UZUSHI Taarifa ya maandamano ya 7/7 kwa wananchuo

UZUSHI Taarifa ya maandamano ya 7/7 kwa wananchuo

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Je taarifa hii ni ya kweli

FB_IMG_1783320944161.jpg
 
Tunachokijua
Kupitia mitandao ya kijamii kumekuwapo na Taarifa kwa umma inayodaiwa kutolewa na wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania kuhusu Maandamano ya Julai 7, 2026 na kuonesha imetolewa Julai 6, 2026.

Taarifa hiyo inaendelea kueleza kuwa inawahimiza wanafunzi wa chuo kushiriki maandamano hayo ka upande wao yakiwa na Ajenda mbili, ya kwanza ni utolewaji wa mikopo a elimu ya juu na ya pili ni kulaani mauaji ya aliyekuwa mwanafunzi wa IFM, James Temba.

Taarifa hiyo ina baadhi ya dosari ikiwemo kutokuonesha imetolewa na nani ama kiongozi wake, lakini pia haina sahihi ya aliyetoa Taarifa hiyo na badala yake imekuwa ni ya jumla. Sambamba na hilo imetumia nembo ya Taifa pekee ambayo si kawaida kutumika nje na shughuli za serikali.

Aidha Jumuiya ambayo inafahamika ya wanayuo ni jumuiya ya wanafunzi Taasisi za elimu ya juu (TAHLISO) ambayo haijachapisha ama kutoa tamko lolote linalofanana na hilo kupitia vyanzo vyao mbalimbali vya mawasiliano.
Mnateseka sana.
Pamoja na kwamba mko madarakani isivyo halali, watumikieni basi watu kwa weledi muache kazi yenu iwatetee.
Vinginevyo mtapata taabu sana....KARMA ipo na inatenda!
Ukitaka kuandamana wewe andamana tuu, kuanza kutoka kauli za uzushi ni kwamba mmeshindwa.
Acheni kuingiza wenzenu chaka kafanyeni KAZI.
 
Ukitaka kuandamana wewe andamana tuu, kuanza kutoka kauli za uzushi ni kwamba mmeshindwa.
Acheni kuingiza wenzenu chaka kafanyeni KAZI.
Ni wazi hukuelewa kabisa nilichoandika, kwaĥiyo hukuwa na haja ya kujisumbua kujibu.
 
Maandamano ya nn watu hatuna hela ya kula *****
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom