Story za Mwinyimkuu

Story za Mwinyimkuu

MR MWINYIMKUU

Member
Joined
Sep 1, 2022
Posts
20
Reaction score
15
STORY: JINI ZUNAIDA
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA KWANZA
Story yetu inaanza katika falme ya majini iliyofahamika kwa jina la kashikashi falme ambayo ilikuwa ina nguvu na haijawahi kushindwa Vita. Falme hii ilikuwa inaongozwa na Mfalme aliyefahamika kwa jina la AMOUR ambae alikuwa na binti mmoja aliyeitwa ZUNAIDAH ambae alizaa na mkewe UMMUKURTHUMU anaetoka Falme ya ALBASH inayoongozwa na kaka take BASHR ambae alikuwa na kijana was kiume anaeitwa YUKTY. Katika kipindi chote wazazi wa Zunaidah walikuwa wamepanga kumuhoza binti yao kwa mtoto wa BASHR ambae in kaka wa Ummukurthum ili Falme zao ziwe zenye nguvu kuliko Falme zingine za Ujinini lakini binti yao Zunaidah alikuwa akipinga swala hilo Siku zote.
***********""**************************************
Ikiwa jumapili tulivu kabisa katika jiji la Dar es Saalam watu wakiwa wapo off baada ya wiki nzima kuchoshwa na KAZI. Mmja ya watu hao akiwa kijana Shabani ambae shyghuli zake zilikuwa ni kuvua samaki lakini Siku hiyo hakwenda kabisa pwani kwasababu ya uchomvu aliyokuwa nao kutokana na Jana yake alilala pwani baada ya kupata bahati ya mtende kuvua samaki wengi na kufanikiwa kupiga bingo ya pesa ndefu. Kijana huyu alikuwa yatima anakaa na MJOMBA wake anaefahamika kwa jina la Sele ambae alimlea toka wazazi wake walipofariki na ndiye aliyemfundisha shughuli za uvuvi.
**************************************************
Majira ya jioni kijana Shabani alikuwa amepumzka lakini ghafla anakuja rafiki yake wa mda mrefu HAMISI....
HAMISI: hoya vp we bishoo?
SHABAN: shwari inakuaje mgumu kufa?
HAMISI: shegaa tu nakuona umeridhiiiiika mtoto was kiume!
SHABAN: Niridhike na nini sasa mbona ngendembwe nyingi!!
HAMISI: ngendembwe? Wakati nakuona umelala kitumbo juu au ndo bingo la jana?
SHABAN: aaaaaah wapi unazinguaa bhana!
HAMISI: sasa sikia hill syo lililonileta kilichonileta hapa nataka ujiandae twende pwani
SHABAN: saizi?
HAMISI: ndiyo
SHABAN: huoni muda kama umeenda saaana
HAMISI: jioni ndo kuna samaki was kumwaga wewe twende tukawazoee
SHABAN: hata kama mzee Mimi Leo nipo off napumzika kaka!
HAMISI: sikia ndugu yangu nakuomba twendwe kama tukikosa samaki Mimi ntakulipa Mara mbili ya usumbufu.
SHABAN: una uhakika?
HAMISI: haswaaaa! Bila shaka.
SHABAN: sawa twende zetu.
**************************************************
Ikiwa jioni ya SAA kumi na mbili bahari imechafuka wavuvi wakiwa wanakimbilia pwani bahari imenuna vijana wawili walionekana kupakia mtumbwi wao na kusonga mbele nao ni HAMISI na rafiki yake kipenzi SHABAN................................... Hivi wale vijana wana akili kweli?...............mi nafikiri wamerogwa maana bahari imechafuka wao ndo wanaikimbilia...................huwezi jua labda wana vizizi vya mababu zao! Au watakuwa wamepewa vizizi na waganga wao walisikika wazee wawili wakiwajadili vijana hao.
**************************************************
Wakiwa wanaendelea kutanda nyavu katika bahari hiyo ya Hindi ghafla SHABAN alisikia sauti ikimwita Shabani! Shabani! Shabani!!
SHABAN: nani ananiita huyoo?
HAMISI: acha uwiga wewe akuite nani wewe
SHABAN: inamaana hujasikia?
Mara sauti ikajibu hawezi kunisikia mpenzi in Mimi na wewe tu.
Ndipo shabani alipoangalia mbele akamuona mwanamke mwembamba mrefu kama mwarabu au shombeshombe wa kihindi akiwa anatembea juu ya maji bila kuzama.... Ndipo alipopiga kelele na kuzimia...........................JE UNAJUA NINI KILIENDELEA?......................usikose sehemu ya pili ya mkasa huu wa kusisimua.
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA PILI
Tunaendelea na story yetu pale tulipoishia ambapo SHABAN alimuona msichana mwenye asili ya kiarabu akiwa anatembea juu ya maji na hali hiyo ilimfanya apige kelele na kuzimia............endeleaa...
HAMISI alikuwa hajui nini cha kufanya baada ya rafiki yake kuzimia. Ndipo alipofanya maamuzi ya kugeuza mtumbwi na kurejea ufukweni ili kwenda kumpa huduma ya kwanza rafiki take
**************************************************
Tunarudi ujinini katika Falme ya KASHIKASH bila shaka tunafahamu kuwa Falme hii inaongozwa na Mfalme AMOUR ambae ni baba yake ZUNAIDAH........
Mfalme AMOUR: binti yangu ZUNAIDAH unajua kiasi gani nakupenda na wala staki upate matatizo.
ZUNAIDAH: ni kweli baba nalijua hilo
Mfalme AMOUR: sasa naomba nikuulze kitu binti yangu!
ZUNAIDAH: niulize tu baba!
Mfalme AMOUR: binti yangu unajua wewe ndo binti yangu wa pekee na katika ufalme huu wewe ndiye mrithi wa pekee sijui unalifahamu hilo?
ZUNAIDAH: nalifahamu baba
Mfalme AMOUR: sasa binti yangu nahitaji uolewe na BINAMU yako YUKTY.
ZUNAIDAH: babaaa!
Mfalme AMOUR: tatizo nini binti yangu? Mbona kijana yule mstaharabu tu, na istoshe anatoka kwenye falme anayotoka mama yako sasa shida nini mwanangu?
ZUNAIDAH: lakin baba Mimi sihitaji kuolewa na YUKTY
Mfalme AMOUR: unataka kuolewa na nani na kama una mchumba mbona hukuwahi kumleta mapema nyumban tumjue? ( kiukali)
ZUNAIDAH: baba kwakweli nna MTU nampenda.
Mfalme AMOUR: nani unaempenda?
ZUNAIDAH: SHABAN
Mfalme AMOUR:SHABAN! Sijawahi kusikia jina LA namna hiyo katika falme hii wala katika ulimwengu wa majini.............(alifikiria kwa kina kisha akaendelea) unamaanisha huyo SHABAN ni binadamu?
ZUNAIDAH: (kwa kusita) ndiyo baba
Mfalme AMOUR: shi ndo ka rabo umtu na mi NAL jin otol shabah bin Adam( wewe mtoto kumbuka wewe jini na SHABAN ni binadamu.
ZUNAIDAH: pa to shiv padal ( lakini nampenda)
Mfalme AMOUR: ZUNAIDAAAAH!
ZUNAIDAH: baba!!
Mfalme AMOUR alinyanyuka na kuondoka na kumuacha binti yake mdomo wazi
**************************************************
Tunarudi duniani upande wa akina SHABAN na MJOMBA wake SELE ikiwa Sikh nyengine kumekucha asubuhi
MJOMBA SELE: Vpi mjomba umeamka?
SHABAN: nimeamka MJOMBA ila kichwa tu ndo kinauma.
MJOMBA SELE: Tatizo lako mjomba wewe mapepe mengi unaogopa wakati wewe mvuvi bwana! Sifa ya mvuvi haogopi bahari.
SHABAN: siyo hivyo MJOMBA ila niliona kitu cha ajabu saana.
MJOMBA SELE: Usinifurahishe MJOMBA uliona nini kwani?
SHABAN: nilimuona mwanamke mweupe anatembea juu ya maji bila kuzama.
MJOMBA SELE: Hahahaha mjomba hicho ndo kimekutisha hao ni vibwengo tu wa baharini wanataka wakutishe ili uogope lakini hawezi kukudhuru
SHABAN: lakini MJOMBA ndo aniite jina langu istoshe kibwengo ni mfupi yule mrefu
MJOMBA SELE: mmmh! Mjomba hebu ngoja niende kupata ulabu nikirudi tutayajenga vizuri ila nikutoe hofu tu mjomba hakuna cha kukudhuru
SHABAN:sawa MJOMBA
MJOMBA SELE: haya baadae
Baada ya MJOMBA yake kuondoka alianza pilika pilika za kujiandalia chakula cha mchana.........Mara ghafla....hodii....hodii.....wenyewe hodii
SHABAN: karibu nani?
Mimi hapa nifungulie................
SHABAN: nakuja
Kwa maajabu alipofika mlangoni hakuona MTU
SHABAN: aaaah watu wengine bhana ..........akafunga mlango na kurudi ndani Mara vyombo vinagongana kabatini.......kwa hofu SHABAN ananyata ili ajue nini kinaendelea ghafla anakuta kabatini hakuna mtu ...............Mara anackia jiko linawashwa hofu inazidi kuongezeka......kwa kijana SHABAN .................wakati akiwa kwenye sitofahamu ..........akasikia tena......jamani SHABAN wangu nikuandalie nini Leo?
SHABAN: wewe nani? ( kwahofu)
Jamani hunikumbuki? Mimi ni yule tuliyokutana Jana baharini mlipokuwa mnavua samaki! Ghafla kicheko......hahahahahahahahahaha
SHABAN: mamaaaaaaaa nakufaaaaaaaa...(huku akitimua mbio) kicheko cha kifedhuli kikifatia.................................JE NINI KITAENDELEA..............USIKOSE.....SEHEMU YA TATU YA MKASA HUU..............BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT:0719013038
WHATSAPP: 0719013038
LOCATION: DARES SALAAM
SEHEMU YA NNE
Baada ya SHABAN kupiga kelele na kukimbilia chumbani kwa MJOMBA make MJOMBA alifungua mlango na kumuulza shida nini..........SONGA NAYO...........
SHABAN: MJOMBA amenifata tena yule mwanamke JINI.....(huku akihema)
MJOMBA SELE: MJOMBA amekufata au ulikuwa unaota mjomba?
SHABAN: haki ya mungu tens mjomba tena ameniambia nisiende kwa MGANGA ( akiendlea kuhema)
MJOMBA SELE: unasemaaa! Inamaana ameshajua mpango wetu?
SHABAN: ndyo mjomba itakuwa hivyo
MJOMBA SELE: mmmh mbona balaaaaa! Basi ngoja tulale kesho tutajua cha kufanya usiwe na wasiwasi yataisha mjomba.
SHABAN: sawa Mjomba. ( kwa unyonge)
**************************************************
Tunarudi katika falme ya ALBASH inayoongozwa na BASHR MJOMBA yake ZUNAIDAH akiwa anazungumza na kijana wake
BASHR: kijana wagu shupavu,naona muda umewadia sasa na wewe uwe na familia yako ili uiongoze.
