Swali kwa wanaume waliooa tu

Swali kwa wanaume waliooa tu

Mkuu hawezi akanishinda hata siku moja. Niko fiti sana kwa upande wangu sijui wewe huko.

Kama haujiamini katika mapambano unajitahidi unatafuta means nyingine ya kumshinda Mkuu.

Bado unaamini katika kupigana kama njia ya kutatua tatizo?
 
Scenario #1, sina jibu na sijui nitamfanya nini.

Scenario #2 tutaachana/ nitamuacha.

Hitimisho, siwezi kuishi na mzinzi wakati najua kabisa ni mzinzi. We'll call it a day.

Shukrani.
 
'Scenario' namba moja:
Unarudi nyumbani toka mizunguko yako ya kila siku, unafika nyumbani hamadi unakutana na mke wako anakusaliti na mwanaume mwingine nyumbani kwako.

'Scenario' namba mbili:
Unapata taarifa kuwa mke wako wa ndoa anakusaliti, unafanya uchunguzi na kujiridhisha ni kweli anafanya hivyo. Na ushahidi unao.

Sasa naomba uniambie, wewe utafanya nini ukikutana na 'scenario' moja wapo hapo juu. Yani nataka uniambie ile 'immediate action' utakayoichukua ndani ya dakika moja unaposhuhudia suala hilo.
Sitaki uniambie utafanya nini baada ya siku au week au miezi kupita baada ya kitendo hiko.

Nadhani nimeeleweka.

Kwa haraka nitarudi nilikotoka kwanza halafu nikajifikirie nadhani nitachanganyikiwa.
 
Bado unaamini katika kupigana kama njia ya kutatua tatizo?
Sio katika mambo yote mkuu but mtu akileta dharau kama scenario zako zinavyosema siwezi vumilia. Mwanaume wa kweli lazima utoe adhabu ya kweli Mkuu ili kulinda heshima yako man.Mwanaume anakuja kulala kwenye kitanda chako halafu wewe unataka kumuacha kisa uonekane mstarabu mbele ya macho ya watu. Hainiingii akilini kwa upande wangu.
 
Sio katika mambo yote mkuu but mtu akileta dharau kama scenario zako zinavyosema siwezi vumilia. Mwanaume wa kweli lazima utoe adhabu ya kweli Mkuu ili kulinda heshima yako man.Mwanaume anakuja kulala kwenye kitanda chako halafu wewe unataka kumuacha kisa uonekane mstarabu mbele ya macho ya watu. Hainiingii akilini kwa upande wangu.

Mwenye kosa ni mwanaume au mkeo aliemleta?
Nani kakuambia kuwa ukimpiga ndo unalinda heshima yako?
Ukikaa kimya nini kitatokea?
 
maamuzi ya haraka ni kufungua friji.. unavuta castle lager.. unawasha TV.. unaangalia huku ukiwa unatafakari kinachofuata.. situation kama hizo sio za kukurupuka unatafuta kisu kiko wapi, uanze kumchoma yupi... Maamuzi ya busara huja ukiwa sober, maamuzi ya busara zaidi huja baada ya kunywa bia.
 
Mwenye kosa ni mwanaume au mkeo aliemleta?
Nani kakuambia kuwa ukimpiga ndo unalinda heshima yako?
Ukikaa kimya nini kitatokea?
Wote wana makosa.

Ukimuekea alama ya ukumbusho atakuwa anatoa salute Mkuu akiona. Ukikaa kimya atajithibitishia kuwa wewe ni boya ndiyo maana mwanamke anakuletea dharau mpaka kuingiza wanaume home kwako.

Kiukweli huezi kufumania mke wako unaempenda ukawa mpole aisee labda uwe umemchoka sana na ulikuwa unatafuta namna ya kuachana nae. Hapo unaweza kuwa kimya.

if you were really down with her, you might be provoked.
 
Ukitaka akuogope hadi kufa kwake wee ukimkuta wala usimuulize jifanye huna lolote la kumuuliza na usimwambie chochote!! (Ila hapo uwe na roho ngumu ya kuvumilia maumivu) wee fanya yako ndani ya nyumba kesho yake asbh uone kama hajaenda kwao bila hata kuaga!!! Huu ni ushuhuda kuna jamaa yangu alikuta hivyo akafanya hivyohivyo yule mwanamke wake kesho yake alikimbilia kwao na kule kwao hakusemabkafanya nini kulekule nako akatimka tena[emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Scenario 1:
Naamini sintoweza kuvumilia kuna kitu kibaya nitafanya ingawa mara nyingi najipa imani nitakausha ila kwa hakika nita react aggressively Mungu ninusuru.
Scenario 2
Baada ya kuoa nilijipa ahadi kua i wont sneak around about my wife sipeleki pua yangu kwenye hizo mbishe labda inikute 1st scenario ila kufukunyua nah nah maana ubavu wa kumuacha sidhani kama ninao na sijawahi kufikiria.
 
maamuzi ya haraka ni kufungua friji.. unavuta castle lager.. unawasha TV.. unaangalia huku ukiwa unatafakari kinachofuata.. situation kama hizo sio za kukurupuka unatafuta kisu kiko wapi, uanze kumchoma yupi... Maamuzi ya busara huja ukiwa sober, maamuzi ya busara zaidi huja baada ya kunywa bia.

Hahaha. Umetisha. Inaelekea wewe sio mzee wa mihemuko na maamuzi ya pupa.
 
Wote wana makosa.

Ukimuekea alama ya ukumbusho atakuwa anatoa salute Mkuu akiona. Ukikaa kimya atajithibitishia kuwa wewe ni boya ndiyo maana mwanamke anakuletea dharau mpaka kuingiza wanaume home kwako.

Kiukweli huezi kufumania mke wako unaempenda ukawa mpole aisee labda uwe umemchoka sana na ulikuwa unatafuta namna ya kuachana nae. Hapo unaweza kuwa kimya.

if you were really down with her, you might be provoked.

Soma ushauri wa wa stendi
 
Hahaha. Umetisha. Inaelekea wewe sio mzee wa mihemuko na maamuzi ya pupa.
ukiona hasira inakuzidi nguvu tafuta bia tu, piga mbili kwanza kichwa kikae sawa halafu ongea na mtu aliekukwaza, lazma muafaka upatikane kwa amani kabisa.. hata ukikwazana na mama watoto kapige bia rudi home, ukimwona lazma utamshushia mabusu, atabaki anashangaa tu..

IT WORKS FOR ME.
 
Na ikitokea huyo muhusika anakuzidi nguvu na ujanja?

Huwezi kuzidiwa ujanja ndani mwako kwani lazima hata silaha za jadi zitakuwepo, hata kama baunsa yaani inakuwa ni lion is cornered and has to find a way to escape!
 
je sisi tulio kwenye uchumba sugu hatujafuzu kujibu hili swali? kibest luza zaidi
 
Scenario ya #1 kikubwa ni kuwapa vilainishi ili wamalize hamu yao kabisa.
 
Bavaria kuna vitu vingi vya muhimu vitakavyopelekea nini kitafanyika ntakavyomkuta wife katika hizo scenario.
Kwa mfano, kama tayari tuna mikwaruzano au nna ukakasi nae kuhusu uaminifu wake, mshtuko hautakua mkubwa sana japo hilo tukio halitaniacha vizuri lakini itakua tofauti sana na kama nimekua nikimwamini mke wangu na sijawahi kusikia chochote kisha nije nikute ananisaliti kwangu, kwa kweli hapo siwezi kuwa na jibu sasa hivi ntachukua maamuzi gani. naweza kukwambia ntatembeza kichapo, lakini ki uhalisia nikaishia kulia na kuumia sana, nnaweza kukwambia ntaondoka zangu niwaache kwanza, lakini hali ikawa tofauti kabisa nikatembeza dozi havy kwa wote au wife peke yake. Vilevile inategemea huyo jamaa niliyemkuta na wife, kama ni mtu ambaye nna uhakika anajua kabisa kwamba huyo ni mke wangu hapo ndio kabisaa option zinazidi kuwa chache mkuu.

Hiyo scenario ya pili, kidogo unakua umeanza kua na picha ya mwendo wa mke wako kwamba ni mzinzi, kitakachokushtua ni siku ya kwanza kupata habari au fununu kwamba mkeo anakusaliti, hizo habari lazima zilete chengachenga licha ya kujali ni za kweli au uongo, habari zenyewe tu zinaweza kusababisha maafa.

Cha msingi, kwa wale tulio kwenye ndoa, tuheshimu wito mkuu na hadhi ya majukumu tuliyoingia, asikudanganye mtu kusalitiwa inauma sana.
 
'Scenario' namba moja:
Unarudi nyumbani toka mizunguko yako ya kila siku, unafika nyumbani hamadi unakutana na mke wako anakusaliti na mwanaume mwingine nyumbani kwako.

'Scenario' namba mbili:
Unapata taarifa kuwa mke wako wa ndoa anakusaliti, unafanya uchunguzi na kujiridhisha ni kweli anafanya hivyo. Na ushahidi unao.

Sasa naomba uniambie, wewe utafanya nini ukikutana na 'scenario' moja wapo hapo juu. Yani nataka uniambie ile 'immediate action' utakayoichukua ndani ya dakika moja unaposhuhudia suala hilo.
Sitaki uniambie utafanya nini baada ya siku au week au miezi kupita baada ya kitendo hiko.

Nadhani nimeeleweka.
Anze wewe utafanyaje??
 
Ndoa Itakoma Endapo Mambo Yafuatayo Yatatokea:-
1. -Mmoja Wa Wanandoa Kufariki
2.- Mmoja Wa Wanandoa Kufumaniwa Katika Uzinzi.
3. -Mmoja Wa Wanandoa Kupatwa Na Kichaa (Insanity)
4 Mmoja Wa Wanandoa Kushindwa Kabisa Kufanya Tendo La Ndoa.

Lakini Kabla Ya Kutekeleza Hiyo Namba 2 Jitathimini Kwanza Wewe Kama ni Msafi. Kama Si Msafi Basi Busara Itumike Na Msamaha Upite.
Asante
 
Back
Top Bottom