Hawezi shindwa: Erdogan achaguliwa kama Rais wa Uturuki kwa mara nyingine tena

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,329
33,139
Erdogan achaguliwa kama rais wa Uturuki kwa mara nyingine tena.jpeg

Baraza Kuu la Uchaguzi nchini humo (YSK) litatangaza matokeo ya mwisho na rasmi ya ushindi wa Erdogan mnamo Juni 1. REUTERS/Murad Sezer

Duru ya pili ya uchaguzi Jumapili ilikuwa ya kwanza katika historia ya nchi kwani hakuna mgombea hata mmoja aliyepata kura za lazima za asilimia 50 katika uchaguzi wa rais wa Mei 14

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameimarisha urithi wake kama kiongozi aliyekaa muda mrefu zaidi nchini humo baada ya kumshinda mgombea mwenza wa upinzani, Kemal Kilicdaroglu, katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais.

Makadirio ya awali siku ya Jumapili yalionyesha Erdogan akipata asilimia 52.11 ya kura dhidi ya mpinzani wake Kilicdaroglu, ambaye alipata chini ya asilimia 48 katika uchaguzi ambao umetajwa kuwa na matokeo mengi zaidi baada ya Uturukiya Ottoman.

Katika hotuba ya ushindi katika makao makuu ya Chama cha AK jijini Istanbul, Erdogan aliyeonekana mwenye furaha tele alikariri mistari michache ya wimbo maarufu wa Kituruki kwa shangwe kubwa za maelfu ya wafuasi wake.

"Tulimaliza uchaguzi wa marudio ya urais kwa kuungwa mkono na watu. Nawashukuru wote waliopiga kura," alisema na kuongeza, "tumepewa jukumu la kutawala kwa miaka mingine mitano."

Erdogan alipata wastani wa kura milioni 27.5, takriban milioni mbili zaidi ya kura milioni 25 za Kilicdaroglu. Tume ya uchaguzi nchini, YSK, itatangaza matokeo ya mwisho Juni 1.

Ushindi wa Erdogan ni wa kustaajabisha zaidi kwani ilimbidi kushinda kampeni ya kutukanwa na vyombo vya habari vya Magharibi.

Valeria Giannotta, Mkurugenzi wa shirika la uangalizi la Uturuki katika kituo cha wataalamu wa Kiitaliano cha Siasa za Kimataifa nchini Italy, alimuelezea Erdogan kama kiongozi "mvumilivu na mwenye nguvu" katika uchambuzi wake wa baada ya kura.

"Matokeo yalionyesha kuwa watu wa Uturuki wanampenda Erdogan na mwendelezo anaowakilisha...miaka mitano ijayo itaangaziwa na mwendelezo, ikiwa ni pamoja na mbinu ya usalama katika mapambano dhidi ya ugaidi. Natarajia kwamba Uturuki itakuwa na nguvu ya kuleta utulivu katika kanda,” aliiambia televisheni ya TRT World.

Duru ya pili ya Jumapili ilikuwa ya kwanza katika historia ya nchi hiyo kwani hakuna mgombea yeyote wa urais aliyepata asilimia 50 ya lazima pamoja na kura moja katika uchaguzi wa rais wa Mei 14.

Katika taarifa baada ya upigaji kura kufungwa, mkuu wa Baraza Kuu la Uchaguzi (YSK) alisema uchaguzi huo ulifanyika kwa amani bila ripoti ya usumbufu.

Katika uchaguzi wa bunge, Muungano wa People’s Alliance unaoongozwa na chama cha AK cha Erdogan, pia ulipata wingi wa vita bungeni ikiwa ni viti 323 katika Bunge Kuu la Kitaifa la Uturuki lenye wanachama 600.
Makadirio ya awali ya duru ya pili ya uchaguzi yalionyesha idadi ya wapiga kura waliojitokeza kuwa zaidi ya asilimia 85, chini kidogo kuliko waliojitokeza kwa asilimia 88.92 Jumapili mbili zilizopita.

Upigaji kura wa watururuki walio nje ya nchi ulikuwa juu zaidi kwa asilimia 55.62 ikilinganishwa na asilimia 52.69 wakati wa duru ya kwanza.

Kuna zaidi ya wapiga kura milioni 64 waliotimiza masharti ya kupiga kura nchini Uturuki na nje ya nchi.
Kwa ushindi huo, Recep Tayyip Erdogan ataongoza kwa miaka mingine mitano ofisini.

