Sumaye haeleweki anachosimamia

Sumaye haeleweki anachosimamia

Jamaa analia lia kweli sasa kama rais analia lia atawezaje kuongoza nchi

Miaka 20 bungeni hajasikika akikemea rushwa wala ufisadi halafu leo eti oooh naunda mahakama ya mijizi; jeuri hiyo ataitoa wapi kama sio porojo za akina mjomba megawati. Watu wameikataa katiba ya wananchi yenye maadili yanayokomesha ufisadi na kulinda rasilimali za taifa halafu leo wanaibuka na porojo hizi. Eti ooh mama ntilie wasisumbuliwe, ooh machinga ni muhimu nitawapa benki na mikopo; unajua hawa jamaa wanatuona sisi ni punguani tangu lini katetea wanyonge bungeni? waliotutetea miaka yote huku wanazomewa leo wanaonekana hawajui kazi anayejua kazi ni huyo wa kupiga domo; inawezekana akili zetu sio nzuri inafaa tupimwe kuwaendekeza watu kama hawa na kuwakenulia meno
 
huyu jamaa amejidhalilisha sana,amekuwa icon ya unafiki na uchu wa madaraka,atajuta sana baada ya october

Kati ya Sumaye na John Pombe Makufuli anayetaka kuingia Ikulu kwa kupiga push ups na kucheza rhumba kwenye jukwaa la kisiasa huku akikurupua ahadi za kila rangi na majigambo milioni kidogo ni nani mwenye uchu wa madaraka?..CCM mpaka wametamka kupitia Kampeni Meneja wao Abdallah Bulembo kuwa Nanukuu “Serikali imefanya makosa mengi na Chama Cha Mapinduzi kimefanya makosa mengi lakini hakitofanya kosa la kuruhusu chama pinzani kuingia Ikulu,” Ni nani mwenye uchu wa MADARAKA?
 
Pamoja na ushabiki wote wa kisiasa na kama unazijua siasa hasa za Tanzania, na dunia kote, huwezi kumtukana mtu kiasi hicho hasa mawaziri wakuu waliopita na binadamu yeyote katika medani za kisiasa vingnevyo unatumika na pia huna akili timamu, Tanzania ni nchi ya mfumo wa vyama vingi na hakuna aliyezaliwa kuwa mpinzani na walioko upinzani wote walikuwa na kadi za ccm chama chetu, kila mwanaccm ana haki ya kujiunga na upinzani kama anadhani anaweza kuwatetea watanzania na yy mwenyewe akiwa nje ya ccm au chama chochote cha upinzani na akiwa upinzani au ccm hawezi kusifia kule alikotoka kwani vingnevyo hakuwa na haja ya kutoka chama kimoja kwenda kingne na anayefanya hivyo watanzania wanasema amenunuliwa naahasimu wao.
Nadhan FS na wenzake wote upande wa upinzani wanahaki kwa kile wanachokisema imradi hawavunji sheria za nchi, na hata mpande wa chama chetu ccm wanasema na wanawasema wapinzani madhaifu yao, thats politics,washabiki,wapenzi wa vyama na wagombea tunatakiwa tuwe na akili zaidi ya wafanye siasa zaidi. Hakuna mwanasiasa ambaye sio mpenda madaraka na ni hulka ya kiumbe hai yeyote yule, binadamu anahitaji kutambuliwa,kuthaminiwa na kuwa maisha mazuri. Na siasa za Tanzania mwanasiasa ndo tajiri kuliko mhadhiri, daktari hata akiwa bingwa,uinginia na wataalamu wote hawana kitu ukilinganisha na mwanasiasa
Huwezi kutumia lugha chafu kiasi hicho kwa viongozi wakuu wa nchi hii hasa wastaafu hasa kwa mambo ambayo ni ya kisiasa.
Naamini hakuna binadamu yeyote yule asiyetaka madaraka yenye tija kwake, vingnevyo hata upande wetu wa ccm kusingekuwa na wagombea wa nafasi zote.

Ndio siasa hizo, unalialia nini sasa ye angekaa kimya watu wangemuheshimu sasa huu mpira unaitwa chandimu, pole.
 
Kenda kuungana na wezi wenzie. Hayo ndo yaliitwa magamba sasa yamevuka na ccm imebaki safiii. ccm oyeeeeeeeeeeeee!

Chenge,Ngeleja, Prof. Tibaijuka, Prof. Muhongo, Mwambalaswa Mwakyembe na Mabehewa ya kupeperushwa na upepo na wengine wengi je? Ufisadi umeisha ccm?
Nape na Mwigulu walikamatwa kwanini na Takukuru?
 
Miaka 53 gani niliodanganywa wakati ccm imeanza mwaka 1977 na mimi nimezaliwa 1980! sasa hata hesabu hujui unapelekwa tu kama ling'ombe! Lowasa out.....!

Akili ziro kabisa,
CCM inatokana na TANU na ASP tangia uhuru mfumo wa utawala ni mmoja tu tena nenda Lumumba utaona bango linakwambia hapa ndipo ilipozaliwa TANU 1954 Sasa ni zaidi ya miaka 61 bado hakizeeki?
 
Sumaye arudishe mahekari ya ardhi kule mvomero na nyumba zaidi ya 5 alizonunua kwa bei ya kutupa, na atuambie miaka 10 Ya u PM wake alishindwaje kutukomboa maskini badala yake akapora mali na ardhi za wanyonge!?

Wewe utakuwa Unamsema Mzee Mwinyi maana ndiye mwenye Shamba Kubwa sana pale Mvomero
 
Tatizo la mtu mwenye mawazo finyu, huwa anadhani kikomo cha mawazo yake, ndio ufahamu wote uliopo. Sasa Nikuulize, umeelewa Nilichokiandika?
Mengi kulalamikia umasikini ni tofauti na hoja niliyoizungumzia hapo. Hao wanane ni mifano tu michache ya waliofanikiwa katika mfumo wa utawala wa CCM na Nimewataja kwa sababu wanajulikana na karibu kila mtu. Hata hivyo, ukiangalia kiuhalisia, kuna mamilioni ya watu walio na nafuu kubwa ya maisha hata kama si mamilionea, sasa wao waliwezaje kujikwamua katika mazingira hayohayo ambayo watu wanadai hayachochei mafanikio?

Akili ndogo haiwezi kuifundisha akili kubwa hata siku Moja. Una Elimu gani mwenzangu?
Kazi ya Serikali ni kutengeneza Sera ambazo zitanufaisha Wananchi.
Kwa Mfano Kenya maBenk yanakuja na mbinu mpya kila siku ya kuwakopesha fendha wakenya wakati hapa ukitaka kukopa uweke bank pesa kwanza miezi sita hadi mwaka tutaendelea kweli?
hauwezi kuwa Tajiri katikati ya dimbwi la Masikini haiwezekani.
Sijui wewe unafurahia pesa za wavija jasho zinavyoliwa na wachache kama vile Tegeta Escrow?
sijui unafurahia kwenda kilomita 7kwa masaa manne?
Sijui unafurahia kwenda Hospital ya Umma usikute Dawa?
Sijui unafurahia Kukosa umeme unapouhitaji?
Sijui unafurahia watoto kukaa chini shuleni?
Sijui unafurahia Mkulima kunyonywa mazao yake na kukopwa?
Una nafasi gani katika wanaowadhurumu watanzania mpaka unatetea hivyo?
 
Haina uhusiano na hoja yangu kama vipi anzisha uzi wa kudai hizo pesa, mi namwambia huyu mwizi Sumaye arudishe ardhi za wanyonge.

Nilidhani unazungumzia Ufisadi in General kumbe unamzungumzia mtu,
Wewe ni hatari kuliko ukimwi virus vyako havina mbadala.
Kama ni kurudisha au kuondoa ufisadi nadhani tungeanza na wa Tegeta Escrow maana tuna mtaji wa Ushahidi wa watu waliokiri.
 
Kwa hiyo wote waliotajirika au kujikomboa kiuchumi ndani ya utawala wa CCM ni mafisadi walioneemeshwa na mfumo usio wa haki wa CCM? Kuwataja Mbowe na Mwenzie, Nilikusidia kumulika wale waliofanikiwa kupitia huo mfumo bila kuwa watawala ndani ya chama tawala lakini hapo hapo wanaupinga huo mfumo.
Pia kuna mamilioni ya watu ambao wako vizuri kiuchumi ambao wamekuza uchumi wao ndani ya huohuo mfumo.
Sijui unasemaje kuhusiana na hilo?

Hakuna aliyekuza Uchumi kwa mfumo wa ccm wewe.
Vipi maana hueleweki kabisa.
Benja alimwaga Ngano ya Bakhressa hii ni.kukuza uchumi?
 
Akili ndogo haiwezi kuifundisha akili kubwa hata siku Moja. Una Elimu gani mwenzangu?
Kazi ya Serikali ni kutengeneza Sera ambazo zitanufaisha Wananchi.
Kwa Mfano Kenya maBenk yanakuja na mbinu mpya kila siku ya kuwakopesha fendha wakenya wakati hapa ukitaka kukopa uweke bank pesa kwanza miezi sita hadi mwaka tutaendelea kweli?
hauwezi kuwa Tajiri katikati ya dimbwi la Masikini haiwezekani.
Sijui wewe unafurahia pesa za wavija jasho zinavyoliwa na wachache kama vile Tegeta Escrow?
sijui unafurahia kwenda kilomita 7kwa masaa manne?
Sijui unafurahia kwenda Hospital ya Umma usikute Dawa?
Sijui unafurahia Kukosa umeme unapouhitaji?
Sijui unafurahia watoto kukaa chini shuleni?
Sijui unafurahia Mkulima kunyonywa mazao yake na kukopwa?
Una nafasi gani katika wanaowadhurumu watanzania mpaka unatetea hivyo?

Umeweka blah blah nyiiingi sana lakini ilichokusaidia ni kuanika mapungufu makubwa uliyonayo. Ndio maana mwanzoni Nilikueleza kuwa mtu mwenye ufinyu wa mawazo huwa anadhani kuwa kile anachokifahamu ndicho kila kitu. Hizo sentensi tano ulizoziandika ungezisummerise kwa neno moja tu, mfumo au mazingira.
Ndio maana basi, hata mwanzoni Nilihoji kuwa pamoja na yote unayodai kuhusu mfumo wa CCM, hao waliofanikiwa, waliweza vipi? Hilo ndilo swali la msingi hapa.
 
Hakuna aliyekuza Uchumi kwa mfumo wa ccm wewe.
Vipi maana hueleweki kabisa.
Benja alimwaga Ngano ya Bakhressa hii ni.kukuza uchumi?

Ina maana ndesamburo sio tajiri? Mbowe sio tajiri? Sijagusia swala la uchumi kama nchi, nimezungumzo ukombozi wa kiuchumi kwa watu na ndio maana tunazungumzia watu.
 
Umeweka blah blah nyiiingi sana lakini ilichokusaidia ni kuanika mapungufu makubwa uliyonayo. Ndio maana mwanzoni Nilikueleza kuwa mtu mwenye ufinyu wa mawazo huwa anadhani kuwa kile anachokifahamu ndicho kila kitu. Hizo sentensi tano ulizoziandika ungezisummerise kwa neno moja tu, mfumo au mazingira.
Ndio maana basi, hata mwanzoni Nilihoji kuwa pamoja na yote unayodai kuhusu mfumo wa CCM, hao waliofanikiwa, waliweza vipi? Hilo ndilo swali la msingi hapa.

CCM haifai hata kwa nini.
Una Elimu ya Kudesa wewe ndiyo maana hata upeo wako wa kuelewa ni mdogo sana.
 
Back
Top Bottom