Nawasihi sana CDM, sasa waanze kwenda ZANZIBAR. Mfano CDM iliweka mikutano Mwanza, Mbeya Na Iringa ambayo nimeisikiliza {niliweka extreme kwenye cm, nikampigia mtu aliyekuwa mkutanoni na kuisikiliza mikutano yote live}.. Viongozi hao wameongea mambo ya mbolea sana sana. CDM ikiongea Mtu unaelewa kitu inayoongelewa, nsikilizie CCM waongee utashangaa sana, Mtu unakuwa busy kusaka lau kitu kimoja tu uipendee CCM unakosa. Sisi tusio Na vyama Mara nyingi hatupendi kuwa biasis but tell me my Friend CCM utaisapot uanzie wapi?
Sasa hivi wamekuja Na Gia ya Kupambana Na CDM Kwa Matusi, tena wanajitapa "Ohoo ukiwaachia CDM wanajidai sana" so CCM mmewaachia Cdm? Kwenye Nini ? So what!!?,.... solution mliyoiona ndio kuwamiminia matusi ya Nguoni?!?! Shit!! Hawa Ccm naamini anaewashauri ni shetani.
Back there, CDM Watumbue Jipu la Muungano, waelezee sintofaham zote zilizojificha Kuhusu yunion hiyo inayolalamikiwa, CDM waelezee A-Z Ya Serikali Tatu, faida Na hasara zake Wazanzibar waelewe hili..
Chonde chonde CDM Hapana kuongelea UDINI, Kwa Uzuri Wala ubaya.. Said Issa Mohamed, Jembe la Ukweli ambaye ni Makam Mwenyekiti CDM Zanzibar alishafafanua Kwa usahihi Na Unyoofu propaganda hii ya Udini Na kuimaliza sidhani Kama kuna haja ya kuinadi popote, Waachiwe CCM wenyewe wahangaike nayo iwatafune.. CCM inakufa vibaya!! TANU died silently lakini CCM inakufa vibaya dear...!!
Wazanzibar ni binaadam kama wewe Na mimi, unajua binaadam yeyote akiambiwa ukweli lazima auelewe Kwa Sababu ukweli ndio asili ya mwanadam Hata kama ni mwovu., CDM wakiongelea ukweli Wa Masuala ya Zanzibar pasipo kuwahadaa kama CCM wanavyofanya, Wala kuleta propaganda zenye Sumu lazima wananchi wote waikubali..
Mie nikwambieni propaganda Za Matusi, ugaidi, udini.. Nasema Hata Kama zingekuwa Za kweli still mwananchi hawezi kuziafiki Wala kuzisikiliza, mwananchi huyu mnyonge, kapigika, yuko chokambaya, Bado Na umaskini wake anadhulumiwa, Watoto wake wako home Kwa kukosa Ada, matibabu hapati Hata akipata amezungushwa mbaya, Hana pa kushtaki akidhulumiwa, kila ataposhtaki atageukwa Vibaya Na kujuta, Haki haipo popote, polisi Na raia ni paka Na panya, Mtu akiibiwa kitu, akipigwa, akigongwa Na gari, bora wamalizane wao Kwa wao ila mkithubutu kumpelekea Kesi yenu mlinda Amani mmekwisha, utasumbuliwa Na polisi zikutoke fedha ilihali wewe Ndo mshtaki[tena nowadays polisi Hata ile chembe ya waoga, haya , Aibu imepungua sana, SIO polisi wote ila wengi wao hawana Cha kuogopa, Mtu anakutupia namba haloo NITUMIE Kwenye hii Tigopesa au mpesa Wala haogopi, au akikunasa njiani akiingia Ndani ya GARI lako Na kuona chenji umeziweka mahali Ndani ya GARI utasikia "Nipe hizi hizi zinantosha" anaziokota mwenyewe zote huyo anashuka jamani??!!?]... Nchi hii? Halafu kitokee Chama Chenye majibu haya kisha Misukule flan waseme hao ni magaidi, Mara wadini ok wawe magaidi au wadini whatever tunawataka Kama watakubali kujaribu kutuondoa huku. Wakishindwa tutawatupa NJE Na kuchagua wengine kulikoni kuwarudisha nyie mlio prove kishindwa..