Story za kusadikika za Mombasa

Story za kusadikika za Mombasa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,520
Reaction score
830,054
Kutokana na story tulizokuwa tukisimuliwa udogoni kuhusiana na Mombasa kulinifanya niogope kabisa hilo eneo.... Tofauti na siku hizi ambapo dunia iko kiganjani miaka ile ya 70-80 upatikanaji wa habari haikuwa rahisi kama leo hii
Basi tulikuwa tukisimuliwa kuwa eti kule Mombasa epuka kabisa ofa! Yani kama wewe si mwenyeji utaona ni ukarimu wa kawaida lakini kumbe kuna tafsiri yake mbaya kabisa.... Nenda tu ushalipiwa ni sentence mbaya kabisa kwa wenyeji wa kule! Ama kunywa tu, kula tu, chukua tu ushalipiwa... ukiuliza nanani utaonyeshwa barobaro moja lenye msuli na midevu! Macho kodo
Story zingine ni zile za kutegeshewa chombo ujisaidie kubwa ili waichinguze bila wewe mwenyewe kujua.... Eti wanaangalia kama UMESHATUMIKA ama bado ni new brand! story nyingine ni zile za kupewa chakula ambacho kitasababisha tumbo lijae gesi na kusababisha kutoa gesi ukaa kwa sauti... Basi wao hutega ukutani chini ya dirisha wakisikilizia tune itakayotoka hapo
Hakika hizi story na nyingine nyingi zilinifanya niogope MNO kwenda Mombasa
Baadae kabisa ukubwani nilikuja kujua kumbe nyingi zilikuwa ni story tu kama zilivyo story nyingi za pwani za mwembe basha, mrembo mwenye miguu ya mnyama nknk.....!!!!
Nilikuja kwenda Mombasa mwaka 1998 lakini nikiwa nimejiandaa hasa kwa lolote!
Nimekumbuka hizi habari za Mombasa baada ya kusoma humu JF kuwa Kiba kapewa Range rover, nyumba na billion kadha baada ya show yake marekani.... Aliyempa ni meya wa jiji la Mombasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Range Rover na bilioni kadhaa???!!Huyo meya ana kipato gani aseee?Kipi kimemfurahisha kwa kiba hadi ampe zawadi nono kiasi hicho???!!Acha tu ziendelee kuwa hadithi za kusadikika
 
kulikuwa na hadithi ya mzamiaji meli kwenda ulaya bahati mbaya meli ilichelewa kuondoka dsm kwa zaidi ya wiki ilipoondoka ikaelekea mombasa ikatia nanga pale jamaa akajua tayari yuko ulaya ndipo mikasa ya ushalipiwa ilipomtokea.
 
Hahahahahahaaa namkimbuka mtu mmoja anaitwa juma bhalo aliimba yangu pete imenitoka aliimba kama analia alikua analilia peteisiyo ya dhahabu wala almasi lakini pete huyu mshenz aliwatisha sama mabarobaro wa dar na maeneo mengine kuiendea mombasa maana waliogopa story ambayo nahis pia ilitungwa ambayo ipo nyuma ya huu wimbo pete (kautafute uusikilize vizuri) inasemekana issa matona alienda mombasa kutokea zenj maana haya ni maeneo ya karib issa hakua mkali sana wa taarab enz za akina bhalo alionekana ni kama muimba kadumbak na disco chakacha bas alipojitambulisha anakuja kufanya onyesho la taarab mombasa juma akamfanyia huu mchezo kila alipoenda kula akipanda daladala mpaka alipoenda kulala akawa anaambiwa ushalipiwa wewe akitoa hela watu hawataki wansema tunepokea mara mbili yake issa akaogopa akasubiri bot ya usiku akarud zanzibar hapo akaimba nyimbo isemayo babu jinga inama ufikiri mali yako inaliwa akimwambia bhalo bhalo nae ndio akaimba wimbo wa pete
huku akilia akimaanisha aliikua anaililia pete ya matona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom