Taarifa za moja kwa moja: Erdogan atangaza ushindi katika uchaguzi wa marudio Uturuki

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,329
33,138
Taarifa za moja kwa moja Erdogan atangaza ushindi katika uchaguzi wa marudio Uturuki.png


Jumla ya masanduku 191,885 ya kupigia kura yameundwa kwa ajili ya wapiga kura nchini. / Picha: TRT World

Rais wa sasa wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ametangaza ushindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais. Akiwahutubia wafuasi wake jijini Istanbul siku ya Jumapili, Erdogan alisema Uturuki ndiye mshindi pekee, akiongeza kuwa raia wote milioni 85 wa taifa hilo wameshinda. Kwa ushindi huu,
mlango wa "Karne ya Uturuki" umefunguliwa, alisisitiza.

Hotuba yake ilikuja baada ya matokeo yasiyo rasmi kuonesha anaongoza kwa asilimia 52.12 ya kura kwa asilimia 98.2 ya kura zilizohesabiwa. Mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu alipata asilimia 47.88 ya kura.
"Matakwa yenu yamekuwa nguvu isiyoyumba ya Uturuki, kwenye sanduku la kura," Erdogan aliongeza.
Zaidi ya watu milioni 60 walijiandikisha kupiga kura, wakiwemo wapiga kura milioni 4.9 wa mara ya kwanza. Jumla ya masanduku 191,885 ya kupigia kura yalikuwepo kwa ajili ya kupiga kura.

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

Waziri Mkuu wa Libya Dbeibeh amempongeza Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kwa "ushindi wake wa uchaguzi", akisema unaonyesha upya imani ya watu katika miradi na sera zake zenye mafanikio.

1657 GMT - Makamu wa Rais wa Uturuki: 'Taifa letu limeshinda, jimbo letu limeshinda'


Makamu wa rais wa Uturuki Fuat Oktay amesema kuwa "Karne ya Uturuki imeanza."
Alisema: "Taifa letu limeshinda, jimbo letu limeshinda, na Uturuki yenye nguvu imeshinda."

1651 GMT - Waziri Mkuu wa Hungary ampongeza Erdogan
Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban pia amempongeza Rais wa Uturuki Erdogan kwa "ushindi wake wa uchaguzi usio na shaka."
1649 GMT - Emir wa Qatar ampongeza Rais wa Uturuki

Emir wa Qatar amempongeza rais wa Uturuki Erdogan kwa ushindi wake wa raundi ya pili ya uchaguzi na kumtakia mafanikio katika muhula mpya.

1646 GMT - Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 97.1 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.21%
• Kilicdaroglu: 47.79%

1630 GMT — Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 94.1 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.43%
• Kilicdaroglu: 47.57%

1620 GMT- Upigaji kura ulifanyika katika mazingira ya amani: Afisa wa Chama cha AK
Msemaji wa Chama cha AK Omer Celik amesema kuwa mchakato wa kupiga kura nchini ulifanyika katika mazingira salama.

Alisema kuwa chama cha upinzani CHP kilikuwa kinajaribu kuwasilisha data zake kana kwamba ni za kweli. "Tutaheshimu matokeo ya mwisho kama mapenzi ya taifa letu," alisema wakati akihutubia wanahabari.

1615 GMT - Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 89.8 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.72 %
• Kilicdaroglu: 47.28%

1600 GMT — Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 85.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 53.15%
• Kilicdaroglu: 46.85%

1556 GMT — YSK: Hakuna tatizo katika mtiririko wa data
Mwenyekiti wa Bodi ya Juu ya Uchaguzi (YSK), Ahmet Yener, amesema kwamba hakukuwa na tatizo na mtiririko wa data na kwamba data hizo walioneshwa pia vyama vya siasa.

Akisisitiza kwamba mtiririko wa data pia unafuatwa na wawakilishi wa vyama vya kisiasa katika YSK, Yener alisema, "Tunaomba wananchi kusubiri matokeo hadi matokeo ya muda yatangazwe. Hakuna shida katika mtiririko wa data, vyama vyetu vya siasa vinashirikiswha".

1550 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 71.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 53.70%
• Kilicdaroglu: 46.30%

1545 GMT - Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 71.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 54.37%
• Kilicdaroglu: 45.63%
1525 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 55.1 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 55.80%
• Kilicdaroglu: 44.20%
1512 GMT - Marufuku ya matangazo ya matokeo ya uchaguzi yaondolewa

Marufuku ya utangazaji ya matokeo ya marudio ya urais wa Uturuki iliondolewa na halmashauri kuu ya uchaguzi nchini humo.

