theriogenology
JF-Expert Member
- Oct 7, 2016
- 8,750
- 15,642
SUMU NA HUDUMA YA KWANZA KWA MBWA ALIEPEWA SUMU
★ UTANGULIZI
Sumu ni kitu chochote hatarishi katika mwili wa mnyama na binadamu vilevile.
Kwa kawaida mbwa huwa wanatabia ya udadisi na udadisi wao huo huwafanya kukutana na mazingira tofoutitofouti ambapo pia yanaweza kuwa hatarishi kwa maisha yao mfano wa mazingira hayo ni kama vile vichakaa au katika stoo za kuhifadhia malighafi mbalimbali.
Udadisi huo huwafanya kukutana na wadudu na wanyama hatari wenye sumu kama vile nyoka na tandu na pia katika udadisi wao huo wanaweza kukutana na chambo (mtego wa sumu).
★ Vitu vya kuzingatia katika kutoa huduma ya kwanza kwa mbwa aliekula au kulishwa sumu
✓ Kama mbwa wako amekula kitu ambacho kitakutatiza kama ni sumu ama sio sumu ni vyema ukachukua container husika uende sehemu ambayo imeandikwa ingridient ainisha kitu kimoja baada ya kingine na iwapo umeshindwa kuelewa kitu mmoja wapo ni vyema ukampigia simu Veterinary Doctor kwa msaada zaidi ili akueleze ni namna gani ya kuondoa sumu hiyo.
✓ Kama dalili za sumu zinazidi kuonekana ni vyema ukamuwaisha mbwa kwa Veterinary clinic yoyote iliyokaribu na wewe kwa msaada zaidi na ni vyema ukabeba container husika la sumu hii mara nyingi hurahisisha kazi na hupelekea mbwa wako kupewa huduma mapema zaidi.
✓ Huwa inashauriwa kumfanya mbwa atapike ili kupunguza kiwango cha sumu ndani ya tumbo lake kabla ya kumpeleka kwa daktari na mara nyingi daktari hutoa ushauri huo
✓ Kwa mfano mbwa kala sumu masaa mawili yaliyopita na itakuchukua wewe muda wa kama nusu saa kumfikia daktari kwa msaada zaidi ni vyema ukamlazimisha mbwa kutapika (First aid) ili kupunguza kiwango cha sumu ndani ya tumbo lake
★ Usimlazimishe mbwa kutapika iwapo;
✓ Kama mbwa alikwishatapika hapo mwanzo
✓ Anapumua kwa shida, anaonesha dalilli za kuishiwa fahamu na pia kutokuwa na hisia za aina yoyote
✓ Kama mbwa anaonesha dalili zozote za msukosuko na pia kama anataka kuzirai
✓ Kama mbwa kala sumu aina ya acid, alkali, mafuta ya taa au petroli na pia dawa za kufanyia usafi ndani ya nyumba
✓ Kama mbwa kala kitu cha ncha kali ambacho kimekwama kwenye mfumo wa chakula ambapo chaweza leta madhara katika kuta zake
✓ Kama container iliyobeba sumu imeandikwa " Do not induce vomiting "
★ Namna ya kumfanya mbwa wako kutapika kama njia ya huduma ya kwanza
✓ Mpe mbwa wako 3% Hydrogen peroxide katika dose ya 5ml ( kijiko kimoja cha chai ) kwa mbwa mwenye uzito wa 4.5-5kg rudia kila baada ya dakika 15- 20 mara tatu mpaka pale mbwa atakapoanza kutapika.
✓ Unaweza mpa chumvi vijiko vya chai vitatu kupitia mdomo wake pia yaweza kumfanya mbwa kutapika
✓ Unaweza mpa mbwa wako pia syrup ya ipeac ambapo ilikuwa inatumika hapo mwanzo kbla hydrogen peroxide haijaja na ufanyaji kazi wake ni 50% lakni pia yweza kuwa hatari kwa mbwa wako usiitumie kabla hujaruhusiwa na daktari na dose yake ni 0.5-1ml kwa mbwa wa uzito wa 4.5-5kg rudia mara moja tu baada ya dakika 20
✓ Baada ya sumu kuondolewa tumboni mpe activated charcoal ili kukamata kiwango cha sumu kilichobakia tumboni na pia kuzuia unyonyaji zaidi wa sumu katika mfumo wa chakula.
