Tabasamu la Tulia

Tabasamu la Tulia

MACHACHE KUHUSU JOB NDUGAI
1. Hakuwa Spika Mtenda Haki.
2. Aliua Ofisi ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
3. Alifukuza Wabunge wa Upinzani Bungeni kadiri alivyotaka.
4. Alimuita Mbunge aliyejiuzulu Ubunge (Cecil Mwambe) aendelee kukaa bungeni.
5. Aliwaruhusu waendelee kukaa bungeni Wabunge wawili waliofukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya Chadema (Lijualikali na David Silinde)
6. Aligoma kuidhinisha fedha za matibabu ya Tundu Lissu
7. Alimfuta Ubunge Tundu Lissu
8. Aliruhusu Watu 19 wasio na vyama kuwapo Bungeni(akina Mdee)
Haya yanatosha kumdiskolifai😁😁😁😁
 
Mi nawaza hivi Kauli ya ....mikopo ya nchi....ndo inakuondoa kwenye nafasi nyeti ki simple simple...hivi? Aisee Askofu Bagonza alinena kweli tuchunge kauli zetu...
Na la masilahi yake limekaaje mtu anapojiuzulu nafasi yake?
 
Mi nawaza hivi Kauli ya ....mikopo ya nchi....ndo inakuondoa kwenye nafasi nyeti ki simple simple...hivi? Aisee Askofu Bagonza alinena kweli tuchunge kauli zetu...
Na la masilahi yake limekaaje mtu anapojiuzulu nafasi yake?
Ya kisheria yapo.. Yale ya kiupigaji na 10% ndio basi tena
 
Screenshot_20220111-063953.jpg
 
Dah...kiuno sasa
Watoto wengi walo na akili huwa hivyo.

Ila shule ya Loleza pale Mbeya maeneo ya majengo wanaielewa uzuri.

Hawa watoto wa ile shule enzi zao pamoja na akili zao za kuzaliwa lakini.....

Ila ni mtu wa heshima sasa apige kazi atengeneze pensheni.
 
Jana nimepata maono;

Ndugai asijiuzulu hili swala limalizwe kwenye vikao vya chama.

Kwani kuna kila dalili ya kuchafuka kwa amani yetu jambo hili likiendelezwa.

Kila upande uretreat amani itawale.

Anayesikia neno hili toka kwa Bwana na asikie.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Na wakiendelea kuchekewa watajimilikisha kila kitu. Na mwisho wa siku, wanaume ndiyo tutaonekana kama wanawake vile.

Siku zote ukicheka na nyani, lazima uje kuvuna mabua.
Kawimbo ka Jd "wanaume kama mabinti"
 
 
UJUMBE WA WAZI WA ASKOFU KWA SPIKA WA BUNGE, DKT. TULIA ACKSON MWANSASU

Hongera Dkt. Tulia! Sasa wewe ndiye Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Waandishi wa Habari wanasema umewashinda washindani wako 8 kwa kupata kura zote na wao wameambulia patupu. Lakini sisi tunajua kuwa wewe haukuwa na mshindani kama jinsi ambavyo hakuna upinzani ndani ya Bunge.

Katika Theologia kuna dhana za predestination na preordination! Dhana hizi mbili zinaeleza wazo moja. Kwamba umeufikia wakati kama huo sio kwa uweza, elimu, ujanja, utendaji, mikakati au hata uadilifu wako! Bali umeufikia wakati kama huo kwa sababu ya predestination na preordination kuchukua mkondo wake. Kwamba hizo predestination na preordination ndizo zilizopelekea kuanguka kwa aliyekuwa Spika Job Ndugai, lisikutoke katika fikra zako!

Tunachoweza kukushauri sisi tulio Askofu ni kwamba uipokee nafasi hiyo kwa kutetemeka huku ukijua kuwa hatima ya predestinationa na preordination haibagui. Wewe ni shahidi wa jinsi ambavyo hatima hiyo iliyowatupa kando baadhi ya miamba iliyowahi kuwepo na kuvaa kiburi, majivuno na kujimwambafai! Wengi wao wamezama na kumbukumbu zao zinaendelea kufutika kama vile 'amatebhe' yaani maji ya mvua yanavyokauka haraka!

Ukipokea kijiti kutokana na mazingira ya nguvu ya predestination na preordination, unatakiwa kuwa makini na kunyenyekea. Katika uso wa dunia, wapo watu ambao walipoonywa, badala ya kupokea maonyo kwa unyeyekevu na upole, walitumia mamlaka na madaraka waliyokuwa nayo katika kuwatweza, kuwanyamazisha na hata ikibidi kuwapoteza wengine. Hatima yao haikuwa ndefu na dunia haijakosa mifano ya watu wa aina hiyo.

Lakini sisi Askofu tunao ujasiri wa kukueleza wewe hayo na wewe unaelewa fika kuhusu ujasiri huo na sababu zetu. Ukiyafuata hayo na kujitenga na kiburi pamoja na mitandio yake, hatima itakupeleka mbali na ukiyapuuza na kujipamba na kiburi pamoja na mitandio yake, hatima itakupa kisogo (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
FB_IMG_1643717062531.jpg
 
Back
Top Bottom