Rakims
JF-Expert Member
- Jun 4, 2014
- 4,982
- 4,481
- Thread starter
- #241
Hapana mkuu nilichokuwa najaribu kueleza ni uwezo wa mwenyezi Mungu katika yaliyopo kwenye mamlaka, rejea nyuma kidogo ukumbuke kuumbwa kwa Adam, hakujua mwenyezi Mungu kama adam atakula tunda? Hakujua kama Allah adam atamtoa bustanini? Hakujua kama Adam atatubu? Hakujua kama atamsamehe?Sasa hapa kwanini tukahukumiwe ukiwa Allah kashaamua wema wetu na ubaya wetu,mimi nikiwa teyari nimeshapangiwa kwenda motoni si nitakuwa napoteza muda kuswali au nikiwa nimepangiwa kwenda peponi si nitakuwa namaliza bure maji kwenye kuratain?
Nalog off
Ukijijibu hayo njoo kwa Firauni, Hakujua kama Firauni hata kubaliana na maneno ya Mussa? Hakujua kama Firauni atatubu wakati anakata roho?
Na mengine mengi maana yake alijua kabisa lakini pia ukumbuke kuwa kila kitu anajua mwanzo na mwisho wake na vyote ni vyake na yeye tu ndio yeye kama alivyomuuliza Mussa, ewe bwana wangu wewe ni nani? Akajibiwa na Mwenyezi Mungu Mimi ni Mimi!!!
Kitu pekee kinachoweza kubadili alichokuandikia ni maombi tu na yeye anajua kama utaomba au huta muomba na atakupa au hata kupa wala huwezi kumlazimisha kwa chochote.
Anajua yote na anafanya kila analotaka, mamlaka ni ya kwake mkuu.
Hadi akili za kuchat na kila kitu ni vyake na haramu kaumba yeye na halali yeye
Rakims