sijui jinsi y kumjibu mtoto, lakini nadhani paka mating rates zao ni ndogo na wakiwa kwenye heat hawawi monitored.
Hivi ni kwanini Paka sio wengi kama Ng'ombe au Mbuzi wakati hawaliwi wala kuuawa na wanazaliana tu kila kukicha tena uzao wao ni wa mkupuo? Tazama jinsi ng'ombe wanavyochinjwa kila kukicha na uzao wao ni mmoja mmoja lakini wako wengi sana.
Wana ecology tunaomba majibu na ukiweza tupia swala ulowahi kushindwa kumjibu mtoto/mwanao
Kweli swali gumu sana; kwani simba na other cats uzazi wao ukoje?
Herbivores wanazaliwa wengi na kukua wengi kuliko carnivores, swala la food chain linahusika l think. Tuwasubili ma-ecologists waje na majibu ya kuridhisha.
mwalimu gfsonwin njoo utuambie kwenye food chIn nyau ana nafasi gani?
Mtoto wangu bint wa miaka mitatu anauliza
Kuna fathercat na mothercat ila atajuaje yupi ni yupi?
Kwake yeye viumbe hawa si wengi ila anaamini ni haohao na akimuona wa rangi nyingine ina maana amebadili nguo
Anauliza,ameivuaje?
Daaahhh sijui umewaza nini maana nimebaki kucheka tu, ila ngoja lifanyiwe uchunguzi,Ni wengi, sema mchana wanakuwa binadamu!
Hivi ni kwanini Paka sio wengi kama Ng'ombe au Mbuzi wakati hawaliwi wala kuuawa na wanazaliana tu kila kukicha tena uzao wao ni wa mkupuo? Tazama jinsi ng'ombe wanavyochinjwa kila kukicha na uzao wao ni mmoja mmoja lakini wako wengi sana.
Wana ecology tunaomba majibu na ukiweza tupia swala ulowahi kushindwa kumjibu mtoto/mwanao
kwenye food chain herbivores wanazaliwa wengi zaid kuliko carnivores. hali huwa mbaya zaid kwa wale carnivores ambao wako wild. omnivores wao wako intermidiate. mara nyingi sana ecosystem huwa ina grow kwa pyramid shape as inaepuka ku exoushoust the lower energy givers.
kwa namna ya kawaida kabisa kama ukigeuza ecosystem ukawa upside down basi tunategemea wale top carnivores washindwe kuwepo as watakosa sources of food.
ingawa hernbivores ni wengi8 but also energy available kwao ni nyingi zaid kuliko ambayo iko kwa top carnivores for that matter hii inachangia uchache wao pia.
Si kweli km paka haliwi..
Anayejibu huwa hafikirii sana kama anayeuliza.
Nianze kwa kusema kwamba sijaweza kuthibitisha kama ngombe ni wengi kuliko paka kwa kuwa sijaona utafiti wanamna hiyo!
Lakini kama hivyo ndivyo haishangazi kutokana na kanuni za ki-ikolojia kama ifuatavyo:
1. Wanyama wenye maumbo madogo hukua na kupevuka kwa haraka, vile vile huishi kwa muda mfupi ukilinganisha na wale wenye maumbo makubwa, with few exceptions - based on r and k strategies.
2. Wanyama wanaokula majani huishi muda mrefu na huwa wengi ukilinganisha na wale wanaokula nyama - based on niche and enegy level concept.
3. Wanyama wanapofugwa hupoteza mbinu na uwezo wao wakuishi porini. Kwa kuwa watu wengi huwa hawapendi kufuga paka zaidi ya mmoja, wanapozaliana hufukuzwa au hulazimika kuondoka kwa kukosa chakula...kwa kuwa hawana uwezo mzuri wa kuweza ku'survive' porini wengi wao hufa na wachacha huweza kuishi na kuwa paka pori.