The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email
akidasiri@gmail.com
Contact 0658328596
MSIMU 3
Sehemu 10C: Wizi wa Benk
Tuendelee...
“ …ni sawa kwa sababu sio mbaya kujua na kuto kujua kubaya ni kufeli mpango, alafu kijana ni lazima utambue kuwa wakati mwengine mapenzi ni sehemu ya matatizo kwa watu wengi lakini kwa wakati mwengine ni sehemu ya kuleta faraja ok ni sawa wacha tuone itakavyokuwa…lakini kwa kuwa mmefika pahala ambapo nilikuwa nimepachelewesha basi ngoja niwajuze jambo moja muheshimiwa Samuel na Peter kwa uchache ni watu ambao tunaenda kuwachunguza in and out yao kwa sababu wamebeba shina la matatizo hii ni taarifa niliyonayo siku nyingi baada ya kurudi kazini” habari hiyo ilitokea kuwashangaza sana Salimu na Karimu wakabaki kutazamana. “Na wanakambi Ngome kubwa huko Lushoto” aliongea tena Komandoo Ochola akalamba midomo yake kisha akawatazama vijana wake kwa zamu.
“Habari za Meroda na timu yake ninazo pia ni wanawake mashujaa sana ila nilichelewa kujua kuwa wasichana hao mmpo karibu nao sana kiasi hicho na kwa kazi yetu kuwa karibu na watu kama hao ni sawa na kukaribia kumshinda adui, nashauri tuendelee kupambana na muendelee kuteka hisia zao na kucheza na udhaifu wao pia ili muweze kuwashinda wote na sio Meroda tu kwa sababu ninacho kiamini ni kuwa si rahisi wao kuwaamini nyinyi kwa asilimia zote muamini kuwa wao watakuwa wanataka kuwajua vizuri nyinyi na mahusiano yenu katika kesi hii ili imani yao iwe yenye kukamilika, na zaidi ni kuwa usikae mbali na Shalon kwa sababu ni sehemu ya kazi yetu” bwana Ochola alimaliza wazi alionekaan kukonga nyoyo za kina Salimu na kuwafanya waanze kutabasamu. “Mkuu unajua sijui nisemeje ila sikutegemea kama utalichukulia jambo hili kwa staili hii niliamini utatupatia adhabu kwa hili jambo la kukuficha…” kabla haja maliza Ochola akaingilia
“No nonoo noo hapana usiseme tena hivyo, ni sahihi mlichokifanya ni sehemu ya kazi pia sio maana kila kitu mniambie mimi noo ila tu lazima kuwe na sababu haimanishi kuwa hampo huru katika majukumu yenu hapana mnao uhuru ila mbaya ni ile kukaa na jambo na kukosa sababu ya msingi huu ni ubaya sawa” Ochola aliongea kwa mfululizo pasina kuweka kituo.
“Sawa mkuu tumekuelewa vyakutosha sana” Karimu aliongea huku akitingisha kichwa.
Basi waliendelea na mazungumzo ambayo asilimia kubwa yalielemea kwa kina Meroda na shughuli zao ambapo taarifa hizo hazikupishana na zile alizokuwa nazo Ochola baada ya kuhama katika habari za kina Meroda. Baada ya hapo walilizungumzia jambo la uvamizi wa benki namna lilivyo kaa na mipango waliyoipanga juu ya kukabiliana kwa ushirikiano wa mawazo madhubuti. “Msishahu lakini nasubiri mnithibitishie tukio hilo hapo kesho kutwa” Komandoo Ochola alinyanyuka kitini kwa ishara ya kuondoka pahala hapo, “Sawa mkuu usiwe na wasiwasi tuachie siku hizi mbili tufanye yetu” Salimu alimtoa hofu huku akimsindikiza kwa macho.
Siku iliyo fuata
Benki kuu ya Tanzania (B.O.T), Kinondoni-Dar es Salam.
