Mroojr
Member
- Nov 15, 2010
- 65
- 8
Jamani kwa wale mnaoijua sheria vizuri swala la kufumania ama kufumaniwa likoje kisheria?Nimeuliza hivyo makusudi kwa sababu mara nyingi sana wafumaniaje huwa wanavifungu vya sheria wao wenyewe vichwani mwao.Mwingine atamuacha mke au mume,mwingine anaweza kutoa kipigo kikali kwa mke au wote kwa pamoja na mwingine anaweza hata kuua kabisa.Sasa kwakuwa haya wanayoyaamua wafumaniaji hayapo kisheria je kwa nyinyi mnaozijua sheria vizuri kesi hizi za fumanizi zinafunguliwa polisi au mahakamani moja kwa moja?