WAZIRI Mkuu mstaafu wa Tanzania, Frederick Sumaye, amewalipua viongozi wa sasa wa serikali akiwemo Rais Jakaya Kikwete kwa hatua yao ya kuruhusu baadhi ya wanafamilia wao kuwania vyeo vya juu vya uongozi.
Akiwasilisha mada kwenye mdahalo wa maadhimisho ya miaka 13 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, jana jijini Dar es Salaam, Sumaye alisema hatua ya viongozi wengi kuandaa watoto na wake zao kwa ajili ya kuwa viongozi wa nchi, ni kinyume na katiba ya nchi, na dalili ya ubinafsi.
Katika chaguzi za sasa ndani ya CCM, Rais Kikwete ni mmoja wa viongozi waandamizi ambao familia zao zimegombea na kushinda nafasi za uongozi ndani ya jumuiya za chama hicho.
Baadhi ya watu kutoka familia ya Rais Kikwete waliojitosa katika chaguzi hizo ni pamoja na mkewe, na watoto wake wawili.
Kauli hiyo nzito ya Sumaye ni ya pili tangu alipoanguka katika kinyang'anyiro cha kuwania ujumbe wa NEC Taifa, akishindwa na Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Mary Nagu.
Mwishoni mwa wiki, Sumaye alikaririwa akisema kuwa, kukithiri kwa rushwa ndani ya chama hicho, ndiyo sababu kubwa iliyomwangusha na kueleza hofu yake ya nchi kupata viongozi wabovu.
Aliongeza kuwa ubinafsi umekuwa chanzo kikubwa cha kukithiri kwa rushwa katika sekta mbalimbali kwa kuwa viongozi wengi wa serikali, hawako tayari kupoteza madaraka yao, hivyo hutumia rasilimali za nchi na uwezo wao wa kifedha kuwahonga wapiga kura ili waendelee kukaa madarakani, hata kama wananchi hawawataki.
"Rushwa imekithiri sehemu muhimu na mtu yeyote anayetaka kwenda Ikulu kupitia rushwa hafai. Mosi hizo fedha za kuwahonga wananchi alipata wapi? Kama amekopa anategemea Ikulu kuna hela ambazo hataweza kurudisha deni hilo?
"Chaguzi zote zimetawaliwa na rushwa moja kwa moja jambo ambalo hayati Mwalimu Nyerere alilikemea hadi mwisho wa uhai wake, na kama hatutaliangalia tatizo hilo kwa makini, kuna athari kubwa kwa taifa," alisema.
Sumaye alikwenda mbali zaidi na kusema kuwa, kama Mwalimu Nyerere angefufuka leo, kusingekuwa na kiongozi wa kumlaki, badala yake watu wengine wangekuwa wa kwanza kukimbilia porini.Mbali ya ubinafsi huo, alisema uchumi wa nchi umeshikiliwa na kundi la wachache, hivyo kuzuka kwa hali ya kutojali kundi la watu masikini ambalo ni tatizo kwa taifa, kwa sababu viongozi hao wamewekeza kwa kuwajali wenye nacho ili wanufaike kama wao.
Naye Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Dk. John Magotti, alitumia fursa hiyo kuzungumzia suala la kiwango cha elimu itolewayo nchini hususani katika shule za kata kuwa ni chachu ya kukwamisha ufaulu sanjari na ajira kwa wahitimu.
"Kuna haja ya serikali kutafuta ufumbuzi katika sekta ya elimu kabla haujaleta madhara makubwa, kwa sababu elimu bora inaendana na nafasi bora ya ajira, hivyo mwito wangu elimu inayotolewa katika shule za kata isitofautiane sana na ile ya shule za watu binafsi," alisema Magotti.
Akiwasilisha mada kwenye mdahalo wa maadhimisho ya miaka 13 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, jana jijini Dar es Salaam, Sumaye alisema hatua ya viongozi wengi kuandaa watoto na wake zao kwa ajili ya kuwa viongozi wa nchi, ni kinyume na katiba ya nchi, na dalili ya ubinafsi.
Katika chaguzi za sasa ndani ya CCM, Rais Kikwete ni mmoja wa viongozi waandamizi ambao familia zao zimegombea na kushinda nafasi za uongozi ndani ya jumuiya za chama hicho.
Baadhi ya watu kutoka familia ya Rais Kikwete waliojitosa katika chaguzi hizo ni pamoja na mkewe, na watoto wake wawili.
Kauli hiyo nzito ya Sumaye ni ya pili tangu alipoanguka katika kinyang'anyiro cha kuwania ujumbe wa NEC Taifa, akishindwa na Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Mary Nagu.
Mwishoni mwa wiki, Sumaye alikaririwa akisema kuwa, kukithiri kwa rushwa ndani ya chama hicho, ndiyo sababu kubwa iliyomwangusha na kueleza hofu yake ya nchi kupata viongozi wabovu.
Aliongeza kuwa ubinafsi umekuwa chanzo kikubwa cha kukithiri kwa rushwa katika sekta mbalimbali kwa kuwa viongozi wengi wa serikali, hawako tayari kupoteza madaraka yao, hivyo hutumia rasilimali za nchi na uwezo wao wa kifedha kuwahonga wapiga kura ili waendelee kukaa madarakani, hata kama wananchi hawawataki.
"Rushwa imekithiri sehemu muhimu na mtu yeyote anayetaka kwenda Ikulu kupitia rushwa hafai. Mosi hizo fedha za kuwahonga wananchi alipata wapi? Kama amekopa anategemea Ikulu kuna hela ambazo hataweza kurudisha deni hilo?
"Chaguzi zote zimetawaliwa na rushwa moja kwa moja jambo ambalo hayati Mwalimu Nyerere alilikemea hadi mwisho wa uhai wake, na kama hatutaliangalia tatizo hilo kwa makini, kuna athari kubwa kwa taifa," alisema.
Sumaye alikwenda mbali zaidi na kusema kuwa, kama Mwalimu Nyerere angefufuka leo, kusingekuwa na kiongozi wa kumlaki, badala yake watu wengine wangekuwa wa kwanza kukimbilia porini.Mbali ya ubinafsi huo, alisema uchumi wa nchi umeshikiliwa na kundi la wachache, hivyo kuzuka kwa hali ya kutojali kundi la watu masikini ambalo ni tatizo kwa taifa, kwa sababu viongozi hao wamewekeza kwa kuwajali wenye nacho ili wanufaike kama wao.
Naye Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Dk. John Magotti, alitumia fursa hiyo kuzungumzia suala la kiwango cha elimu itolewayo nchini hususani katika shule za kata kuwa ni chachu ya kukwamisha ufaulu sanjari na ajira kwa wahitimu.
"Kuna haja ya serikali kutafuta ufumbuzi katika sekta ya elimu kabla haujaleta madhara makubwa, kwa sababu elimu bora inaendana na nafasi bora ya ajira, hivyo mwito wangu elimu inayotolewa katika shule za kata isitofautiane sana na ile ya shule za watu binafsi," alisema Magotti.