Milango ya gari ikafunguliwa karibu kabisa na eneo la maegesho vijana Salimu na Karimu wakashuka wakiwa ndani ya suti nyeusi na miwani zao pamoja na viatu vyao wakashuka katika gari ya kifahari kila mmoja akiwa na briefcase nyeusi na kuelekea kwa mwendo wa sina haraka kwenye lango lango kuu. Kwa dakika kazaa walitazama kushoto na kulia. Hao kwa hatua za taratibu mguu mbele mguu nyuma wakielekea katika lango kuu la benki hilo huku walinzi waliokaa kikakamavu na kutapakaa katika kona nyingi wakihakikisha usalama walisimama kikakamavu wakiwatolea macho wageni Salimu alitabasamu tu na kujisemea ‘Huenda mjambazi wakawa ni moja ya fidi force hawa’.
Vijana hao waliingia kama wateja wengine na kila mmoja akaingia katika jukumu lake la siku hiyo akitafuta lililompeleka asubuhi hio katika Benk hiyo. “Habari dada naweza kupata huduma ya kubadili fedha za Uero kuwa Tanzania shilingi” Salimu aliongea akiwa kasimama mbele ya kiambaza kilicho mtenganisha yeye na mtoa huduma aliyemuongelesha upande wa ndani.
Dada kwa tabasamu aliaacha kubofya bofya keybord katika meza yake na kuachia tabasamu laini “Salama tu…ndio unaweza kufanya hivyo akavuta simu yake ya mezani ya TTCL na kuandika namba Fulani na kuzipiga “Habari naomba uje hapa na pana mteja umuhudumie” alimaliza dada huyo kisha punde alionekana kuja binti mwengine aliyevalia sale mfano wa huyo aliyekuwa pahala hapo. “Habari unaweza nifata huku” dada shapu alitoa salamu na kumchukua Salimu. Karimu kwa upande wake tayari alikuwa yumo ndani ya eneo la ndani akiwa na mavazi ya fundi umeme akipita na kofia yake ya cape iliyo na nembo ya shirika la TANESCO na overall lake akipita akiingia huku na kule pasina wasiwasi wowote ule.
Kawe, Kinondoni-Dar es Salam
Laptop zao zilikuwa mezani Salimu alikuwa bize akiangaika na kubofya huku aakitafuta vitu flani Karimu akiwa pembeni yake, jasho lilimtoka Karimu alitoka na kurudi na kahawa na kumpatia huku wakiendelea kushauriana mambo. “Bingoooo” Salimu aliongea kwa sauti akakusanya viganja vyake nyuma ya kichwa chake na kuanza kunesesha mwili wake akitabasamu “Well done bro CCTV kamera zote umezihack, hakuna chenga wala mchele”
Karimu aliongea kwa furaha “Nina wazo la kupindua wazo la kwanza, kwa kuwa muda tunao tufatilie CCTV kamera maana kama ramani ya jengo tumeshaidadavua mipango yetu ya namna tutakavyolicheza sebene tumelimaliza mapema asubuhi hili la CCTV kamera ndio lililobaki tuweke nguvu pamoja kabla mizuka haijachuja” aliongea Karimu Salimu akatingisha kichwa kukubari wote wakaungana kufatailia kamera kumi na tano zilizounganishwa katika laptop yao kutumia kifaa maalumu. Masaa yakakata haraka haraka macho kodo wakizoom picha na kusikiliza maongezi kwa kila video iliyowapa mashaka “Mzee wa kazi muda umeenda naona umetulia unajambo unalolifikiria” Karimu aliuliza.
“Yea ninayo, kwanza nawazia hawa walinzi waliongia sasa hivi na watakao pokea lindo saa kumi na mbili asubuhi watakuwa ni watu wakawaida au laaa pili namna walivyoingia kuingia katika mjengo inanipa sintofahamu” aliongea Salimu “…ni kweli haijulikani lakini tusisahau kesho kuna ratiba ya kusafirisha pesa kwenda mikoani huenda hiyo ndiyo trick watakayotumia” aliongea Karimu na Salimu akadakia “…na kwa mantiki hiyo sisi hatupaswi kulala hapa tutoke twende tukakomae huko huko alimradi mazingira ya benki tumeshayajua sisi hatuna budi kujiandaa kwa kazi asubuhi itukute huko huko” “…sahihi kabisa” Karimu akampa tano Salimu.
Itaendeleaa...