Taasisi ya Moyo Tanzania yafungwa!

pole sana dr masau....rudi Texas..,TZ ni kama nyani...siku zote nyani haoni kundule..
Hana leseni Texas na huko ameshawatapeli sana waliomsaidia hivyo ni vigumu na akirudi aanze upya kufuata taratibu za kuomba leseni na kusoma upya.Kwani program aliyosoma yeye si ya American residency!
 
Miaka mitano (5) iliyopita, hapa JF kulikuwa na mjadala endelevu mkali sana juu ya ugomvi kati ya Taasisi ya Moyo (THI) na Serikali kupitia Wizara ya Afya. Sakata hili sasa limehitimishwa rasmi kwa kunadishwa kwa mali za THI na huduma kufungwa. Kwangu binafsi hii ni habari mbaya katika mfululizo wa taarifa chungu juu ya matendo ya Serikali kwa Wazalendo wanaojitoa kwa Taifa lao na watu wa nchi yao. Kwa masikitiko makubwa tukio hili linatokea wakati huduma katika Sekta ya Afya zimepolomoka na wadau muhimu wako katika mgomo wa kupigania kuboreshwa kwa mazingira bora ya kazi.

JF imekua sana. Wanachama wa leo karibu ni zaidi ya mara 15 ya wanachama wa mwaka 2007. Wako waliotoka ujana kuja utu uzima na wako waliotoka dalaja la kukosa taarifa kuja kwenye ulimwengu wa habari (hasa mitandao/simu). Hawa wote wanaweza kuwa hawajui mlolongo wa matukio na historia nyuma ya Watendaji kugoma kuboresha mazingira (vifaa, huduma, maslahi ya watumishi, n.k) au kupolomoka kwa UZALENDO wa kweli. Lakini kwa kupitia mfululizo huu ninahakika kwa kiwango fulani watafumbua mawazo na kupata mitazamo sahihi juu ya yote mawili.

Enzi za Kumkoma Nyani Giledi Mchana Kweupe!
Tulisema huko nyuma lkn hatukueleweka na tulioneka hatumpendi Dr Masau,It was just a matter of time,Yametimia!
 
Ukiwa na jibu la kuibia au kukaririshwa kama mwanafunzi unachoweza kufanya ni kulazimisha njia iende kwenye jibu.
Hoja ya msingi ni kuondolewa kwa THI toka nyumba za NSSF,na hapo kuna mkataba wa kupangishana nyumba.Kwenye hili mpangaji ana haki ya kuishi kwenye nyumba iwapo amelipa pango kikamilifu.Kimsingi mara ya mwisho mtakumbuka kuwa THI waliwatumia wagonjwa pia kama kinga kwamba wakiondolewa itahatarisha maisha yao.KWA NINI THI imekiuka mkataba na NSSF?
Hili la hujuma silijui vizuri maana Masau angeweza kupangisha walau Hospitali RAFIKI kama Kairuki akaendelea na huduma pia!Tunaomba anayejua kwa kina hili jambo atupe stori chini ya carpet,tukizingatia kuwa Dr Masau hajalalamika hadharani tangu mali zipigwe mnada,na angeweza kupinga hilo maana tangazo lilitoka siku nyingi kwenye magazeti
 
Ni kweli tunahitaji, lakini ni LAZIMA zianzishwe katika misingi ambayo ni sustainable. Ikianzishwa katika msingi mbovu, inakufa kama ilivyokufa THI kwa kuanzishwa katika msingi mbovu.
Kupeleka wagonjwa wa myoyo na mafua ktk hospitali za nje ndo sustainable kwa selikali?
 
Kisa ni kupotea kwa 10 % ya wakubwa wizarani na wao kukosa perdiemkwenda India etc .
Laana kubwa CCM nyie


Hii ni zaidi ya laana Lunyungu yaani hawa ccm hawa Mungu anawaona na siku sio nyingi atawachapa fimbo ya hatari!
 
Last edited by a moderator:
11.jpg
 
Maadam THI wameshindwa kulipa deni walokopesha mkuu wangu tutashindwa kuwatetea isipokuwa haya matatizo yana mwanzo wake ambao nyie wenyewe hamtaki kutazama upande huo, mmelifumbia macho kabisa tatizo linakoanzia wakati mnajua fika wapi tumeharibu...

Sababu kubwa ya kushindwa ama kufa kwa THI ni fedha - wameenda Bankrupt! na pengine credit yao mbovu vile vile maana kufikia kunadiwa mali zao sijui tuwahurumie vipi wao ama wananchi..Makosa yapo ktk muundo wa AFYA nchini (the making of EL wenu mnayemsifia sana. Kama serikali inaunda Muafaka na makanisa wakati fedha zote za mikopo na grants zinazotolewa nchini Hospital za watu binafsi hazipati kitu hata tax exemptions sasa mnategemea nini kitokee maana tukisema wengine mnasema ni Udini na Uislaam. Ukiuliza utaambiwa hii THI ilikuwa private, sijui hizo za makanisa sio private? Haya madaktari wanagoma hadi Bugando ukiuliza ati wanaunga mkono wenzao, jamani jamani tunadanganyana nini hapa?..

Lini Private hospital doctors wanaweza kuingia ktk mgomo wa watumishi wa serikali ktk mafao yasiyowahusu?, lini madaktari wa private wakagoma kwa madai ya vifaa vya kutendea kazi ikiwa Hospital zao hazihusiki wala hazina matatizo hayo?. Tusidanganyane...Something has to be done nacho ni kuua kabisa hii bureaucracy na kuunda Upya mfumo mzima wa Elimu na AFYA otherwise kuna walimu wanakuja nao na mgomo, utasikia hadi shule za makanisa wakigoma kosa bado ni la JK...

Fedha zipo lakini inakuwa allocated kwa mambo mengine kabisa tena bado ni matumizi ya kawaida halafu tunailalamikia serikali ya JK afanye nini yeye ikiwa wananchi wenyewe hamtaki kuona muafaka unakufa?. Hii ni sawa kabisa na wakazi wa bondeni Jangwani ambao wamekufa kwa mafuriko wakaambiwa wahame wakakataa katakata na wananchiu mkawaunga mkono, yametokea tena mafuriko wakafa wengine imekuwa kosa la serikali, wasamaria wema wakaweka kambi zao kusaidia huku wakiilaumu serikali kutowahamisha watu wale. Yaani tafran tupu, maana matukio mengi nchini ni ya kujitakia sisi wenyewe.
Heshima yako mkuu! Iliyofutwa ni tofauti na hii?!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom