Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?
mimi naichukia ccm kwa sababu nakiona ni chama kinachojitahidi kuficha mabaya yanayofanywa na serikali,na yakijitokeza wanayatetea kwa nguvu zote na wanawachukia wale walioyatoa hayo mabaya.
 
Mwanakijiji ee...., kuna mtu hapa jirani yangu ajui kutumia computer.
Nimemsoma uzi kaniomba nikujibu hivi?!...CCM inanuka kama choo cha kudondoshea kisichofunikwa.

Siipendi CCM kwa sababu Katibu wake mmoja alificha fomu zangu za Chuo Kikuu nikose nafasi Mlimani...
CCM ilinizibia nafasi ya kusoma na sitaisamehe milele!!!. Umemuelewa?

_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?
 
Ahsante mzee mwanakijiji kwa swali hili zuri.
CCM imepoteza mwelekeo haina vision leo hii Tanzania hatujui tunaelekea wapi na tutafika lini na tutafikaje hii yote ni sababu ya CCM. Wangekuwa na nia ya kweli ya kulinda na kusimamia rasillimali ya Nchi positively hiyo miaka 50 tungekuwa mbali sana zaidi hata ya Kenya na Rwanda. Viongozi wengi wa hiki chama hawafikiri nje ya Fikra za mwenyekiti wao na Ilani yao. NCHI imekuwa ya dili kwa sababu viongozi wake ni watu wa dili hakuna pa kukimbilia. Miaka 50 hatuna infrustructure ya maana. CCM sio chama tena bali ni mfumo uliojaa rushwa na takataka gandamizi(huwezi kutenganisha Rushwa na CCM). ili tuweze kusonga mbele angalau tuwe kwenye ramani ya Dunia kama nchi zilizopiga hatua tunahitaji vijana kufanya maamuzi magumu ya kulifuta neno CCM.
 
wezi,mafisadi na zaidi ni nyoka ndio maana hata wao wenyewe wanalitambua hilo ndio maana wanavuana magamba.
 
  1. 7. tunaambiwa tulipe land survey fees sh.2400 kwa meta ya eneo kwenye kiwanja kilichokwishapimwa na kujenga wakati wa kudai HATI miliki. Huu ni uwizi wa wazi wa serikali ya CCM. Kiwanja pamoja na Blocks zinapimwa, kuuziwa kwa wananchi na kupewa fomu ya ofa, unajenga , ukienda kuomba hati miliki unaambiwa lipa survey fees. Mfano kiwanja cha m.30x20= 600x2400=1,440,000(survey fees) WIZI MTUPU
 
Mi naikataa ccm kwasababu kwa muda mrefu imelinda aman ya nchi,ikimekuwa na mtaji wa wanachama kiasi cha kuleta ugumu wa kukiondoa madarakani, kinaongoza serikali inayoheshimu utawala wa sheria,inayoruhusu uhuru wa maoni japo inadhibit kwa kiasi unapokiukwa sana,inayowapa ruzuku vyama kadiri ya matakwa ya sheria licha ya kwamba inasababisha wapinga ufisadi kufanya ufisadi.
 

swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa ccm. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa ccm ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa ccm wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa ccm kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa ccm hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

je wewe unaikataa ccm? Umewahi kujiuliza ni kwanini?

nime-highlight hiyo sentensi kwa maana kwamba, hao ambao wanaichukia ccm kwa sababu ulizozisema wanaweza wakawepo, lakini pia ujue hao wanaoipenda na walioko ccm ni just the opposite wa hiyo sentensi, bila ya faida wanayoipata kule wala wasingekuwa huko, na hiyo iko wazi na wengine huwa wanasema kabisa, tena wengine wako huko lakini wanakiri kufagilia na kupigia kura upinzani, believe me.
Chama chenyewe kinatangaza kuwaharibia biashara na kazi watu ambao hahaiungi mkono! Wengi wako huko kwa uoga wa kupoteza mali na line za kazi/biashara zao. Tana mwanakijiji ungewahofia zaidi hao walio huko bila mapenzi kuliko hawa ambao unahisi wanachukia kwa sababu wako nje
 
Ukweli ni kwamba hiki ni chama cha wapiga dili. Nchi haiwezi kuendelea kwa kuungaunga na kutoa data za uongo. Hapa walipotufikisha panatosha tunahitaji mawazo chanya yenye kufikiri nje ya ilani ya chama. Tunahitaji kiongozi mwenye nia ya dhati ya kututoa hapa tulipo. Huyu huwezi kumpata ndani ya CCM. Kumbuka CCM ni mfumo wa kulinda dili za wapiga dili.
Hadi sasa wamepoteza mwelekeo mfano angalia hili la elimu bure. Ilani yao inakataza elimu kutolewa bure, wanaotekeleza ilani wanasema elimu bure inawezekana (Ref, Lowasa na Makamba). Je wakati wa kutayarisha ilani hawa hawakuhusishwa. Ulaghai mtupu
 
Naikataa ccm kwa Kuwa bado inaendesha serikali kwa mfumo wa kizamani, hawaendi na wakati, mpaka sasa hawajui watanzania wanakua nini? Bado wanajilimbikizia posho, wanabambika bei manunuzi ya serikali, wana malipo hewa ya mabilioni ya shilingi, matumizi ya fedha za watanzania kwa mambo yasiyo ya lazima........natokwa machozi.......
 
Hiki Chama kimegeuzwa kuwa ni cha Kifalme, madaraka wanaachiana watu na watoto wao. Watoto wa Vigogo ndio wamekuwa mstari wa mbele kuiibia nchi na hawaguswi. Viongozi wake wengi ni Mafisadi na ndio waliotufikisha hapa tulipo lakini wanalindana. Wamewauzia nchi Wahindi. Mhindi nchi hii ana sauti kubwa kuliko Mtanzania asilia. Na wanatunyanyasa kweli kweli lakini Viongozi wa serikali kucha kutwa wanakwenda majumbani kwa wahindi kupewa kitu kidogo.
 
Kiukweli siichukii CCM, kwani hata TANU yalikuwepo madudu
KILICHOPO: Uwepo muarobaini wa madudu ndani ya CCM, sera zao zitekelezeke sio kiujanja-ujanja, uwepo uwazi mwema wa kupokezana vijiti
Narudia, siichukii CCM kwani hata mie niibuke na chama changu na kuwepo madarakani, lazima yatakuwepo makundi kunichukia tu
 
Wanaoikataa CCM wanasaidia maendeleo ya nchii hii kwa kuwasaidia CCM kujirekebisha.
Mambo yakiendelea hivi, baada ya miaka kadhaa wote tutakuwa tunaimba CCM kama enzi zileeee tulizokuwa tukiimba mashuleni
 
Kiukweli siichukii CCM, kwani hata TANU yalikuwepo madudu
KILICHOPO: Uwepo muarobaini wa madudu ndani ya CCM, sera zao zitekelezeke sio kiujanja-ujanja, uwepo uwazi mwema wa kupokezana vijiti
Narudia, siichukii CCM kwani hata mie niibuke na chama changu na kuwepo madarakani, lazima yatakuwepo makundi kunichukia tu

Vizuri chama kina ujanja, wanachama wake ni wajanja, Nchi ni ya ujanja ujanja tu. Hebu jaribu kufikiri nje ya CCM USILIMIT Fikra zako au unafaidika na kuwepo hapo
 
aaaaa bwanae sijui hata shule zinasaidia nini kila kitu tuna import..barabara wanajenga wachina ...degree zetu za nini?
 
Sababu zangu za kuichukia CCM ni hizi hapa
1. Ahadi
ni wazuri sana kwenye kutoa ahadi lakini hawana utekerezaji. Kwa mfano ahadi za JK za 2010 nyingi sana bado na ukiangalia muda aliobaki nao, hautoshi kuzitekeleza zote. Mfano hospitali za rufaa, viwanja vya ndege, viwanda huko mtwra ndo vinaleta shida hadi sasa, meli ziwa victoria na nyasa, machinga complex, etc etc
2. Kuutazama upinzani kama uadui. Kada wa CCM akimwaga matusi hadharani siyo issue, lakini wa upinzani inakuwa issue. Why double standard? Mfano kesi ya ubunge wa Lema na matusi Mwigulu Nchemba.
3. Bunge kuwa under CCM. Hadi leo sijaona lolote baada ya kumba mwongozo wa waziri mkuu kulidanganya bunge. Ulitakiwa ushahidi na ukaletwa, lakini hadi leo hauna kitu. Wabunge wa CUF waliwapa passport vimada na wote tunajuwa yaliyowakuta. Why double standard?
4. Kauli ya waziri mkuu kuhusu meremeta inaonyesha kuna watu wapo juu ya serikali na serikali inalitambua hilo. Na kwamba serikali inawaogopa watu hao.
5. WanaCCM kutoa kauli zinazopingana juu ya jambo moja. Na ile tabia ya kumuita mtu dodoma na kumtishia lolote haionyeshi uwepo wa demokrasia. Angalia yaliyomtokea Samwel Sitta. Mara atishiwe kunyang'anywa kadi hii yote ni kutokana na msimamo wake juu ya maswala ya kitaifa.
6. Haya, makundi ndani ya CCM ni alama tosha kuwa wapo mle kwa maslahi binafsi. Hata Nape alisema kwenye mkasi kuwa Lema alishinda kwa sababu ya ugomvi ndani ya chama.
7. Kila mtu ndani ya CCM amegeuka mlalamikaji. Huwezi jua nani wa kutengeneza, mfumuko wa bei, siyo sisi tu hata nchi nyingine upo, huduma za kijamii bure jibu haiwezekani kwa vile nchi zingine wanachangia, lakini wanasahau nchi hizo hawana mali asili kama zetu. Huko kwingine hawaibiwa hadi nembo ya taifa, mfano twiga, ndani ya kiwanja chenu cha ndege. Yaani kila mtu analalamikia mgawanyo wa vitalu, hakuna mtekelezaji.

Jamani nina mengi, nasikia uchungu sana pale ninapomwona mwana CCM anajisifia kuhusu shule za kata wakati mtoto wake hasomi huko.

mwingine naye anajisifia kwa urefu wa foleni eti ni maendeleo....

Na hizo kauli zao ndo zinakera kweli, kwa mfano eti hata nyasi tule lakini ndege ya raisi lazima inunuliwe... Khaaaaa, mwingine naye eti waTZ tuna wivu wa kijinga kwa wawekezaji... Mhnnn...
 
Hili swali lina majibu mengi sana lakini tuseme tu kuwa CCM naichukia kwa kukumbatia rushwa, rushwa ni adui wa haki bila haki mnyonge hana chake, kila nikienda kwenye mahospitali ya umma naona jinsi watanzania wanavyohangaika kwa huduma mbovu, hasa wale wanaoshindwa kutoa rushwa.
 
Back
Top Bottom