St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,634
- 4,519
Rafiki yangu ameoa,na mungu amewajalia ndoa yenye furaha tele na watoto wawili juu.Bwana ni bosi mkubwa tu katika wizara moja,na mama naye ni katibu muhtasi katika moja ya idara nyeti serikalini inayoshughulika na masuala ya fedha.Hivyo katika maisha yao shida ya maisha wanaisikia kwa wengine tu.Sasa siku ya siku jamaa yangu akampigia simu mkewe kuwa atachelewa kurudi kwani kazi zimemzidi,mke naye bila hiyana akamwambia usiwe na wasiwasi mimi utanikuta nyumbani.kumbe jamaa ana lake moyoni,baada ya kumaliza kazi siku hiyo akamchukua sekretari wake ambaye ni binti mdogo na mbichi kabisa na kwenda naye guest house moja maeneo ya sinza ambayo inasifika kwa maficho yake .Kufika tu kabla hata hajaingia ndani akashangaa kukuta gari ya mke wake iko parking.Ile tu anatoka kutaka kujua kulikoni anamuona mke wake anatoka huku akijifunga vizuri bazee lake na pembeni yake ameandamana na kijana ambaye wamemuajiri shambani kwao ili awasaidie kutunza mifugo yao.Ingekuwa wewe ndio limekukuta balaa hilo ungefanyaje?