Swali la kidemokrasia/kiuchaguzi: Uchaguzi wa Serikali za Mitaa hauna 'kupita bila kupingwa'?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Niko njiani kutokea nyumbani Visiga, Kibaha mkoa wa Pwani. Jana, nilishuhudia uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za wagombea wa CCM, Mtaa wa Visiga A kwa ngazi ya Mwenyekiti na Wajumbe. Leo, uzinduzi utaendelea kwa Mitaa mingine ya Visiga B, Madafu na Maili Thelathini na Tano.

Kadiri nijuavyo, katika mitaa yote hiyo hakuna mgombea wa chama cha upinzani ambaye alichukua na kurejesha fomu au kuteuliwa kugombea. Kadiri nijuavyo, Mitaa hiyo ina wagombea wa CCM pekee.

Imezoeleka na kueleweka kwenye chaguzi kuwa endapo atabaki mgombea mmoja kwenye uchaguzi, mgombea husika hutangazwa mshindi katika kile kinachojulikana kama 'kupita bila kupingwa'. Tena hutangazwa tu na Msimamizi wa Uchaguzi husika.

Je, uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa ni tofauti? Kwenye uchaguzi huu hakuna 'kupita bila kupingwa'? Kama 'kupita bila kupingwa' kupo, kwanini kampeni zimezinduliwa na zinafanyika?
 
Kama 'kupita bila kupingwa' kupo, kwanini kampeni zimezinduliwa na zinafanyika?
Lengo ni kujitoa ufahamu na kutaka kuuonyesha Umma (wa Tanzania na "Mabeberu") kwamba zoezi la uchaguzi lilikuwa "free and fair" na kwamba kanuni na taratibu zote zilifuatwa including uzinduzi wa kampeni - as per calendar ya uchaguzi. Usishangae kwenye majumuisho ya kura za mwisho majina ya wale woote waliojitoa au kunyimwa form yakarudishwa na kuwekewa kura sifuri. Hii ndio CCM
 
CCM wanajitekenya na kucheka wenyewe.
Wenzao huwa wanaiba kura kwenye hatua mwisho.
Tatizo la kuwatumia wenye akili ndogo kama Bashite na Polepole kama wapanga mikakati.
 
Mkuu, kwa vile wewe ni Mwanasheria Msomi tungetegemea uje kufafanua badala ya kutuuliza maswali......!!!
 
CCM wanapenda sana mtelemko, wanatuona sisi watanzania wote ni wajinga, wanataka tuwe wanafiki, angalia sasa vijana wetu wanakata kadi za CCM ili kupata ajira sio kwa kuipenda CCM
 
Mkuu, kwa vile wewe sio msimamizi wa uchaguzi, huwezi kusema waliochukua fomu na kurejesha ni CCM pekee, unless fomu ulikuwa unatoa wewe na kuzipokea wewe.

Ukiona tuu kampeni mahali, ujue kuna upinzani, kupita bila kupingwa kupo, na tayari CCM iliishapita bila kupingwa ni more than 50 %, hivyo huu uchaguzi ni wa kukamilisha taratibu za ushindi wa kishindo cha 99.9%, na hii ndio taarifa tuu ya awali, kazi yenyewe haswa ni 2020!.
P
 
Viongozi wa ccm huu ndio msimu wao wa kupiga ela za chama na ela za wagombea, usiwaone wajinga wenye dili zao wanajuwa wanàchokifanya.
Safari hii hela haipigiki sana, maana uchaguzi hauna amsha amsha
 
CCM imeishapita bila kupingwa kwenye mita, vijiji na vitongoji zaidi 5,000. Ukiona kuna kampeni kwenye mtaa jua kuna mgombea zaidi ya mmoja.
 
Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kufanya mapinduzi hasi kwa sasa huku kikikiuka kwa makusudi kabisa katiba na sheria zilizopititwa na waasisi wake, ikiwa ni jitihada ya kuzidi kufanya mapinduzi hasi ili waweze kuwaletea wananchi maendeleo.
 
Kadiri nijuavyo, katika mitaa yote hiyo hakuna mgombea wa chama cha upinzani ambaye alichukua na kurejesha fomu au kuteuliwa kugombea. Kadiri nijuavyo, Mitaa hiyo ina wagombea wa CCM pekee.


Mkuu kachunguze tena kuna uwezekano asilimia 99. kuna wapinzani amjina yamepitishwa hapo kama sio TLP then ni vyama vikuu yamerudishwa kimyakimya.
 
Ni wakati muafaka sasa wa kumshughulikia baba mkorofi umefika, watoto wote ni kuungana pamoja na kumsubiri yaani akirudi tu na kupiga teke mlango huku kusema...." Haya nyie kunguru humu ndani mno? haya fungueni mlango wangu haraka" Sasa hapo mwenye kijiko, mwenye mwiko haya!! atakayepiga mtama haya!!! Ili mradi tu tumwonyeshe kwamba tumechokaa..uonevu huu hadi lini...hapana.
 
Back
Top Bottom