YUKTY: hahaha baba bhana familia so ndo wewe na mama
BASHR: hapana mwanangu familia nnayoizungumzia hapa ni wewe uwe na mke pamoja na watoto wako wakuite baba kama wewe unavyoniita Mimi baba.
YUKTY: aaaaaah sasa hapo nimekuelewa kumbe unataka nioe baba
BASHR: sio nataka ila muda umefika na kwa kawaida mtoto wa kwanza katika koo zetu za falme za kijini lazima achaguliwe.
YUKTY: hahah baba kwa hiyo umenichagulia?
BASHR: hapana tumekuchagulia Mimi na mama yko siyo peke yangu
YUKTY: nani huyo binti?
BASHR: unataka kumjua?
YUKTY: ndiyo baba
BASHR: BINAMU yako ZUNAIDAH unamuonaje?
YUKTY: aaaaah baba bwana (akiona aibu)
BASHR: najua umempenda au siyo mwanangu?
YUKTY: Mimi baba sina cha kuwapinga kwasababu hilo ni chaguo lenu nami nalipitisha,kwasababu ZUNAIDAH ni binti ambae anatabia njema na amelelewa katika maadili mazuri.
BASHR: safi saana mwanangu huo ndo uamuzi wa kiume hahaha umefanya maamuzi ya busara teh teh teh
**************************************************Tunarudi upande wa pili ambapo tunamuona rafiki kipenzi wa SHABAN akiwa anasuka nyavu zake
Mara mda huo huo anakuja mama yake
MAMA: hamisi mwanangu Leo huingii pwani?
HAMISI: kwa nini mama
MAMA:naona kitendea kazi unakirekebisha kuna safari hapo?
HAMISI: hamna mama kuna matundu kidogo narekebisha, arafu tena nimekumbuka unajua Mama SHABAN ana matatizo saana
MAMA: matatizo! Matatizo gani tena?
HAMISI: tika Sikh ya kwanza tulienda kuvua baharini alidai kuwa kuna kiumbe wa ajabu alimuona na mpaka Jana alimfata nyumbani kwao pia istoshe hata mjomba yake alishakutana nae akiwa anatoka kilabuni
MAMA:mmhhh mwanangu hilo litakuwa jini linawasumbua hapa cha msingi kutafuta tiba mbadala kabla ya tatizo halijawa kubwa
HAMISI: kweli mama yaani SHABAN amekuwa kama kachanganyikiwa tumsaidie kwakweli
MAMA: ndo hivyo tumuombe mungu hatujalie tufanikiwe
HAMISI: mungu atafanya wepesi tu
MAMA: Aaamiiin haya ngoja nikuache nikaandae chakula.
HAMISI: sawa mama Mimi ngoja nimalizie malizie hapa
............JE NI MSAADA GANI ANAOTAKA KUSAIDIWA SHABANI........NA JE WATAFANIKIWA KUMFUKUZA JINI ZUNAIDAH? USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU WA JINI ZUNAIDAH.............BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT:0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA SITA
Tunaendelea pale tulipoishia ambapo ZUNAIDAH anapewa sharti na mama yake.......Songa nayo.....
UMMUKURTHUM: nataka mje mfunge ndoa huku na muishi huku kama huwezi basi siwez kukusaidia!
ZUNAIDAH: mmmhh mama naomba nipe mda wa kufikiria kwasababu siyo rahisi hivyo
UMMUKURTHUM: najua kwamba ni ngumu lakini mwanangu hili jambo linamaana kubwa sana kwako na kama utashindwa basi utaolewa na BINAMU yako YUKTY
ZUNAIDAH: mama naomba unipe mwezi mmoja niongee na mwenzangu naamini atakubali tu.
UMMUKURTHUM: hilo Mimi silijui kama atakubali au atakataaa Mimi ntasubiri jibu. Na kumbuka ntakuwa namzuga baba ako mpaka unipe jibu sawa?
ZUNAIDAH: sawa mama nimekuelewa
**************************************************
Mama ZUNAIDAH ambae ni mke wa AMOUR alipotoka kwa mwanae alienda kuzungumza na mumewe juu ya ombi la binti yao....
AMOUR: eeeh nipe ripoti anasemaje hiyo binti yako!
UMMUKURTHUM: mmmh jamani baba zuu mbona unaharaka hivyo hebu tumpe nafasi binti yetu ya kutafakari hili jambo ili aweze kufanya maamuzi ya busara
AMOUR: hapo hakuna maamuzi ya busara zaidi ya kuolewa na BINAMU yake tu
UMMUKURTHUM: jamani baba ZUNAIDAH hivi unakumbuka hata wewe hukuwahi wala hukutaka kuingiliwa katika jambo LA kuchaguliwa mke?
AMOUR:nakumbuka mke wangu
UMMUKURTHUM: kama unakumbuka kuna mtu wlikuchagulia mchumba wa kuoa si uliamua kuoa kijakazi wa ndani ambae ni Mimi!
AMOUR: lakini mke wangu hayo yalishapita tunazungumzia sasa
UMMUKURTHUM: sawa basi tumpe muda wa kufikiria
AMOUR: kwa siku ngapi?
UMMUKURTHUM: mwezi mmja
AMOUR: lakini mama Zuu...
UMMUKURTHUM: tatizo nini babaa wewe si unataka majibu basi tuvumilie tu
AMOUR: sawa hakuna taabu
**************************************************
Tunarudi duniani ambako tunaziona familia mbili zikiwa zimekutana, MJOMBA SELE na mpwa wake SHABAN pamoja na MAMA HAMISI na HAMISI mwenyewe
MJOMBA SELE: kama nilivyo waambia ndugu zangu yaani hili tatzo kinamsumbua mpwa wangu anakuwa kama amechanganyikiwa yaani sielewi nifanyaje
MAMA: hatuna cha kujilaumu kwasababu hakuna ambae anayafurahia matatizo cha msingi tupambanevili tulimalize hili swala
MJOMBA SELE: kweli kabisa maana hata mm nishachoshwa na vibweka vya JINI huyu
MAMA: sasa ndugu yangu kuna MGANGA kutoka Tanga nimeongea nae amesema tumrushie nauli elfu kumi na yeye tiba yake itaghalimu shilingi laki moja
MJOMBA SELE: hilo halina shida sisi tunachotaka uzima tu
SHABAN: kwa hiyo mama huyo MGANGA anaweza kuja lini ??
MAMA: hata kesho anaweza kuja kama tumejiandaa vizuri
MJOMBA SELE: basis Dada chukua pesa hii hapa utamrushia ya nauli kesho aje tuanze KAZI
MAMA: kabisaaa liwezekano Leo lisingoje kesho
MJOMBA SELE: Mimi naona hili limeisha ngoja sisi twende tukashughulikie majukumu mengine
MAMA: eeeh nilikuwa nataka kuingia jikoni
SHABAN: usijali mama acha twende
MAMA: hata karibuni
Usikose sehemu inayofuata ya mkasa huu wa kusisimua*** by MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA TANO
Baada ya kumaliza KAZI ya kushona nyavu yake aliitwa na mama yake kwani chakula kilikuwa tayari hivyo aliingia ndani kwa ajili ya kupata chakula na maongezi yaliendelea...
MAMA: mwanangu nimepata wazo
HAMISI: wazo gani tena mama?
MAMA: kuna mganga yupo Tanga nitafanya mawasiliano nae kama tukikubaliana nae tutamtumia nauli aje.
HAMISI: hiyo safi saana mama nnahamu ya kumsaidia rafiki yangu aepukane na kibwengo huyu maana daah
MAMA: usijali mwanangu SHABAN namchukulia kama mwanangu kwa hiyo nipo nae bega kwa bega.
HAMISI: ntashukuru saan mama yangu
**************************************************
Tunarudi upande wa pili ambapo tunamuona MJOMBA SELE na SHABAN wakiwa wanazungmza
MJOMBA SELE: MJOMBA mi naona hili swala lishakuwa gumu tukilidharau litakuwa kubwa saana
SHABAN: ni kweli mjomba ila tutafanyaje?
MJOMBA SELE: inabidi twende kwa MGANGA
SHABAN: mjomba kwa MGANGA tena?
MJOMBA SELE: ndiyo MJOMBA ndo njia sahihi ya kumkomesha huyu kisabengo.
SHABAN: mjmba kwa MGANGA hapana!
MJOMBA SELE: nini wewe? Yaani wewe matatizo yote hayo bdo hujijali mwenyewe na unavyonisumbua usiku? Nakwambia utakwenda.
SHABAN: MJOMBA kumbuka yule jini alishanikataza kwenda kwa mganga
MJOMBA SELE: sikia wewe MGANGA anauwezo wa kumtuliza jini wa aina yoyote ndomana akakukataza kwenda kwa MGANGA kwasababu atamzidi nguvu.
SHABAN: kweli mjombaa eeeh?
MJOMBA SELE: kabisa mjomba wewe ngoja uone atakimbia nyumba hii na atarudi kuzimu shenziii!!
SHABAN: sawa MJOMBA Niko pamoja na wewe
MJOMBA SELE: poa mjombaaa usijali tutalimaliza
**************************************************
Tunarudi upande wa Ufalme wa KASH KASH hapa tunamuona mama yake ZUNAIDAH ambae anaitwa UMMUKURTHUM akiwa na binti yake wanaongea
UMMUKURTHUM:hivi mwanangu nilichikisikia kwa baba yako ni cha kweli?
ZUNAIDAH: kipi mama?
UMMUKURTHUM: baba yako ameniambia kwamba unataka uolewe na binadamu ni kweli?
ZUNAIDAH: kweli mama (kwa uwoga)
UMMUKURTHUM: kwa hiyo hiyo kijana unaempenda anakupenda?
ZUNAIDAH:ndiyo mama tena ananipenda saana
UMMUKURTHUM: sasa sikia mwanangu Mimi sitaki kukuingilia maamuzi yko ila so unajua mila na tamaduni zetu za ujinini lazima uolewe na JINI mwenzio tena mwanamke anaetoka katika koo ya kifalme kama wewe lazima uolewe na mfalme au mtoto wa mfalme.
ZUNAIDAH: lakini mama....
UMMUKURTHUM: najua mwanangu kumchagua mume ni HAKI yako lakini angalia heshima ya wazazi wako.
ZUNAIDAH: mama Mimi nampenda lakini...
UMMUKURTHUM: sijakukataza wala sikupingi ila tu angalia heshima yetu sisi
ZUNAIDAH: kwa hiyo mama unamsaport baba niolewe na BINAMU yangu YUKTY?
UMMUKURTHUM: nilitaka Iwe hivyo lakini siwezi kukulazimisha umpende au uolewe na YUKTY wakati humpendi
ZUNAIDAH: sasa mama kama unazielewa hisia zangu basi nisaidie
UMMUKURTHUM: mmmh sijui kama ntaweza ila ntajaribu
ZUNAIDAH: ntafurahi saana mama
UMMUKURTHUM: ila kina sharti....
ZUNAIDAH: lipi tena mama?
.............JE UNAJUA SHARTI GANI QNALOAMBIWA ZUNAIDAH? ..........USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU......WA KUSISIMUA .....BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY : JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT :0719013038
WHATSAPP : 0719013038
MAHALI😀AR ES SALAAM
EMAIL : hafidhushabani75@gmail.com
Tunaendelea pale tulipoishia ambapo mjomba sele ameenda kwa mama hamisi ili kueleza furaha aliyonayo... Songa nayo...
MJOMBA SELE : Yaani nimepata bonge la mama mkwe mwenzio nafaidije!
MAMA: mmh yaani nashindwa kukuelewa mwenzio huyo mkwe ni yupo? Kwa nani? Na unafaidi nini?
MJOMBA SELE : mkwe wangu kwa SHABAN ana uwezo wa kipesa basi mwanzo mwisho napombeka tu.. haha haha kwa raha zangu wala sigombwi teh teh teh!
MAMA : nashindwa kukuelewa mwezangu kwahiyo huyo mkwe anakupa wewe hela ya pombe?
MJOMBA SELE : ndiyo
MAMA: Bado hujanijibu SWALI langu lakini... huyo mkwe kwa nani?
MJOMBA SELE : Inamaana we hujui au? Si kwa sheby!
MAMA: hehehe! Usinichekeshe wewe huyo sheby Kakua lini?
MJOMBA SELE : kama huniamini sawa ila ukweli ndo huo.
MAMA : huyo binti asiyekuwa na kazi anatokea wapi na anaishi wapi?
MJOMBA SELE : aaah acha dharau mama hamisi bwana kwani sele ana mapungufu gani?
MAMA: haya basi kaa chini unieleze kwa kina.... Au umenuna?
MJOMBA SELE : utaniudhu bhana (huku akikaa)
**************************************************************
Tunarudi upande wa pili ambapo tunamuon ZUNAIDAH akiwa na YUKTY wakiwa wanazozana..
ZUNAIDAH :hivi kaka kwanini unanifatilia saana?
YUKTY: kukufatilia kivipi? Mbona sikuelewi Zuu?
ZUNAIDAH : sikia YUKTY mimi sikuhitaji wewe na kumbuka mimi ni dada yako siwezi kuolewa na wewe Katy!
YUKTY : Zuu hata kama wewe ni binamu yangu inaruhusiwa kukuoa na mimi NakuPenda saana na unajua hilo.
ZUNAIDAH : Lakini mimi sikupendi!
YUKTY : ZUNAIDAH hata kama hunipendi Si kuamua kunidharirisha na kwenda kumpenda binadamu... Hii.. Si... Sawa na..
ZUNAIDAH : haikuhusu kwanza kilichokufanya uende duniani kumtishia nani? Mimi sikupendi YUKTY kama wewe unanipenda niache huru na mtu nimpendae na siyo kumnyima amani
YUKTY :yule binadamu hatoishi kwa amani mpaka ukubali kuolewa na mimi na yeye aoe mwanadam mwenzie!
ZUNAIDAH : aroshooo! (Nyamaza) kama ukithubutu kumgusa hata nywele yake sitokuacha mzima utaingia vitani na mimi.
YUKTY : kumbuka mimi ni ndugu yako na mimi ni chimbuko lako na hupaswi Kupambana na mimi.
ZUNAIDAH : nalifahamu hilo kaka na ndomana nikakuonya usimsogelee nimpendae ni Kheri unique mimi nikiwa napambana na wewe.
YUKTY : lakini Zuu.....
ZUNAIDAH : letashruu (NIMEMALIZA)
Alipomaliza kusema hayo anaondoka zake na kumuacha YUKTY akipiga kelele za Hasira. Kumbe muda wote huo MFALME BASHR alikuwa kajificha mahali anashuhudia ugomvi huo.
**************************************************************
Tunarudi upande mwingine ambao anaonekana sheby akiwa anaendelea na shughuli zake za nyumbani mara wanakuja washikaji wa mtaani na kuanza kumuita........ Sheby.... Sheby... Hoya sheby... We sheby..
SHABAN: Hoya nani weweee!?
MSHIKAJI 1: Aaaah hunajifany hutujui muhuni wetu leo? Hebu toka nje bwana tuongee!
SHABAN : Poa wait dk sifuri basi!
MSHIKAJI 2: chap basi!
Baada ya kufanya kazi zake zote anatoka na kuwakuta masela wake wa vijiweni.
SHABAN :Mmmh nambieni maze!
WOTE: dah shwari
SHABAN : kuna habari gani?
MSHIKAJI 1:Mwanangu sikia unajua mzee baba sasa hivi hatukusomi wala nini?
SHABAN : Kivipi?
MSHIKAJI 1: umebadilika kabisa skani hutokei kazi tukija kukustua hutokei lakini unavimba mtaani na unatuzidi matumizi nini siri ya maFanikio yako?
SHABAN :Hebu acheni ujinga wenu bhana yaani hicho ndo kilichowaleta hapa au kuna kingine?
MSHIKAJI 2: sikia sheby wewe mwanetu we tupange tu maana kuna skendo mtaani zinavuma kuwa ndugu unaishi na kigagula sijuhi kibwengo..
SHABAN : hoya habari za kiboya sizifagilii kama vipi sepeni msiniharibie siku.
MSHIKAJI 2: sheby watu tumeachiwa ufundi na mababu zetu nishakuzoom na ntajua tu huenda UKAWA Chuma ulete Wewe
SHABAN : chunga kauli yako dogo usijifanye mjuaji?
MSHIKAJI 2: sisi tunaenda lakini kitaeleweka mshenzi wewe mtoto MdoGo unamiliki majini tutakuonesha bwege wewe.
Sheby akawaangalia kwa makini kisha anajua kuna vita itakuja mda Si mrefu.
Hivyo alitakiwa ajipange kwa vita hiyo isiyojulikana itaanza lini na itaisha lini.
JE NINI AMBACHO KITATOKEA? USIKOSE KUFATILIA SEHEMU INAYOFUATA.
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA TISA
Baada ya jini ZUNAIDAH kumtishia amani mganga wa kienyeji kutoka tanga alitoweka na kumuacha mganga asijue cha kufanya......SONGA NAYO......
MGANGA: yaani jini yule anauwezo wa kuingia nyumbani kwangu bila kudhulika? Jini wa haina gani yule, mbona haijawahi kutokea miaka yote toka nianze Kazi yangu ya uganga kuja kutishwa na JINI katika himaya yangu? Nuksi gani hili hebu ngoja niwapigie simu.....( baada ya muda akawa anaongea na simu mpaka ikakata) siwezi kwenda kutengeneza vita na majini kizembe nawarudishia nauli yao wamtafute mtaalamu mwengine.
**************************************************
MJOMBA SELE na SHABAN walifika kwa akina HAMISI mchana na kuwakuta wakiwa wanaandaa chakula hivyo walijumuika kula kwa pamoja...baada ya muda walikuwa washamaliza na mazungumzo yakaanza....
MAMA: yaani afadhali mlivyokuja mapema maana kuna mapya yamezuka!
MJOMBA SELE: yapi tena hayo?
MAMA: yule jini si kwenda Tanga kwenda kumtisha mtaalamu.
WOTE: eeeeeeeeeh!
MAMA: hivyo hapa kanipigia simu kanieleza kila kitu pia kanirudishia ile pesa tuliyomtumia kwa ajili ya nauli.
MJOMBA SELE: daah mbona balaa tena hili sijui tufanyaje?
MAMA: na kwa ushauri tu alionipa kasema mtu yeyote atakae thubutu kuingilia mahusiano haya cha moto atakiona kwasababu huyu JINI ana nguvu saaana na wala siyo mbaya
MJOMBA SELE: awe mbaya asiwe mbaya we umeona wapi jini kaishi na binadamu?
HAMISI: kwa hiyo turafanyaje MJOMBA?
MJOMBA SELE: hapa kukaza msuli tu mwanzo mwisho mpaka kieleweke
SHABAN: Mimi sielewi hata nifanyaje
MAMA: usijali mwanangu ndo mitihani hiyo ya dunia
SHABAN: mama yangu imezidi mpaka vibwengo?
HAMISI: usijali ndugu tutapata solution tatizo litakwisha kabisaaa!
SHABAN: haya tuombe mungu
**************************************************
Tunarudi ujinini kwenye ufalme ALBASH hapa tunamuona mama baba na mtoto
YUKTY: baba toka ulivyoniambia swala LA kuoa naona hujanigusia chochote kuhusiana na ZUNAIDAH!
BASHR: ni kweli mwanangu hatujazungumza chochote na hii kutokana na zunaidah kuomba mda wa kufikiria kwa wazazi wake juu ya ombi letu
MAMA: na kwa kukutoa shaka mwanangu zunaidah lazima awe mkeo
YUKTY: hahah ntafurahi saana mama kwasababu nampenda hakuna mfano.
BASHR: tunalijua hilo kwa hiyo tulia tufanye mpango mambo yanyooke!
YUKTY: Mimi sina presha baba nawasikiliza ninyi tu
MAMA: basi toa shaka juu ya hilo kabisa
YUKTY: hahah nawategemea saana na najivunia kuwa na wazazi kama nyinyi.
Kwa pamoja walikuwa wanafurahi na kumpa moto kijana wao kuhusu kumpata binti ZUNAIDAH ili afunge nae ndoa awe mkewe.
..............NINI KITAKACHOJIRI SEHEMU YA KUMI KATIKA MKASA HUU WA KUSISIMUA........
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CINTACT:0719013038
WHAT'S APP: 0719013038
NAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA SABA
Baada ya kutoka nyumbani kwa akina HAMISI, SHABAN na MJOMBA yake wakiwa njiani MJOMBA SELE alimwambia SHABAN awahi nyumbani kwenda kuandaaa mapishi ya mchana kwani yeye anaenda kufatilia madeni yake kwa watu aliowakopesha......SONGA NAYO.......
Baada ya kuachana na mjomba yake aliendelea kupiga hatua kuelekea nyumbani lakini ghafla alikutana na msichana mremboo saaana ambae alikuwa hana mfano akamsimamisha SHABAN......
ZUNAIDAH: mambo kaka
SHABAN: poa Dada
ZUNAIDAH: samahani naomba kukuuliza
SHABAN: bila samahani Dada uliza tu
ZUNAIDAH: kuna mvuvi maarufu anaitwa SELE na anauza samaki nyumbani kwake sijui kwake wapi?
SHABAN: unashida nae ya kibiashara au binafsi?
ZUNAIDAH: kibiashara kwasababu nataka nimpe pesa ambazo baba ameniagiza ili ampelekee mzigo wa samaki
SHABAN: aaaah sawa kiufupi hujapotea Mimi ni mpwa wake naitwa....
ZUNAIDAH: nakufahamu kwamba unaitwa shabani
SHABAN: umenijuaje?(kwa mshtuko)
ZUNAIDAH: baba alinambia mvuvi SELE anaishi na mpwa wake anaeitwa SHABAN kwa hiyo ulivyosema wewe mpwa wake moja kwa moja nikajua ndo wewe
SHABAN: aaaah kumbe hivyo ulnistua nikawa najiulza umenijuaje
ZUNAIDAH: hahahaha acha uwoga wewe
SHABAN: hamna siyo uwoga ila lazima nishangae OK haya twende nyumbani ukamsubiri maana kuna sehemu amepitia, si utamngoja?
ZUNAIDAH: haina shida
**************************************************
Upande wa MJOMBA SELE alikuwa akigombana na wavuvi wenzie ambao amewakodisha nyavu hawajamlipa pesa yake
MJOMBA SELE: ndomana Mimi sipendi kutoa nyavu yangu kwasababu nyinyi sio walipaji washenzi tuuu
Mvuvi: ndugu biashara haikuwa nzuri naomba utuvumilie kwa Leo
MJOMBA SELE: niwavumilie Mara ngapi mbwa nyinyi KAZI kunywa pombe na kutumia na wanawake Mimi hamtaki kunilipa
Mvuvi wa pili: basi ndugu nakuhaidi Mimi kesho ndo uchukue hela yako wala hamna tabu.
MJOMBA SELE: sawa kwa heshima yako tu nakwenda kesho mkiiona sura hii mjue tutaonana wabaya
Mvuvi: wewe kesho njoo usijali
MJOMBA SELE: sawa mi naenda tutaonana kesho *************TUKUTANE SEHEMU INAYOFUATA*********BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CINTACT:0719013038
WHAT'S APP: 0719013038
NAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA SABA
Baada ya kutoka nyumbani kwa akina HAMISI, SHABAN na MJOMBA yake wakiwa njiani MJOMBA SELE alimwambia SHABAN awahi nyumbani kwenda kuandaaa mapishi ya mchana kwani yeye anaenda kufatilia madeni yake kwa watu aliowakopesha......SONGA NAYO.......
Baada ya kuachana na mjomba yake aliendelea kupiga hatua kuelekea nyumbani lakini ghafla alikutana na msichana mremboo saaana ambae alikuwa hana mfano akamsimamisha SHABAN......
ZUNAIDAH: mambo kaka
SHABAN: poa Dada
ZUNAIDAH: samahani naomba kukuuliza
SHABAN: bila samahani Dada uliza tu
ZUNAIDAH: kuna mvuvi maarufu anaitwa SELE na anauza samaki nyumbani kwake sijui kwake wapi?
SHABAN: unashida nae ya kibiashara au binafsi?
ZUNAIDAH: kibiashara kwasababu nataka nimpe pesa ambazo baba ameniagiza ili ampelekee mzigo wa samaki
SHABAN: aaaah sawa kiufupi hujapotea Mimi ni mpwa wake naitwa....
ZUNAIDAH: nakufahamu kwamba unaitwa shabani
SHABAN: umenijuaje?(kwa mshtuko)
ZUNAIDAH: baba alinambia mvuvi SELE anaishi na mpwa wake anaeitwa SHABAN kwa hiyo ulivyosema wewe mpwa wake moja kwa moja nikajua ndo wewe
SHABAN: aaaah kumbe hivyo ulnistua nikawa najiulza umenijuaje
ZUNAIDAH: hahahaha acha uwoga wewe
SHABAN: hamna siyo uwoga ila lazima nishangae OK haya twende nyumbani ukamsubiri maana kuna sehemu amepitia, si utamngoja?
ZUNAIDAH: haina shida
**************************************************
Upande wa MJOMBA SELE alikuwa akigombana na wavuvi wenzie ambao amewakodisha nyavu hawajamlipa pesa yake
MJOMBA SELE: ndomana Mimi sipendi kutoa nyavu yangu kwasababu nyinyi sio walipaji washenzi tuuu
Mvuvi: ndugu biashara haikuwa nzuri naomba utuvumilie kwa Leo
MJOMBA SELE: niwavumilie Mara ngapi mbwa nyinyi KAZI kunywa pombe na kutumia na wanawake Mimi hamtaki kunilipa
Mvuvi wa pili: basi ndugu nakuhaidi Mimi kesho ndo uchukue hela yako wala hamna tabu.
MJOMBA SELE: sawa kwa heshima yako tu nakwenda kesho mkiiona sura hii mjue tutaonana wabaya
Mvuvi: wewe kesho njoo usijali
MJOMBA SELE: sawa mi naenda tutaonana kesho *************TUKUTANE SEHEMU INAYOFUATA*********BY MELI YA MGIRIKIView attachment 2348432
 
STORY:JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Tumeishia pale ambapo SHABAN anamuonesha mjomba yake yule JINI ZUNAIDAH ambae akipita nyuma ya mgobgo wa mjomba yake.........SONGA NAYO.....
SHABAN: khaaaaa! Mjombaaaaa!
MJOMBA SELE: nini wewe mbona unapiga kelele?
SHABAN: mjomba nimemuona tena yule JINI
MJOMBA SELE: umemuona wapi?
SHABAN: kapita sasa hivi nyuma yako
MJOMBA SELE: sasa kaenda wap? (Akiangaza macho)
SHABAN: sijui ila kapita. (Kwahofu)
MJOMBA SELE: hebu nenda nyumbani Mimi acha niende sokoni nikakusanye hivyo vitu vya kupika.
SHABAN: sawa uncle
Baada ya kuambiwa hivyo SHABAN alimuacha mjomba yake akienda sokoni na yeye akielekea nyumbani.
**************************************************
Akiwa njiani anaelekea nyumbani hajui hili wala lile ghafla njiani alikutana na msichana ambae hakuweza kumtambua kwa nataka......
ZUNAIDAH: mambo mkaka?
SHABAN: poa dada !
ZUNAIDAH: sheby unanikumbuka my dia? ( huku akiachia tabasamu)
Ile sauti ilimstua SHABAN na kumfanya astuke na kunyanyua USO wake kumtazama MTU aliyemsalimia na kumuita jina lake......lahaula hakuamini macho yake alipoiiona sura ya binti wa kijini ZUNAIDAH.....
SHABAN: wewe nani? Na u unataka nini?
ZUNAIDAH: sheby mpenzi usijifanye umenisahau wakati tushaonana si chini ya Mara 3.
SHABAN: unataka nini mbona unaninyima raha?
ZUNAIDAH: Mimi nakunyima raha au wewe unajinyima mwenyewe? Hebu nisikilize sheby mapenzi yangu kwako ndo yananifanya nikufatilie nakupenda saana.
SHABAN: Mi...mi sik....up....endi ( kwa sauti ya uwoga)
ZUNAIDAH: hahahaha sheby huwezi kunikwepa na nakuhaidi utanioa tu.
SHABAN: siwezi kuoa mwanamke shetani kama wewe..
ZUNAIDAH: shabani chunga mdomo wako usinifanye nikasirike! Huo ubishi wako utakuponza
SHABAN: utanifanya nini? Unanitisha au? Niue basi kuliko kuninyima raha
ZUNAIDAH: kufa utakufa lakini kwa mipango ya mungu bila ukiendelea kuwa mbishi cha moto utakiona...naenda bila baadae narudi kufata jibu langu
Pale pale akapotea machoni mwa SHABAN... Baada ya kutoweka ZUNAIDAH, SHABAN alichanganyikiwa mwisho akatimua mbio kwenda kwao.
*************"************************************
Tunarudi kwa mjomba SELE akiwa anatoka sokoni ghafla njiani akakutana na sheby...
MJOMBA SELE: we sheby unatoka wapi wakati nmekwambia nikukute nyumbani?
SHABAN: Dan MJOMBA bwana mi naenda kwa akina HAMISI Mara moja narudi sasa hivi
MJOMBA SELE: wewe mtoto unanishangaza saana hivi we una maisha ya kuigiza saaana siyo?
SHABAN: aaaah mjomba ushaanza misamiati yako mi naenda bhana..
MJOMBA SELE: kwa hiyo tunarudi mda gani?
SHABAN: jioni kidogo
MJOMBA SELE: na likikukuta usije kunisumbua shenzi wewe
**************************************************
Wakati MJOMBA SELE akiwa ametudi nyumbani alipata mstuko baada ya kumuona SHABAN yupo nyumbani..
MJOMBA SELE: we SHABAN? (Kwa mshtuko)
SHABAN kwa hofu alistuka na kumtazama mjomba wake...
MJOMBA SELE: umefika SAA ngapi?
SHABAN: mda tu mjomba
MJOMBA SELE: wewe si tumekutana sasa hivi umesema unaenda kwa HAMISI?
SHABAN: Mimi mjomba?
MJOMBA SELE: kumbe awe nani? (Kwa ukali)
SHABAN: mmmh mjomba kwa kweli mi sijatoka hapa
MJOMBA SELE: kama hujatoka yule nani? We sheby usinitanie ujue!
SHABAN: mjomba mi nahisi yule JINI kajibadilisha sababu nilikutana nae
MJOMBA SELE: unasemaaa!
SHABAN: ndio uncle
MJOMBA SELE: hivi inawezekanaje?
Mara mlango ukagongwa.......hodi..hodi....hodi....
MJOMBA SELE: nani?
Hakujibiwa kitu bila mlango uliendelea kugongwa....hodi....hodi...hodi...
MJOMBA SELE: naniiii wewe( kwa ukali)
Ndipo alipoenda kufungua mlango lakini cha ajabu hakuna MTU,alizunguka nyumba nzima huku na huko lakini hakuona mtu.
JE UNAFIKIRI NANI ALIYEKUWA ANAGONFA MLANGO?............USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY:JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA KUMI
Tumeishia katika ufalme wa ALBASH ambapo familia ya Mfalme BASHR wakiwa wanapanga mikakati ya ndoa ya kijana wao na binti mrembo zunaidah ambae ni BINAMU yake . Baada ya kukubaliana nini cha kufanya waliacha muda uchukue nafasi
**************************************************
Tunarudi kwenye ufame mwengine wa KASHKASH ambapo tunamuona Mfalme AMOUR na mkewe UMMUKURTHUM wakijadiliana maswala ya kifamilia....
AMOUR: umeongea na binti yako vizuri? UMMUKURTHUM:kiasi chake
AMOUR: si unajua hatuna mda!
UMMUKURTHUM: lakini lazima tumpe mda binti yetu wa kufikiria vizuri tusimlazimishe
AMOUR: hakuna mtu aliyemlazimisha ila lazima tulinde heshima yetu na ufalme wetu
UMMUKURTHUM: kwani hata kama ataolewa na binadamu heshima haitakuepo?
AMOUR:mama zuuh!!
UMMUKURTHUM: nimezungumza tu wala siyo wazo langu ni la zuuh kwhiyo usipandishe munkali baba eeeh!
AMOUR: yaani we mama zuuh na mwanao ajili zenu sawa sawa!
UMMUKURTHUM: eti nini?
AMOUR: nakutania tu mke wangu
UMMUKURTHUM: nashukuru ( huku akiondoka)
**************************************************
Tukirudi duniani huku tunakutana na MJOMBA SELE na SHABAN wakiwa wanarudi nyumbani kwao wakiwa wanatoka nyumbani kwa akina HAMISI...
MJOMBA SELE: unajua uncle mi nishakata tamaa kabisa
SHABAN: hunishindi Mimi uncle yaani mwili WOTE nahisi siyo wangu jinsi nlivyochoka
MJOMBA SELE: yaani hiki kibwengo kweli kimedhamiria maana siyo kwa taabu hizi
SHABAN: mjomba Mimi Nina wazo!
MJOMBA SELE: wazo gani tena mjomba?
SHABAN: twende kwa shehe tukapate kisomo
MJOMBA SELE: daah mjomba kama ulikwa kwenye ajili yangu mi naona tufanye mpango twende huko huenda tutafanikiwa.
SHABAN: sasa tutaenda lini uncle
MJOMBA SELE: nafikri tufanye kesho kutwa kwasababu kesho inabidi tuingie pwani kuvua.
SHABAN: poa tutaenda hiyo hiyo kesho kutwa
MJOMBA SELE: sasa jioni tunakula nini?
SHABAN: hata sijajua uncle labda tupike ugali samaki
MJOMBA SELE: siyo mbaya tutakula hata hicho
SHABAN: au siyo ngoja tukaanze kukusanya zaga.
Wakati wanaendelea kupiga story ghafla SHABAN alimuona mtu kama ZUNAIDAH akipita nyuma ya mjomba yake huku akiwa anatabasamu...
SHABAN:khaaaaa! Mjombaaaaaa!
..........JE NINI KITATOKEA......USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU WA KUSISIMUA...BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY:JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU. S. MWINYIMKUU
CONTACT:0719013038
MAHALI😀AR ES SALAAM
WHATSAPP:0719013038
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Baada ya kutoka njee na kukuta akuna mtu Ndipo alipo rudi ndani huku akiwa ana hofu kwakitendo cha kuto ona mtu
SHABANI mjomba vipi? Nini kinaendelea (kwa hofu)
MJOMBA SELE dah! Wee acha tu haya mauzauza mbona yamepamba moto mwaka huu (akishusha pumzi)
SHABANI inamana mjomba ujaona mtu yoyote!
MJOMBA SELE Mjomba sikutanii akuna CHOCHOTE nilicho kiona yani ata kuku ajaonekana
SHABANI sasa mjomba......!
hodiii....! hodii..! hodiii..!
SHABANI Mjomba unaisikia hiyo hodii?
MJOMBA SELE Hebu kaa kimya (akisikiliza kiumakini)

Hoya wee Sheby unazingua acha umama bhana fungua mlango bhana (Ilisikika SAUTI ya HAMISI)
SHABANI Mjomba mbona kama sauti ya hamisi hiyo?
MJOMBA SELE hata mimi nasikia SAUTI ya hamisi
SHABANI Hebu nenda kafungue mlanGo basi?
MJOMBA SELE kwanini usiende wewe?
SHABANI mjombaaa...............
MJOMBA SELE Nenda kafungue mlango mara ya kwanza niLienda mimi?
SHABANI Haya bhana (kiunyonGe huku akienda kufungua MilanGo baada ya kufungua mpango anakutana na HAMISI)
*******************************
*******************************
HAMISI Hoya wewe babu vipi mbona una gwaya yani kufungua mlango mara moja tu unalemba sana!
SHABANI dah...! Sorry mwanangu kuna mauzauza leo umu ndani ataliii
HAMISI Mauzauza gani wewe? Hebu acha uboya sikia mimi sijajua na stori hizo nimekufata twende zetu home kuna mtaalamu wamekuja sasa hivi amesema tatizo lako ataki shuqhuri kua
MJOMBA SELE HUyo mtaalamu katokea wapi? Mbona mama yako ajanipigia simu?
HAMISI Mjomba bhana! Hili jambo limekuja gafra Hivyo atuna muda wa kupoteza tunatakiwa tuondoke sasa hivi
MJOMBA SELE Basi naomba mnisubili nibadili nguo.
HAMISI Mjomba bwana utatukuta utatuchelewesha Hebu sheby tuondoke bhana.
SHABANI mjomba acha tutangulie bhana.
MJOMBA SELE poa tangulieni nitawakuta
*******************************
*******************************
TUNARUDI KWENYE UFALME WA KASH KASH AMBAPO MFALME AMOUR AKIWA METEMBELEWA NA SHEMEJI YAKE MFALME BASHR KUTOKA KATIKA FALME YA AL_BASHR
MFALME AMOUR karibu sana shemeji yangu jisikie uko nyumbani.
MFALME BASHR Asante sana shemeji yangu na nimefurahi kua hapa kwa mara nyengine tena.
MFALME AMOUR ha.! ha.! ha.! Kwani mara ya mwisho kuja hapa Kwenye ufalme wangu ni lini (aKiuliza kiutani)
MFALME BASHR Nakumbuka toka nilipo msindikiza dada yangu baada ya ndoa yenu (akitani)
MFALME AMOUR Hebu acha utani wako bwana leta maneno ya busara
MFALME BASHR bwana mzee mwezanGu kilicho nileta hapa ni jambo la Kheri tu.
MFALME AMOUR Kheri gani hiyo tena mbona unanitamanisha kujua zaidi
MFALME BASHR SWALA la ndoa.
MFALME AMOUR ndoa? Ndoa ya nani tena? Au Unataka kuongeza mke wa pili?
MFALME BASHR Hapana ni kijana wangu YUKTY anataka kuposa katika uFALME huu
MFALME AMOUR Unamaaanisha kijana wako yukty anataka kumpa binti yangu ZUNAIDAH?
JE nini kitaendelea.... Usikose kufatilia.... Mkasa huu wa kusisimua.... By Meli ya mGiriki
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Tunaanzia pale tulipoishia ambapo MJOMBA SELE na mama HAMISI wakiwa wanazidi kuchanganyikiwa bila kujua wafanye nini ndipo wakashauriana kwenda kumtafuta
MAMA: sijui labda tutamfute lakini tutamtafutia wapi?
MJOMBA SELE: hebu twende tutajua huko huko mbele ya safari.
Huku wakinyanyuka na kutoka nje.
MAMA: eeeh bwana wewe hebu ni subiri nifunge mlango wangu.
MJOMBA SELE: hebu Fanya haraka mwenzio nimechanganyikiwa !
MAMA: sasa we ukic hang any ikiwa na Mimi nisemeje? Punguza jazba tujue tunaanzia wapi!
Baada ya kutoka nyumbani kwa mama HAMISI wakaanza kuzunguka kumtafuta ili wajue ameenda wapi lakini jibu walilokutana nalo halikuwaridhisha kwani walienda mpa ka kwenye vijiwe anavyopendelea kwenda waliambulia patupu.
MAMA: mi naona tukatoe taarifa polisi!
MJOMBA SELE: nini? Huko ndo utaharibu kabisaa we umeona wapi vita ya kuku na nyoka anaamulia binadamu?
MAMA: sasa kumbe tufanye je
MJOMBA SELE: hebu rudi kapumzike kwanza na Mimi niende nyumbani mpaka kesho nipate akili nyengine!
MAMA: simu yake umempigia ?
MJOMBA SELE: hapatikani we nenda mwengine tutaongea kesho!
MAMA: sawa ila lolote likitokea naomba tujulishane.
MJOMBA SELE: hamna shida.
**************************************************
Tunarudi upande ambao yupo ZUNAIDAH na SHABAN waliendelea na safari yao isiyokuwa na muelekeo kwa SHABAN mpaka wakafika kwenye jengo moja zuuuri.
SHABAN hakuamini kufika sehemu kama ile aliona kama anaota machni mwake au yupo usingizini anaota kwani Mara kwa Mara alijaribu kufikicha macho yake na kujifinya kama anaota akurupuke kutokana na maumivu anayoyasikia.
ZUNAIDAH: sheby mpenzi karibu nyumbani kwangu! (Akiachia tabasamu mwanana)
SHABAN: asa...nte...I...la...ha..pa...ni wapi?
ZUNAIDAH:mbona kama hujiamini? Hebu twende ndani ( akimvuta mkono)
Kiukweli Sheby mtoto wa kitaa toka azaliwe hakuwahi kufika sehemu nzuri kama hiyo kwani kwake ilikuwa ngekewa kufika eneo hilo.
ZUNAIDAH: sheby!
SHABAN: naam! (Kwa upole)
ZUNAIDAH: bado unaniogopa mpenzi?
SHABAN: hapana sikuogopi!
ZUNAIDAH: nafurahi kusikia hivyo! Na vipi kuhusu ombi langu la kuwa mume wangu?
SHABAN: ni..ni..nime..Ku..ba..li
ZUNAIDAH: mbona kigugumizi? Jibu kama mwanaume basi! ( akijidekeza)
SHABAN: nimekubali
ZUNAIDAH: woow! Nafurahi kusikia hivyo na nakuhaidi nabadilisha maisha yako, sheby huyo atakuwa tajiri ataishi vizuri na hatofkiria shida zaidi ya kuzunguka na magari majini na kila MTU atakujua wewe nani! Ila tu kwa sharti
SHABAN: sharti lipi hilo?
ZUNAIDAH: sitaki unywe pombe, ufanye uzinifu wala kucheza kamali Upo tayari?
SHABAN: je vipi nikitaka kuoa?
ZUNAIDAH: utanioa Mimi
SHABAN: noo! Inabidi nioe binadamu mwenzangu ili niwe na familia yangu
ZUNAIDAH: kwani Mimi siwezi kukuletea familia?
SHABAN hakujibu kitu alikaa kimya
ZUNAIDAH: sawa najua binadamu mnaroho za tamaa saana siwezi kulikwepa hilo, kuoa utaoa lakini mke ntakuchagulia Mimi
SHABAN: khaaa! Mbona unaninyima Uhuru?
ZUNAIDAH: sikunyimi Uhuru ila nakulinda na najilinda mwenyewe.
SHABAN: kivipi?
ZUNAIDAH: mda ukifika unajua,pia Leo hutorudi nyumbani tutakua pamoja hapa!
SHABAN: hapana mjomba atakuwa na wasiwasi
ZUNAIDAH: nimeshampumbaza usijali! Utarudi kesho
**************************************************
Tukirudi upande wa falme ya KASH KASH ambp tunamuona Mfalme AMOUR akiwa ana jadili na mkewe kuhusiana na binti yao.
Mfalme AMOUR alikuwa analalamika kuhusiana na mkewe kushindwa kucheza na akili za mwanae ZUNAIDAH ambapo mpaka leo hajatoa jibu lolote kuhusiana na kukubali kuolewa na BINAMU yake YUKTY kijana kutoka Falme ya ALBASHR.
Mfalme: mama ZUNAIDAH nimechoka kusubiri nini kinaendelea mpaka sasa?
UMMUKURTHUM: Hebu vuta subra kidogo mumewe wangu
Mfalme AMOUR: hapana siwezi kupoteza muda zaidi nahitaji ZUNAIDAH aolewe na YUKTY!
UMMUKURTHUM: lakini hampendi
Mfalme AMOUR: sitojali anampenda au hampendi lazima aolewe na YUKTY
UMMUKURTHUM: hivi kwa nini unamchagulia mtoto mwanaume wa kumuona? We mbona hujawahi kuchaguliwa? Inamaana hukumbuki ulivyokuwa unanivizia Kyle maktaba unajifanya kuja kusoma vitabu wakati wewe umezoea kushika mapanga?
Mfalme AMOUR: sihitaji kukumbuka ya zamani! Kwanza hayo hayahusiani na sasa!
UMMUKURTHUM: sawa lakini mchumba uliyechaguliwa na wazazi wako ulimuoa?
Hapo Mfalme alishikwa na kigugumizi kisha akajikaza
Mfalme AMOUR: naomba usinikumbushe mambo ya zamani
UMMUKURTHUM: nijibu swali langu
Mfalme AMOUR: naomba tulizungumze baadae!
Alinyanyuka na kuingia ofisini kwake.
UMMUKURTHUM: ntakunyoosha tu ( alijisemea)
**************************************************
Ikiwa ni siku nyengine ambapo kumekucha tunamuona MJOMBA SELE akiwa anajiandaa kutoka kwenda kwenye mizunguko ya kumtafuta sheby Mara ghafla ugeni...
SHABAN: shkamoo mjomba
MJOMBA SELE: khaaaa! Wewe ulikuwa wapi mjomba? (Kwa mshangao)
SHABAN: hamna mjomba nilikuwa kwa kina hamisi nikaona usiku umeingia ndomana nikalala huko huko!
MJOMBA SELE: sheby staki uongo, Jana mama HAMISI nilikuwa nazunguka nae kukutafuta wewe na hukuwepo Kule, naomba nijibu ulikuwa wapi?
SHABAN: mjomba umesahau kama niliondoka na HAMISI? Na akakwambia kuna mtaalamu ananihitaji hivyo niwahi na wewe tukakubaliana utatukuta umesahau?
MJOMBA SELE: sawa na hiyo Pete ya dhahsbu umeitoa wapi?
SHABAN akaanza kuumauma meno... Aaaah mjomba bhana hii nimeokota
MJOMBA SELE: wapi?
SHABAN: njiani! Kwani unadhani nimeiba?
MJOMBA SELE: mmmmh! We mjomba yangu kweli? Hebu nisubiri nakuja sasa hivi usitoke sawa?
SHABAN: mi nipo!
JE NINI KITATOKEA ......UNAFIKIRI MJOMBA ANAENDA WAPI?.....USIKOSE KUFATILIA KISA HIKI CHA KUSISIMUA.......BY MELI YA MGIRIKI....
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU. S. MWINYIMKUU
CONTACT:0719013038
MAHALI😀AR ES SALAAM
WHATSAPP:0719013038
SEHEMU YA KUMI NA TATU
Tuna anzia pale tulipo ishia ambapo wafalmee wanaongea
MFALME AMOUR Unamaanisha yukty anataka kumuo bint yangu yangu ZUNAIDAH
MFALME BASHR swadakta mzee mwezanGu kijana wangu anampenda SANA bint yako hivyo nimeona bora tuje tuongee mimi na wewe MKUBWA mwezanGu
MFALME AMOUR Lakini yukty amekwisha ongea na ZUNAIDAH
MFALME BASHR mhhhh! KwakweLi mzee mwezanGu awajawahi KUONGEA ila tuliitaji kutumia busara na sheria zetu ili wasije kuzini.
MFALME AMOUR iLa sawa nimekuelewa iLa..
MFALME BASHR iLa nini tena mzee mwezanGu mbona mambo yapo wazi tu
MFALME AMOUR Ebu tupe muda wakufikiria tuta kujibu.
MFALME BASHR Sawa hilo nazani alina tabu. Tuta subiri mpaka mtakapo pata jibu LA kutupayia kwani mambo mazuri ayaitaji haraka. Kwaiyo tuna tarajia jibu zuri...
MFALME AMOUR mhhhh! Sharapat tarito ( Hebu tuombe munGu
*********************************
*********************************
Tunarudi upande mwengine ambapo tunamuona HAMIS na SHABANI
SHABANI mmmh mbona huku siyo kwenu? Unanipeleka wapi hamisi
HAMISI Kwani uniamini au? (Akacheka) ( mara gafra akageuka na kua JINI zunahidah)
SHABANI khaa wewe ! (kwa mshituko)
JINI ZUNAIDAH Vipi kwani uhamini unacho kiona au? haya haaaa haaaa haaaa nilikuambia Uwezi kunikimbia umeona sasa?
SHABANI Unataka nini wewe mbona unani fata fata unatakanini?
JINI ZUNAIDAH Nakutakia wewe Unataka Nikwambie mara ngapi?
SHABANI kwani majini wenzio hakuna?
JINI ZUNAIDA Hiyo jeuri yako itakuponza' na ukiendelea na ubishi WAKO nitakugeuza kuku wakuchinje au uliwe na mwewe
SHABANI potelea mbali?
JINI ZUNAIDAH Unajidanganya Sheby unachakufanya na usijidanganye kwenda kwa mganga akuna mganga yoyote ATAKAE kusaidia
SHABANI Sawa niambie Unataka nini?
JINI ZUNAIDAH Unataka kujua NATAKA nini? ah ah ah ha mbona unanijua ninachotaka sheby unajua wazi NakuPenda kwanini unaniTesa lakini
SHABANI Kwaiyo shida yako ni mapenz tu?
JINI ZUNAIDAH naitaji uwe mume wangu wa ndoa
SHABANI Nikikukubalia Uwezi kuniua? Mana nasikia majini mnakunywa damu za binadamu
JINI ZUNAIDAH Siwezi kumua mtu ninaempenda ata mara moja
SHABANI sitaki uitese familia yangu wala kuidhuru
JINI ZUNAIDAH Usiwe na wasi wasi ila naomba usinGizi kwenda kwa mganga na ukinifatilia utakuta ni Kheri ufate matakwa yangu Nitayabadilisha maisha yako utakua mtu maharufu na tajiri kAfika ulimwengu huu je upo teyari kuwa na mimi?
SHABANI Ndiyo bila shaka
JINI ZUNAIDAH Woooow nimefurahi SANA kusikia hivyo ila naomba tutoke twende sehem nzurii.
SHABANI Wapi? (kwa unyonGe)
JINI ZUNAIDAH usiwe na wasi wasi nikumbatie
SHABANI sawa
PALE PALE ALIMKUMBATIA NA WAKAPOTEA PALE PALE
*********************************
*********************************
TUNARUDI UPANDE WA PILI NYUMBANI KWA MAMA HAMISI' TUNAMUONA MJOMBA SELE AKIWA ANA WASILI HARAKA HARAKA
MAMA Kwani wewe vipi mbona unaharaka hivyo unawahi wapi!?
MJOMBA SELE khaa! Yani Mguu huu unakuja hapa kwako
MAMA ndo kwa speed hiyo? Haya niambie
MJOMBA SELE huyo mganga Kashaondoka
MAMA Mganga yupi tena? ( akishaangaa)
MJOMBA SELE mama hamis ebu acha masikhara basi ujuhe hamis kaja kumfata SHABANI nyumbani aje nae hapa etii kuna mtaaramu kaja anataka kumtibia
MAMA HAmis kaja kumchukua SHABANI? MBona mpya? Ujue hamis ajatoka leo tangu asubuhi anajisikia vibaya!
MJOMBA SELE ajatoka wakati nimemuona kwa macho yangu kaja nyumbani! Aaah haya masihara mama hamis
MAMA sasa mimi nikutanie wewe! Ebu subiri (akifikiria) isiwe huyo JINI kaja kwa sura ya mwananGu kumchukua SHABANI
MJOMBA SELE hiyo inawezekana je? Hinamana kajibadIKISHA
MAMA Inawezekana mana majini wanauwezo wa kujibadilisha hata ngombe kuku wakati mwengine hata gari
MJOMBA SELE sasa hatakua kampeleka wapi?
MAMA sijuhi labda tumtafute. Na hata hivyo tutamtafutia wapi?
**********************************
**********************************
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
SEHEMU YA KUMI NA SABA
Tunaanzia pale tulipoishia baada ya ZUNAIDAH kutamka maneno ya kutisha mbele ya HAMISI na SHABAN na kuwa acha wasielewe nini cha kufanya.....SONGA nayo....
Baada ya kuzungumza maneno Yale ZUNAIDAH alipotea pale pale na kuwafanya SHABAN na HAMISI kuduwaa kama awaamini walichokiona wakidhani movie!
SHABAN: hivi Huyu mwanamke ana nini mbona ghafla tu kabadilika?
HAMISI: baada ya Mimi nikuulize wewe ,wewe unajiuliza mwenyewe mimi nimuulize nani?
SHABAN: hebu acha makorokocho yako bwana!
HAMISI: makorokocho? Mi naongea makorokocho?
SHABAN akafikiri kwa kina kisha akamwambia hamisi.....mjomba umekutana nae wakati unatoka kwenu?
HAMISI: hapana vipi kwani?
SHABAN: mjomba atakuwa amekuja kwenu na kumchukua mama yako kwenda kwa mganga sasa nahisi ZUNAIDAH amejua mlango hivyo ngoja nipige simu..
Baada ya kuitafuta namba ya mjomba wake kwa muda akaipiga haikuchukua muda ikapokelewa ........
....hallo....
Eeeh hallooo! Mjomba!
...unasemaje SHABAN?
....mjomba Upo na mama HAMISI?
....ndiyo..kwani vipi?
....mnaenda kwa mganga...?
...we umejuaje?
...haraka saana rudini nyumbani msitafute matatizo...kisha akakata simu.
....hallo....hallo.... Dash kakata simu!
MAMA:Nani huyo?
MJOMBA SELE: sheby huyu sijui kajuaje kama tunaenda kwa mganga!
MAMA: amejua?
MJOMBA SELE: sijui tena kasema tukikaidi tutapata matatizo!
MAMA: mmmh matatizo tena? Kurudi mwenzangu!
Baada ya kushauriana kwa muda wakakubaliana kurudi nyumbani lakini waliongozana mpaka nyumbani kwa MJOMBA SELE WOTE wawili na kuwakuta sheby na hamisi wakiwa wamekaa kwa makini kama wanatathimini jambo Fulani
**************************************************
Hamisi alikuwa wa kwanza kumuona mama yake hivyo alijikuta akiita kwa sauti ....mama..!
Ndipo sheby akanyanyua kichwa na kumuona MJOMBA yake akiingia ndani na kuketi katika kitu
MJOMBA SELE: hivi sheby nini kinaendelea mbona sielewi?
SHABAN: has a mjomba huelewi nini?
MJOMBA SELE: hivi sheby umejuaje kama sisi tuna kwenda kwa mganga?
SHABAN: mi nilivyokuona umetoka asubuhi kama u mechang any ikiwa hivi nikajua lazima umfate mama hamisi muende kwa mganga kujua tatizo bila mjomba nataka nikutoe hofu mi sina tatizo sasa hivi wala usisumbuke!
MAMA: huna tatizo wakati toka Jana umeondoka hujarudi arafu unasema huna tatizo? Kwanza hiyo Pete umeitoa wapi?
SHABAN: nimeokota
MJOMBA SELE: muongo Mkubwa we! Hivi ungeokota ungeivaa hiyo si ungeenda kuiuza!
MAMA: tena ya dhahabu hiyo
SHABAN: nimeshasema nimeokota mnataka nisemeje nimeiba au? Mbona hamisi anajua !
MJOMBA SELE: eti hamisi ya kweli hayo?
HAMISI: ndiyo mjomba!
MJOMBA SELE: Mimi siamini hebu ngoja!
Alimsogelea sheby na kumvuta mkono aliovaa ile Pete na kuishika kisha kutoka kuivua Mara Pete ika piga shot na kumfanya MJOMBA SELE ashangae kama asiamini kilichotokea..
Lakini akukata tamaa akajaribu tena kuivuta ndipo akaanza kuna vitu vilivyikuwa vinamsumbua sheby toka siku ya kwanza Kyle pwani alipokutana na JINI ZUNAIDAH mpaka akajifanya HAMISI NA kuondoka nae mpaka akaingia mkataba na JINI huyo .
Baada ya maono hayo akaanza kumuona ufalme wa KASH KASH anapotokea binti hiyo na familia yake kiujumla na ufalme wa ALBASHR ambao anatoka mama yake baada ya maono hayo akamuona ZUNAIDAH akiwa amevaa vazi LA malkia na akiwa ameketi katika kitu chake cha heshma..kisha akamwambia...
......karibu baba mkwe naona umekuja kunitembelea......
MJOMBA SELE: wewe ni nani (kwa hofu...)
....naitwa ZUNAIDAH binti AMOUR natoka kwenye falme ya KASH KASH pia nimechanganya na falme ya ALBASHR na ni mkwe wako mtarajiwa kwani mke mtarajiwa wa sheby.
.....naona unashangaa kumuona hapa....tatizo lako unapenda kufatilia vitu usivyotakiw kujua.......hivyo basi nakuonya wewe na yule mwanamke unaejipendekeza kwake .....mkiendelea kunifatilia....mtakiona cha moto.... Na sitawasamehe, hahahahahahaha, ha!ha!ha!ha!ha!
Kicheko cha kifedhuli kilichofatia ambacho kilimrudisha kimawazo duniani MJOMBA SELE jasho likimtoka!
Watu wote walikuwa wanashangaa kwani muda WOTE huo MJOMBA SELE walimuona ameganda kwa hofu akiwa azungumzi zaidi ya nusu saa hivyo alivyokurupuka kila MTU alishtuka.
JE MJOMBA SELE ATASEMA ALICHOKIONA? NA NINI HATMA YA PENZI LA ZUNAIDAH NA SHABAN USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DAR ES SALAAM
SEHEMU YA KUMI NA TANO
Tunarudi upande wa Falme ya ALBASHR ambapo tunamuona YUKTY akiwa anazungumza na mama yake...
MAMA YUKTY: mwanangu nimekuita hapa ili tujadili mambo kadha wa kadha
YUKTY: mama bwana mambo gani tena hayo?
MAMA YUKTY: ya kawaida tu mwanangu hebu sogea karibu kwanza.
Baada ya kusogea karibu kwa mama yake!
MAMA YUKTY: mwanangu hivi huna binti yoyote unaempenda zaidi ya binti Mfalme ZUNAIDAH?
YUKTY: daah mama bwana kwa nini unasema hivyo?
MAMA YUKTY:nimekuuliza tu mwanangu maana nyinyi vijana bwana.
YUKTY: mama mi sijaona msichana yoyote zaidi ya ZUNAIDAH nampenda saana mama na moyoni mwangu hakuna kama yeye.
MAMA YUKTY: sawa mwanangu ila nahisi ZUNAIDAH kuna MTU anampenda japo sina uhakika.
YUKTY: mama unathubutu vipi kuniambia hayo?
MAMA YUKTY: sina maana hiyo mwanangu ila ukweli ni kwamba ZUNAIDAH hakauki na safari za duniani na nasikia kuna kijana huko duniani anampagawisha binti yule.
YUKTY: si to g**CH sho fe! (Haiwezekani)
MAMA YUKTY: sho GI ko pash! (Tulia mwanangu)
YUKTY: opotevishevi pash lash navo poh!( siwezi kukubali ntapambana)
MAMA YUKTY: usiwe na haraka baba taratibu taratibu!
YUKTY: pash eeh! To to ti (mama niache peke yangu) huku akiondoka.
**************************************************
Tunarudi upande mwingine wa duniani ambapo tunamuona Sheby akiwa yupo sokoni ananunua zaga za kwenda kupika nyumbani.
Baada ya kununua mahitaji yote akiwa anarudi nyumbani anakutana na HAMISI
SHABAN: haya nambie hivi wewe mwenyewe au Copy?
HAMISI: aaaah kwa nini mzee?
SHABAN: we nijibu kwanza!
HAMISI: sawa Mimi ulijino.
SHABAN: una uhakika?
HAMISI: huniamini kaka? Au unajua JINI lako?
SHABAN: wee usimtaje usije ukamuita bure!
HAMISI: akija nakuachia msala wako
SHABAN: thubutuuuu unaweza kumkimbia? Yaani hufiki hata kwa majemba pale gengeni.
HAMISI: mmmh haya asije akanifata bure bila mwambie aache kuja kwa sura yangu atakufanya uniogope!
SHABAN: je akija kwa sura yangu arafu akikufata wewe! Wee na urafiki navunja!
SHABAN: hahahaha acha uwoga wewe ! Unaelekea wapi?
HAMISI: nilikuwa nakuja kwenu!
SHABAN: poa twende zetu
**************************************************
Tunarudi upande wa mama HAMISI akiwa na MJOMBA SELE wakiwa wanajadili mambo ya SHABAN..
MAMA: unajua maisha ya mpwa wako siyaelewi! Yaani toka arudi nyumbani siku ya pili kabadilika kabisa haogopi anafurahi hivi nini kinaendelea maana sielewi mnanichanganya?
MJOMBA SELE: hata Mimi sielewi kwa kweli yaani haogopi kama mwanzo wala hata vitisho sivisikii tena, sijui ana siri gani?
MAMA: kwa nini usimuulize? We si mpwao yule mbona inakuwa hivyo mjinga au unamuogopa?
MJOMBA SELE: hayo matusi sasa Mimi namuogopaje mpwa wangu siwezi kumuogopa
MAMA: kumbe unashindwa nini kumbana akakwambia alikuwa wapi mpaka anarudi siku ya pili?
MJOMBA SELE: siyo kama nashindwa amekuja na mambo mapya yaani nashindwa nianzie wapi!
MAMA: mapya gani tena? Mbona unanitisha?
MJOMBA SELE: sheby amerudi na Pete ya ajabu.
MAMA: Pete ya ajabu? Mbona mapya!
MJOMBA SELE: siyo Pete tu sheby sasa hivi kawa mcharo vichenji avimpigi chenga na sijui anavipata wapi na siku mbili hizi hatujaenda pwani.
MAMA: mmmh mapya haya.
**************************************************Tunarudi upande wa akina sheby na hamisi wakiwa wamefika nyumbani kwa akina sheby...
HAMISI: hivi sheby hiyo pesa ya kununulia vitu vyote hivyo umepata wapi?
SHABAN: aaaah hebu acha maswali yako subiri nipike ule.
HAMISI: Mimi ni rafiki yako hebu funguka bwana au tunafichana Mimi na wewe?
SHABAN: unataka kujua siyo?
HAMISI: na ndomana nikauliza kwasababu nataka kujua.
SHABAN: OK kanipa SHEMEJI yako.
HAMISI: ZUNAIDAH?
SHABAN: yap!
HAMISI: kwa hiyo menyu ya Leo ina muhusu?
SHABAN: yah
HAMISI: sasa mbona una pika wewe kwanini asije kupika yeye tukala chakula cha shemeji?
SHABAN: unahitaji aje kupika?
HAMISI: jibu hilo (akijiachia kwenye kochi)
SHABAN: sawa ZUNAIDAH!! (Akiita)
Mara sauti ikajibu ......abee!..Pale pale HAMISI akakurupuka kutoka kwenye kochi na kukaa kitako....mzaha mzaha hutumbua usaha.....JE NINI KITAENDELEA USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT: 0719013038
WHATSAPP: 0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA TISA
Baada ya jini ZUNAIDAH kumtishia amani mganga wa kienyeji kutoka tanga alitoweka na kumuacha mganga asijue cha kufanya......SONGA NAYO......
MGANGA: yaani jini yule anauwezo wa kuingia nyumbani kwangu bila kudhulika? Jini wa haina gani yule, mbona haijawahi kutokea miaka yote toka nianze Kazi yangu ya uganga kuja kutishwa na JINI katika himaya yangu? Nuksi gani hili hebu ngoja niwapigie simu.....( baada ya muda akawa anaongea na simu mpaka ikakata) siwezi kwenda kutengeneza vita na majini kizembe nawarudishia nauli yao wamtafute mtaalamu mwengine.
**************************************************
MJOMBA SELE na SHABAN walifika kwa akina HAMISI mchana na kuwakuta wakiwa wanaandaa chakula hivyo walijumuika kula kwa pamoja...baada ya muda walikuwa washamaliza na mazungumzo yakaanza....
MAMA: yaani afadhali mlivyokuja mapema maana kuna mapya yamezuka!
MJOMBA SELE: yapi tena hayo?
MAMA: yule jini si kwenda Tanga kwenda kumtisha mtaalamu.
WOTE: eeeeeeeeeh!
MAMA: hivyo hapa kanipigia simu kanieleza kila kitu pia kanirudishia ile pesa tuliyomtumia kwa ajili ya nauli.
MJOMBA SELE: daah mbona balaa tena hili sijui tufanyaje?
MAMA: na kwa ushauri tu alionipa kasema mtu yeyote atakae thubutu kuingilia mahusiano haya cha moto atakiona kwasababu huyu JINI ana nguvu saaana na wala siyo mbaya
MJOMBA SELE: awe mbaya asiwe mbaya we umeona wapi jini kaishi na binadamu?
HAMISI: kwa hiyo turafanyaje MJOMBA?
MJOMBA SELE: hapa kukaza msuli tu mwanzo mwisho mpaka kieleweke
SHABAN: Mimi sielewi hata nifanyaje
MAMA: usijali mwanangu ndo mitihani hiyo ya dunia
SHABAN: mama yangu imezidi mpaka vibwengo?
HAMISI: usijali ndugu tutapata solution tatizo litakwisha kabisaaa!
SHABAN: haya tuombe mungu
**************************************************
Tunarudi ujinini kwenye ufalme ALBASH hapa tunamuona mama baba na mtoto
YUKTY: baba toka ulivyoniambia swala LA kuoa naona hujanigusia chochote kuhusiana na ZUNAIDAH!
BASHR: ni kweli mwanangu hatujazungumza chochote na hii kutokana na zunaidah kuomba mda wa kufikiria kwa wazazi wake juu ya ombi letu
MAMA: na kwa kukutoa shaka mwanangu zunaidah lazima awe mkeo
YUKTY: hahah ntafurahi saana mama kwasababu nampenda hakuna mfano.
BASHR: tunalijua hilo kwa hiyo tulia tufanye mpango mambo yanyooke!
YUKTY: Mimi sina presha baba nawasikiliza ninyi tu
MAMA: basi toa shaka juu ya hilo kabisa
YUKTY: hahah nawategemea saana na najivunia kuwa na wazazi kama nyinyi.
Kwa pamoja walikuwa wanafurahi na kumpa moto kijana wao kuhusu kumpata binti ZUNAIDAH ili afunge nae ndoa awe mkewe.
..............NINI KITAKACHOJIRI SEHEMU YA KUMI KATIKA MKASA HUU WA KUSISIMUA........
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY: JINI ZUNAIDAH
MTUNZI: HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT:0719013038
WHATSAPP:0719013038
MAHALI: DARES SALAAM
SEHEMU YA KUMINANANE
Tunaanzia paletulipoishia ambapo MJOMBA SELE alikurupuka kutoka kwenye Yale maono na kujikuta anahema kwa kufo huku kijasho chembamba kiki mtoka...songa nayo...
MAMA: vipi ndugu mbona hivyo?
HAMISI: mjomba vipi umeona nini Mwana uliganda tu huzungumzi wala nini?
MJOMBA SELE: Jamani nyie acheni tu hili swala kuanzia leo tuliache kama lilivyo
MAMA: bado sijakuelewa! Tuliache kivipi?
MJOMBA SELE: mama hamisi usitake kupata matatizo nimekwambia huli swala tuliache kama lilivyo, Mimi mwenyew nilichokiona hakifai kusimuliwa, hivyo basi tuliache na tu siliax ngu mzima kwasababu tumeprwa onyo Mimi na wewe kwaiyo tukae mbali kabisaaa!
MAMA: hilo onyo katupa nani?
MJOMBA SELE: ZUNAIDAH
MAMA:ZUNAIDAH ndio nani? Au bado Huyo jini?

MJOMBA SELE: Tafadhali usimtaje asije akaja hapa tens naomba muende nyumbani
MAMA: mmmh sawa we HAMISI hata twende nyumbani
Walitoka na kuwaacha shaban na HAMISI wakiwa wanawasindikiza na macho wakati wanatoka nje.
Baada ya kutoka mjomba SELE akaanzisha maongezi.
MJOMBA SELE: hivi sheby hii kitu IPO serious kweli?
SHABAN:ndio mjomba
MJOMBA SELE: Daah hana madhara lakini?
SHABAN: wala hana madhara hivyo usijali mjomba
MJOMBA SELE: kwaiyo umekubali kumuoa?
SHABAN: eeh
MJOMBA SELE: utaishi nae wapi?
MJOMBA SELE: atanipa utajiri
MJOMBA SELE: we we we unamaana utakuwa tajiri?
(Kwa mstuko)
SHABAN: Ninikwani?
MJOMBA SELE: utajiriwa kishetani huo unapitea mda wowote uncle!
SHABAN: uncle bwana haiwezi kuwa hivyo bwana!
MJOMBA SELE: Una uhakika na unacho kisema?
SHABAN: Mjomba niamini wala usiwe na shaka!
MJOMBA SELE: sawa mjomba ila asijekutunyonya damu tu.
Huku akinyanyuka na kuingia nani kwake(chumbani) na kuacha jibu LA sheby likimfata nyuma......aaah! Mjomba.....unazingua.....akininyonya damu tampata wapi kama Mimi na mjomba kama wewe!
****************************************
Turudi upande wa Falme ya ALBASHR ambapo tunamuona mtoto wa mfalme BASHR akiwa anafikiria kwa kina na wimbi LA mawazo likiwa limemtawala.
Mara anakuja mama take na kuzungumza nae pamoja na kumpa moyo kwamba asiwe na moyo mdhaifu kwani yeye Ufalme wake unamtegemea na yeye ndiye mrithi wa ufalme huo hivyo hivyo hakutakiwa kuonesha udhaifu machoni mwa watu kisa mapenzi.
YUKTY anamtazama mama yake kwa huzuni kisha anamkumbatia na kujiona mwanayme asiye na lolote kama atamkosa ZUNAIDAH kwani ndio mwanamke ampendae.
Mbali na kuwa mtoto pekee wa mfalme pia ni jemedari mkuu katika jeshi LA ufalme LA Mfalme BASHR hivyo hakutakiwa kuwa mnyonge kama alivyoonekana machoni mwa mama yake kwani ni udhaifu mkubwa.
Alichotakiwa kufanya ni kuwa na subra tu.
YUKTY: mama kuna kitu nataka nikwambie..
JE YUKTY ATAMWAMBIA NINI MAMA YAKE.........USIKOSE KUFATILIA MKASA HUU WA KUSISIMUA.....BY MELI YA MGIRIKI
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
STORY : JINI ZUNAIDAH
MTUNZI:HAFIDHU MWINYIMKUU
CONTACT :0719013038
WHATSAPP : 0719013038
MAHALI😀AR ES SALAAM
EMAIL : hafidhushabani75@gmail.com
Tunaendelea pale tulipoishia ambapo mjomba sele ameenda kwa mama hamisi ili kueleza furaha aliyonayo... Songa nayo...
MJOMBA SELE : Yaani nimepata bonge la mama mkwe mwenzio nafaidije!
MAMA: mmh yaani nashindwa kukuelewa mwenzio huyo mkwe ni yupo? Kwa nani? Na unafaidi nini?
MJOMBA SELE : mkwe wangu kwa SHABAN ana uwezo wa kipesa basi mwanzo mwisho napombeka tu.. haha haha kwa raha zangu wala sigombwi teh teh teh!
MAMA : nashindwa kukuelewa mwezangu kwahiyo huyo mkwe anakupa wewe hela ya pombe?
MJOMBA SELE : ndiyo
MAMA: Bado hujanijibu SWALI langu lakini... huyo mkwe kwa nani?
MJOMBA SELE : Inamaana we hujui au? Si kwa sheby!
MAMA: hehehe! Usinichekeshe wewe huyo sheby Kakua lini?
MJOMBA SELE : kama huniamini sawa ila ukweli ndo huo.
MAMA : huyo binti asiyekuwa na kazi anatokea wapi na anaishi wapi?
MJOMBA SELE : aaah acha dharau mama hamisi bwana kwani sele ana mapungufu gani?
MAMA: haya basi kaa chini unieleze kwa kina.... Au umenuna?
MJOMBA SELE : utaniudhu bhana (huku akikaa)
**************************************************************
Tunarudi upande wa pili ambapo tunamuon ZUNAIDAH akiwa na YUKTY wakiwa wanazozana..
ZUNAIDAH :hivi kaka kwanini unanifatilia saana?
YUKTY: kukufatilia kivipi? Mbona sikuelewi Zuu?
ZUNAIDAH : sikia YUKTY mimi sikuhitaji wewe na kumbuka mimi ni dada yako siwezi kuolewa na wewe Katy!
YUKTY : Zuu hata kama wewe ni binamu yangu inaruhusiwa kukuoa na mimi NakuPenda saana na unajua hilo.
ZUNAIDAH : Lakini mimi sikupendi!
YUKTY : ZUNAIDAH hata kama hunipendi Si kuamua kunidharirisha na kwenda kumpenda binadamu... Hii.. Si... Sawa na..
ZUNAIDAH : haikuhusu kwanza kilichokufanya uende duniani kumtishia nani? Mimi sikupendi YUKTY kama wewe unanipenda niache huru na mtu nimpendae na siyo kumnyima amani
YUKTY :yule binadamu hatoishi kwa amani mpaka ukubali kuolewa na mimi na yeye aoe mwanadam mwenzie!
ZUNAIDAH : aroshooo! (Nyamaza) kama ukithubutu kumgusa hata nywele yake sitokuacha mzima utaingia vitani na mimi.
YUKTY : kumbuka mimi ni ndugu yako na mimi ni chimbuko lako na hupaswi Kupambana na mimi.
ZUNAIDAH : nalifahamu hilo kaka na ndomana nikakuonya usimsogelee nimpendae ni Kheri unique mimi nikiwa napambana na wewe.
YUKTY : lakini Zuu.....
ZUNAIDAH : letashruu (NIMEMALIZA)
Alipomaliza kusema hayo anaondoka zake na kumuacha YUKTY akipiga kelele za Hasira. Kumbe muda wote huo MFALME BASHR alikuwa kajificha mahali anashuhudia ugomvi huo.
**************************************************************
Tunarudi upande mwingine ambao anaonekana sheby akiwa anaendelea na shughuli zake za nyumbani mara wanakuja washikaji wa mtaani na kuanza kumuita........ Sheby.... Sheby... Hoya sheby... We sheby..
SHABAN: Hoya nani weweee!?
MSHIKAJI 1: Aaaah hunajifany hutujui muhuni wetu leo? Hebu toka nje bwana tuongee!
SHABAN : Poa wait dk sifuri basi!
MSHIKAJI 2: chap basi!
Baada ya kufanya kazi zake zote anatoka na kuwakuta masela wake wa vijiweni.
SHABAN :Mmmh nambieni maze!
WOTE: dah shwari
SHABAN : kuna habari gani?
MSHIKAJI 1:Mwanangu sikia unajua mzee baba sasa hivi hatukusomi wala nini?
SHABAN : Kivipi?
MSHIKAJI 1: umebadilika kabisa skani hutokei kazi tukija kukustua hutokei lakini unavimba mtaani na unatuzidi matumizi nini siri ya maFanikio yako?
SHABAN :Hebu acheni ujinga wenu bhana yaani hicho ndo kilichowaleta hapa au kuna kingine?
MSHIKAJI 2: sikia sheby wewe mwanetu we tupange tu maana kuna skendo mtaani zinavuma kuwa ndugu unaishi na kigagula sijuhi kibwengo..
SHABAN : hoya habari za kiboya sizifagilii kama vipi sepeni msiniharibie siku.
MSHIKAJI 2: sheby watu tumeachiwa ufundi na mababu zetu nishakuzoom na ntajua tu huenda UKAWA Chuma ulete Wewe
SHABAN : chunga kauli yako dogo usijifanye mjuaji?
MSHIKAJI 2: sisi tunaenda lakini kitaeleweka mshenzi wewe mtoto MdoGo unamiliki majini tutakuonesha bwege wewe.
Sheby akawaangalia kwa makini kisha anajua kuna vita itakuja mda Si mrefu.
Hivyo alitakiwa ajipange kwa vita hiyo isiyojulikana itaanza lini na itaisha lini.
JE NINI AMBACHO KITATOKEA? USIKOSE KUFATILIA SEHEMU INAYOFUATA.
FB_IMG_1662527186340.jpg
 
Back
Top Bottom