Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

ingeweza kushughulikia mambo hayo yote ungeiunga mkono na kuikubali? Vipi kama ikianza kufanya hivyo sasa?

Hilo ni wazo la kinadharia sana. Haiwezekani CCM (ikiwa madarakani) kufanya la maana bila mapinduzi makubwa kutokea yatakayoibandua CCM toka kwenye makucha ya mafia (mafisadi) wa ndani na nje. Kazi yao ni moja tu hivi sasa: ni kusimamia na kuratibu uporaji wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya kikundi maalumu cha "mabwana" ndani ya chama. Wana-CCM wasio na "nasaba" wanatumika tu kama vibarua (watwana) kwa ujira/ushawishi wa makombo.

Baada ya kuimarisha mfumo wa rushwa/ufisadi, hao mafia sasa wamefikia hatua ya kutumia mauaji na hofu kama mkakati wa kubakia madarakani na kukandamiza haki zote na utu wa Mtanzania ili kila mtu aishie kutegemea fadhila zao ili aweze kuishi na kupata "maendeleo"; wanaendesha kampeni ya udini, ukabila na ukanda(?) ili kuligawa kabisa taifa lipoteze kabisa umoja mradi tu wao wabakie na kudumu madarakani kama nyenzo pekee yenye uwezo wa kuunganisha nchi!

Sioni namna CCM kinaweza kurejea kwenye misingi ya ustaarabu zaidi ya kuwekwa nje ya madaraka ya serikali ili angalau mafia wakikimbie na kukiacha kianze upya - kama kitaweza kupona hilo likitokea. Hiki chama hivi sasa ni kama vile kimekumbatiwa kikamilifu na shetani ambaye hakina namna ya kumponyoka!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
ingeweza kushughulikia mambo hayo yote ungeiunga mkono na kuikubali? Vipi kama ikianza kufanya hivyo sasa?

Kwa hali ilivyo ndani ya ccm ni ndoto kugeuka na kufanya yale watanzania tunayotaka,
unajua yale watanzania tunayoyaona kwa macho yanayofanywa na serikali ya ccm ni
kidogo sana,hali ni mbaya sana huko kweye wizara na manispaa,kuna ujambazi unafanyika
wa kutisha na hakuna mtu anaweza kumwambia mwenzie kwa nini unafanya hivi,watu wanajichotea
mahela ya miradi kwa maslahi yao binafsi na kuacha miradi hiyo inakufa,hakuna mtu anajali mali za
umma,ukifuatilia eti kuna magari yamepaki humo kwenye wizara na manispaa kwa mwaka au miaka
ukiuliza unaambiwa Insurance imeisha,only that mwisho wa siku wanauziana.
Tanzania ilipofikia inahitaji kiongozi mwenye dhamira ya dhati ya kuibadilisha hii nchi kuanzia juu
mpaka chini.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?

vipi wewe unaipenda?ni kwa nini?
 
NAICHUKIA CCM KWA SABABU ZIFUATAZO
1. ccm imefanya sula ra rushwa lliwe la kawaida tanzania mfano rejea chaguzi zao
2. ccm ni chama ambacho kimejaa mafisad ambao wameshindwa kuwajibika kwa wananchi, mfano ni mfumuko wa cement kutoka 50000/= mwaka 2005 had kufikia 210000/= 2013 kwa watu wa kanza za kaskazin na kanda ya ziwa victoria
3. ccm inafanya kila aina ya ubadhirifu apa nchini kupitia miladi mbalimbali na watu wanaofanya hivyo wako mtaani wanakula bata, mfano rejea EPA,RICHMOND ,KAGODA,TICS NA N.K
4.NAICHUKIA CCM kwa maana viongoz wake wanafanya biashara haramu rejea KINANA AMBAYE MELI YAKE INAFANYA KAZ YA KUSAFILISHA RASIMALI ZA NCHI HII KWENDA CHINA
5.NAICHUKIA CCM KWA SABABU IMESHINDWA KUWEKLKA MAZINGIRA MAZURI KWA VIJANA WA KITANZANIA
6. CCM INAFANYA BIASHARA YA RASILIMALI YA TANZANIA KWA 10% AMBAYO INAWANUFAISHA WAO ,REJEA MIKATABA MIBOVU AMBAYAO HAD KWA SASA NI MZIGO KWA WATANZANIA
 
_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?

Pamoja na majibu mazuri ya wachangiaji wengi ambayo kimsingi yanafanya niichukie CCM, sio tu kuichukia bali

NAICHUKIA CCM KWA MOYO WANGU WOTE, KWA NGUVU ZANGU ZOTE NA KWA NA KWA FIKRA ZANGU ZOTE!
 
Naikataa CCM kwa sababu zifuatazo:-
1. Kutokuwa makini hususani katika idara nyeti kama elimu na afya. Mfano matokeo mbaya ya darasa la 7 hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa na namna ya kuboresha elimu.

2. Kuifanya rushwa itangulie haki. Ukiwa mwanachama wa CCM lazima rushwa uione kama jambo la kawaida kutoa na kupokea ni jambo la kawaida hata rais wao analijua hilo.

3. Kurithishana madaraka na hata nafasi za kazi katika wizara, halmashauri, mahakamani, hata ofisi za mkoa. Hawazingatii taaluma ya mtu aliyonayo.
 
Kwa sababu imechakaa na imepitwa na wakati.CCM ni analog mpango mzima saiv digital.Kwaheri CCM.
 
kwa mimi naikataa sisiem kwasababu haithamini watanzania wa level ya chini kuna ubaguzi kati ya walichonacho na wasionacho.pia swala lingine la kushangaza ni hili: inawezekanaje mtu anayeiba kuku afungwe miaka 5 au zaidi ili hali anayeiba mabilioni ya pesa za wananchi kwa siku yupo tu anakula bataaa.
 
Sasa kama wewe hujui kwanini watu hawaitaki ccm si ujifie tu jamani:majani7:
 
Mimi ninasababu moja tu kimetengeneza mfumo wa kipuuzi katika nchi hii, kuanzia uraisi mpka ngazi ya familia. Kila mtanzania anawaza kuiba sasa hivi.
 
Mitazamo ya wanachama na wake ni tofauti na mtazamo wangu. Mimi ni mwana mageuzi. CCM na mageuzi ni vitu viwili tofauti. I believe in freedom, human rights, the rule of law, the right of the people to own their natural resources, equal opportunity and social justice. To me CCM does not in any way represent these values.
 
*Hawasimamii chochote - haieleweki kama ni wajamaa ni mabepari au wachumia tumbo
*CCM imetoka kuwa chama na sasa imegeuka kuwa genge la watu wanaoongozwa na personal interests
*Wamepoteza mvuto kama chama cha siasa na sasa wamekuwa ni political survivors
*Hawana utaratibu mzuri wa ku-solve problems za wananchi - na sasa kila solution ni za kisiasa na uongo
* Hawasimamiii misingi iliyoanzisha chama na hawajui kama kuna haja ya kubadilisha misimamo ili wawe tofauti.
*Wamekuwa arrogant
*
 
Nilipewa homework ya kujibu swali hili na mwalimu wangu "Analyze alternative development strategies for African countries that are struggling to attain rapid socio-economic development' miongoni mwa majibu yangu ilikuwa Nchi zimetengeneza miundombinu,zimejenga shule kama Tanzania,kuna 2025 vision.....mwalimu akaniuliza kwa hiyo sasa hivi tumeendelea nikamjibu hapana,akasema What are the alternative strategies.... kwa msingi huo licha ya mengi ambayo CCM wamefanya kwa sababu bado tupo masikini we need the alternative political party with the alternative strategies because CCM strategies have failed
 
Wanaoikataa CCM wanasaidia maendeleo ya nchii hii kwa kuwasaidia CCM kujirekebisha.
Mambo yakiendelea hivi, baada ya miaka kadhaa wote tutakuwa tunaimba CCM kama enzi zileeee tulizokuwa tukiimba mashuleni
Masalia at work....toka mmesambaratishwa na Ben saanane sasa naona wote mmeamua kuwa watetezi wa ccm
 
_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?

Kwasababu naipenda CDM
 
Naikubali CCM ila kwa sasa ninaamini WAMECHOKA na inabidi wapumzishwe pembeni wajipange upya.

"Insanity is doing the same thing over and over again but expecting different results."

 
Last edited by a moderator:
Samahani MMM, kama swali lako lingekuwa "...Kwanini Unaichukia CCM?" ningejibu 'I loathe everything about CCM'
 
Back
Top Bottom