Taarifa: ACT-Tanzania hatuna ushirika na CUF

Taarifa: ACT-Tanzania hatuna ushirika na CUF

Tayari tumekusikia Nyakarungu, Dotto Rangimoto alishatoa ya kwake hapa sasa tunasubiri tamko la Mwl. Kaijage
 
what is the problem with mkumbo and mwigamba?well,najua mwigamba ana njaa kali,but what is happening to kitila?
 
Sijakuelewa uliposema mwanachama ana haki ya kuhudhuria mikutano ya vyama vingine lakini isiwe ya mikoa ya mbali na wasichangishane nauli ulikuwa na maana gani.
 
Napata shaka kama Prof. Mkumbo ni kiongozi mzuri kwasababu kila anapopita hali ya hewa inachafuka, tumeona wakati yupo CDM na sasa ACT. kwenye taarifa iliyotolewa na ACT kupitia Grayson Nyakarungu (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/782893-taarifa-act-tanzania-hatuna-ushirika-na-cuf.html) ukisoma kwenye hiyo link kuna paragraph inayosema "Bw. Mwigamba na Prof. Kitila, ni watu wakaidi mno, wabinafsi na waroho wakubwa wa madaraka. Kuwavumilia katika taasisi yoyote ile kunahitaji kuwa na moyo wa chuma; historia zao huko walikofukuzwa zinajulikana" hii paraghraph imenishtua sana na kwa vile yeye sasa ni mwenyekiti wa UDASA ambayo ilishaanza kusuasua huko nyuma, sijui ndio atainyanyua au ataimaliza kabisa. Nafikiri wanaUDASA wamchunguze mapema ikiwezekana wachukue hatua kabla hajaimaliza kabisa UDASA.
 
Hawa jamaa nawashauri wajikite katika kuongoza familia zao tu. Nje ya hapo hali yao itaishia hivi hivi.
 
Ila huyo mwenezi fundi sana wa kuandika. Yaani amewakandia hao jamaa na saizi hapo walipo wananuka tehe tehe.
 
Mmehama chama cha CHADEMA na tabia zote za kichadema. Matamko kila kukicha ndio staili yenu ya kukuza chama. Kuna wakati mtakuja toa roho za watu ili tu mpande chati.
 
usichoke mkuu hapa ndipo Ofisi ya Itikadi na Uenezi ACT Tanzania. Kama unaweza kuwaomba Pasword za hizi akaunti za ACT humu unaweza hata uka preview muhutasari, mikataba, matamko mbalimbali na mipango mikakato(work plans) za chama hiki na vyote vipo kwenye inbox ya Nyakarungu, mwalimu kaijage na doto rangimoto.

Zitto yeye ofisi zake zipo Facebook na Twitter hapa ameshakimbia.
 
Tayari tumekusikia Nyakarungu, Dotto Rangimoto alishatoa ya kwake hapa sasa tunasubiri tamko la Mwl. Kaijage

Kwenye mada kama hizi nisipomsikia ndugu yangu Betlehem nakosa raha sana! Au yeye kitengo chake ni cha kutuletea "Mapato na Matumizi ya ACT ya kila baada ya miezi mitatu"! Japo sasa tunaelekea mwezi wa saba toka alipotuletea kwa mara ya mwisho!
Hahahahahaaaaa!!!!
 
"Bw. Mwigamba na Prof. Kitila, ni watu wakaidi mno, wabinafsi na waroho wakubwa wa madaraka. Kuwavumilia katika taasisi yoyote ile kunahitaji kuwa na moyo wa chuma; historia zao huko walikofukuzwa zinajulikana."

Ukweli utajulikana tu! Wakati CHADEMA wakiondoa magugu waliitwa kila aina ya maneno lakini sasa ukweli umeanza kuonekana. Asante Viongozi wa chadema kwa umakini wakuwaondoa watu hawa na zitto wao.
 
Mmehama chama cha CHADEMA na tabia zote za kichadema. Matamko kila kukicha ndio staili yenu ya kukuza chama. Kuna wakati mtakuja toa roho za watu ili tu mpande chati.

Unawashwa washwa wewe si bure! Bila kuitaja chadema hupati buku 7
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom