Tabia ya kuaga maiti ni ya hatari sana

Tabia ya kuaga maiti ni ya hatari sana

wiseboy.

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2014
Posts
2,931
Reaction score
4,550
Binadamu anapokufa mwili wake huachana na roho,(nafsi /uhai) mwili huo hubaki kasha tupu lisilo na chembe yoyote ya uzima.

Na roho yake huenda sehemu inayostahili kulingana na matendo yake duniani.

Roho ndo uzima, roho ndo nafsi kamili, roho ndo uzima wenyewe. Kifupi ni kwamba binadamu hufa mwili ilihali roho ikiendelea kuishi katika ulimwengu mwingine wa roho ambao huwezi kuuona kwa macho ya damu na nyama.

Binadamu akifa anatisha, ukiambiwa ulale chumba kimoja na maiti huwezi, Hata Kama ni maiti ya mtoto bado utaogopa tu .

Sura ya maiti hukaa kwenye kumbukumbu ya ubongo kwa muda mrefu sana, kwa mtu yoyote atakayeikodolea macho maiti usoni.

Tabia ya kuaga maiti haina mashiko na sababu yoyote ile.
Kuaga maiti ni kuisanifu maiti, unaagaje kitu kisicho na uhai? Ni kipi kinakusaidia kumwangalia mfu?

Napenda sana utaratibu wa ndugu zangu waislamu, wao huiandaa maiti na kwenda kuzika basi, kuliko tabia ya mabwana wale wanaopenda kupanga foleni ili kuaga maiti msibani, foleni kubwa utadhani walimu wanachukua mshahara kwenye ATM ya NMB.

Mwisho wake huwa ni mayowe, watu kuzimia na kuanguka hovyo msibani.

Sura ya marehemu unaitakia nini? Unamuaga marehemu ili iweje?
 
Mila, desturi, taratibu na tamaduni hazifanani......utapata tabu sana kufatilia mambo ya watu, unajiumiza bure....ukitoka hapo utakuja kula nyoka kubaya, konokono haliwi, budha wanaabudu sanamu.....Mungu atamuhukumu kila mtu kulingana na utashi wake
 
Unatakiwa kujua lengo kubwa la kuaga maiti ni nini, then ndo uje na hoja ya kukosoa na kutoa alternative ya nini kifanyike. Nkuulze k2 kmoja, ulshawah kufiwa na m2 wa karbu (ndugu au rafiki) na wakat anakufa hukua umeonanana nae muda labda mwez au zaidi?
 
2015 ndo ilikua mara ya kwanza kuaga na kuona maiti..
Nilienda kumuaga Headmaster wetu aligongwa na gari akafariki.
Alibadirika sura ikwa nyeusi Hafu imevimba inatoa jasho.

Kidogo nianguke kwa uoga mpaka leo sura yake naiona..

Siagi tena mm labda ndugu.
 
kuna kitu kinaitwa mila na desturi nadhani hukitambui vyema, au darasa lilikupita kando....
kuna kitu kinaitwa miiko ya kwenye jamii husika, nikupe mfano kidogo jamaa zetu wahindi huwa wanaichoma maiti na kuiteketeza , kwa nn na sisi tusifanye hivo ? jibu ni kwamba huo sio utamaduni wetu.
nirudi kwenye mada yako ya msingi, ni kwa nini tunaaga maiti ? kwanza nianze kukujibu kuwa umetudanganya kuwa waislam huwa hawaagi, kuna mdau kakujibu hapo juu kuwa wanaaga ndugu wa karibu tu. je kwa hawa wengine ipoje ? huwa wanaaga, sawa ni utamaduni wao, lakni pia hujalazimishwa kupanga foleni kwenda kuaga, kama unajiona huwezi na una roho ndogo usiende... simply usiingilie tamaduni za watu
 
2015 ndo ilikua mara ya kwanza kuaga na kuona maiti..
Nilienda kumuaga Headmaster wetu aligongwa na gari akafariki.
Alibadirika sura ikwa nyeusi Hafu imevimba inatoa jasho.

Kidogo nianguke kwa uoga mpaka leo sura yake naiona..

Siagi tena mm labda ndugu.
jasho!!!!!!!!
 
MANASWARA WANAFANYA HIVO ILI WAPATE HELA ZA TUNZO WAO WANAIPAMBA LUGHA NAKUIITA RAMBIRAMBI
HUWEZI MFANYA NDUNGUYO MAITI AKAWA MNADA MBELE YA KADAMNASI KILA ANAEPITA AMUONE,,Atiii KISA WANAMUAGA,,BADO ANAVISHWA HADI SUTI KAMA NI WA KIKE ANAVISHWA VELI
MMMHHHH,,,,,kumfanya mwenzio ATM inataka MOYO SANA[emoji1321]

Haya wenye POVU KARIBUNI,,lakini UKWELI NDIO HUO[emoji1321]
 
Hujawahi fiwa na ndugu au rafiki wewe, halafu wakati anafariki haukwepo. Nakwambia akizikwa bila kuona maiti yake itakuchukua muda sana kuamini aliyezikwa ni yeye kweli au utani tu. Kuaga maiti humpunguzia mfiwa maumivu ya kuondokewa na mpendwa, huongeza imani kwamba fulani kweli ameondoka , na kuondoa kujiulizauliza . Na tena watototo wadogo usipowaambia ukweli na kuwaonyesha kila jambo linalotendeka msibani, waone maiti kwenye jeneza na uwaeleze what is going. Usipo fanya hivyo watakuuliza daily where is fulani na ukiwaeleza amekufa hawatakubali. so kuaga maiti ni afya ya akili na roho.
 
Binadamu anapokufa mwili wake huachana na roho,(nafsi /uhai) mwili huo hubaki Kasha tupu lisilo na chembe yoyote ya uzima.

Na roho yake huenda sehemu inayostahili kulingana na matendo yake duniani.

Roho ndo uzima, roho ndo nafsi kamili, roho ndo uzima wenyewe.
Kifupi ni kwamba binadamu hufa mwili ilihali roho ikiendelea kuishi ktk ulimwengu mwingine wa roho ambao huwezi kuuona kwa macho ya damu na nyama.

Binadamu akifa anatisha, ukiambiwa ulale chumba kimoja na maiti huwezi, Hata Kama ni maiti ya mtoto bado utaogopa tu .

Sura ya maiti hukaa kwenye kumbukumbu ya ubongo kwa muda mrefu Sana,kwa mtu yoyote atakayeikodolea macho maiti usoni.

Tabia ya kuaga maiti haina mashiko na sababu yoyote ile.
Kuaga maiti ni kuisanifu maiti, unaagaje kitu kisicho na uhai? Ni kipi kinakusaidia kumwangalia mfu?

Napenda Sana utaratibu wa ndugu zangu waislamu, wao huiandaa maiti na kwenda kuzika basi, kuliko tabia ya mabwana wale wanaopenda kupanga foleni ili kuaga maiti msibani, foleni kubwa Utadhani walimu wanachukua mshahara kwenye ATM ya NMB.

Mwisho wake huwa ni mayowe, watu kuzimia na kuanguka hovyo msibani.

Sura ya marehemu unaitakia nini? Unamuaga marehemu ili iweje?
Huwa napita mbele ya maiti bila kumtazama. Usipoenda kuaga hawachelewi kukusingizia ushirikina
Waislamu hua wanaaga ila ni wanandugu wa karibu tu, tena mwili ukiwa ndani kama haujui ni vema kukaa kimya
 
2015 ndo ilikua mara ya kwanza kuaga na kuona maiti..
Nilienda kumuaga Headmaster wetu aligongwa na gari akafariki.
Alibadirika sura ikwa nyeusi Hafu imevimba inatoa jasho.

Kidogo nianguke kwa uoga mpaka leo sura yake naiona..

Siagi tena mm labda ndugu.
Maiti haitoi jasho, kile unacho ona kama jasho ni ule ubaridi au unyevu nyevu wa barafu anapokuwa kahifadhiwa chumba cha kuhifadhia maiti katika friji za maiti.
 
Labda logic yake ni kuthibitisha na kujiridhisha kuwa maiti ile ni yenyewe (ya mhusika) na sii ya mtu mwingine
 
Kuna mambo mawili hapo

Kudhibitisha kama aliyekufa/anayeenda kuzikwa ni yeye kweli

Kuangalia kama hana uhai yaani kafa kweli maana nyuma waliamini huenda atafufuka baada ya muda fulani

Sasa hivi vyote vinafanywa na umati wote uliohudhuria ili kuweka ushahidi kwa wengi lakini kwa zama tulizonazo hatujui maana ya kuaga ni kutafutia vipicha na yafananayo ndio maana mtoa mada umeona hakuna haja

Tukirudi kwenye uhalisia wa kuaga utaona umuhimu wake
 
Kuna rafiki yangu sana alifariki gafla, niliudhuria msiba ila sikuona maiti yake na tulikuwa hatujaonana miezi mitatu, alikuwa muislamu. Miezi minne imepita ila taswira inayonijia ni kwamba jamaa yu hai tu hajafa kwa kuwa sina taswura ya jamaa akiwa mfu.
 
Kuna Jambo wengi wanafanyaga baada ya kuaga Maiti wananza Kuisimanga, Mara hivi, Mara vile hii si sawa hata kidogo kwasababu tumefunzwa kutoizungumzia vibaya Maiti kwani hata ukimzushia jambo hana uwezo wa kujitetea tena!
 
Back
Top Bottom