Baraza Kuu la Uchaguzi (YSK) liliondoa marufuku hiyo hadi saa 12:15 jioni kwa saa za ndani (1515GMT), Mwenyekiti wa baraza hilo Ahmet Yener aliwaambia waandishi wa habari katika mji mkuu Ankara.

1415 GMT - Baraza la uchaguzi la Uturuki halijaripoti tukio lolote
Rais wa Baraza Kuu la Uchaguzi la Uturuki Ahmet Yener amesema kuwa hakuna matukio mabaya ambayo yameripotiwa kwa baraza la uchaguzi wakati wa mchakato wa upigaji kura.

Akihutubia wanahabari baada ya kufungwa kwa uchaguzi huo, Yener alisema pingamizi zote zimeshughulikiwa na mamlaka husika na anawashukuru wote waliosaidia chombo hicho kuandaa uchaguzi huo wenye mafanikio.

1414 GMT - Erdogan atoa wito masanduku ya kura kulindwa
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amewataka maafisa wa uchaguzi kulinda masanduku yote ya kura hadi matokeo yatakapokamilika.

Katika chapisho lake kwenye akaunti yake ya Twitter, Erdogan alimshukuru kila mmoja wa wenzake ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii katika vituo vya kupigia kura tangu asubuhi.
Nawaomba ndugu zangu wote kusimama kwa ajili ya masanduku ya kura hadi matokeo yatakapokamilika. Sasa ni wakati wa kulinda mapenzi ya taifa letu hadi dakika ya mwisho," Erdogan alisema.

1400 GMT - Upigaji kura umekwisha
Upigaji kura umekamilika kote Uturuki kwa duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi.
Kura hizo zilifunguliwa saa mbili asubuhi kwa saa za ndani (0500GMT) na kufungwa saa kumi na moja jioni (1400GMT).

0940 GMT - Matokeo yanayotarajiwa mapema
Mustafa Fatih Yavuz wa TRT World, akiripoti kutoka Ankara alisema, kwamba mkuu wa baraza kuu la uchaguzi anatarajia matokeo ya haraka zaidi wakati huu.

"Watu wanaofuatilia uchaguzi wanasema wanatarajia kura chache zisizo halali katika uchaguzi huu kwa sababu wakati huu karatasi ya kura ni rahisi kueleweka kwa kulinganisha na siku ya Mei 14 ambayo ilijumuisha vyama 24 vilivyogombea ubunge na wagombea wanne wa urais," Yavuz. sema.

0910 GMT - Erdogan na Kilicdaroglu walipiga kura zao
Rais Erdogan, akiwa na mkewe, aliwasili katika Shule ya Kati ya Uskudar Saffet Celebi mjini Istanbul ili kushiriki katika shughuli ya upigaji kura.

Alipokuwa akiingia katika kituo cha kupigia kura katika kitongoji cha Uskudar, ambako rais wa Uturuki anaishi, umati wa watu ulimshangilia kwa shauku kiongozi huyo.
Mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu pia alipiga kura yake katika mji mkuu wa Uturuki Ankara.

0750 GMT - Kura nyingi sana za Hatay kwa Muungano wa Watu
Rahul Radhakrishnan, akiripoti kutoka jimbo la kusini la Hatay, alisema Muungano wa Watu ulipata uungwaji mkono mkubwa katika uchaguzi wa bunge. Hata hivyo, katika kinyang'anyiro cha urais, Kilicdaroglu alipata tofauti ndogo ya kura kutoka kwa watu wa Hatay".

“Rais Erdogan alisema katika hotuba yake mapema wiki hii kwamba anaheshimu kura ya wakazi na serikali yake itaendelea kudumisha ahadi zao ili kujenga upya sehemu kubwa ya jiji hili na kuendelea kutoa huduma kwa wale wanaohitaji zaidi,” Radhakrishnan anasema.

0730 GMT - Mabadiliko katika kampeni ya Kemal Kilicdaroglu
Mabango ya kampeni ya mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu yenye ujumbe, "Wasyria watarejea," yalifurika katika mitaa ya Istanbul, kuashiria tishio la kuwarejesha makwao mamilioni ya wakimbizi wa Syria, lengo ambalo litapata upinzani mkubwa kutokana na sheria za kimataifa.

Ravza Kavakcı Kan, mchambuzi wa kisiasa aliiambia TRT World kwamba katika muda wa wiki mbili zilizopita, kulikuwa na mabadiliko makubwa katika jinsi Kilicdaroglu alivyojibeba. "Hapo awali, alikuwa mkarimu sana na mwenye mtazamo chanya.

Lakini mara baada ya raundi ya kwanza, tulisikia ujumbe mzito hasa ujumbe wa chuki dhidi ya wageni kuhusu wahamiaji na wakimbizi. Kwa hiyo kulikuwa na mabadiliko makubwa katika njia ambayo Kilicdaroglu alianza kujiwakilisha baada ya uchaguzi wa awamu ya kwanza.

0510 GMT - Waturuki wanaanza kupiga kura
Upigaji kura sasa unaendelea na utaisha saa 11:00 jioni kwa saa za ndani (1400GMT).

0500 GMT - Vituo vya kura vya funguliwa Uturuki kwa marudio ya uchaguzi wa urais
Kura za maoni zimefunguliwa kote Uturuki kwa awamu ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi hiyo.
Kulingana na Baraza Kuu la Uchaguzi la Uturuki (YSK), zaidi ya watu milioni 1.92 walipiga kura zao katika vituo vya kigeni na lango la forodha la Uturuki kufikia saa kumi jioni kwa saa za ndani (1300GMT) siku ya Jumamosi.
Katika uchaguzi wa Mei 14, raia wa Uturuki milioni 1.84 walio ng'ambo walipiga kura katika uchaguzi wa rais na bunge.

chanzo. Taarifa za moja kwa moja: Erdogan atangaza ushindi katika uchaguzi wa marudio Uturuki - TRT Afrika
 
kichwa cha habari kinaweza kuzua taharuki..Tume imemtangaza au yy kajitangaza kama Lissu 2020?
 
kichwa cha habari kinaweza kuzua taharuki..Tume imemtangaza au yy kajitangaza kama Lissu 2020?
Mkuu una point nzuri kuhusu kichwa cha habari; lakini sasa ulivyomtumia lissu kama mfano ndipo umeniacha hoi. Lisu hana akili sawa na watu wengine, anaweza kusema chochote!
 
View attachment 2638711

Jumla ya masanduku 191,885 ya kupigia kura yameundwa kwa ajili ya wapiga kura nchini. / Picha: TRT World

Rais wa sasa wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ametangaza ushindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais. Akiwahutubia wafuasi wake jijini Istanbul siku ya Jumapili, Erdogan alisema Uturuki ndiye mshindi pekee, akiongeza kuwa raia wote milioni 85 wa taifa hilo wameshinda. Kwa ushindi huu,
mlango wa "Karne ya Uturuki" umefunguliwa, alisisitiza.

Hotuba yake ilikuja baada ya matokeo yasiyo rasmi kuonesha anaongoza kwa asilimia 52.12 ya kura kwa asilimia 98.2 ya kura zilizohesabiwa. Mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu alipata asilimia 47.88 ya kura.
"Matakwa yenu yamekuwa nguvu isiyoyumba ya Uturuki, kwenye sanduku la kura," Erdogan aliongeza.
Zaidi ya watu milioni 60 walijiandikisha kupiga kura, wakiwemo wapiga kura milioni 4.9 wa mara ya kwanza. Jumla ya masanduku 191,885 ya kupigia kura yalikuwepo kwa ajili ya kupiga kura.

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

1701 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 97.9 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 52.14%
• Kilicdaroglu: 47.86%
1700 GMT - Waziri Mkuu wa Libya: Ushindi wa uchaguzi unaonyesha upya imani ya watu

Waziri Mkuu wa Libya Dbeibeh amempongeza Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kwa "ushindi wake wa uchaguzi", akisema unaonyesha upya imani ya watu katika miradi na sera zake zenye mafanikio.

1657 GMT - Makamu wa Rais wa Uturuki: 'Taifa letu limeshinda, jimbo letu limeshinda'


Makamu wa rais wa Uturuki Fuat Oktay amesema kuwa "Karne ya Uturuki imeanza."
Alisema: "Taifa letu limeshinda, jimbo letu limeshinda, na Uturuki yenye nguvu imeshinda."

