Paul Kijoka
JF-Expert Member
- Oct 25, 2010
- 1,399
- 255
Pumba vu tu
Siamini kama umeangalia ulichokuwa unaandika hapa, ebu rudia kidogo kusoma ulichoandika upime kama unaweza kukiandika tena?Narudia kuuliza 'ivi' kwa wale walosoma science kidogo mambo ya mendelia theory,genetic na makromozome ivi yale makengeza ya Mbowe yana mahusiano kidogo na ya Baba mkwe wake Mtei maana kama uoni wao unafanana kidogo? Anaejua embu afunguke!!! Madhara ya kumtimua Zitto yapo wazi mbona wote hawayaoni?
Mkuu hivo ndo inapaswa kuwa, hata ccm kikwete hapaswi kuwa juu ya ccm.
....sababu kuu ni kumpiga mchungaji ili kondoo watawanyike. Hivi ubora wa zitto dhidi ya mbowe ni nini?
Nawashukuru Zito na Mkumbo kwa angalau kuonyesha some loyalty kwa chama chao. Kwa hili kidogo wameonyesha wanaweza 'kusikilizika'. Hii ni pale walipouhakikishia Umma wa Tanzania kuwa hawatakuwa wa kwanza kujiondoa CDM. Hata hivyo, nikianza na Zito nipende kumshangaa kama kweli yeye ni mwanasiasa mkomavu sasa iweje aitishe press conference na kuanza kujibu ambacho 'hajatuhumiwa nacho'? Ingetosha sana kuiambia hadhara ya watanzania kuwa kilichosababisha nisimamishwe sicho kilichotolewa hadharani. Baada ya hapo ukaisubiri barua ya kujieleza ndipo kama kweli unayo nia ya kujibizana ukarudi na kututhibitishia kwa ushahidi wa umeandikiwa nini ujieleze. Iwapo barua ya tuhuma zako ikiwa ni sawa sawa na alichotueleza Tundu utatuambia nini tena ambao hatukuwa kwenye kikao cheni cha CC? Na iwapo tuhuma zikija zaidi ya 'ulizojibu' utakuja na nyimbo gani tena?
Dakta huyu naye kanishangaza sana. Dokta mzima unakiri.....yaani kweli ulishiriki katika ujinga huu? Kwamba 'mpinzani wenu' aharibu chama mkitazama tu ili baadae 'mnayemtaka' awe mwenyekiti? Hii ni bila hata kuona hatari ya kutengeneza ushindi kwa wapinzani wa chama chenu. huyu ni daktari kabisa! Busara pekee uliyoionyesha angalau ni kuomba radhi lakini sympathy ya wenye kufikiri huwezi kuipata. Utetezi eti hata Barack Obama alitengenezewa mkakati na kupata urais! Hii ndo justification? Obama akiuza ikulu na sisi tuuze! Usomi wetu unanipunguzia sifa kama huku ndiko kufikiri kwa wasomi wetu. Mkumbo, hata kama kweli unampenda kiasi hicho rafiki yako aongoze CDM huwezi kutumia mambo yaleyale yanayodaiwa kutumiwa na JK na wana mtandao wenzie kumwingiza madarakani. Huoni/husikii ambavyo hadi leo CCM inahangaika na hii mitandao?
Ingalikuwa ni mimi ningetulia pasina kuanza malumbano na kutafuta namna ya kurejesha tumaini jipya kwangu toka kwa wanachama wenzangu. Kwa sasa mlilolifanya ni sawa na kuwahimiza CDM wawafukuze kundini. Aliyewadanganya kuwa mnakubalika sana huku uraiani, pasipo kumung'unya maneno ANAWADANGANYA!
Akili ndogo kutawala akili kubwa. PhD mzima anakubali kuwa kikaragosi cha Zitto!
kaka unamponda dokta, waraka umeusoma lakini madini ya SWOT yaliyofanyika humo ndani au umekurupuka tu..???
Kama ni uasisi hata TANU NA CCM zinawaasisi, hoja yako haina mashiko. MSALITI WENU AMETEMWA NYADHIFA ZOTE, angojee baraza kuu na hiyo 14days. kwa kashfa hizo ni maoni yangu hafai hata kuwa kiongozi wa tawi, sembuse taifa??wewe makalio kweli_nani kakwambia CDM ni mali ya wanachama? unajielewa kweli? MTEI asikusikie
Mchango wa zzk kwa taifa hili na kwa chama chake ni wa kiwango cha kupigiwa mifano, badala yakumtia moyo au kujifunza na kufanya vizuri zaidi yake.. wengi wenu inawauma kwa wivu wa kijinga.....!Acheni porojo, majungu na unafiki!
Propaganda na Ushabiki wakujipendekeza upande wa wenye madaraka/fedha hauta wapeleka kokote kisiasa!
Nmeamini CDM ni saccos eti kwanini hakuwatonya akina slaa warudishe mzigo walijikopesha
hiyo siyo hoja unampa umaarufukwanza anakotoka zitto na dr kitila wanajisaidia porini hadi leo.!!!!!wanachofanya tusishangae.watataka wote tukajisaidie porini.nawaomba wanacdm wote popote mlipo tuwaogope watu hawa kama ukimwi.viashiria vinaonyesha hawa watu wamekuwa wakitumiwa kwa maslahi yao binafsi.sasa wanataka kufanya wanacdm wengine wawafuate.mwana cdm atakayewaamini atakuwa anafikiri kwa kutumia makalio for sure
TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHAMA CHANGU CHA CHADEMA
===========
Taarifa ya Dk. Kitila Mkumbo kwa Umma kuhusu Kuvuliwa nafasi za mamlaka ndani ya CHADEMA
SITOKI CHADEMA - YouTube
[video=youtube_share;[U]8HAPGQ0GkZA[/U]]SITOKI CHADEMA - YouTube[/video]
Kuwa chadema ni upuuzi
Sinto kujibu kwakuwa wewe kwasasa ni mwanachama wangu na paswa kukushauri maadili ya chama na misingi yake.. Kuwa huru karibu ofisi za mkoa nitakuelekeza mwanachama wangu.daa zitto ana busara sana.
Kila mtu anajua kuwa tatizo si waraka bali ni
ZITTO KUTAKA VYAMA VIKAGULIWE.
ZITTO KUKATAA POSHO.
ZITTO KUWA TISHIO KWA UENYEKITI WA MBOWE.
YANI MTU ANATAKA KUONGOZA MILELE KAMA MFALME.
HIVI KWA NINI WATU WACHAGULIWE VIONGOZI?
WALE WAADISHI WA HILE RIWAYA YA SIRI NI LAZIMA WACHUKULIWE HATUA.
ZITTO TUTAENDELEA KUKUOMBEA HILI KUKULINDA DHIDI YA MATOFALI KUTOKA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA BAUNSA.
Henry Kilewo, Godbless J Lema.