Unajua humu watu wamemeza maji ya chadema, huna utakalowaambia wasilitetee hata kama baya. Sasa hizi hoja za CDM hazihitaji majibu ya serikali, bali wao wenyewe tu wanaweza kujipatia majibu. Mbona katika masuala ya ufisadi ni wazuri chadema kufatilia, au kwa sababu kuna madonge kule wanapata kutia matumboni?
Hill suala la wajumbe, halitizami Quantity, muungano huu haujatizama quantity, wajumbe kutoka Zanzibar lazima wawe sawa na wale kutoka Bara, ili ikitokezea suala la kupiga kura iwe Fair, wale wajumbe wamekuja kuwakilisha wananchi au taifa? Kama wananchi waende bungeni basi!
Hili la mfuko wa jimbo mie huwa linanishangaza, sasa Jimbo lolote la Zanzibar LAZIMA LITAPATA RUZUKU KUTOKA KATIKA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR NA YA JMT, sasa nyie CDM, baada ya jimbo la bara lolote kupata ruzuku ya JMT mlitegemea ruzuku ya pili itoke serikali gani? Ivi mnaa akili lakini au ushabiki tu kama wa simba na yanga ndo mlokua nao? Ardhi, ile ardhi iliokuwepo Zanzibar itafika kipindi itakuwa adimu hasa, ndio maana asiekuwa mzanzinari haruhusiwi kumiliki ardhi, kwa sababu ya uhaba wa ardhi, leo hii nna uhakika kuna wabara mamilioni wanataka waende wakaishi Zanzibar sasa ikiwa shughuli ndio hyo wapewe ardhi, mwisho Zanzibar itajaa wa bara mana ndio wengi wenye hela na hasa za ufisadi.....
Pesa za elimu ya juu, labda hapa ifafanuliwe kidogo nijue izo pesa zinahusu nini, kama mkopo basi sijaona hoja mana pesa inatoka kwa JMT na sio serikali ya tamganyika, kwaiyo ile hela ni ya kila mtanzania.
Matuta yawe ya muungano?? Lolz! Ivi madini yalikuwa yawe ya muungano? Kisha ndugu zanguni, sio baada ya zanzibar kujijua kuwa kuna mafuta ndo wakataka kujitenga, mafuta zanzibar yaligundulikana tangu enzi za mwarabu, na Alama ikawekwa, na ukenda mida ya mchana katika hilo eneo, unajua kabisa kama hapa pana mafuta, kwaiyo msidanganyane bureee eti mafuta yaligundulika juzi juzi, ni lazima tuyatoe katika muungano kwa sababu hatutaki kudhulumiwa, mlikuwa na gesi ya songo songo sijawahi kuskia zanzibar ikipata mapato kupitia iyo kitu ama na sisi ilikuwa tunapewa bure kwa serikali kisha wananchi wanalipishwa ili serikali ipate hela.
Nendeni mkatapike maji mlokunywa, ushabiki wenu unawafanya muwe vipofu, kama CDM wanataka kuisaidia Zanzibar ipate uhuru mi naona kama ni wanafiq tu, kwanini wasianze kampeni za wao kudai taifa la tanganyika? Wao wakidai Tanganyika, na zanzibar wakidai yao for sure idadi ya wananchi itakuwa kubwa ambayo inataka nchi 2 zirudishe sovereignty, hamuoni happ kama CDM ndi itakuwa imeisaidia znz na tng? Eti Mnakaa mnasema CDM wanataka kuisaidia Znz, how? Kwa kuchukua ardhi yao ndogo? Kwa kiwanyima hela ya chuo? Kwa kuwachukulia mafuta yao?
CDM kaeni mtafute TANGANYIKA na sio Kujifanya mnaitetea Znz kwa kutaka kuwaibia!