Swali kwa Waziri wa Elimu na IGP kuhusu kukatwa posho za ulinzi wa mitihani strong Room kuwalipa ma OCD

Brightg

JF-Expert Member
Sep 24, 2013
373
660
Mhe. Waziri wa Elimu na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, naomba ufafanuzi natumai mnasoma swali hili, ni kwamba inapofika wakati wa Mitihani ya Form 6 na Form 4 Askari huwa ni walinzi pale Strong Room yalipo Mitihani, na huwa wanapewa posho kwa ajili ya ulinzi huo, sasa imeanza kuwa desturi au tamaduni za ma OCD na wakuu wa vituo kukubaliana na ma Afisa Elimu na Watendaji husika kuwa Fedha wanazolipwa ASkari kama posho kwenye ulinzi wa Mitihani ma OCD au wakuu wa vituo huwa wanaomba wamegewe sehem ya posho hizo nao walipwe wakati wao hawalali usiku kucha wakilinda mitihani hiyo (Askari hujikuta hapewi pesa iliyo kadiriwa kama posho kwenye ulinzi)isingekuwa utaratibu unaopangwa mhasibu asingekuwa na mamlaka ya kupunguza posho hizo.

Ni sheria ipi inayotumika kumega kwenye posho hizo za askari ili na wao ma OCD wapate, zoezi hili ni la muda mrefu hawajaanza leo ndio maana wamekuwa wakiendelea tu kufanya hivyo.

Askari wenye Nyota wao pia huenda hawaruhusiwi kwenda kulinda mitihani HUKO MA SHULENI, ila kwa sasa wana wanyanyasa ma coplo na constable kuwazuia wasiende wao ndio waende huku wakijua wao hawawezi kubeba silaha kwenye lindo hilo. Kupata uhakika zaidi kagueni shule zote mtawakuta askari wenye Nyota wapo wa kutosha karibia kila baada ya shule 3 lazima utamkuta askari mwenye nyota mmoja yupo kwenye kituo wanafunzi wanapofanyia mtihani, Msaada wa ufafanuzi kama kuna sheria inayo walinda au la. Kwako Mhe. Waziri wa Elimu na IGP.
 
Nadhani Mimi Ndiyo Sijakuelewa
Masuala Ya Kijeshi Hujayajua
Askari Hufanya Kwa Taratibu Nzuri
Kama Umepita JKT Utakuwa Unajua Mambo Ya Mfano, Brigedi, Kikosi, Kombania, Platuni, Section
 
Mhe. Waziri wa Elimu na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, naomba ufafanuzi natumai mnasoma swali hili, ni kwamba inapofika wakati wa Mitihani ya Form 6 na Form 4 Askari huwa ni walinzi pale Strong Room yalipo Mitihani, na huwa wanapewa posho kwa ajili ya ulinzi huo, sasa imekuwa tamaduni za ma OCD na wakuu wa vituo kukubaliana na ma Afisa Elimu na Watendaji husika kuwa Fedha wanazolipwa ASkari kama posho kwenye ulinzi wa Mitihani ma OCD au wakuu wa vituo huwa wanaomba wamegewe sehem ya posho hizo nao walipwe wakati wao hawalali usiku kucha wakilinda mitihani hiyo (Askari hujikuta hapewi pesa iliyo kadiriwa kama posho kwenye ulinzi).

Ni sheria ipi inayotumika kumega kwenye posho hizo za askari ili na wao ma OCD wapate, zoezi hili ni la muda mrefu hawajaanza leo ndio maana wamekuwa wakiendelea tu kufanya hivyo.

Askari wenye Nyota wao pia huenda hawaruhusiwi kwenda kulinda mitihani HUKO MA SHULENI, ila kwa sasa wana wanyanyasa ma coplo na constable kuwazuia wasiende wao ndio waende huku wakijua wao hawawezi kubeba silaha kwenye lindo hilo. Kupata uhakika zaidi kagueni shule zote mtawakuta askari wenye Nyota wapo wa kutosha karibia kila baada ya shule 3 lazima utamkuta askari mwenye nyota mmoja yupo kwenye kituo wanafunzi wanapofanyia mtihani, Msaada wa ufafanuzi kama kuna sheria inayo walinda au la. Kwako Mhe. Waziri wa Elimu na IGP.
Kabla ya yote ungesema sheria inayowazuia askari wenye nyota kubeba silaha au kulinda mitihani.

Kuhusu posho kumegwa hii nimewahi kuiona somewhere lakini kama unavyojua hii ni bongo, JPM kajitahidi kumaliza hii tabia lakini bado wezi na wala rushwa wapo wengi sana tena unaibiwa ukiwa unashuhudia mchana kweupe.

Shida askari akiamua kupaza sauti hapatatosha, kwanza next time hatapangwa kwenda kwenye mitihani, pili atachezewa fitna nyingi kazini ikiwemo uhamisho na kupangwa malindo ya hovyo mwanzo mwisho.
 
Hongera askari...
Unapotaka kusimamia haki sharti moja muhimu ili isikugjalimu wewe uwe msafi hapo ndipo maaskari wote wanakuwa sawa hakuna askari msafi ktk mazingira ya kawaida.
Hakuna sheria ya askari yeyote asibebe silaha km ipo hebu nitaje ila ni kawaida mkubwa kutobeba silaha ikiwa mdogo yupo.hao wenye nyota kwenye vita hawabebi?kiafrika huwezi ukatembea na mzazi/mtu mzima au kiongozi wako yeye kabeba mzigo ww hauna labda uwe na udhuru ila kubeba mizigo ni heshima.
Pia kuna suala la majungu baina yenu yaani kazi yenu imefitinika.

Mwisho km ni km desturi umeikuta umejaribu kuuliza kwa nn iwe ivyo?faida na hasara zake ni zipi?
Pia ningependa kujua kuwa km ww ungekuwa ndo ocd ungeleta huo uzi hapa au mtu angeleta huo uzi ungemuonaje?
Kikubwa ni busara ila ujue napo hali ikikuendea vibaya huko lindoni msaada uujue pia unaupatia wapi.
Kwa muda huu si la mwisho ila nakumumbusha unaweza pia kumwambia afande apangwe mtu mwingine badala ya wewe maana jambo hilo hulikubali na halikupi amani ya kweli..hivyo kwenye iyo kazi hautakuako na sababu za kijeshi ukazitafuta zinazokubalika halafu maisha yakaendelea.
 
Askari unalalamika wakati mkononi una SMG na risasi 30???!!!

Wamwage k.inyesi hao upate haki yako.

Haki inadaiwa haiombwi!
Mdanganye ma Ocd tupo macho sana kabla yajatoa usalama na kuelekezea mtutu kwangu tiari nisha mmwanga mavi yeye.
 
Mkuu upo Wilaya gani? Ni bora ungekua specific hayo yanatendeka eneo lipi la nchi kwasababu ni kweli kuna miongozo kutoka Baraza la Mitihani la Taifa juu ya posho za wote wanaohusika na usimamizi wa mitihani hasa ya darasa la saba, kidato cha nne na ile ya kidatu cha sita

Kwenye muongozo wa Baraza, OCD yupo kwenye Kamati za Mitihani za Wilaya ambazo zipo chini ya Wakurugenzi wa Halmashauri. Wajumbe wengine ni pamoja na Maofisa Elimu Wilaya na Wasaidizi wao wa Taaluuma, maofisa usalama Wilaya nk na wote hao posho zao zimetajwa kwenye muongozo wa Baraza na fungu lake husimamiwa na Wakurugenzi

Askari wanaosindikiza misafara ya mitihani na wale wanaolinda siku za mitihani na strong rooms za kuhifadhia mitihani posho zao pia zimeainishwa na kanuni na miongozo hiyo, kwa hiyo mleta mada ana hoja ya msingi japo sifahamu kanuni zao za kuhusu askari mwenye cheo gani ndio anapaswa kubeba silaha

Ni kweli pia kuna malalamiko kua baadhi ya ma OCD ambao ndio wanajukumu la kuchagua na kuwapanga askari kushiriki zoezi la uangalizi wa mitihani wamekua na tabia za kukata posho za askari wanaowachagua kushiriki kwenye zoezi hilo. Lakini hili linafanyika kwenye baadhi ya Wilaya tena kwa kutumia ubabe tu au makubaliano ya hao askari na huyo anae wapangia kwani posho zao hua wanalipwa moja kwa moja na wahasibu/makeshia wa Halmashauri husika

Nakushauri umfate ofisa elimu wa Wilaya uliyopangiwa lindo na umuulize kuhusu haki zako ila utambue kua tofauti na wewe ambaye umechaguliwa kwa bahati tu kusimamia/kulinda mitihani, OCD yeye kwa mujibu wa Muongozo wa Malipo ya posho za kusimamia mitihani yeye anaingia moja kwa moja kwenye kamati ya mtihani ya Wilaya japo hapaswi kuchukua posho za anaowapanga kwenda kushiriki zoezi la uangalizi wa mitihani
 
Haya ni mambo ya enzi hizi? Sijawahi kuona askari analinda mitihani enzi zetu, na wala sikujua inawekwa wapi zaidi ya kuingia kwenye chumba cha mitihani na kupewa mtihani.
 
Tatizo la kwanza:
Miongozo ya malipo ipo lakini haiwekwi wazi kwa askari, wengi wanapokea tu kiasi watakachopewa lakini hawajui kwenye miongozo wanapaswa kupewa kiasi gani.

Tatizo la pili:
Ubabe na ukoloni wa jeshi la polisi, kama tu vile jeshi linavyoishi vibaya na kuchukiwa na wananchi, ndivyo askari na maofisa wanavyoishi. Kuna ubabe mwingi wa kijinga na dhulma hususani kwa askari wadogo. Pia hakuna mfumo mzuri wa askari kufikisha malalamiko yake bila kuingia matatizoni.
 
Nadhani Mimi Ndiyo Sijakuelewa
Masuala Ya Kijeshi Hujayajua
Askari Hufanya Kwa Taratibu Nzuri
Kama Umepita JKT Utakuwa Unajua Mambo Ya Mfano, Brigedi, Kikosi, Kombania, Platuni, Section
Maswala ya Kijeshi yana utaratibu wake ulio ainiswa, askari akipangiwa posho huwezi kumkata posho ili wewe unufaike pia, kuna sehem na ww una posho yako kama kwenye vikao ambayo yeye askari mdogo hausiki na hawezi kumegewa, na askari wa Nyota huwa habebi silaha.
 
Back
Top Bottom