Sumaye haeleweki anachosimamia

Sumaye haeleweki anachosimamia

Ni katika mazingira yapi ambamo Mbowe na Ndesamburo walitajirikia?

Urithi. Chimbuko lao walikuwa manyapara wa kikoloni. Na bado huwezi kulinganisha utajiri wa watu wa kuhesabika wakati majority ni maskini wa kutupwa. Jifunze uchumi
 
Urithi. Chimbuko lao walikuwa manyapara wa kikoloni. Na bado huwezi kulinganisha utajiri wa watu wa kuhesabika wakati majority ni maskini wa kutupwa. Jifunze uchumi

Utajiri wa kurithi kutoka Ukoloni? Acha kudanganya watu, hujui chochote kuhusiana na utajiri wa hao watu. Kwa hiyo watu wote waliofanikiwa na kuboresha uchumi wao binafsi walirithi toka zama za ukoloni?

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini (Chadema), Philemon Ndesambro, amewataka wakazi wa Moshi kutoogopa kukopa fedha kwenye taasisi za fedha nchini kwa sababu, hata yeye amekuwa akikopa kuendesha biashara zake.

Siri hiyo ya Ndesamburo ambaye anamiliki vitega uchumi mbalimbali nchini, ikiwamo Hoteli za kitalii na Kampuni ya Utalii ya Keys miji ya Moshi na Dar es Salaam, alisema kinachotakiwa ni nidhamu katika urejeshaji mikopo hiyo.

Ndesamburo alitoa kauli hiyo juzi mjini Moshi, wakati akifungua mkutano wa tano wa Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos) cha Usharika wa Karanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini.
“Msiogope kukopa na baada ya kukopa lazima mkumbuke kurejesha mkopo kwa uaminifu…hii ndio siri ya utajiri na hata mimi ninatumia mikopo kufanya biashara zangu kwa mafanikio,” alisisitiza.

Mbunge huyo alitaka uongozi wa Saccos hiyo kuangalia uwezekano wa kuanzisha idara maalumu ya wataalamu wa masuala ya ujasiriamali, ambao watakuwa na wajibu wa kutoa mafunzo na ushauri kwa kila mkopaji.

Katika taarifa yake kwa mbunge huyo, Mwenyekiti wa chama hicho, Humphrey Urassa, alisema chama hicho kinakabiliwa na changamoto ya kusaidia makundi maalumu, wakiwamo wajane, yatima na walemavu.

Urassa alisema kama wangepata ufadhili wa Sh10 milioni kutoka kwa mbunge huyo na wengine, wangeweza kukopesha makundi hayo maalumu kwa sababu hayana uwezo wa kununua hisa wala kuweka akiba.

Akijibu maombi hayo, Ndesamburo aliahidi kukisaidia chama hicho fedha, lakini akakataa kutaja kiwango zaidi aliwataka viongozi wa chama hicho kukutana naye ofisini kwake ili kukubaliana jinsi atakavyosaidia.
 
Aliondoa deni la Taifa na kufikia tilioni 6.8 Mkwere kalipaisha na kufikia tillion 48 hapo nadhani utajua yupi alikuwa mwadilifu.

Kupunguza deni la taifa sio kigezo cha kufanya vizuri. Unadhani hizo barabara; miradi ya gesi; kbadili kutoka umeme wa maji kwenda gesi; Kupanua bandari etc - inafanyika kwa kutumia makaratasi??? Ni pesa hizo zinatumika!!! Kupunguza deni ni uoga wa kuleta maendeleo.
 
Mimi nikajua unabonge ya hoja kumbe ni unafiki tu wasalimie wanafiki wenzako
 
huyu jamaa amejidhalilisha sana,amekuwa icon ya unafiki na uchu wa madaraka,atajuta sana baada ya october

... Sumaye ni mtu muhimu katika upinzani anayo mambo wengi serikalini ana vijana kibao unayo mengi ambayo bado atayasema kuiokoa tanzania na watanzania tunaomba MUNGU ukawa iingiemadarakani tanzania aondokane na ulaghai wa CCM
 
Sifa za kiongozi ninayemtaka
1.asiwe mbabaishaji
2.awe mwadilifu
3.awe mwenye maamuzi magumu ya busara
4.asiwe mwepesi wa hasira
5.awe mwenye maono ya mbali kwa maslahi ya watanzania wote
6.awe mtu anayejali wanyonge
7.awe mcha mungu
8.awe mzalendo wa kweli
9.asiwe na uchu wa madaraka
10. Awe anajua shida za watanzania na awe tayari kuzishughulikia kwa wakati
11.awe mtu mwenye msimamo wenye tija kwa wote/asiwe mkurupukaji afanye upembuzi yakinifu kabla ya kuamua jambo lolote linalogusa maslahi ya nchi hii
12.awe na uwezo wa upatanishi
13.asiwe mchokozi mchokozi
14. Awe mpenda amani
15. Awe mtu anayejipatia mali kwa haki / asiwe mtu wa dhuluma
16.asiwe fisadi
17.awe mtu asiyelipa kisasi
18.awe mtu wa watu/asiwe mbaguzi kwa aina yoyotte ile
19.awe na sifa kikatiba (raia, umri, nk)
20.awe mtu msikivu /asiwe mbabebabe kwa watu anaowaongoza
21.mtu anayejali wenye shida katika jamii

#########kama ni wewe #####kura yangu umepata mkuu####
 
Kwa hiyo wote waliotajirika au kujikomboa kiuchumi ndani ya utawala wa CCM ni mafisadi walioneemeshwa na mfumo usio wa haki wa CCM? Kuwataja Mbowe na Mwenzie, Nilikusidia kumulika wale waliofanikiwa kupitia huo mfumo bila kuwa watawala ndani ya chama tawala lakini hapo hapo wanaupinga huo mfumo.
Pia kuna mamilioni ya watu ambao wako vizuri kiuchumi ambao wamekuza uchumi wao ndani ya huohuo mfumo.
Sijui unasemaje kuhusiana na hilo?

Mkuu, mada hii inamlalamikia Sumaye na ndugu yake Lowassa kwa kukosa shukrani kwa mfumo uliowafanikisha. Hao wengine wanaingizwa kupanua mjadala na, nahisi, kupoteza mwelekeo (focus) ya mjadala. Mtei, Mbowe na Mengi ni wapambanaji; wametajirika kwa juhudi zao binafsi huku wakikwamishwa sana na mfumo huo. Kuwajumlisha na Manji, Bakhresa, n.k. ni kutaka kuzungusha blanketi kufunika watu wasiolingana. Ukweli unabaki palepale kwamba mfumo uliopo ni wa kifisadi. Kuna wanaouendesha na kunufaika nao ambao wamo ndani ya CCM na serikali yake na kuna wasiohusika na uendeshaji wake lakini wananufaika nao ama moja kwa moja au kupitia makandokando yake. Ni rahisi kuwasoma hata hapa JF.

Tatizo la kubwa la mfumo wa aina hiyo kwanza kabisa unaacha idadi kubwa ya wananchi na taifa kwa ujumla wakiwa wahanga wakiishia kuwa hohehahe wa kibinafsi na kukosa huduma muhimu za kijamii ambazo angalau zingepunguza makali ya umasikini wa kibinafsi. Unaongeza kero na hasira dhidi yake kwa wengi nchini. Lakini, uzuri wake hasa ni kwamba kutokana na kutokuwa na haki wala maadili ndani ya mfumo huo, hata wale wenye kuuendesha na kuufaidi huishia kudhurika na kuanza kuuona ukweli. Just a matter of time. Wezi, hatimaye, hushindwa kuheshimiana (No honour among thieves). Ndicho kilichowatokea akina Sumaye na Lowassa. Baada ya kugundua mfumo huo si endelevu na una madhara makubwa kwa taifa, sasa wameamua kujiunga na wahanga wakuu wa mfumo huo (wananchi wenzao) ili kuutokomeza. CHADEMA/UKAWA nao wameona fursa hiyo na kuamua kuitumia ipasavyo.

Na dalili zinaonyesha mkakati unafanya kazi ya uhakika ukisikiliza vilio, mayowe, mahangaiko yanayotokea kwenye kambi ya chama tawala. Magufuli mwenyewe amekitelekeza chama; anaongea kama mpinzani mkubwa wa mfumo huo na kila kukicha anatishia watendaji wa serikali yake; sio mgambo, sio polisi, sio wawekezaji waliowauzia viwanda, n.k. Kifupi nikuwa wagombea wote wanaupiga vita mfumo huo! Got the message?
 
Kwa kweli nimekuwa najiuliza alikuwaje pm kwa miaka 10? ni MNAFIKI, MBEYA, na MUONGO.
Eti pale kawe akasema eti sisiemu WALITUAHIDI maisha bora ila mpaka sasa bado, kweli? hii kitu ni ya yeye kusema hivyo? NIMEMDHARAU sana huyu babu. Yeye kawa pm wa sisiemu juzi juzi tu kwa miaka 10, leo anaongea pumba!

Unaposifia serikali ya Mkapa kuwa angalau ilifanya vizuri, ukumbuke pia kuwa iliongozwa na Sumaye.
 
Utajiri wa kurithi kutoka Ukoloni? Acha kudanganya watu, hujui chochote kuhusiana na utajiri wa hao watu. Kwa hiyo watu wote waliofanikiwa na kuboresha uchumi wao binafsi walirithi toka zama za ukoloni?

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini (Chadema), Philemon Ndesambro, amewataka wakazi wa Moshi kutoogopa kukopa fedha kwenye taasisi za fedha nchini kwa sababu, hata yeye amekuwa akikopa kuendesha biashara zake.

Siri hiyo ya Ndesamburo ambaye anamiliki vitega uchumi mbalimbali nchini, ikiwamo Hoteli za kitalii na Kampuni ya Utalii ya Keys miji ya Moshi na Dar es Salaam, alisema kinachotakiwa ni nidhamu katika urejeshaji mikopo hiyo.

Ndesamburo alitoa kauli hiyo juzi mjini Moshi, wakati akifungua mkutano wa tano wa Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos) cha Usharika wa Karanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini.
“Msiogope kukopa na baada ya kukopa lazima mkumbuke kurejesha mkopo kwa uaminifu…hii ndio siri ya utajiri na hata mimi ninatumia mikopo kufanya biashara zangu kwa mafanikio,” alisisitiza.

Mbunge huyo alitaka uongozi wa Saccos hiyo kuangalia uwezekano wa kuanzisha idara maalumu ya wataalamu wa masuala ya ujasiriamali, ambao watakuwa na wajibu wa kutoa mafunzo na ushauri kwa kila mkopaji.

Katika taarifa yake kwa mbunge huyo, Mwenyekiti wa chama hicho, Humphrey Urassa, alisema chama hicho kinakabiliwa na changamoto ya kusaidia makundi maalumu, wakiwamo wajane, yatima na walemavu.

Urassa alisema kama wangepata ufadhili wa Sh10 milioni kutoka kwa mbunge huyo na wengine, wangeweza kukopesha makundi hayo maalumu kwa sababu hayana uwezo wa kununua hisa wala kuweka akiba.

Akijibu maombi hayo, Ndesamburo aliahidi kukisaidia chama hicho fedha, lakini akakataa kutaja kiwango zaidi aliwataka viongozi wa chama hicho kukutana naye ofisini kwake ili kukubaliana jinsi atakavyosaidia.

Haya maelezo yako bado hayajitosherezi kuonyesha walipata wapi utajiri.
Kama hujui kaa kimya
 
Wewe ulikuwa wapi wakati wa Mbowe Club?
baba yake Mbowe anamiliki Mali tangua zamani sana unaonekana ni Mgeni sana ww?

Naona ndio umeipata hoja. Naijua Historia ya Mbowe vyema sana , Baba yake alikuwa na uwezo enzi hizo na alimsponsor hata Nyerere kipindi fulani, lakini ilikuwa enzi hizo. Mbowe Club si kitu cha ajabu kwani kila mtu aliekulia Dar tangu enzi hizo, haiwezi kuwa kitu kigeni kwake. Mazingira yasingekuwa favourable kwa mtu alie na juhudi kujikwamua kiuchumi, hiyo club isingekuwapo na kudumu mpaka leo. Unajua Mbowe amewahi kufanya kazi BOT?
1233479_616741195037584_290424736_n.jpg

Ulikuwepo enzi hizi? Hapo ni Bilicanas na huyo kushoto ni Mbowe
 
Naona ndio umeipata hoja. Naijua Historia ya Mbowe vyema sana , Baba yake alikuwa na uwezo enzi hizo na alimsponsor hata Nyerere kipindi fulani, lakini ilikuwa enzi hizo. Mbowe Club si kitu cha ajabu kwani kila mtu aliekulia Dar tangu enzi hizo, haiwezi kuwa kitu kigeni kwake. Mazingira yasingekuwa favourable kwa mtu alie na juhudi kujikwamua kiuchumi, hiyo club isingekuwapo na kudumu mpaka leo. Unajua Mbowe amewahi kufanya kazi BOT?

Sasa kwann asifanye wakat mke wake mboye alikua mtoto wa GAVANA BOT?????Hiyo pia mbowe utajir wake umeboostiwa na utajir kutoka upande wamkewe!!!!!!Ndio maana ITV ilimuhoj mkewe mbowe ambaye ni daktar bingwa muhimbil kwann ameacha kaz mke akajib kaacha ili kusiamia biashara zake na mmewe maana zinamlipa kuliko shahara ya udaktar bingwa!!!!!!!!Sasa umenipata
 
Haya maelezo yako bado hayajitosherezi kuonyesha walipata wapi utajiri.
Kama hujui kaa kimya

Wewe unaedhani unaelewa zaidi historia yao, leta hapa hoja za kunipinga. Wenzio wote wanajua hao walitajirika kwa juhudi zao binafsi, sasa wewe unaejua zaidi leta hoja za kupinga hilo.
 
Kwa kweli nimekuwa najiuliza alikuwaje pm kwa miaka 10? ni MNAFIKI, MBEYA, na MUONGO.
Eti pale kawe akasema eti sisiemu WALITUAHIDI maisha bora ila mpaka sasa bado, kweli? hii kitu ni ya yeye kusema hivyo? NIMEMDHARAU sana huyu babu. Yeye kawa pm wa sisiemu juzi juzi tu kwa miaka 10, leo anaongea pumba!

Sa kwa nini hawamuulizi kama mafao yake hapati? Au hakuna muda wa maswali?
 
Back
Top Bottom