Swali: Escrow ilikuwa abrakadabra? Zitto na PAC watujibu

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,218
25,633
Pamoja na Ripoti 'nzuri' ya PAC chini ya Zitto Kabwe iliyojadiliwa na kuazimiwa na Bunge, mambo yanakwenda tofauti. Wapo watu waliohusishwa na kashfa hiyo ya Escrow lakini CCM na Serikali yake wanaendelea kuwaamini na kusonga nao mbele.

Waziri Muhongo (Profesa Sospeter Muhongo) alijiuzulu kutokana na kashfa hiyo ya Escrow. Alikuwa Wizara ya Nishati na Madini. Mwaka huu, amerejeshwa tena kwenye Wizara hiyo hiyo kwa cheo kile kile (Waziri).

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ndugu Eliakim Maswi naye aliondolewa kwa kadhia hiyo hiyo. Lakini, ameendelea kuaminiwa na Serikali na ni jana tu ameteuliwa kuwa Kaimu Naibu Kamishna Mkuu wa TRA.

Wapo Wabunge akina Prof. Tibaijuka, Ndugu Andrew Chenge na William Ngeleja ambao wote walihusishwa na kashfa hiyo lakini CCM imeendelea kuwaamini na wameshinda majimboni mwao. Hata viongozi wa kidini na hata wa kimahama waliohusishwa nao wanaendelea kudunda. kimsingi hapa patakuwa na jambo kubwa.

Kama si PAC kuudanganya umma, basi Bunge limepuuzwa vya kutosha. Ndiyo maana najiuliza, sakata la Escrow lilikuwa si kitu halisi yaani abrakadabra?
 
Kwangu mimi report ya Escrow ndiyo ilikua report mbovu kuliko zote kuwahi kutolewa katika nchi hii. Nadhani 'utoto' wa wanakamati nao ulichangia. Ubora wa report ya Dr. Mwakyembe ulichangiwa zaidi na ukweli uliosemwa wazi na hadharani kwamba kuna mambo wameyaondoa/wameyaficha ili 'kulinda heshima' ya serikali.
 
Last edited:
Pamoja na Ripoti 'nzuri' ya PAC chini ya Zitto Kabwe iliyojadiliwa na kuazimiwa na Bunge, mambo yanakwenda tofauti. Wapo watu waliohusishwa na kashfa hiyo ya Escrow lakini CCM na Serikali yake wanaendelea kuwaamini na kusonga nao mbele.

Waziri Muhongo (Profesa Sospeter Muhongo) alijiuzulu kutokana na kashfa hiyo ya Escrow. Alikuwa Wizara ya Nishati na Madini. Mwaka huu, amerejeshwa tena kwenye Wizara hiyo hiyo kwa cheo kile kile (Waziri).

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ndugu Eliakim Maswi naye aliondolewa kwa kadhia hiyo hiyo. Lakini, ameendelea kuaminiwa na Serikali na ni jana tu ameteuliwa kuwa Kaimu Naibu Kamishna Mkuu wa TRA.

Wapo Wabunge akina Prof. Tibaijuka, Ndugu Andrew Chenge na William Ngeleja ambao wote walihusishwa na kashfa hiyo lakini CCM imeendelea kuwaamini na wameshinda majimboni mwao. Hata viongozi wa kidini na hata wa kimahama waliohusishwa nao wanaendelea kudunda. kimsingi hapa patakuwa na jambo kubwa.

Kama si PAC kuudanganya umma, basi Bunge limepuuzwa vya kutosha. Ndiyo maana najiuliza, sakata la Escrow lilikuwa si kitu halisi yaani abrakadabra?

Umeuliza maswali ya msingi sana lakini naamini maazimio ya bunge kuhusu escrow yatatekelezwa kikamilifu chini ya rais JPM. Kwa hiyo usihusishe CCM na serikali hii. pale penye jinai hakuna atakayesalimika CCM or anyone else. Wewe subiri majipu hayo yatafikiwa maadam sasa safu za watendaji zimekamilika. We want a new Tanzania isiyovumilia uchafu wa aina yoyote.
 
Mkuu Escrow hata kama ingekua ni uzushi mtupu
mradi ilisomwa bungeni na ikapita na kutoka na maazimio
Zitto hawezi kulaumiwa
kama kunakosa itakuwa bunge lote now....

Bunge lilikuwa na nafasi ya kujiridhisha na kila kitu
 
Mkuu Escrow hata kama ingekua ni uzushi mtupu
mradi ilisomwa bungeni na ikapita na kutoka na maazimio
Zitto hawezi kulaumiwa
kama kunakosa itakuwa bunge lote now....

Bunge lilikuwa na nafasi ya kujiridhisha na kila kitu

Nakupata Mkuu. Nauliza maswali haya kwakuwa siamini kinachotokea. Kuna vita dhidi ya ufisadi kweli hapa nchini?
 
Tumuulize huyu Mbadala wa Mrema wa TLP yeye na kamati yake PAC alikuwa na lengo gani?
Pia walikuwa name report mbili kama ilivyokuwa Richmond?
 
Tatizo la Magufuli anawaamini sana TISS..
kwa hiyo TISS wakikupenda hata uwe mwizi kwa Magufuli utapeta
cc @Pasco ....huyo Maswi ni 'mwanakitengo'
mkuu magufuli amekuepo ndan ya bunge lililopta, pengine labda kuna mengi anayajua kuhusu undani wa ESCROW zaid ya sisi wananchi wa kawaida 2navyoifaham ESCROW, haraf pia 2kimnnkuu huyu ztto mwenyewe 'usiamini maneno ya mwanasiasa yeyote hata mm (mwenyewe zitto)' haraf pia mkuu THE BOSS unaposema kwamba maguful anawaamin xana TISS, hv nkuulize labda unafikiri mh. rais amwamini nani mwingine ikiwa hata wanasiasa wenyewe hawaaminiki? mm kwa haya anayoyafanya maguful iman yangu kwa wabunge inazd kufifia naona kama huwa wako pale kufitiniana2, yaan ilianza RICHMOND nafkir mmeona CDM walicho2fanyia kwa lowaxa, imekuja ESCROW nafkir 2meona alicho2fanyia maguful na CCM yake kwa kuwarudsha MUHONGO na MASWI. hawa wanasiasa hawaaminiki kabxa
 
Last edited:
mkuu magufuli amekuepo ndan ya bunge lililopta, pengine labda kuna mengi anayajua kuhusu undani wa ESCROW zaid ya sisi wananchi wa kawaida 2navyoifaham ESCROW, haraf pia 2kimnnkuu huyu ztto mwenyewe namnukuu 'usiamini maneno ya mwanasiasa yeyote hata mm (mwenyewe zitto)' haraf pia mkuu THE BOSS unaposema kwamba maguful anawaamin xana TISS, hv nkuulize labda unafikiri mh. rais amwamini nani mwingine ikiwa hata wanasiasa wenyewe hawaaminiki? mm kwa haya anayoyafanya maguful iman yangu kwa wabunge inazd kufifia naona kama huwa wako pale kufitiniana2, yaan ilianza RICHMOND nafkir mmeona CDM walicho2fanyia kwa lowaxa, imekuja ESCROW nafkir 2meona alicho2fanyia maguful na CCM yake kwa kuwarudsha MUHONGO na MASWI. waha wanasiasa hawaaminiki kabxa
kama anawaamini tiss 100 %
na hao TISS sio waadilifu basi kazi anayo
 
Escrow ilikua nifitina za matajiri kuzibiti wazalendo.
Nashukuru Mheshimiwa rais kaliona hilo.
Magufuli go! go!go!
 
Tumuulize huyu Mbadala wa Mrema wa TLP yeye na kamati yake PAC alikuwa na lengo gani?
Pia walikuwa name report mbili kama ilivyokuwa Richmond?
Maazimio ya PAC ndio yaliyopitishwa?.

Umesahau kama yalikataliwa,ikabidi iundwe kamati ndogo ya mashauliano ambayo na Mbowe,Zitto,Lukuvi na Wasira walikuwa ndani?.

Wakaja na maazimio ya bunge na sio tena ya PAC?.

Chuki na mihemko huondoa maalifa,kama unamchukia Zitto ni wewe.

Badala yakulaumu bunge zima we unaleta chuki zako kwa Zitto.

Weka mihemko pembeni tujenge nchi.
 
Pamoja na Ripoti 'nzuri' ya PAC chini ya Zitto Kabwe iliyojadiliwa na kuazimiwa na Bunge, mambo yanakwenda tofauti. Wapo watu waliohusishwa na kashfa hiyo ya Escrow lakini CCM na Serikali yake wanaendelea kuwaamini na kusonga nao mbele.

Waziri Muhongo (Profesa Sospeter Muhongo) alijiuzulu kutokana na kashfa hiyo ya Escrow. Alikuwa Wizara ya Nishati na Madini. Mwaka huu, amerejeshwa tena kwenye Wizara hiyo hiyo kwa cheo kile kile (Waziri).
Prof. Sospeter Muhongo alikuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati wa sakata la TegetaEscrow Kamati ya Bunge ilipendekeza na Bunge kuazimia kuwa Muhongo avuliwe madaraka yake ya Uwaziri. Prof. Muhongo alijiuzulu. Akafanyiwa uchunguzi na Kamishna wa Maadili kutamka kuwa hakukutwa na kosa la kimaadili. Unajengaje hoja kuwa hana haki ya kuteuliwa kuwa Waziri? Keshaadhibiwa kwa kosa la awali, kwa kujiuzulu. Sheria ipi inasema hana haki ya kuteuliwa tena?

Niliongoza Kamati ya PAC. Nina uhakika Waziri muhongo kwenye sakata lile alishauriwa vibaya na kujikuta anatetea ubadhirifu. Lile ni funzo kubwa kwake na ninavyomuona sasa hatarudia tena makosa yale.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ndugu Eliakim Maswi naye aliondolewa kwa kadhia hiyo hiyo. Lakini, ameendelea kuaminiwa na Serikali na ni jana tu ameteuliwa kuwa Kaimu Naibu Kamishna Mkuu wa TRA.
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telegrams : "CABINET"

DAR ES SALAAM

Telephone : 2116898, 2116900/6

E-mail : chief@ikulu.go.tz

E-mail : ikulu@ikulu.go.tz

Fax : 2113425/2116914/2117272

ngao.png

PRESIDENT’S OFFICE,

THE STATE HOUSE,

1 BARACK OBAMA ROAD

11400 DAR ES SALAAM.

MATOKEO YA UCHUNGUZI WA AWALI KUMHUSU NDUGU ELIAKIM

C. MASWI, KATIBU MKUU, WIZARA YA NISHATI NA MADINI

_________________________________________________


1.0 Utangulizi



1.1 Katika mkutano wake wa 16 na 17, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na mambo mengine, lilijadili Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali iliyotokana na Taarifa ya Ukaguzi wa Akaunti ya Tegeta Escrow uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.



1.2 Baada ya majadiliano, Bunge lilipitisha maazimio kadhaa yaliyoelekezwa kwa Serikali kwa ushauri na utekelezaji. Mojawapo ya maazimio hayo yalimtaja Ndugu Eliakim C. Maswi, ambaye ndiye Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kuwa amehusika kijinai au kimaadili katika miamala iliyotokea katika akaunti ya Tegeta Escrow.



1.3 Wakati anahutubia Taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam tarehe 22 Desemba, 2014, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema ifuatavyo:-



“Kuhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kwa vile ni Mtumishi wa Umma, anatawaliwa na Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma. Hivyo, nimeshaelekeza Mamlaka kuchunguza tuhuma zake na hatimaye ikibainika ana makosa hatua za kinidhamu zitachukuliwa.”



1.4 Tuhuma dhidi ya Ndugu Eliakim C. Maswi zimeshughulikiwa katika ngazi mbili tofauti. Amechunguzwa na Sekretarieti ya Maadili ya Umma, kisha baada ya hapo alichunguzwa pia na Kamati ya Uchunguzi wa Awali iliyoundwa na mamlaka yake ya nidhamu.



2.0 Sekretarieti ya Tume ya Maadili


2.1 Kifungu 18 (2) (c) na (3) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kinaipa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma mamlaka na uwezo wa kuchunguza tuhuma yoyote ya kuvunjwa kwa maadili ya uongozi wa umma yanayotawaliwa na Sheria hiyo. Tuhuma dhidi ya Ndugu Eliakim C. Maswi zilizomo kwenye maazimio ya Bunge zinatawaliwa na Sheria hiyo.



2.2 Katika kutekeleza majukumu yake, Sekretarieti ya Maadili ya Umma ilifanya uchunguzi wa awali na kisha kumhoji Ndugu Eliakim C. Maswi tarehe 19 Desemba, 2014.



2.3 Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma haijabaini kuwepo kwa maslahi binafsi katika uamuzi uliofanywa na Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini wa kuruhusu fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow kutolewa. Aidha, hawakubaini ukiukwaji wowote wa maadili ya viongozi wa umma uliofanywa na Ndugu Eliakim C. Maswi. Waliona kuwa yote aliyoyafanya yalizingatia matakwa ya Sheria, ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na ridhaa ya TANESCO. Hivyo, Sekretarieti ya Maadili haikuona msingi wowote wa kuendelea na shauri la Ndugu Eliakim C. Maswi, na wamelihitimisha.



3.0 Kamati ya Uchunguzi wa Awali ya Mamlaka ya Nidhamu


3.1 Kwa mujibu wa Kifungu 4(3) (d) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 (kama ilivyorekebishwa) Katibu Mkuu Kiongozi ndiye Mamlaka ya Nidhamu ya Makatibu Wakuu.



3.2 Kwa kuzingatia Azimio husika la Bunge, na kwa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katibu Mkuu Kiongozi aliunda Kamati ya Uchunguzi wa Awali dhidi ya Ndugu Eliakim C. Maswi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, chini ya Kifungu cha 36 cha Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003 kinachotamka ifuatavyo:-

“Where it is necessary to institute disciplinary proceedings against a public servant, the disciplinary authority shall make preliminary investigations before instituting disciplinary proceedings.”


3.3 Kwa mamlaka aliyonayo chini ya Kanuni 35(2)(b) na Kanuni 37 ya Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, Katibu Mkuu Kiongozi alimpumzisha Bwana Eliakim C. MASWI kutekeleza majukumu yake ya kazi ya Katibu Mkuu ili kupisha uchunguzi wa awali. Uchunguzi wa awali ulifanyika chini ya Kanuni ya 36 ya Kanuni za Utumishi wa Umma zilizotajwa, pamoja na Kifungu 4(3) (d) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002, kama ilivyorekebishwa.



3.4 Kwa mamlaka aliyonayo chini ya Kanuni zilizotajwa kwenye ibara 3.3 hapo juu, Katibu Mkuu Kiongozi aliteua Kamati ya Uchunguzi wa Awali na kuipa Hadidu za Rejea zifuatazo:



3.4.1 Kubainisha wajibu na madaraka halisi ya Katibu Mkuu, Wizaraya Nishati na Madini, kwenye uendeshaji wa TANESCO kwa ujumla, na hususan kwenye kufungua, kuendesha na hatimaye kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow.



3.4.2 Kubainisha na kupata maelezo ya kina juu ya kuhusika kwa Bwana Eliakim C. Maswi katika mchakato na mtiririko mzima wa akaunti ya Tegeta Escrow, tangu kufunguliwa hadi kufungwa.



3.4.3 Kubainisha na kupata maelezo ya kina iwapo kuna jambo lolote ambalo Bwana Eliakim C. Maswi alilifanya au ambalo alipaswa kulifanya lakini hakulifanya, linalomstahilisha achukuliwe hatua za nidhamu.



3.4.4 Kubainisha na kupata maelezo ya kina iwapo katika hatua yoyote ya mchakato na mtiririko wa tangu kufunguliwa hadi kufungwa kwa akaunti ya Tegeta Escrow, Bwana Eliakim C. Maswi alifanya jambo lolote linalodhihirisha matumizi mabaya ya mamlaka yake kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kwa namna iliyosababisha hasara ya aina yoyote ile kwa Taifa la Tanzania.



3.4.5 Kubainisha na kupata maelezo ya kina iwapo katika hatua yoyote tangu akaunti ya Tegeta Escrow ilipofunguliwa hadi ilipofungwa, Bwana Eliakim C. Maswi hakuchukua tahadhari ya kutosha kulinda maslahi ya umma na kusababisha kupotea kwa fedha za umma kwa uzembe au matumizi mabaya ya madaraka.



3.4.6 Kubainisha iwapo kuna mahali popote katika mchakato wa akaunti ya Tegeta Escrow ambapo Bwana Eliakim Chacha Maswi alifanya jambo lolote linaloashiria kitendo cha kijinai, au kukiuka maadili ya viongozi wa umma.



3.4.7 Kuandaa taarifa ya uchunguzi wa awali kwa msingi wa Hadidu za Rejea zilizomo humu na kuiwasilisha kwa Katibu Mkuu Kiongozi. Taarifa hiyo, pamoja na mambo mengine, ipendekeze hatua za kuchukuliwa kwa kila eneo ambalo Kamati itabaini umuhimu wa hatua kuchukuliwa.



3.5 Mapendekezo ya Kamati ya Uchunguzi wa Awali



3.5.5 Kamati haijabaini kosa lolote ambalo linaweza kusababisha Ndugu Eliakim Chacha Maswi, Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, kufunguliwa mashtaka ya kinidhamu kwa kukiuka Sheria ya Utumishi wa Umma Sura 298 ikisomwa pamoja na Kanuni zake za mwaka 2003 kwa kuruhusu Benki Kuu ya Tanzania kutoa fedha zilizokuwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow.



4 Hitimisho la Uchunguzi wa Awali


4.4 Uchunguzi wa Awali uliofanywa na Sekretarieti ya Maadili umebaini kuwa Ndugu Eliakim C. Maswi hana makosa yoyote ya kimaadili katika mchakato wa fedha za akaunti ya Tegeta Escrow.



4.5 Hali Kadhalika Uchunguzi wa Awali uliofanywa na Kamati ya Uchunguzi wa Awali iliyoundwa na Katibu Mkuu Kiongozi umebaini kuwa Ndugu Eliakim C. Maswi, “hakutenda au kuhusika na jambo lolote linaloashiria vitendo vya jinai au kukiuka Maadili ya Viongozi wa Umma”.



4.6 Ushahidi wa vielelezo uliotolewa kwenye Sekretarieti ya Maadili na kwenye Kamati ya Uchunguzi wa Awali umejitosheleza kuthibitisha kwamba Ndugu Eliakim C. Maswi alitenda kazi yake kwa kiwango kinachoridhisha kwa kufanya mawasiliano na mamlaka mbalimbali na kwa nyakati tofauti kwa lengo la kuhakikisha na kujiridhisha kwamba kufungwa kwa Akaunti ya Tegeta Escrow kunafanyika kwa usahihi.



4.7 Hakuna ushahidi wowote kuwa Ndugu Eliakim C. Maswi alikuwa miongoni mwa waliopata mgao wa fedha au fadhila yoyote kutokana na kufungwa Akaunti ya Tegeta Escrow.



4.8 Kwa nafasi yake ya mamlaka ya nidhamu Katibu Mkuu Kiongozi, ameridhika kuwa Ndugu Eliakim C. Maswi hana makosa yoyote aliyoyafanya katika mchakato wa akaunti ya Tegeta Escrow yanayostahili adhabu. Hivyo, mchakato wa kinidhamu, kimaadili na kijinai dhidi yake umefikia mwisho wake. Mwenye mamlaka ya uteuzi atatafakari taarifa hizi na kuamua cha kufanya kuhusu ajira yake baadaye.

Imetolewa na;

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu – Dar es Salaam.

8 Mei, 2015

Wapo Wabunge akina Prof. Tibaijuka, Ndugu Andrew Chenge na William Ngeleja ambao wote walihusishwa na kashfa hiyo lakini CCM imeendelea kuwaamini na wameshinda majimboni mwao. Hata viongozi wa kidini na hata wa kimahama waliohusishwa nao wanaendelea kudunda. kimsingi hapa patakuwa na jambo kubwa.
HAO MUULIZE MWENYEKITI WA CCM NA WANANCHI WALIOWACHAGUA KWA KURA NYINGI KUWA WAWAKILISHIwao.Hawako na wala si SEHEMU YA serikali

Kama si PAC kuudanganya umma, basi Bunge limepuuzwa vya kutosha. Ndiyo maana najiuliza, sakata la Escrow lilikuwa si kitu halisi yaani abrakadabra?
PAC ILITUMIA REPORT YA CAG,PAC HAIFANYI UCHUNGUZI WOWOTE.
N.B.ACHENI UNAFIKI na Mwogopeni Mungu Japo Kidogo................
======================================
================================
580332_497379423765479_8145705626867977364_n.jpg

MR RUGEMALIRA WA ESCROW Akiwa amealikwa na Wilfred Lwakatale kama mdau wa Maendeleo.
 
Deo Fulikunjombe upumzike kwa amani najaribu kuunganisha dots sipati majibu ila kuna siku ukweli utajulikana
Na Ndio maana Kafulila kafanyiwa ubabe tu asishinde ubunge
 
Last edited:
kama anawaamini tiss 100 %
na hao TISS sio waadilifu basi kazi anayo
cha msingi na cha muhimu kwa mh. rais ni kwamba awe 'anachukua za TISS anachanganya na ZAKE' yy anauzoefu na serikal karibia zote zilizopta akiwa wazir kamili na pia kama naib waziri, kwa hyo anajua wapi pa bovu na wapi pazma, au wapi panahtaj kufanyiwa marekebsho, lakini kama mheshmiwa rais akijiloga na kufanya kazi 'kisiasa' kama wanavyodai kina ZITTO and company. nakuhakikishia mkuu maguful hatafka ppte,
 
cha msingi na cha muhimu kwa mh. rais ni kwamba awe 'anachukua za TISS anachanganya na ZAKE' yy anauzoefu na serikal karibia zote zilizopta akiwa wazir kamili na pia kama naib waziri, kwa hyo anajua wapi pa bovu na wapi pazma, au wapi panahtaj kufanyiwa marekebsho, lakini kama mheshmiwa rais akijiloga na kufanya kazi 'kisiasa' kama wanavyodai kina ZITTO and company. nakuhakikishia mkuu maguful hatafka ppte,

labda mahitaji ya hii kazi ni makubwa kuliko uwezo wa TISS na washauri wake
 
Mkuu nimependa hiyo pamoja na ripoti 'nzuri'. Hata hivyo, sikumbuki kama watanzania kuna siku tulikuwa la ripoti 'mbaya'.

Kujua kama Escrow ni kitu halisi au la, tunatumia bunge kupitia kwa ripoti ya ile kamati kutafuta majibu. Lakini kwa kuwa Mwenyekiti wa ile kamati kwa maana hiyo bunge kukubali maelezo ya tume ya maadili kwamba mmoja wa wale watuhumiwa ni msafi, hiyo inafuta uhalisia wa kazi ya ile kamati lakini haufuti ukweli kwamba Escrow scandal is real.

Nilitegemea na niliamini kuwa kamati ilifanya kazi nzuri, ikiwa ni pamoja na kuilinda ile ripoti usiku na mchana. Nakumbuka hata wapishi ilibidi watoke majumbani kwao. Kwa kuwa wao kwa maoni yangu kirahisi sana wamenyosha mikono, wananchi tumekwama.

Hivyo basi, matokeo ya ile kamati ilikuwa siasa zaidi. Swali lingine linaingia hapa, je, tunaweza kuamini bila shaka yoyote matokeo ya ripoti za kamati za bunge? Zina tija au nazo ni majipu?

Mwaka 2015 ulikuwa mzuri kwa wale walio amua kujifunza kitu kuhusu siasa za nchi yetu.
 
Back
Top Bottom