Taarabu ni burudani, Siasa ni maisha ya watu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Tumeamua kugeuza siasa za Tanzania kuwa kama taarabu!!!?

Imekuwa sasa ni kitu cha kawaida watu kusubiria kuona nani kamnanga nani kisha nani kamjibu na kamjibu nini.Au watu kusubiria waone nani anamzodoa nani ili wajibu. Basi unaibuka ushabiki wa pande zote zinazodoana na siku zinaendelea kwenda. Kadhalika kuna kundi ambalo liko standby kuripoti nani kamzodoa nani na nani kamjibu.

Kwa bahati mbaya hata wale ambao wanatajwa kama wasomi; wengine wakiwa hata na shahada kadhaa, hukikuta kwenye mtego huo. Yaani hatimae tunajikuta kwa asilimia kubwa tunapofikiri na kujadili siasa za Tanzania, badala ya kujadili ni nini hatma yetu kama watanzania na Tanzania kwa ujumla; tunajadili jinsi tunavyozodoana tu! Zaidi ya hapo mambo ya msingi hakuna Mwenye muda wa kufikiri wala kujadili.

Nijuavyo Mimi kuzodoana ni Tania ya kwenye morden taarab kwa kuwa inalenga burudani, lakini hatupaswi kutumia akili, rasilimali na muda wetu wa thamani kufanya kazi ya kuzodoana tu kwani siasa ndio huamua hatma ya maisha yetu.

Hebu tulitafakarini hili kwa kina na tuone kama inafaa kubadilika ama la! Ila kwa maoni yangu tukiamua kubadilika itapendeza.

Aidha, silazimishi mtu kukubaliana na mawazo yangu ila kama mtaniunga mkono nitafarijika kwani naamini mabadiliko haya ni muhimu kwa ustawi wetu sote.

Wengi kuna vitu vingi hatuna ila angalau muda ni rasilimali muhimu ambayo wote Mungu katupa. Nafikiri inafaa kuutumia vyema kujadili mambo yenye maslahi mapana kwetu sote na nchi yetu kwa ujumla. Nchi zilizoendelea na jamii zake kusrawi vyema aghalabu hutumia muda wao vyema.
 
Na wakati mwingine tunawalaumu viongozi wetu bure tu, na pengine maweza kusema tunawaonea bila sababu. Kinachotokea wanatusoma vile tulivyo na kuamua kutupeleka kama tulivyo.Ni sawa na unawaza uchawi, unajadili uchawi na mtu akikuambia habari za uchawi jinsi alivyologa mtu au kulogwa unafurahi kweli kweli, mtu anayetaka umuunge mkono ni rahisi sana kukuchagulia habari zinazohusu uchawi badala ya habari za Mungu kwa kuwa kwa kufanya hivyo utamkubali bila kutumia msuli. Simple logic! Lakini wengi hatujui masikini!
 
Wewe ukitaka kujua tumefikia hatua ngumu, kwamfano toa habari kama hii " Mh. Abdulazizi mbunge wa Jf abambwa akivizia puchi, makamanda waliombamba wambwatukia" halafu utaona ushirikiano utakaojitokeza watu wakipongeza na kukemea. Lakini kwa mfano sema " Serikali yaanzisha mradi wa kuhakikisha kila kijiji kinapata Maji nchi nzima wananchi wote wameombwa kutoa ushirikiano wa hali na Mali ili kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa ifikapo 2020" halafu utaona kama kuna atakayehangaika kuona hata undani wa taarifa hiyo na kutoa mchango wowote wa maana
 
Tumeamua kugeuza siasa za Tanzania kuwa kama taarabu!!!?

Imekuwa sasa ni kitu cha kawaida watu kusubiria kuona nani kamnanga nani kisha nani kamjibu na kamjibu nini.Au watu kusubiria waone nani anamzodoa nani ili wajibu. Basi unaibuka ushabiki wa pande zote zinazodoana na siku zinaendelea kwenda. Kadhalika kuna kundi ambalo liko standby kuripoti nani kamzodoa nani na nani kamjibu.

Kwa bahati mbaya hata wale ambao wanatajwa kama wasomi; wengine wakiwa hata na shahada kadhaa, hukikuta kwenye mtego huo. Yaani hatimae tunajikuta kwa asilimia kubwa tunapofikiri na kujadili siasa za Tanzania, badala ya kujadili ni nini hatma yetu kama watanzania na Tanzania kwa ujumla; tunajadili jinsi tunavyozodoana tu! Zaidi ya hapo mambo ya msingi hakuna Mwenye muda wa kufikiri wala kujadili.

Nijuavyo Mimi kuzodoana ni Tania ya kwenye morden taarab kwa kuwa inalenga burudani, lakini hatupaswi kutumia akili, rasilimali na muda wetu wa thamani kufanya kazi ya kuzodoana tu kwani siasa ndio huamua hatma ya maisha yetu.

Hebu tulitafakarini hili kwa kina na tuone kama inafaa kubadilika ama la! Ila kwa maoni yangu tukiamua kubadilika itapendeza.

Aidha, silazimishi mtu kukubaliana na mawazo yangu ila kama mtaniunga mkono nitafarijika kwani naamini mabadiliko haya ni muhimu kwa ustawi wetu sote.

Wengi kuna vitu vingi hatuna ila angalau muda ni rasilimali muhimu ambayo wote Mungu katupa. Nafikiri inafaa kuutumia vyema kujadili mambo yenye maslahi mapana kwetu sote na nchi yetu kwa ujumla. Nchi zilizoendelea na jamii zake kusrawi vyema aghalabu hutumia muda wao vyema.

KUJADILI HAYO SI NI UCHOCHEZI, TRA, UHAMIAJI, POLISI NK WAPO MACHO KWELI KWELI!
 
Kwa mfano mtemi Kisandu amekuwa akituletea stori kama vile alivyomeza shilingi Mara akiwa na homa Kali akaguswa na kitu kama nyoka. Mtemi kashatusoma na kubaini ni nini tunapenda ku- consume na yeye anachofanya ni kutupa product ambayo tunaweza Ku - consume bila shida , na katika hili kafanikiwa sana ndio maana unaona wengi tunamfuatilia na kula kila anachotupa kwa kadiri kila mmoja awezavyo


Kwa mantiki hiyo, bila kulaumiwa mtu anaweza kusema Mtemi is very intelligent kutuzidi wengi wetu sisi wengine.
 
Vyuma wakaze wao, na taarabu unataka aimbe nani?? Wee jamaa unataka tukose vyote.TUBUU AISEEE
 
Wewe ukitaka kujua tumefikia hatua ngumu, kwamfano toa habari kama hii " Mh. Abdulazizi mbunge wa Jf abambwa akivizia puchi, makamanda waliombamba wambwatukia" halafu utaona ushirikiano utakaojitokeza watu wakipongeza na kukemea. Lakini kwa mfano sema " Serikali yaanzisha mradi wa kuhakikisha kila kijiji kinapata Maji nchi nzima wananchi wote wameombwa kutoa ushirikiano wa hali na Mali ili kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa ifikapo 2020" halafu utaona kama kuna atakayehangaika kuona hata undani wa taarifa hiyo na kutoa mchango wowote wa maana
sawa
 
Yaani kuna vitu havitusaidii ila tunatumia muda adhimu kuvijadili. Kwa maoni yangu kufanya hivyo ni sawa na kutumia dakika 40 za mtihani muhimu kwa kuchora mazombi huku ukichekacheka huku ukiamini utafaulu.
 
CCM ndio waasisi na Vinara wa hiyo taarab.
Suala sio nani muasisi, suala ni kwa nini tuendekeze kitu ambacho tunajua wazi kinatupeleka kubaya?

Haina maana mtu na akili zako timamu unafanza upuuzi ukiulizwa kwa nini unasema alianzisha Fulani, hoja kama hizo tunategemea zitolewe na watoto Wa darasa LA tatu.
 
Tunatarajia sasa kuwa watu watajiyokeza kumjibu Lowasa kila mtu kwa namna yake.
 
Back
Top Bottom