Taarifa ya kifo cha wazazi wangu

Taarifa ya kifo cha wazazi wangu

pole sana mpendwa hao watu wabaya sana maeneo ya ngara uko walimuua rafiki yangu kwa kumpiga risasi niliumia sana ila muachie Mungu tu mpendwa
 
Pole sana, Mola akupe nguvu ya kuhimili msiba huu mkubwa.
 
Pole sana mkuu, May God give you and your family strength kwa kipindi hiki kigumu na cha majonzi
R.I.P our parents 🙁
 
Ndugu zangu wana JF, Asanteni sana kwa kunifariji kwa jumbe zenu. Mimi na familia yangu tuna wakati mgumu sana hasa ukizingatia mimi ndiye kijana mkubwa kwetu na nimeachiwa yatima watano. Ni kazi kubwa kuhimili kishindo hiki!!Kusema ukweli wazazi wangu walichinjwa kiasi kwamba hadi vichwa vilikiondolewa. Imagine kitendo hicho, na watoto walikuwa wakitazama hivi....!!

Tumeumia sana, make binafsi hata machozi sikupata, nilibaki nimeduwaa tuu, na hadi sasa, kila ninachokitazama, nawaona wazazi wangu wapendwa...
 
Please wapendwa, kati ya tarehe 3 hadi 6 Mei 2011, Radio Uhuru wakati wa uchambuzi wa magazeti, zilikuwemo taarifa za mauaji ya marehemu wazazi wangu. Aliyenipa hizo taarifa hakumbuki ni tarehe ipi na katika gazeti lipi. Ningeomba msaada wa namna ambavyo naweza kupata gazeti hilo amgalau hata kipande tu cha taarifa hiyo. Tafadhali nisaidieni!!!
 
Jamani poleni sana....ni kwa uweza wa Mungu tu mnaweza kukabiliana na yaliyopo mbele yenu!!!Hao watoto watakua wameathirika sana kushuhudia kitendo hicho cha kinyama....jaribuni kuongea nao kama sio kuwatafutia mtaalamu wa mambo ya saikolojia.Kuhusu kuwalea wala usifikirie sana....kwa sasa hivi hakikisha tu wanajisikia kwamba wako salama mengine yatarekebishika tu huko mbeleni!!Wengi wamepita huko na wameishinda mitihani kwahiyo na nyie mtashinda tu!!Narudia tena poleni sana...mtakua kwenye sala zangu!
 
mkuu pole sana...ni msiba mkubwa umenitia huzuni...mungu akupe nguvu na faraja
 
Pole sana ndugu yangu kwa msiba huu mzito na inahudhunisha sana sana, Mungu akupe nguvu ktk kipindi hiki kigumu.
 
Ndugu wa JF, Salaam,

Nasikitika kuwafahamisha kuwa wazazi wangu usiku wa kuamkia tarehe 2 May 2011 walivamiwa na majambazi wasiojulikana WAKAWAUA WAZAZI wangu wote kwa kuwachoma visu huko Muganza, Rulenge, Ngara.

Nimasikitiko makubwa sana.

Inna li Llahi wa Inna ilayhi rajiun. Pole sana.
 
Ndugu wa JF, Salaam,

Nasikitika kuwafahamisha kuwa wazazi wangu usiku wa kuamkia tarehe 2 May 2011 walivamiwa na majambazi wasiojulikana WAKAWAUA WAZAZI wangu wote kwa kuwachoma visu huko Muganza, Rulenge, Ngara.

Nimasikitiko makubwa sana.

My condolences!!
 
Pole sana mkuu! Mungu akuimarishe!
Serikali ione jinsi ambavyo wananchi wake wanavyoteseka katika nhi yao. Na sasa iweke mazingira salama kwa wananchi wake.
 
Mkuu pole sana kwa msiba huu mkubwa katika familia yenu.

Steve Dii
 
Oooow! Pole sana mkuu,Mungu awape pumziko la heri,...Majambazi! Wasiojulikana! Kuua kwa kuchoma visu!...perhaps ni ujambazi kweli...
 
Yani hii habari imeniharibia siku. Pole sana. Nitakupa rambirambi zangu. Hao mashetani watapata malipo yao hapahapa duniani.
 
Ila ni majambazi kweli au visasi? Kwanini wafanye jitihada yote mpaka kutenganisha vichwa?
 
Ndugu zangu wana JF, Asanteni sana kwa kunifariji kwa jumbe zenu. Mimi na familia yangu tuna wakati mgumu sana hasa ukizingatia mimi ndiye kijana mkubwa kwetu na nimeachiwa yatima watano. Ni kazi kubwa kuhimili kishindo hiki!!Kusema ukweli wazazi wangu walichinjwa kiasi kwamba hadi vichwa vilikiondolewa. Imagine kitendo hicho, na watoto walikuwa wakitazama hivi....!!

Tumeumia sana, make binafsi hata machozi sikupata, nilibaki nimeduwaa tuu, na hadi sasa, kila ninachokitazama, nawaona wazazi wangu wapendwa...


Pole ndugu yangu sipati picha unajisikiaje kwa kweli. Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu cha msiba mzito.
 
Back
Top Bottom