Ila hili la kula hela ya msiba is too much hata Kama serikali imefilisika. Kuna watu duniani hawana soni Kabisa!
hahaha nashukuru mi sidanganyiki kirahisi kwa kweli kwenye hii nchi tena likija suala la fedha.Bora niende mwenyewe huko kwa wana kagera hata nikawanunulie bati chache kulikon nitoe fedha yangu kwenye mifuko ya ...........
ahhh Ndugu Paskali,wanazibalishia matumizi mara moja.Binadamu ni watu wenye upendo daima, japo ni rahisi kukasirika ila ni wepesi kusamehe na wepesi kusahau ila sio kurudia makosa, hivyo hata maafa mengine yakitokea tena leo, watu bado tutachangia tuu ila this time ni lazima tuelezwe tunaombwa kuchangia nini kama ni wahanga au ni miundombinu.
Hivyo tutalazimisha kuwekwe matangazo ya michango miwili
1.Michango ya kuchangia wahanga wa tetemeko ambalo litaendena na picha za jinsi watu wanavyoteseka.
2. Michango ya kuchangia ukarabati wa miundo mbinu ya umma likiendana na picha za uharibifu wa miundombinu ya umma.
Hivyo kila mchangiaji atakuwa anajua kabla anachangia nini kama ni waathirika au miundombinu sio kuonyeshwa picha za wahanga jinsi watu wanavyoteseka hivyo watu kuhamasika kuchangia, lakini michango ilipopatikana kumbe ulikuwa ni ya kuchangia miundombinu ya umma na sio waathirika.
Paskali