-- Mara nyingi huja kwa mfumo wa kidonge cha 5 grams na dose inayohitajika ni kidonge kimoja kwa mbwa wa 4.5 - 5kg
-- Na pia yaweza kuja kwa mfumo wa powder au maji ambapo husumbua sana kumnyweesha mbwa incase umekosa vitu kama sindano au chupa maalamu ya kumyweeshea mbwa
✓ Kama umekosa activated charcoal ni vyema ukampa mbwa mchanganyo wa maziwa ( 60ml) na ute wa yai ule mweupe ( 60ml) kwa mbwa wa uzito 4.5 -5kg kwa kutumia syringe maalamu yenye gauge kubwa
✓ Then baada ya hapo mpeleke mbwa wako kwa Veterinary Docror kwa msaada na matibabu zaidi maana kuna vitu mbwa wako itabidi apewe ili kuweza kurudia katika hali yake ya kawaida
★ Baadhi ya sumu hatari kwa mbwa wako
✓ Drug poisoning mara nyingi wamiliki wa mbwa huwapa mbwa wao dawa zinazotumiwa na binadamu mbwa wao hii kisheria hairuhusiwi na mara nyingi yaweza kuleta madhara kwa mbwa mfano wa dawa za kupunguza maumivu kama vile Ibuprofen ( advil) na pia acetominophen yaweza kuwa sumu kwa mbwa wako pia dawa kama vitamin, sleeping pills na heart pills
✓ Antifreeze agent kama vile ethylene glycol huwa ni tamu na huwavutia sana mbwa
✓ Dawa za kutegea wanyama waharibifu kama vile strychnine, sodium fluorate, phosphorus, zinc phosphide na metaldehyde hutumika kuua na kuzuia wanyama pori huko vijijini
✓ Dawa za kuzuia wadudu (insecticides) kama vile organophosphate, organochlorde, pyrethrin, pyrethroids na carbamate
✓ Sumu za chakula ( food poisoning) kama vile chocolates, vitunguu, tangawizi, zabibu, macadania nuts na pia xylitol hii hutumiwa sana na watu wenye kisukari
✓ Mimea ya sumu pamoja na bidhaa za mafuta kama vile mafuta ya taa, petrol na tuperntine
✓ Sumu za panya na Contact poisoning
Imeandaliwa na C.E.O
JM Veterinary Centre ( JMVC)
Phone: +255712784472
Motto: We save You and your animal as family
Karibu tukuhudumie
★ UTANGULIZI
Sumu ni kitu chochote hatarishi katika mwili wa mnyama na binadamu vilevile.
Kwa kawaida mbwa huwa wanatabia ya udadisi na udadisi wao huo huwafanya kukutana na mazingira tofoutitofouti ambapo pia yanaweza kuwa hatarishi kwa maisha yao mfano wa mazingira hayo ni kama vile vichakaa au katika stoo za kuhifadhia malighafi mbalimbali.
Udadisi huo huwafanya kukutana na wadudu na wanyama hatari wenye sumu kama vile nyoka na tandu na pia katika udadisi wao huo wanaweza kukutana na chambo (mtego wa sumu).
★ Vitu vya kuzingatia katika kutoa huduma ya kwanza kwa mbwa aliekula au kulishwa sumu
✓ Kama mbwa wako amekula kitu ambacho kitakutatiza kama ni sumu ama sio sumu ni vyema ukachukua container husika uende sehemu ambayo imeandikwa ingridient ainisha kitu kimoja baada ya kingine na iwapo umeshindwa kuelewa kitu mmoja wapo ni vyema ukampigia simu Veterinary Doctor kwa msaada zaidi ili akueleze ni namna gani ya kuondoa sumu hiyo.
✓ Kama dalili za sumu zinazidi kuonekana ni vyema ukamuwaisha mbwa kwa Veterinary clinic yoyote iliyokaribu na wewe kwa msaada zaidi na ni vyema ukabeba container husika la sumu hii mara nyingi hurahisisha kazi na hupelekea mbwa wako kupewa huduma mapema zaidi.
✓ Huwa inashauriwa kumfanya mbwa atapike ili kupunguza kiwango cha sumu ndani ya tumbo lake kabla ya kumpeleka kwa daktari na mara nyingi daktari hutoa ushauri huo
✓ Kwa mfano mbwa kala sumu masaa mawili yaliyopita na itakuchukua wewe muda wa kama nusu saa kumfikia daktari kwa msaada zaidi ni vyema ukamlazimisha mbwa kutapika (First aid) ili kupunguza kiwango cha sumu ndani ya tumbo lake
★ Usimlazimishe mbwa kutapika iwapo;
✓ Kama mbwa alikwishatapika hapo mwanzo
✓ Anapumua kwa shida, anaonesha dalilli za kuishiwa fahamu na pia kutokuwa na hisia za aina yoyote
✓ Kama mbwa anaonesha dalili zozote za msukosuko na pia kama anataka kuzirai
✓ Kama mbwa kala sumu aina ya acid, alkali, mafuta ya taa au petroli na pia dawa za kufanyia usafi ndani ya nyumba
✓ Kama mbwa kala kitu cha ncha kali ambacho kimekwama kwenye mfumo wa chakula ambapo chaweza leta madhara katika kuta zake
✓ Kama container iliyobeba sumu imeandikwa " Do not induce vomiting "
★ Namna ya kumfanya mbwa wako kutapika kama njia ya huduma ya kwanza
✓ Mpe mbwa wako 3% Hydrogen peroxide katika dose ya 5ml ( kijiko kimoja cha chai ) kwa mbwa mwenye uzito wa 4.5-5kg rudia kila baada ya dakika 15- 20 mara tatu mpaka pale mbwa atakapoanza kutapika.
✓ Unaweza mpa chumvi vijiko vya chai vitatu kupitia mdomo wake pia yaweza kumfanya mbwa kutapika
✓ Unaweza mpa mbwa wako pia syrup ya ipeac ambapo ilikuwa inatumika hapo mwanzo kbla hydrogen peroxide haijaja na ufanyaji kazi wake ni 50% lakni pia yweza kuwa hatari kwa mbwa wako usiitumie kabla hujaruhusiwa na daktari na dose yake ni 0.5-1ml kwa mbwa wa uzito wa 4.5-5kg rudia mara moja tu baada ya dakika 20
✓ Baada ya sumu kuondolewa tumboni mpe activated charcoal ili kukamata kiwango cha sumu kilichobakia tumboni na pia kuzuia unyonyaji zaidi wa sumu katika mfumo wa chakula.
-- Mara nyingi huja kwa mfumo wa kidonge cha 5 grams na dose inayohitajika ni kidonge kimoja kwa mbwa wa 4.5 - 5kg
-- Na pia yaweza kuja kwa mfumo wa powder au maji ambapo husumbua sana kumnyweesha mbwa incase umekosa vitu kama sindano au chupa maalamu ya kumyweeshea mbwa
✓ Kama umekosa activated charcoal ni vyema ukampa mbwa mchanganyo wa maziwa ( 60ml) na ute wa yai ule mweupe ( 60ml) kwa mbwa wa uzito 4.5 -5kg kwa kutumia syringe maalamu yenye gauge kubwa
✓ Then baada ya hapo mpeleke mbwa wako kwa Veterinary Docror kwa msaada na matibabu zaidi maana kuna vitu mbwa wako itabidi apewe ili kuweza kurudia katika hali yake ya kawaida
★ Baadhi ya sumu hatari kwa mbwa wako
✓ Drug poisoning mara nyingi wamiliki wa mbwa huwapa mbwa wao dawa zinazotumiwa na binadamu mbwa wao hii kisheria hairuhusiwi na mara nyingi yaweza kuleta madhara kwa mbwa mfano wa dawa za kupunguza maumivu kama vile Ibuprofen ( advil) na pia acetominophen yaweza kuwa sumu kwa mbwa wako pia dawa kama vitamin, sleeping pills na heart pills
✓ Antifreeze agent kama vile ethylene glycol huwa ni tamu na huwavutia sana mbwa
✓ Dawa za kutegea wanyama waharibifu kama vile strychnine, sodium fluorate, phosphorus, zinc phosphide na metaldehyde hutumika kuua na kuzuia wanyama pori huko vijijini
✓ Dawa za kuzuia wadudu (insecticides) kama vile organophosphate, organochlorde, pyrethrin, pyrethroids na carbamate
✓ Sumu za chakula ( food poisoning) kama vile chocolates, vitunguu, tangawizi, zabibu, macadania nuts na pia xylitol hii hutumiwa sana na watu wenye kisukari
✓ Mimea ya sumu pamoja na bidhaa za mafuta kama vile mafuta ya taa, petrol na tuperntine
✓ Sumu za panya na Contact poisoning
Imeandaliwa na C.E.O
JM Veterinary Centre ( JMVC)
Phone: +255712784472
Motto: We save You and your animal as family
Karibu tukuhudumie