Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

Swali la Ugomvi: Kwanini unaikataa CCM?

Naikataa kwa sababu imelitafuna taifa muraaaaaaaaaaaaa na kutuacha makabwera tukitaabika kwa maisha magumu.
 
_41113236_tanzania_ap_416.jpg

Swali hili ni kwa wale ambao katika fikra zao na mioyo yao wameamua kuikataa CCM. Wameamua kutokujiunganisha wala kujiambatanisha na chama tawala. Kwa hawa CCM ni kinyume nao. Napenda kujua hasa wale wanaoikataa CCM wanaikataa kwa sababu gani hasa? Maana wengine wanaikataa CCM kwa kadiri ya kwamba wako nje lakini wakiingia ndani au wakionjweshwa vya ndani wanakuwa wa kwanza kuitetea. Inawezekana wanaoikataa CCM hawaikatai kwa sababu moja ya msingi isipokuwa sababu nyingi za binafsi?

Je wewe unaikataa CCM? umewahi kujiuliza ni kwanini?

Hili swali ni mtego mkubwa kwa atakayelijibu kwa nadharia za kijujuu, fanya justification ya majibu yako kwa kulinganisha ni kile unachoshabikia na kukiamini kama mbadala wa CCM , kwangu siamini vyama naangalia watu ndani ya vyama kote kote.
 
Majibu yenu haya nitayatoa kwenye gazeti next week....
Mwanakijiji, naikataa CCM kwa sababu moja kubwa... siyo tu imepoteza dira, haina sifa wala uhalali wa kuitwa chama cha siasa. Hakikutimiza, hakiendeshwi na hakiheshimu miiko na masharti yaliyoambatana na uanzishwaji na uendeshaji wa mfumo wa vyama vingi. CCM ni serikali, ni bunge na ni mahakama vyote kwa pamoja na hii imepelekea nchi kuendeshwa si kwa kufuata katiba bali miongozo ya CCM.

Kwa maana nyepesi ni kwamba CCM iko juu ya katiba na ndiyo maana wabunge wanaotokana na CCM, wanaweza kuamriwa kutanguliza maslahi ya CCM mbele ya Taifa na wao wakitikia hewala bwana. CCM iko juu ya utawala wa kisheria na ndio maana hadi leo vyombo vya dola vinawagwaya wahalifu wanaovunja sheria mradi tu ama wana uhusiano wa kimaslahi au ni viongozi wa CCM.

CCM imekuwa pasipoti, kimbilio na hifadhi ya mafisadi, wahujumu uchumi, matapeli, wala rushwa na watoa rushwa na kila aina ya adui wa usitawi wa taifa mradi kwa namna fulani wanainufaisha CCM. Viongozi karibu wote wa CCM, tangia kwenye kata hadi taifa wamepatikana kwa njia isiyo halali, hivyo CCM imetokea kuwa kama taasisi ya kulindana kwa watu wenye tabia zinazoshabihiana.

Kwa tabia hii CCM imeweza kuwa kivutio kwa watu wenye malengo sawa wanaotanguliza utii wa kinafiki katika kutetea na kulinda maslahi yao kwa njia yoyote ile. Salama ya kikundi hiki ni umoja wao katika kuhakikisha kinang'ang'ania madarakani kwani bila dola hakiawezi kudumu hata kwa masaa ishirini na nne, sawa na siku moja. Ukweli ni kuwa si rahisi kwa mabadiliko yoyote kutokea ndani ya kikundi hiki.

Mwanakijiji, naichukia CCM na sina matumaini yoyote yale kuwa hili zimwi linaweza siku moja kubadilika, hapana hiyo ni ndoto kama ya Alnacha. CCM ni saratani inayolimaliza taifa na mpaka siku itakapotokomezwa, nchi haiwezi kusitawi wala kuwa salama...ni swala la muda tu. CCM ni gari lililozeeka na halihitaji tena matengenezo yoyote ile, ni kuvunjwa vunjwa labda kwa njia hiyo tutaambulia "scrap metal".
 
naikataa only because I hate Green n Yellow colour.
:x
 
Mimi nakataa zaidi ya CCM. Nakataa tabia na tamaduni zisizokumbatia innovation na plurality.

Habari za kukataa uwazi, kulindana, kutokukubali makosa, kutojali matatizo, kutokubali mabadiliko, kutokuwajibika, kutojisumbua kufikiri kwa makini kabla ya kutoa majibu rahisi kwa maswali magumu, rushwa, umangimeza, kukosa dira na muelekeo, kutotekeleza ahadi, kuwafanya wananchi wajinga, kuendekeza makundi, kupandisha watu ngazi kwa nasaba na hashuo badala ya uwezo, orodha ni ndefu sana.

Na CCM haina hodhi ya ugavi wa haya mambo. Ni mambo ya tabia na tamaduni kwa hivyo hayana chama.

Na inawezekana yakaonekana sana CCM kwa sababu kimekuwepo siku nyingi zaidi na hivyo kimepata nafasi ndefu zaidi ya kuonyesha makucha yake.

Hata vyama vyetu vya upinzani navyo vina hatari ya kuingia katika lindi hili hili lisilo mwisho.
 
Siipendi ccm kwa sababu,
viongozi wake wengi hawana uzalendo, wanafisadi mali za taifa, wanakula rushwa nene nene na wanalindana kimtandao na makundi,
wanasaini mikataba ya kugawa raslimali kwa wageni,
wanatufanya sisi tuonekane kama ombaomba kwa sababu wamezidi kupokea misaada inayotugharimu utu wetu na uhuru wa kuendesha nchi.
wanawasiliza zaidi matajiri na wawekezaji kuliko wananchi (mwekezaji kutoka nje ya nchi hawezi kuelewa matatizo ya mwanakijiji kuliko mwanakijiji mwenyewe)
wameendesha nchi kwa miaka 51 bila maendeleo hasa vijijini ambako ndiko walipo wa tz wengi ..elimu, afya mbovu hakuna huduma za jamii wala mpangilio.
sababu ni nyingi lakini kwa kifupi viongozi wa CCM walio wengi wana UCHU wa mali na madaraka, na wanaweza kufanya lolote kuvipata.
 
ingeweza kushughulikia mambo hayo yote ungeiunga mkono na kuikubali? Vipi kama ikianza kufanya hivyo sasa?


Hili haliwezekani..
Hawawezi kujirekebisha wakiwa uwanjani...lazima wakashauriane wakati wa mapumziko.

Ni kama inavyosema Newton's first law of Motion

An object at rest stays at rest and an object in motion stays in motion with the same speed and in the same direction unless acted upon by an unbalanced force.
 
naikataa sisiem,kwa nguvu zangu zote!! wawekezaji wa kizungu hawalipigi kodi ila sisi walala hoi ndio tunakomaliwa,viongozi wa ccm wanatibiwa nje sisi tunabanana temeke hospt,na mwananyamala.nitaipendaje sisiem barabara wanajenga kwa mikopo huku madini na wanyama hai wakitoroshwa mchana kweupe.mabilion wameficha uswis na haijulikani pesa ni za nani,nitaipendaje ccm jamani?
 
Back
Top Bottom