Taarifa ya Msiba...!

Mkuu Freetown pole sana kwa msiba huo mzito sana....Mungu akupe nguvu na upite kipindi hiki kigumu salama

Mungu amlaze marehenu mahala pema,..Amen
 
.........Kiongozi Teamo na Mkuu Next Level...wengineo wawili waliofika kijijini hapo tutawataja tu pale tutakapopata ruksa toka kwao.....

NL, Teamo, PJ, SaharaVoice, Derimto & JF Arusha na wengineo mliohusika kwenye kutoa faraja kwa familia ya FT HAKIKA hamtaziepuka baraka za Mungu kwa hili mlilofanya.
Mara nyingi binadamu tunatoa with an expectation of receiving back, hili la kwenu is purely giving out of LOVE.
Ni matendo ya Msamaria ambayo hata wakuu wa dini hawakumtendea wasiyemjua.
Tulifundishwa "Ni Heri kuiendea nyumba ya Matanga..."

May the Almighty God Bless you all Abundantly!!!!!!!!!!!!!
 
R.I.P shemeji yetu.. Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake. Inauma sana mzazi mmojawapo kufariki na kuacha watoto. So painful and sad wakuu.
 

Asante mkuu RM! You know what, kama hujawahi pata na tatizo kama hili wakati mwingine unaweza shindwa jua umuhimu wa ''friends in need'' ...unapo ondokewa na mpendwa wako, unahitaji sana faraja ya watu wanaokufahamu, faraja ya rafiki zako, ndugu na jamaa! Sasa kama people waliokaribu na wewe wakikususa wakati huu na faraja hiyo kukosekana unaweza ukakufuru kabisa.....!

tusali sana ndugu zanguni
....unalikumbuka neno la Mchungaji?

Thanks Mkuu NL kwa kutuwakilisha, pole sana kwa msiba na dhoruba iliyowapata njiani.

Asante sana na tumeshapoa sasa......! leo kwake, kesho kwangu na kesho kutwa kwako! Pamoja sana!
 

Ni kweli mkuu uyasemayo.
 
Bro juzi tukiwa pale kwenye msiba kuna wazo nilipata, nitakutext baadae kukueleza.
My ears are attentive Msindima, and my eyes are wide open, ready to receive what you are About to tell me!
Please!:coffee:
 
FL1,
Maji yameshamwagika, na hayazoleki.
Cha maana kwasasa ni kujiandaa sisi tuliobali.
 

Kiongozi Next Level,
Natoa heshima zangu nyingi kwenu wote mliofika kijijini kuzika.
Mmeonyesha kwamba hatima ya maneno na balah blah za kwenye keyboard, ni kusimama na kufanya matendo.
Bila hivyo tusitegemee mabadiliko...Hata haya mambo ya siasa tunayocommet hapa kila siku, bila kusimama na kuchukua hatua pana ugumu sana kupata mabadiliko.
Sasa katika kujitoa kwenu, Ona Mungu amekupeleka kwa ndugu zako, ambapo hukutegemea kuwaona, na Mungu amewakweza.
Mbarikiwe sana pamoja na hawa "ANONYMOUS WAWILI" ambao sasa nawataja rasmi (baada ya kupata go-ahead yao)kuwa ni @Maty @Firstlady.
 

FirstLady naomba nikupe wewe na wengine wote mlioshiriki kikamilifu katika kuupumzisha mwili wa wifi yetu, mpendwa wetu, ndugu yetu katika nyumba yake ya milele. JF ipo kwa ajili ya yote. Mbarikiwe sana sana na mungu azidi kuwalinda ninyi na familia zenu na awatangulie kwa kila jambo. Sisi tulio mbali na nyumbani mchango wetu ni mdogo sana lakini natumaini mnazipokea rambi rambi zetu na tupo pamoja kwa kila jambo. Paka Jimmy umefanya kazi kubwa na nzuri lakini nadhani ni moyo wako na upendo wako umeweza kuyafanya haya yote. Tunawapenda wote na tuzidi kuombeana.
 
Pole sana kwa msiba huo ndugu yangu Freetown.
Ndiyo njia yetu sote, na kazi ya Mungu haina makosa. Nakuombea mwenyezi Mungu akuzidishie amani na ujasiri wa kukabiliana na changamoto mpya katika maisha yako bila ya huyo kipenzi chako na mshauri wako mkuu. Vile vile tuendelee kumwomba Muumba wetu apumzishe roho ya marehemu huyo pema peponi.

Kich;
 
well....!

ujumbe nilioupata kutoka kwa freetown ni huu

''NAOMBA UNISAIDIE KUWEKA BANDIKO DOGO TU LA KUWASHUKURU WANAJAMIIFORUMS KWA NAMNA WALIVYONIPA NGUVU KATIKA KIPINDI HICHI KIGUMU KWANGU....!NINATAFUTA NENO M'BADALA NA ZAIDI YA AHSANTE LAKINI NINASHINDWA!..ahsanteni sana...KWA SASA (AMBAYO NI TAR 06/03/2011 MIDA YA SAA SABA MCHANA) NIPO NAIROBI AIRPORT NINASUBIRI NDEGE YA KUNIRUDISHA ENEO LANGU LA KAZI....nitawashukuru mwenyewe pindi nitakapo tulia!AHSANTENI SANA JAMIIFORUMS''

huo ndio ujumbe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…