Mliokasirishwa kuhusu Rais Samia kutoa msaada Uturuki hii sio awamu ya Magufuli

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
9,000
17,909
Kuna watu wana makasiriko hadi mambo kama haya!! Sasa kuna ubaya gani kwa nchi kusaidia wahanga wa tetemeko? Hivi tumekuwa wabinafsi kiasi gani? Tunasahau kuwa majanga ya asili hayana mwenyewe na hayazuiliki kirahisi.

Tunasahau kuwa leo kwao kesho kwetu, tusipojitoa kwa kidogo chetu siku yatatukumba ni nani atatukimbilia? Famasiala nini? Usiombe yakukute.

Mtu analeta hoja za kijinga eti tunatoa msaada wakati vitu vimepanda bei, hizo bilioni 2.3 ndo zinawahenyesha na kuwatoa watu mapovu hivi? Bilioni 2.3 zinaweza vipi kupunguza bei ya unga au vitu kupanda kama sio roho mbaya tu?

Tumezoea kupewapewa tu, na sisi siku moja tukijitoa sio mbaya!! Tatizo bongo wengi hawajui diplomasia ya kiuchumi, Samia sio hayati mwendazake yule ambaye hela za tetemeko rambirambi alikula yeye na genge lake bila aibu. Alikuwa rais wa hovyo sana na hakuwa na hata na chembe ya aibu usoni na moyoni mwake.
Tujikumbushe : "Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewaomba wakazi wa Kagera walioathirika na tetemeko kufanya jitihada za kujijengea nyumba zao wenyewe kwani michango iliyochangwa na wadau imeelekezwa kwenye taasisi za serikali. Mkuu wa Mkoa amedai kuwa jumla ya fedha zilizochangwa ni zaidi ya Bilioni 5.4 na kusema kuwa zimeelekezwa katika kukarabati miundombinu ya taasisi za Serikali na kuwataka wananchi wanaosubiri msaada wa serikali kusubiri mchango itakayotolewa na wadau walioahidi kuwasaidia waathirika moja kwa moja."

Uturuki wametusaidia mangapi nchi yetu tokea uhuru? Yaani tatizo ni hiko kibilioni 2.5 ndo tunang'aka kiasi hiki angetoa bilioni 100 jee??

Kuna watu hawafurahii utawala na mageuzi aliyoyafanya Rais Samia hususan maridhiano na kurudisha maridhiano na demokrasia iliyokuwa imeporwa na dikteta katili wa awamu ya tano. Hawa Sukumagang ndio wanaopinga kila kitu. Mimi naona kama wamenunishwa na maridhiano kati ya Chadema na Mama, basi wahame nchi.
 
Hivi kumbe tumetoa msaada ?!!!!

Mbona mimi kama mdau / mmoja wa wachangiaji sijui ?!!

By the way ni yeye ametoa au sisi tumetoa (sababu there is a difference)...

Ila kuweka mambo sawa hivi vitu vingekuwa na pre-amble (for the lack of a better word)..., yaani ikiwa hivi inakuwa vile sababu hatuchelewi nikipata nafasi nikaamua kumchangia Snoop Dog katika maandalizi ya album yake kwa jina la Tanzania......

Anyway kwa yale mambo ya Scratch my Back I will Scratch yours huenda ika-pay off in the future..., sababu tulivyo wazembe majanga kwetu are around the corner and sooner rather than later tutahitaji msaada.... (Ni kama yale ya Harusi unachanga ili uchangiwe; sio kusaidia penye uhitaji, wala roho nzuri)..., That's the current world we live in....

NB: Where's My Snare...., There's no Snare in my Headphone...., Am Just Cleanin Out my Closet....
 
Hata Samia akigawa pesa Kwa wananchi. ..bado atatukanwa Tu na wafuasi wa lile kundi ...

Hata akigawa vipande vya Dhahabu Kwa kila Mtanzania bado lile kundi litamtukana tu
Ni vigumu sana kwa mtu kujitangaza hadharani kwamba ni mdini!

Rais wetu kupeleka msaada ni jambo la maana sana, kwani hakuna baraka kwa apokeaye tu bali amebarikiwa mtu amkunjuliaye masikini mkono wake!

Ila wengi wenu hapa huwa mnasumbuliwa na udini!
 
Bukoba siku ya Tetemeko serikali ilikataa kutoa msaada kwa wahanga I felt the pain, nadhani utu ni muhimu.
Yule shetani alikula hela za rambirambi za wahanga wa tetemeko siwezi msamehe yule shetani.aliwachukia wahaya kwasababu walimzidi sana na wivu kwasababu walimchallenge kwa hoja na usomi wao maana mtaji wa yule kichaa ni watu wasio na elimu

 
Kuna watu wana makasiriko hadi mambo kama haya!! Sasa kuna ubaya gani kwa nchi kusaidia wahanga wa tetemeko? Hivi tumekuwa wabinafsi kiasi gani? Tunasahau kuwa majanga ya asili hayana mwenyewe na hayazuiliki kirahisi.
Watanzani waache roho mbaya huu sio wakati wa mwenda zake Mama ana utu na anaendelea kuimarisha diplomasia na mahusiano
 
Kuna watu wana makasiriko hadi mambo kama haya!! Sasa kuna ubaya gani kwa nchi kusaidia wahanga wa tetemeko? Hivi tumekuwa wabinafsi kiasi gani? Tunasahau kuwa majanga ya asili hayana mwenyewe na hayazuiliki kirahisi.
Pesa ya MKOPO unaweza itoa kama ramborambi kwenye msiba wa Jirani na Benk uliyokopa ikakusamehe riba na MKOPO sababu ya huruma Yako?
 
Hata Samia akigawa pesa Kwa wananchi. ..bado atatukanwa Tu na wafuasi wa lile kundi ...

Hata akigawa vipande vya Dhahabu Kwa kila Mtanzania bado lile kundi litamtukana tu

..mimi sio sukuma gang lakini sikubaliani na kitendo cha Tz kutoa msaada kwa Uturuki, au nchi yoyote iliyoendelea.

..ningeunga mkono kama msaada huo ungekuwa ni kwa nchi ya Afrika haswa majirani zetu.

NB.

..hayo mabilioni tuliyowapa Waturuki yangetosha kujenga vyuo viwili vya Veta, au kuanzisha block farming vijana wetu wakapata ajira.
 
..mimi sio sukuma gang lakini sikubaliani na kitendo cha Tz kutoa msaada kwa Uturuki, au nchi yoyote iliyoendelea.

..ningeunga mkono kama msaada huo ungekuwa ni kwa nchi ya Afrika haswa majirani zetu.

NB.

..hayo mabilioni tuliyowapa Waturuki yangetosha kujenga vyuo viwili vya Veta, au kuanzisha block farming vijana wetu wakapata ajira.
Uturuki wanatusaidia mengi sana kuliko hata hao majirani zako
 
Mleta mada ni mjinga, bila kututajia waliokasirika naongezea tena, mleta uzi ni mpumbavu

Nathibitisha tena kwamba, mleta uzi ni miongoni mwa watanzania wajinga na wenye mwelekeo wa udiniudini tuu!

Kwani hakuna aliyenuna wahanga kupewa msaada! Ila kuna hoja jadidi kuhusu hilo iwapo kweli nasi twaweza kutoa msaada!

Ukimuuliza hata yeye mleta uzi kwamba, Tanzania inaweza bila kuwezeshwa? Bado atakwambia tunahitaji misaada mingi tu bila idadi kwa sababu sisi huwenda ndo tunahitaji msaada kuliko hata wahanga wa tetemeko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom