipiga masafa marefu tukiendelea kuskiliza mlio wa yule mtoto

Baadae akanyamaza kikaingia kikwazo kingine,,,, alivobanwa na mkojo akawa anaonesha ishara za kutaka kukojoa Sasa yule mama yake ujinga aliokua anaufanya ndo ulikua unanikera Sana,. Alikua anampa kanga yule mtoto na anamwambia haya kojoa yaani alikua anaikojolea Ile kanga halaf anaendelea kuipakata ...Ile kanga ilikojolewa Mara nying Sana Jambo lililopelekea harufu kwenye eneo tulilokaa kubadilika na kuwa sio salama Tena




Tukio lingine hili mnisamehe tu kwaa kulichomekea

Mimi nikiendaga kazin huwa sinyoagi nywele kabisa had navokua narud hom so huwaga nakuwa na kale kamuonekano ka matajiri wakinga au wabena

Kuna safar nilikosa ndege nnayoipenda Ivo ikabidi nipande fly Dubai, Kama unavojua Tena Ile ndege kwa wadada wengi wanaopanda wanakuwaga ni mabeki tatu na kawaida ya Hiv viumbe Mara nyingi huwa vinatokea uswahilini na kwao ndege ni big deal

Hiyo siku nilikaa siti moja na beki tatu mmoja alikua ndo anarud bongo, jaman hakuna siku nilinyanyapaliwa Kama Ile siku yaan nilitaman mle ndan kuwepo na saloon nipunguze nywele.

Yule dada alikua ananiona Kama kichaa iv.
Tulivofika zenji watu wengi walishuka so kulikua na siti nyingine zipo wazi, nikajitosa kwenda kukaa siti moja na mzungu(mdada) Yan tulivokua tunapiga stori unaweza kusema tumewah kuonana sehem na hakuwa na nyodo yyte

All in all wadada sometimes wanakosaga bahati kwa fikra zao potofu japo yule beki tatu hakunivutia kwa chochote Ila kunidharau na wakat nimemzd vitu vngi hyo kitu iliniuma sana
 
Hamna tabia inanikwaza na kuniudhi kama kuweka nyimbo za dini za kikristo full time,basi bora hata wangekuwa wanabalance na nyimbo za wenzetu waislam Hanna.

Yani watendaji wa maabasi hawana ubunifu kabisa.
Udini huo
 
Mimi nikiwa na safiri iwe ndege au basi lazima nilale sema huwa sikoromi na siegemei mtu nikifunga mkanda..

Siongei na mtu hadi nafika ..


Sema sipendi

1. Kukaa na mtu anakulakula.mavyakula

2. Kina mama wenye watoto wadogo

3. Wenye simu ya nokia unakuta anawasha radio au mziki wakati kwenye gari kuna mziki

4. Wapambe wa safari mara dereva ongeza mwendo etc

5.. waxhimba dawa maarufu... kila kituo anachimab dawa na mara nyingine anasimamisha basi achimbe dawa..


Niliwahi safiri kwenda tanga na simba mtoto ya jioni.. nilijuta

Wewe hujawahi kusafiri umechoka.. Wewe snoring is inevitable
 
Bila kusahau wale kina mama wanaosafiri na watoto wawili huku wamekata seat moja

Nilishawahi kujikuta dada msaidizi wa mtoto mwanzo hadi mwisho wa safari,yaaani kale kadogo nimekashikilia mimi,kale kengine kadada mtu kameshikwa na mama yake

Mbaya zaidi kale katoto kalinipenda na kunizoea mapema sana,kila muda dada hivi dada vile mara kanilishe vitu kanavyopewa na mama yake

Sio kwa ubaya,lakini ni usumbufu...kama una watoto wadogo wawili jitahidi kuweka seat mbili aseee

Siku hizi namuagiza anayenikatia ticket ahakikishe nakaa na mkaka
Haswa seat za nyuma kule wasukuma, wagogo na wamasai na yale makoti mazito utafikiri walinzi wanawekwa kule, huwa hawalipii nauli kamili, baba mama watoto na shemeji yake na mke wa shemeji yake wanapachikwa kule.

Hili route ya morogoro to mwanza, ukichagua gari za ajabu kama ile inaitwa ya kiazi cha bibi hatari sana.

Mara nyingi ili kuepuka huu shida kata ticket mapema acha kukatia kituoni wakati wa safari.
 
Nilishangaa sana jamaa aliponiomba ear phones asikilize muziki. Seriously unaomba earphones za mtu humjui hakujua. Niliona kama kanidharau, hivi unaanzaje kuomba earphones.
Mtu anapanga safari kabisa halafu hafanyi maandalizi ya vitu atatumia njiani.

Vitu kama waya wa chaji, powerbank, earphones, tissues, dawa ya maumivu ya kichwa na ya kuzuia tumbo kuchafukwa. Sweater, au shuka ya kimasai, pocket money ni baadhi ya vitu vya kubeba.
 
Bora wawili, niliwahi kukaa na mama ana watoto watatu imagine, halafu kakata siti moja tu!!!
Ilibidi tu nimuelewe tubanane hivyo hivyo na kupakata mmoja maana hakukua na namna.

Sent using Jamii Forums mobile app
maisha hayapo sawa, mshukuru.mungu kwa kidogo alichokujalia, hata yeye angependa watoto wake wakae kila mtoto na siti yake lakini ameshindwa. msiwaseme vibaya

Sent from my MI NOTE Pro using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom