Stronghold ya CCM imebaki sehemu gani?

Stronghold ya CCM imebaki sehemu gani?

Ujinga wa magamba ni kuzidi kujidanganya kuwa salama eti wana wanachama na ngome zao kumbe watu walishahama kitambo sana...mtakufa bila kujijua wapuuzi nyie,mmekalia kubambikiza kesi za ugaidi na kuiandama chadema huku mkisahau wajibu wenu kwa jamii.
 
Ukitoa arusha kwingine kote ni ccm. Polisi ni ccm,jeshi ni ccm, tume ya uchaguzi ccm,wafadhili wote ccm.
 
ccm ipo kila sehemu. kuuliza ngome ya ccm ni ipi? ni upunguani
 
Mada inaaongelea stronghold, sio uwepo.

kila mkoa ni strong hold ya ccm. labda mikoa ya Kilimanjaro na kigoma peke yake ndiyo nadhani wabunge wa upinzani wamewazidi wa ccm. arusha inayo itwa ngome ya chadema, ccm ina wabunge zaidi ya chdm. halmashauri zote (madiwani) zinaendeshwa na ccm nchi nzima kasoro halmashauri zisizo zidi 10 ndiyo ziko upinzani. this is why nasema ccm nchi mzima ni ngome yake. jibu kwa takwimu dogo. acha blabla na porojo za mitaani. chdm ina halmashauri ngapi hapa nchini? au ni shabiki wa kufuata mkumbo hufanyi uchunguzi wa kisomi?
 
ndugu idimi kama unasisitiza neon strong hold, basi nakuomba uiondoe ccm kwa sababu yao imejikita kila wilaya. hebu waombe wadau wajadili strong hold za chdm, cuf, nccr na tlp. nikizungumza kama political analyst kwa kuweka ushabiki pembeni, lazima nizeme hivyo. huo ndiyo ukweli. nimefuata takwimu za matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010
 
ndugu idimi kama unasisitiza neon strong hold, basi nakuomba uiondoe ccm kwa sababu yao imejikita kila wilaya. hebu waombe wadau wajadili strong hold za chdm, cuf, nccr na tlp. nikizungumza kama political analyst kwa kuweka ushabiki pembeni, lazima nizeme hivyo. huo ndiyo ukweli. nimefuata takwimu za matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2010

Kama unafikiri uchaguzi na idadi ya wachaguliwa ina-determine stonghold ya chama, basi kwa ccm ni kila mahali. Lakini tukitizama sababu za kuchaguliwa kwa ccm na chadema ni tofauti. Wengi wanachaguwa ccm sio kwa sababu sera zina mvuto au watu wana imani nayo, bali kwa sababu za uoga, vitisho vitakavyofuata na rushwa. Watu wengi wanaochagua chadema wanataka mabadiliko ya ccm. Cha ajabu watanzania wengi wanataka mabadiliko lakini kwa uoga wanachagua ccm. Ndio maana leo kila mahala wana ngome yao
 
Tuwape wananchi Maendeleo ndo watatukubali
"Vox populi vox dei"
 
Wakuu naomba mnisaidie hasa wana CCM wenzangu kwa sasa stronghold yetu iko sehemu gani ya Tanzania?. Kwa sababu Visiwani ni CUF wanatamba, kasikazini na kasikazini magharibi ni CDM inatamba Magaribl na kusini magaribi ni CDM na NCCR wanatamia. Kusini kwa gesi haitoki wote tunaelewa , kwa hali ilivyo sasa tunaweza hata tusipate mgombea uchaguzi ukifanyika huko sasa. Hapo ndipo najiuliza strong hold yetu ni ipi?
tutafahamu mwaka kesho kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa. vuta subira.
 
tutafahamu mwaka kesho kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa. vuta subira.


Nakubali kuwa mwakani kuna uchaguzi, mbona vyama vya upinzani havionyeshi jitihada ya kweli ya kuwafikia wananchi na kuandaa wagombea wao?.
CHADEMA ambayo inajitahidi kuwafikia wananchi bado inarudia mulemule mijini. Sijasikia Mboe anafanya mkutano wa hadhara kijiji fulani au wanaogopa mahudhurio yatakuwa kidogo. Bila kwenda vijijini mwaka kesho mambo yatakuwa yaleyale CCM itachukua mitaa asilimia 90
 
Ukitoa arusha kwingine kote ni ccm. Polisi ni ccm,jeshi ni ccm, tume ya uchaguzi ccm,wafadhili wote ccm.


Kwa hiyo stronghold ya kwingine hamna kitu. CHADEMA ni Arusha pekee?
 
STRONGHOLD ya CCM imeendele kupungua kwa kuwa sasa Bukoba inabidi tuiondoe kwenye stronghold ukizingatia uhuni unaofanywa na makao makuu ya CCM dhidi ya misuli ya ccm mkoa . Hapa ulipizaji visasi na hujuma lazima zitakuwepo hasa wakibadilisha uamuzi wa REC mkoa wa Kagera.
 
Sasa chama changu CCM kinazidi kuchanganyikiwa sijui mawimbi haya yataisha lini masikini chama changu kilichonilea na kunitunza miaka yote hii...!!!!
 
Back
Top Bottom