Swali Chokonozi: Mwaka huu Waislamu hawasusii Sensa kama mwaka 2012? Madai yao ya mwaka 2012, mwaka huu yametatuliwa?

Dx and Rx

JF-Expert Member
Jul 16, 2017
1,303
3,085
Salamu wakuu, naomba kuuliza swali kama linavyojieleza hapo juu. Sio kwa nia mbaya(naomba nieleweke hivi), bali napenda kujua.

Mwaka 2012, Waislamu walifikia hatua ya kususia sensa kwa madai kuwa kwenye dodoso la sensa kulikuwa na kipengele cha nyumba za Ibada(Msikiti, Kanisa) bila kuwepo kipengele cha Dini, jambo ambalo lilitafsirika kuwa kulikuwa na nia ya kupata takwimu za nyumba za Ibada bila kupata takwimu za watumiaji(waumini) wa hizo nyumba za ibada.

Waislamu walileta hoja yao ya kutaka pawepo na kipengele cha dini kwenye dodoso baada ya kuhisi kuwa kuna upotoshaji wa takwimu za idadi ya Waislamu na Wakristo Nchini, sasa kukata huo mzizi wa fitina walishauri kwenye dodoso pawekwe kipengele cha dini ili takwimu sahihi zijulikane ila mamlaka(Serikali) ilikataa kusikiliza hoja yao.

Baada ya hapo Waislamu nchi nzima walianza kuhamasishana kususia Sensa ingawa kuna wapo waliweza kuhesabiwa na wengine hawakuhesabiwa.

Je mwaka huu hii agenda haipo? Takwimu sahihi walizokuwa wanadai kupotoshwa walishapata usahihi wa hizo takwimu?

Nimeamua kuuliza baada ya kuona Shule moja ya Kiislamu inahamasisha Sensa ya Mwaka huu kupitia tangazo lao la kutangaza nafasi za masomo.
 
Duuh nchi ngumu hii yaani swala dogo tu la kuhesabiana linakuwa na complications namna hii??
 
Wewe Muongo Unafikiri 2012 Hatukuwepo?? Hawakuwa na hoja hiyo,Kasome vizuri Ndio Ulete Uzi hapa Unakurukupuka tuu...
 
Wewe Muongo Unafikiri 2012 Hatukuwepo?? Hawakuwa na hoja hiyo,Kasome vizuri Ndio Ulete Uzi hapa Unakurukupuka tuu...
Walikuwa na hoja gani mkuu.

Ebu ieleze hapa ili tuweze kusahihisha uzi
 
Sawa mkuu, ikiwa hivyo basi haina mkanganyiko kama ilivyokuwa kipindi kilichopita jambo ambalo liliibua hoja ya kwanini Nyumba za Ibada zihesabiwe na wala si Waumini/watumiaji wa hizo nyumba na walichomekea hoja ya kupata takwimu sahihi ya Waislamu na Wakristo
 
Ila hawa jamaa yani vitu vidogo ambavyo huwezi kuwadhania lakini wanaviwekea bunge
 
Salamu wakuu, naomba kuuliza swali kama linavyojieleza hapo juu. Sio kwa nia mbaya(naomba nieleweke hivi), bali napenda kujua...
Data za CIA za miaka ya 2000 za kusema kwamba Dini ya uislamu inawaumini 63% ndi yenye majorityTz, zilileta ukakasi kwa viongozi kuamini kwa hiyo hawata kuja ku-reprove kwenye sensa yoyote kwasabb linaumiza nyoyo zao.
 
Back
Top Bottom