1651 GMT - Waziri Mkuu wa Hungary ampongeza Erdogan
Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban pia amempongeza Rais wa Uturuki Erdogan kwa "ushindi wake wa uchaguzi usio na shaka."
1649 GMT - Emir wa Qatar ampongeza Rais wa Uturuki

Emir wa Qatar amempongeza rais wa Uturuki Erdogan kwa ushindi wake wa raundi ya pili ya uchaguzi na kumtakia mafanikio katika muhula mpya.

1646 GMT - Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 97.1 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.21%
• Kilicdaroglu: 47.79%

1630 GMT — Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 94.1 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.43%
• Kilicdaroglu: 47.57%

1620 GMT- Upigaji kura ulifanyika katika mazingira ya amani: Afisa wa Chama cha AK
Msemaji wa Chama cha AK Omer Celik amesema kuwa mchakato wa kupiga kura nchini ulifanyika katika mazingira salama.

Alisema kuwa chama cha upinzani CHP kilikuwa kinajaribu kuwasilisha data zake kana kwamba ni za kweli. "Tutaheshimu matokeo ya mwisho kama mapenzi ya taifa letu," alisema wakati akihutubia wanahabari.

1615 GMT - Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi ya urais yanaonyesha asilimia 89.8 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 52.72 %
• Kilicdaroglu: 47.28%

1600 GMT — Matokeo ya hivi punde ya kura za uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 85.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 53.15%
• Kilicdaroglu: 46.85%

1556 GMT — YSK: Hakuna tatizo katika mtiririko wa data
Mwenyekiti wa Bodi ya Juu ya Uchaguzi (YSK), Ahmet Yener, amesema kwamba hakukuwa na tatizo na mtiririko wa data na kwamba data hizo walioneshwa pia vyama vya siasa.

Akisisitiza kwamba mtiririko wa data pia unafuatwa na wawakilishi wa vyama vya kisiasa katika YSK, Yener alisema, "Tunaomba wananchi kusubiri matokeo hadi matokeo ya muda yatangazwe. Hakuna shida katika mtiririko wa data, vyama vyetu vya siasa vinashirikiswha".

1550 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 71.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 53.70%
• Kilicdaroglu: 46.30%

1545 GMT - Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 71.4 ya kura zilizohesabiwa
• Erdogan: 54.37%
• Kilicdaroglu: 45.63%
1525 GMT — Matokeo ya hivi punde ya uchaguzi wa urais yanaonyesha asilimia 55.1 ya kura zilizohesabiwa

• Erdogan: 55.80%
• Kilicdaroglu: 44.20%
1512 GMT - Marufuku ya matangazo ya matokeo ya uchaguzi yaondolewa

Marufuku ya utangazaji ya matokeo ya marudio ya urais wa Uturuki iliondolewa na halmashauri kuu ya uchaguzi nchini humo.

Baraza Kuu la Uchaguzi (YSK) liliondoa marufuku hiyo hadi saa 12:15 jioni kwa saa za ndani (1515GMT), Mwenyekiti wa baraza hilo Ahmet Yener aliwaambia waandishi wa habari katika mji mkuu Ankara.

1415 GMT - Baraza la uchaguzi la Uturuki halijaripoti tukio lolote
Rais wa Baraza Kuu la Uchaguzi la Uturuki Ahmet Yener amesema kuwa hakuna matukio mabaya ambayo yameripotiwa kwa baraza la uchaguzi wakati wa mchakato wa upigaji kura.

Akihutubia wanahabari baada ya kufungwa kwa uchaguzi huo, Yener alisema pingamizi zote zimeshughulikiwa na mamlaka husika na anawashukuru wote waliosaidia chombo hicho kuandaa uchaguzi huo wenye mafanikio.

1414 GMT - Erdogan atoa wito masanduku ya kura kulindwa
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amewataka maafisa wa uchaguzi kulinda masanduku yote ya kura hadi matokeo yatakapokamilika.

Katika chapisho lake kwenye akaunti yake ya Twitter, Erdogan alimshukuru kila mmoja wa wenzake ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii katika vituo vya kupigia kura tangu asubuhi.
Nawaomba ndugu zangu wote kusimama kwa ajili ya masanduku ya kura hadi matokeo yatakapokamilika. Sasa ni wakati wa kulinda mapenzi ya taifa letu hadi dakika ya mwisho," Erdogan alisema.

1400 GMT - Upigaji kura umekwisha
Upigaji kura umekamilika kote Uturuki kwa duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi.
Kura hizo zilifunguliwa saa mbili asubuhi kwa saa za ndani (0500GMT) na kufungwa saa kumi na moja jioni (1400GMT).

0940 GMT - Matokeo yanayotarajiwa mapema
Mustafa Fatih Yavuz wa TRT World, akiripoti kutoka Ankara alisema, kwamba mkuu wa baraza kuu la uchaguzi anatarajia matokeo ya haraka zaidi wakati huu.

"Watu wanaofuatilia uchaguzi wanasema wanatarajia kura chache zisizo halali katika uchaguzi huu kwa sababu wakati huu karatasi ya kura ni rahisi kueleweka kwa kulinganisha na siku ya Mei 14 ambayo ilijumuisha vyama 24 vilivyogombea ubunge na wagombea wanne wa urais," Yavuz. sema.

0910 GMT - Erdogan na Kilicdaroglu walipiga kura zao
Rais Erdogan, akiwa na mkewe, aliwasili katika Shule ya Kati ya Uskudar Saffet Celebi mjini Istanbul ili kushiriki katika shughuli ya upigaji kura.

Alipokuwa akiingia katika kituo cha kupigia kura katika kitongoji cha Uskudar, ambako rais wa Uturuki anaishi, umati wa watu ulimshangilia kwa shauku kiongozi huyo.
Mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu pia alipiga kura yake katika mji mkuu wa Uturuki Ankara.

0750 GMT - Kura nyingi sana za Hatay kwa Muungano wa Watu
Rahul Radhakrishnan, akiripoti kutoka jimbo la kusini la Hatay, alisema Muungano wa Watu ulipata uungwaji mkono mkubwa katika uchaguzi wa bunge. Hata hivyo, katika kinyang'anyiro cha urais, Kilicdaroglu alipata tofauti ndogo ya kura kutoka kwa watu wa Hatay".

“Rais Erdogan alisema katika hotuba yake mapema wiki hii kwamba anaheshimu kura ya wakazi na serikali yake itaendelea kudumisha ahadi zao ili kujenga upya sehemu kubwa ya jiji hili na kuendelea kutoa huduma kwa wale wanaohitaji zaidi,” Radhakrishnan anasema.

0730 GMT - Mabadiliko katika kampeni ya Kemal Kilicdaroglu
Mabango ya kampeni ya mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu yenye ujumbe, "Wasyria watarejea," yalifurika katika mitaa ya Istanbul, kuashiria tishio la kuwarejesha makwao mamilioni ya wakimbizi wa Syria, lengo ambalo litapata upinzani mkubwa kutokana na sheria za kimataifa.

Ravza Kavakcı Kan, mchambuzi wa kisiasa aliiambia TRT World kwamba katika muda wa wiki mbili zilizopita, kulikuwa na mabadiliko makubwa katika jinsi Kilicdaroglu alivyojibeba. "Hapo awali, alikuwa mkarimu sana na mwenye mtazamo chanya.

Lakini mara baada ya raundi ya kwanza, tulisikia ujumbe mzito hasa ujumbe wa chuki dhidi ya wageni kuhusu wahamiaji na wakimbizi. Kwa hiyo kulikuwa na mabadiliko makubwa katika njia ambayo Kilicdaroglu alianza kujiwakilisha baada ya uchaguzi wa awamu ya kwanza.

0510 GMT - Waturuki wanaanza kupiga kura
Upigaji kura sasa unaendelea na utaisha saa 11:00 jioni kwa saa za ndani (1400GMT).

0500 GMT - Vituo vya kura vya funguliwa Uturuki kwa marudio ya uchaguzi wa urais
Kura za maoni zimefunguliwa kote Uturuki kwa awamu ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi hiyo.
Kulingana na Baraza Kuu la Uchaguzi la Uturuki (YSK), zaidi ya watu milioni 1.92 walipiga kura zao katika vituo vya kigeni na lango la forodha la Uturuki kufikia saa kumi jioni kwa saa za ndani (1300GMT) siku ya Jumamosi.
Katika uchaguzi wa Mei 14, raia wa Uturuki milioni 1.84 walio ng'ambo walipiga kura katika uchaguzi wa rais na bunge.

chanzo. Taarifa za moja kwa moja: Erdogan atangaza ushindi katika uchaguzi wa marudio Uturuki - TRT Afrika
Habari mbaya sana Kwa chadomo hizi.
 
Wapiga kura milioni 60
Uchaguzi jana
Matokeo rasmi leo

Safi sana
 
Back
Top Bottom