Taasisi na Makampuni yenye majina makubwa ila malipo kiduchu, mnatugombanisha waajiriwa wenu na ndugu zetu

BabaMorgan

JF-Expert Member
Dec 18, 2017
4,050
10,489
Kwanza napenda kutoa shukrani kwa muumba na pia kwa wale wote waliofanikisha Mimi Baba Morgan kupata hii kazi kwenye moja ya kampuni maarufu hapa nchini japo nipo katika ngazi ya chini ila sina budi kushukuru maana ni bora kidogo kuliko kukosa kabisa.

Napenda kutumia fursa hii kuwakumbusha waajiri wa makampuni makubwa kujali maslahi ya wafanyakazi wao kama vile wanavyojali brand name zao, yaani ukubwa wa kampuni uendane na uwezo wa uchumi wa mfanyakazi.

Mimi kule kwetu Namtumbo wanajua nimeajiriwa kwenye taasisi kubwa ila wanapata wakati mgumu na kupelekea kuulizwa maswali ambayo hata mimi binafsi yananiumiza kama vile ni wapi napeleka pesa maana sina maendeleo yoyote na ninapoombwa msaada nakuwa mgumu kusaidia.

Mwisho, nipende kuwakumbusha ndugu zetu sio kila anaefanya kwenye taasisi hizi kubwa ana wadhifa mkubwa; wengine tupo kwenye ngazi za chini kabisa ni vibaraka hatuna kitu mfukoni, tupo tupo tu tunasubiri kuiona kesho.
 
Kuhusu swala la malipo makampuni mengi ya Tanzania yananyonya sana wafanyakazi, embu fikiria kuna baadhi ya kampuni hufikia kutumia CV za graduates kuombea kazi za mabilion ya fedha na kuhaidi kuja kuwapa mshahara mzuri pindi wapatapo hiyo kazi badala yake wakipata kazi wanamlipa fedha kiduchu bila posho wala fedha ya chakula, hakuna likizo, hakun mapumziko, na kazi zinapigwa hadi muda wa ziada. Wahanga wakubwa hapa huwa ni vijana hasa Engineers na kwa sababu wanakuwa hawana cha kufanya inabidi wakubali mikataba mibovu ambayo huishia kuwanufaisha contractors.

Huwa napata wakati mgumu pale ninapoana hata wale waliopewa dhamana na serikali kwa ajili ya kulinda na kutetea maslahi ya wafanyakazi wanakuja site na kufumbia macho hii tabia. Unakuta wafanyakazi hawajavaa safety , wanafanyishwa kazi overtime kwa posho kiduchu halafu wao wanafumbia macho hii dhulma.
 
Mambo ya mwamedi ayo
tapatalk_1589816017200.jpg
 
Kuhusu swala la malipo makampuni mengi ya Tanzania yananyonya sana wafanyakazi, embu fikiria kuna baadhi ya kampuni hufikia kutumia CV za graduates kuombea kazi za mabilion ya fedha na kuhaidi kuja kuwapa mshahara mzuri pindi wapatapo hiyo kazi badala yake wakipata kazi wanamlipa fedha kiduchu bila posho wala fedha ya chakula, hakuna likizo, hakun mapumziko, na kazi zinapigwa hadi muda wa ziada. Wahanga wakubwa hapa huwa ni vijana hasa Engineers na kwa sababu wanakuwa hawana cha kufanya inabidi wakubali mikataba mibovu ambayo huishia kuwanufaisha contractors.
Hili tatizo kubwa sana, ila nashauri sana kwa vijana hasa fani ya uhandisi, wajitahidi kujipa thamani kwa kuwa registered katika board ya wahandisi pindi wanapo kidhi vigezo.

Pili, siku hizi vijana wamejanjaruka hasa ma PE, kwanza kutoa tu CV bila 3mil mpaka 1mil,mtu hakupi CV na kuna makampuni wanatoa hela kwa ajili ya kulipia CV, na kampuni ikipata kazi inabidi ikuchukue,na hili linaruhusiwa mtu kufatilia CV zako kama zilitumika kwenye kampuni, bila ridhaa yako na mwisho wa siku kuidai fidia, hii naiona sana kwa PE. Kwahiyo kwa Graduates wanatakiwa kujua haki zao, sema njaa nazo huwa zina wanyima stahiki zao vijana.
 
Hili tatizo kubwa sana, ila nashauri sana kwa vijana hasa fani ya uhandisi, wajitahidi kujipa thamani kwa kuwa registered katika board ya wahandisi pindi wanapo kidhi vigezo.

Pili, siku hizi vijana wamejanjaruka hasa ma PE, kwanza kutoa tu CV bila 3mil mpaka 1mil,mtu hakupi CV na kuna makampuni wanatoa hela kwa ajili ya kulipia CV, na kampuni ikipata kazi inabidi ikuchukue,na hili linaruhusiwa mtu kufatilia CV zako kama zilitumika kwenye kampuni, bila ridhaa yako na mwisho wa siku kuidai fidia, hii naiona sana kwa PE. Kwahiyo kwa Graduates wanatakiwa kujua haki zao, sema njaa nazo huwa zina wanyima stahiki zao vijana.
Mkuu njaa mbaya sana wengi tunaumia unakuta CV imetumika unaambulia laki na kazi yenye mshahara kiduchu.
 
Mkuu njaa mbaya sana wengi tunaumia unakuta CV imetumika unaambulia laki na kazi yenye mshahara kiduchu.
Poleni sana, ila inabidi mjitahidi kujisadili katika board za wahandisi na EWURA pia hii huwa inasaidia sana kuwapandisha thamani.
 
Poleni sana, ila inabidi mjitahidi kujisadili katika board za wahandisi na EWURA pia hii huwa inasaidia sana kuwapandisha thamani.
Asante mkuu ERB tushajisajili lakini njaa mbaya sana mkuu usiombe mtu atake CV yako kipindi hauna ajira na unanjaa hutojiuliza mara mbili mbili kumpatia maana utahaidiwa vinano, na huwa ni wajanja sana wanakutumia ka hela kadogo cha kuianda CV.
 
Back
Top Bottom