Masalu Jacob
JF-Expert Member
- Jul 26, 2017
- 1,339
- 1,493
Habari Tanzania !
Naomba kuweka wazo langu hapa jukwaani. Nawaomba taasisi za Elimu ya kati na juu kupitia Wizara ya Elimu mkaja na hii huduma kwa hawa vijana wanaohitimu chuo hususani ngazi ya kati na juu ( Diploma & Degree holders) tuwapatie kadi maalumu kwaajili ya kupata kibali cha ajira za muda mfupi mfano miezi 9 mpaka mwaka 1 na miezi 6.
LENGO: Kuwapa uzoefu na kuwasaidia kuonyesha ujuzi na uwezo wao wa kitaaluma kwenye taasisi tutakazo wapangia kwa hicho kipindi. Hii huduma itaondoa ushindani usio na maana kwa vijana wa taifa hili na kuwapa uwezo zaidi Wizara ya Elimu na Vyuo husika kuwa na mipango endelevu na hawa wahitimu watumike kulitumikia taifa kwa kipindi kifupi huku wakisubiri ajira za kudumu ama kujiajiri.
WALENGWA/ WAHUSIKA: Hii huduma iwe maalumu kwa vijana wote ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu na kati kwa kuanzia ( Diploma & Degree ).
NAMNA YA KUPATA KADI: Hii huduma itolewe mara tu muhitimu anapomaliza elimu yake chuo husika kupitia Chuo chake (Pawepo na Muhudumu toka wizara ya Elimu kila chuo itapendeza).
MAENEO YA KUTUMIKA KADI HIZI: Huduma hii itumike taasisi zote za umma zenye upungufu wa watumishi hawa vijana waelekezwe na kupangiwa huko kwenye hayo maeneo. Pia kwa taasisi binafsi zitakazoingia mikataba na Vyuo husika na taarifa zao zitumwe Wizara ya Elimu na Wizara ya Ajira kwa utunzaji mzuri wa kumbukumbu.
MALIPO NA POSHO: Hii huduma iwe na malipo na posho maalumu ya kujikimu tu. Mfano Fedha ya Chakula, Usafiri (Nauli), Nyumba na Mavazi (Fedha hizo zikizi hizi huduma pekee).
HITIMISHO
Wahitimu wafanye kazi kwa bidii na watuletee maendeleo. Tusiwaache wazagae na elimu zao zilitumikie taifa barabara.
Hii huduma inanyika pia kwa nchi za wenzetu kama UFARANSA, AUSTRALIA NA POLAND (UHOLANZI).
Karibu.
Naomba kuweka wazo langu hapa jukwaani. Nawaomba taasisi za Elimu ya kati na juu kupitia Wizara ya Elimu mkaja na hii huduma kwa hawa vijana wanaohitimu chuo hususani ngazi ya kati na juu ( Diploma & Degree holders) tuwapatie kadi maalumu kwaajili ya kupata kibali cha ajira za muda mfupi mfano miezi 9 mpaka mwaka 1 na miezi 6.
LENGO: Kuwapa uzoefu na kuwasaidia kuonyesha ujuzi na uwezo wao wa kitaaluma kwenye taasisi tutakazo wapangia kwa hicho kipindi. Hii huduma itaondoa ushindani usio na maana kwa vijana wa taifa hili na kuwapa uwezo zaidi Wizara ya Elimu na Vyuo husika kuwa na mipango endelevu na hawa wahitimu watumike kulitumikia taifa kwa kipindi kifupi huku wakisubiri ajira za kudumu ama kujiajiri.
WALENGWA/ WAHUSIKA: Hii huduma iwe maalumu kwa vijana wote ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu na kati kwa kuanzia ( Diploma & Degree ).
NAMNA YA KUPATA KADI: Hii huduma itolewe mara tu muhitimu anapomaliza elimu yake chuo husika kupitia Chuo chake (Pawepo na Muhudumu toka wizara ya Elimu kila chuo itapendeza).
MAENEO YA KUTUMIKA KADI HIZI: Huduma hii itumike taasisi zote za umma zenye upungufu wa watumishi hawa vijana waelekezwe na kupangiwa huko kwenye hayo maeneo. Pia kwa taasisi binafsi zitakazoingia mikataba na Vyuo husika na taarifa zao zitumwe Wizara ya Elimu na Wizara ya Ajira kwa utunzaji mzuri wa kumbukumbu.
MALIPO NA POSHO: Hii huduma iwe na malipo na posho maalumu ya kujikimu tu. Mfano Fedha ya Chakula, Usafiri (Nauli), Nyumba na Mavazi (Fedha hizo zikizi hizi huduma pekee).
HITIMISHO
Wahitimu wafanye kazi kwa bidii na watuletee maendeleo. Tusiwaache wazagae na elimu zao zilitumikie taifa barabara.
Hii huduma inanyika pia kwa nchi za wenzetu kama UFARANSA, AUSTRALIA NA POLAND (UHOLANZI).
Karibu.