Hongerana taasisi ya kiislam ya ISLAMIC PEACE FOUNDATION{IPF} na BARAZA LA MIKUTANO YA KIISLAM{BATAMIKI}.Tamko lenu limesomeka na ninaomba msiishie kwenye hilo tamko peke yake,embu pigeni hatua moja mbele,waelimishen waumini wenu elimu ya uraia ili waweze kupata ufaham mzuri wa kufikia maamuzi yatakayo lisaidia taifa hili kupata maendeleo.Tamko lenu limeeleza vizuri sana mwanzo wa hizo propaganda za udini zilivyoanza kwa kukiita chama cha CUF kuwa ni cha kidini.Chama cha CUF kilipachikwa sifa hiyo mbaya kwa sababu kilikuwa kinanguvu na mvuto ktk zama hizo za kupendwa,na kwakuwa leo Chadema nayo inanguvu na kimekuwa kimbilio la wanyonge si ajabu nacho kupewa/kupachikwa sifa hii ya kibaguzi,na hatuta shangaa kama kesho chama cha UDP au TLP ikatokea kimaja wapo kikapata nguvu kikaitwa chama cha kidini.TAIFA liko hatarini kuingia ktk vurugu za kidini kama viogozi hamtajitokeza kama Islamic Peace Foundation na Baraza la Mikutano ya Kiislam,na kuwa waeleza waumini wenu ubaya wa ubaguzi bilakujali ni wadini,wakikabila au wa inayoyote ile.Tusingoje hadi mambo yaharibike kabisa na kuanza kuunda mahakama za usuruhishi kama Afrika Kusini ama Rwanda,tuchukue atua sasa kukomesha hizo propaganda za kidini.