Alichaguliwa kuwa rais kwa mara ya kwanza mnamo 2014 na alichaguliwa tena mnamo 2018.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 69 pia aliwahi kuwa waziri mkuu kuanzia 2003 hadi 2014. Hapo awali alihudumu kama meya wa Istanbul kuanzia mwaka1994 hadi 1998.

Mapema Jumapili, Erdogan na mkewe, Emine Erdogan, walipiga kura zao mjini Istanbul na kuwataka wananchi "kujitokeza na kupiga kura bila kuridhika".

Katika mkesha wa duru ya pili ya uchaguzi, rais aliwakusanya wafuasi wake mjini Istanbul, na kutangaza kwamba raia milioni 85 wa Uturuki watakuwa washindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais Jumapili.

"Wote ambao wana imani na utashi wa kitaifa, wana ndoto kwa nchi yetu na wanaona kuwa ni wa ardhi hizi watakuwa washindi katika uchaguzi wa Mei 28."

Zaidi ya watu milioni 64.1 walijiandikisha kupiga kura, wakiwemo zaidi ya milioni 1.92 ambao awali walipiga kura katika vituo vya kupigia kura vya ng'ambo.

Jumla ya masanduku zaidi ya 192,000 ya kura yaliwekwa kote Uturuki.

Vituo vya kupigia kura kwenye lango la forodha pia vilifungwa Jumapili, wakati upigaji kura katika misheni ya kidiplomasia ya Uturuki nje ya nchi ulimalizika mnamo Mei 24.

chanzo. Hawezi shindwa: Erdogan achaguliwa kama rais wa Uturuki kwa mara nyingine tena - TRT Afrika
 
Walau wenzetu wanapata chaguo lao sahihi na kura zinahesabika kihalali.

Siyo ile nchi ya Guam iliyojaa ubabe, wizi,ufisadi na on top of that Kura kuibiwa waziwazi


“Nireeeeeteeeeeni Gwajimaaaa”
 
View attachment 2638810
Baraza Kuu la Uchaguzi nchini humo (YSK) litatangaza matokeo ya mwisho na rasmi ya ushindi wa Erdogan mnamo Juni 1. REUTERS/Murad Sezer

Duru ya pili ya uchaguzi Jumapili ilikuwa ya kwanza katika historia ya nchi kwani hakuna mgombea hata mmoja aliyepata kura za lazima za asilimia 50 katika uchaguzi wa rais wa Mei 14

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameimarisha urithi wake kama kiongozi aliyekaa muda mrefu zaidi nchini humo baada ya kumshinda mgombea mwenza wa upinzani, Kemal Kilicdaroglu, katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais.

Makadirio ya awali siku ya Jumapili yalionyesha Erdogan akipata asilimia 52.11 ya kura dhidi ya mpinzani wake Kilicdaroglu, ambaye alipata chini ya asilimia 48 katika uchaguzi ambao umetajwa kuwa na matokeo mengi zaidi baada ya Uturukiya Ottoman.

Katika hotuba ya ushindi katika makao makuu ya Chama cha AK jijini Istanbul, Erdogan aliyeonekana mwenye furaha tele alikariri mistari michache ya wimbo maarufu wa Kituruki kwa shangwe kubwa za maelfu ya wafuasi wake.

"Tulimaliza uchaguzi wa marudio ya urais kwa kuungwa mkono na watu. Nawashukuru wote waliopiga kura," alisema na kuongeza, "tumepewa jukumu la kutawala kwa miaka mingine mitano."

Erdogan alipata wastani wa kura milioni 27.5, takriban milioni mbili zaidi ya kura milioni 25 za Kilicdaroglu. Tume ya uchaguzi nchini, YSK, itatangaza matokeo ya mwisho Juni 1.

Ushindi wa Erdogan ni wa kustaajabisha zaidi kwani ilimbidi kushinda kampeni ya kutukanwa na vyombo vya habari vya Magharibi.

Valeria Giannotta, Mkurugenzi wa shirika la uangalizi la Uturuki katika kituo cha wataalamu wa Kiitaliano cha Siasa za Kimataifa nchini Italy, alimuelezea Erdogan kama kiongozi "mvumilivu na mwenye nguvu" katika uchambuzi wake wa baada ya kura.

"Matokeo yalionyesha kuwa watu wa Uturuki wanampenda Erdogan na mwendelezo anaowakilisha...miaka mitano ijayo itaangaziwa na mwendelezo, ikiwa ni pamoja na mbinu ya usalama katika mapambano dhidi ya ugaidi. Natarajia kwamba Uturuki itakuwa na nguvu ya kuleta utulivu katika kanda,” aliiambia televisheni ya TRT World.

