Taarifa kamili kuhusu adhabu ya Dk. Mwaka na wenzake hii hapa kuhusu tiba mbadala na dawa asili

Hawa waliowafungia waganga wa jadi wanajiamini sana, labda wanae Mungu wa kweli. Jamaa wakicharuka na minguvu yao ya giza si wataisha? Haya.
 
upload_2016-7-13_9-48-51.jpeg


Vipi kama hawa walioko Tandale, Buguruni, Mbagala na kwingineko?

Ubani dhukra
Ubani Mashtaka
Udi
Marash Muje
Maji Maiti
Nazi Mbovu
Mayai Viza
Vyungu

Hawa wanasajiliwa na TFDA au baraza la tiba asili?
 
afadhali wafungiwe tu, afya ya mtu si ya kuichezea...
wanawake wenzangu kuliko kumwaga mihela kwa hawa matabibu ni bora uende kufanyiwa vipimo vya kisayansi ujue tatizo lako.
 
afadhali wafungiwe tu, afya ya mtu si ya kuichezea...
wanawake wenzangu kuliko kumwaga mihela kwa hawa matabibu ni bora uende kufanyiwa vipimo vya kisayansi ujue tatizo lako.
Tusisahau hata wanaoenda India na kwingineko baadhi wanarudi wakiwa wamerest in peace!
 
nawashangaa sana hawa watu kama wataendelea kumuacha avunje maadili ya udaktari kwakua matangazo ya huyu mtu yalizidi; sisi wanasheria hua haturuhusiwi kufanya matangazo sasa sijui kama madaktari wameshaamua kwamba wafanye matangazo kama huyu bwana anavyofanya.
 
Ngoja waje hapa wenyewe
Mbona yule mwenye dawa alfulela ulela za kutibu kila ugonjwa duniani na kuwa na maduka ya dawa zake nchi nzima na matangazo lukuki; lakini mwenyewe alishindwa kujisaidia na akaanguka hadharani siku ya harusi yake hayumo? Hii siyo "double standard"?
 
Ulimbukeni wa kuamini zaidi matibabu ya dawa za kizungu ndio yanayo tutesa, hakuna alie lalamika kwa kupata madhara kwa nini watu wafungiwe? uko mahospital watu wanakufa hovyo kwa kukosa matibabu sahihi lakini inaitwa bahati mbaya, kweli ukoloni haujaondoka kwenye fikra za mtu mweusi.
unataka kusema hadi tuone madhara ndio tuchukue hatua?
madhara yakitokea nyie ndio mtakua wa kwanza kudai serikali haifanyi kazi
kuna watu hamna jema kabisa.
by the way mwaka ameshalalamikiwa sana na hizo tiba zake kama hujasikia ni wewe.
afya ya mtu haichezewi
 
"Je wagonjwa amabao wameshatibiwa na matabitu hao wanasemaje?, ni vizuri kuwasikiliza ili kuchukua maamuzi mazuri"
 
Mwaka niliwahi kumuambia lifestyle yake umaarufu,na gari lenye plate no MWAKA itakuwa anguko lake hakunisikia
Hairuhusiwi kumzidi Prof Dr Kigwangala aiiyesota darasani miaka dahari kimaisha
 
Tena serikali imechelewa sana kuwapa adhabu hawa wajanja wachache waliokuwa wakipata pesa kupitia mgongo wa wagonjwa maskini kujipigia pesa pasipo mafanikio kwa asilimia kubwa kwa wagonjwa hao. Ujue hii inchi serikali mlikuwa mmelala sana hasa kwenye hii sekta ya tiba asilia kwani watu wengi wamedhulumiwa kwa sababu ya homa zinazo wasibu kwa uzembe wa serikali. Sasa muanze na ukaguzi wa kina wa hivi vituo asilia na serikali ithibitishe hizo tiba zao kuwa zinaponya ndipo matangazo yao ya weze kwenda hewani. Tiba zihakikiwe kwa kina na wizara ya afya na kufanyiwa majaribio kuona kama ni tiba kweli na hazina madhara kwa binadamu. Mtu ukiwa mgonjwa unaweza kula chochote kinachotangazwa ukajua ni tiba kwa huo ugonjwa kutokana na maumivu uliyonayo kumbe siyo tiba wala chochote. Ni wakati wa kazi kwa vitendo sasa.
 
Mimi nimesoma kidogo na naishi maisha ambayo huwezi kuyaita duni (japo sio bora), nikiugua magonjwa yasiyoeleweka kama kuhisi malaria option yangu ya kwanza huwa ni herbs (mitishamba) na huwa zinanisaidia sana. Sana sana hospitali nakwenda kupima tu na pale daktari anapoona malaria ndio naweza kutumia vidonge huku vikenda simultaneously na mitishamba.
Sio busara kuwakatisha tamaa walioamua kuventure katika mitishamba maana hata makampuni makubwa kama Colgate yanahamia kwenye herbal na hata Glaxo wana dawa nyingi sasa za herbal.
Mkuu sio kuwakatisha tamaa tatizo watu wengi waliopo kwenye hii tasnia wamekuwa matapeli. Hilo ni jambo baya. Pia unapo kuwa umetengeneza hiyo tiba asilia peleka kwenye wizara ili kuihakiki ndipo upewe go ahead ya kuisambaza na kuitangaza hiyo tiba
 
Mkuu sio kuwakatisha tamaa tatizo watu wengi waliopo kwenye hii tasnia wamekuwa matapeli. Hilo ni jambo baya. Pia unapo kuwa umetengeneza hiyo tiba asilia peleka kwenye wizara ili kuihakiki ndipo upewe go ahead ya kuisambaza na kuitangaza hiyo tiba
Nakubaliana nawe mkuu lakini hapa tatizo ni elimu! Elimu tunayohitaji haitolewi na Dr. Mwaka bali inapaswa kutolewa na serikali na kwa vile haikuitoa hivyo kututumbukiza kwenye lindi hili la ujinga, sidhani kama kumzuia huyu Mwaka itasaidia bali msaada ilikuwa ni kumguide ili kuwapunguza hawa wahanga wa ujinga wetu!
 
Mwaka hakuelewa mchezo huu unavyochezwa hakuweza hata kujiuliza kwa nini Dr.Kigwangala alimlenga yeye hadi kumfuata kwenye kituo chake pale bungoni.Kwa maana halisi ya tiba asili yeye kwa kupitia matangazo ya kwenye TV,REDIO NA MAGAZETI maelezo yake yalikuwa yanavuka mipaka utadhani ni daktari wa kusomea,alionywa lakini hakusikia,hiyo ni dharau kwa mamlaka husika.Ajitathimini yeye mwenyewe atafanya nini baada ya hilo tamko hajaonewa ila kayataka mwenyewe.
 
Back
Top Bottom