KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,181
- 17,174
Ni jambo lipi au mradi gani aliowahi kuufanya John Pombe Magufuli, akiwa mbunge na sasa akiwa rais aliowahi kuubuni na kuukamilisha kwa utulivu, bila ya mitifuano na watu, wafanya kazi, contractors, raia au taasisi.
Ukiangalia barabara zilizojengwa, utakuta mikwaruzano kila sehemu. Naikumbuka ile Shell ya Mwanza; samaki wa Magufuli; wakazi wa Kimara; Kivuko cha Kigamboni, na mengi mengineyo.
Pamoja na kusifika kupiga kazi kwa nguvu, lakini weledi ni mpungufu anaposimamia kazi hizo. Kwake, kufuata taratibu zilizopo hakuna maana sana, mradi kazi inafanyika.
Kujifanyia yake nje ya katiba na sheria zilizopo ni kielelezo tosha cha tabia zake hizi mbaya.
Anasifika kwa kupambana na rushwa, lakini kwa taratibu zipi, na matokeo yake yatapimwa vipi?
Kuna taratibu za kisiasa zinazofahamika nchini, yeye kaja na njia zake za kununua wapinzani na vurugu tu nyingine nyingi.
Bunge na Mahakama zina taratibu zake, hata huko hakupaacha, mihuri ya utendaji wake wa vurugu inaonekana wazi kabisa.
Sasa tabia hizo hizo zinajirudia wakati akiwa rais. Kila sehemu ni mikwaruzano tu, hakuna linalofanyika bila kupigishana kelele, kutumbua, na mengine yasiyofaa.
Hili la COVID-19, ndilo linaloonyesha wazi kabisa tabia yake ya kutotaka kufuata taratibu. Yeye anajipigia tu anavyoona/hisi inafaa hata mahali asipokuwa na ufahamu napo
Hatari kubwa zaidi inayotokana na tabia yake hii ya kutofuata taratibu ni kwamba hata kama Taifa, sote tumeanza kuangukia kwenye tabia hiyo hiyo ya kutofuata taratibu zinazoeleweka katika kufanya mambo yetu; na hii imetugharimu na itaendelea kutugharimu sana tusipobadilika haraka.
Kuna umhimu mkubwa sana, kama taifa, turudi kwenye kufanya kazi zetu kwa kufuata taratibu zilizowekwa. Hili lisisitizwe sana hasa kwa watoto na vijana ambao bado wapo mashuleni. Taifa haliwezi kujengwa kwa kufanya mambo bila ya mipangilio isiyoeleweka.
Najua chini ya utawala wake hakuna kitakachoweza kubadilika. Bahati yetu kama taifa, huyo mwingine atakayekuja baada ya Kajoni, awe ni mtu msikivu na awe na ari ya kutuweka kwenye taratibu zinazoeleweka.
Ukiangalia barabara zilizojengwa, utakuta mikwaruzano kila sehemu. Naikumbuka ile Shell ya Mwanza; samaki wa Magufuli; wakazi wa Kimara; Kivuko cha Kigamboni, na mengi mengineyo.
Pamoja na kusifika kupiga kazi kwa nguvu, lakini weledi ni mpungufu anaposimamia kazi hizo. Kwake, kufuata taratibu zilizopo hakuna maana sana, mradi kazi inafanyika.
Kujifanyia yake nje ya katiba na sheria zilizopo ni kielelezo tosha cha tabia zake hizi mbaya.
Anasifika kwa kupambana na rushwa, lakini kwa taratibu zipi, na matokeo yake yatapimwa vipi?
Kuna taratibu za kisiasa zinazofahamika nchini, yeye kaja na njia zake za kununua wapinzani na vurugu tu nyingine nyingi.
Bunge na Mahakama zina taratibu zake, hata huko hakupaacha, mihuri ya utendaji wake wa vurugu inaonekana wazi kabisa.
Sasa tabia hizo hizo zinajirudia wakati akiwa rais. Kila sehemu ni mikwaruzano tu, hakuna linalofanyika bila kupigishana kelele, kutumbua, na mengine yasiyofaa.
Hili la COVID-19, ndilo linaloonyesha wazi kabisa tabia yake ya kutotaka kufuata taratibu. Yeye anajipigia tu anavyoona/hisi inafaa hata mahali asipokuwa na ufahamu napo
Hatari kubwa zaidi inayotokana na tabia yake hii ya kutofuata taratibu ni kwamba hata kama Taifa, sote tumeanza kuangukia kwenye tabia hiyo hiyo ya kutofuata taratibu zinazoeleweka katika kufanya mambo yetu; na hii imetugharimu na itaendelea kutugharimu sana tusipobadilika haraka.
Kuna umhimu mkubwa sana, kama taifa, turudi kwenye kufanya kazi zetu kwa kufuata taratibu zilizowekwa. Hili lisisitizwe sana hasa kwa watoto na vijana ambao bado wapo mashuleni. Taifa haliwezi kujengwa kwa kufanya mambo bila ya mipangilio isiyoeleweka.
Najua chini ya utawala wake hakuna kitakachoweza kubadilika. Bahati yetu kama taifa, huyo mwingine atakayekuja baada ya Kajoni, awe ni mtu msikivu na awe na ari ya kutuweka kwenye taratibu zinazoeleweka.