Duru ya pili ya Jumapili ilikuwa ya kwanza katika historia ya nchi hiyo kwani hakuna mgombea yeyote wa urais aliyepata asilimia 50 ya lazima pamoja na kura moja katika uchaguzi wa rais wa Mei 14.

Katika taarifa baada ya upigaji kura kufungwa, mkuu wa Baraza Kuu la Uchaguzi (YSK) alisema uchaguzi huo ulifanyika kwa amani bila ripoti ya usumbufu.

Katika uchaguzi wa bunge, Muungano wa People’s Alliance unaoongozwa na chama cha AK cha Erdogan, pia ulipata wingi wa vita bungeni ikiwa ni viti 323 katika Bunge Kuu la Kitaifa la Uturuki lenye wanachama 600.
Makadirio ya awali ya duru ya pili ya uchaguzi yalionyesha idadi ya wapiga kura waliojitokeza kuwa zaidi ya asilimia 85, chini kidogo kuliko waliojitokeza kwa asilimia 88.92 Jumapili mbili zilizopita.

Upigaji kura wa watururuki walio nje ya nchi ulikuwa juu zaidi kwa asilimia 55.62 ikilinganishwa na asilimia 52.69 wakati wa duru ya kwanza.

Kuna zaidi ya wapiga kura milioni 64 waliotimiza masharti ya kupiga kura nchini Uturuki na nje ya nchi.
Kwa ushindi huo, Recep Tayyip Erdogan ataongoza kwa miaka mingine mitano ofisini.

Alichaguliwa kuwa rais kwa mara ya kwanza mnamo 2014 na alichaguliwa tena mnamo 2018.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 69 pia aliwahi kuwa waziri mkuu kuanzia 2003 hadi 2014. Hapo awali alihudumu kama meya wa Istanbul kuanzia mwaka1994 hadi 1998.

Mapema Jumapili, Erdogan na mkewe, Emine Erdogan, walipiga kura zao mjini Istanbul na kuwataka wananchi "kujitokeza na kupiga kura bila kuridhika".

Katika mkesha wa duru ya pili ya uchaguzi, rais aliwakusanya wafuasi wake mjini Istanbul, na kutangaza kwamba raia milioni 85 wa Uturuki watakuwa washindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais Jumapili.

"Wote ambao wana imani na utashi wa kitaifa, wana ndoto kwa nchi yetu na wanaona kuwa ni wa ardhi hizi watakuwa washindi katika uchaguzi wa Mei 28."

Zaidi ya watu milioni 64.1 walijiandikisha kupiga kura, wakiwemo zaidi ya milioni 1.92 ambao awali walipiga kura katika vituo vya kupigia kura vya ng'ambo.

Jumla ya masanduku zaidi ya 192,000 ya kura yaliwekwa kote Uturuki.

Vituo vya kupigia kura kwenye lango la forodha pia vilifungwa Jumapili, wakati upigaji kura katika misheni ya kidiplomasia ya Uturuki nje ya nchi ulimalizika mnamo Mei 24.

chanzo. Hawezi shindwa: Erdogan achaguliwa kama rais wa Uturuki kwa mara nyingine tena - TRT Afrika
Ila jamaa alikuwa kamkaba kweli kweli yani kashinda kwa 52%. Semw raia wanamwelewa sana Edo maana niliona wakati akihutubia waendesha teksi yani wanamwona kama nabii
 
Erdogan kachokwa hapo turkiye ni vile bas tu
Erdogan kachokwa ila Kemal Kılıçdaroğlu hakuwa na sera za kushawishi. Na kuna wapinzani wawili wale mmoja angesimamishwa angeshinda. Upinzani ulinchukua KK ana sera za kupendelea wageni wakati Waturuki wengi ni nationalists.

Sasa unashindwaje kumtoa Erdogan na uchumi mbovu hivi, inflation, tetemeko na matatizo kibao. Huyo mpinzani dhaifu sana, na Ogan aliharibu kazi since day one
 
Ila jamaa alikuwa kamkaba kweli kweli yani kashinda kwa 52%. Semw raia wanamwelewa sana Edo maana niliona wakati akihutubia waendesha teksi yani wanamwona kama nabii
Ile Ijumaa ya mwisho Erdogan alikusanya raia milioni 2 uwanjani kwenye kufunga kampeni.
Alafu uchaguzi ulikuwa wa haki na wazi sana, yani hamna sababu ya msingi ya kulalamika.
Erdogan mwenyewe nguvu zinaisha miaka sijui 72 ila mara kama mbili hivi alikuwa anahutubia akasinzia
 
Back
Top Bottom