Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

The Hidden Truth (Ukweli uliofichika)

Nani Anahusika?!!

Mtunzi Akida Siri Rambao
email akidasiri@gmail.com
Contact 0658328596

Sehemu 12 G: Ahadi Iliyotimia

Ilipoishia...

.....ikawa ndio habari ya mjini. Tuhuma ya mauaji ya familia ya Richard iliyoteketezwa na moto takribani miaka ishirirni iliyopita ndiyo iliyokuwa inamkabiri Samuel wakati huo, kila aliyekuwa katika zama zile alishtuka na kuziba mdomo na kuachwa midomo wazi pia taarifa ya kuwepo hai kwa mtoto pekee wa Muheshimiwa Richard nayo kwa uzito wake iliamsha hisia mpya na zilizo lala kwa mikutano iliyojengwa na vikundi katika sehemu zote za shughiuli za kijamii. It

Tuendelee

*****

Kawe, Kinondoni-Dar es Salam
Salimu simu ilikuwa sikioni mkono mmoja ukiwa umeshikilia kikombe chenye kahawa kifua wazi amekaa katika moja ya kiti katika ofisi ya siri macho yakiwa katika screen ya desktop “…nimekuelewa vizuri ndoo natazama hapa kupitia google application…yeahhh nimeona hapa” muda huo huo Mlango ukafunguliwa na Meroda akaingia “Vipi baby amekutimia tayari” Salimu akapelea kikombe mdomoni akavuta fundo moja na kukiweka kikombe mezani. Kisha akalitazama toto la kihaya likiwa na nguo ya kulalia transparent vichuchu kufuli la rangi nyeupe likionekana huku chuchu zikitaka kutoboa vazi hilo zitoke kwa msimamo,

Salimu akatabasamu “Yea teyari honey nataka kuhamishia katika Computer nijionee mwenyewe sogea karibu” aliongea na sasa umakini ukaongezeka katika desktop akitazama ramani ya msitu wa Magamba Lushoto. Baada ya dakika chache simu ikiwa sikioni “… yea nimekupata vizuri mzee nakata simu sasa hivi” alikata na kuchukua USB HD ndogo akachomeka kwenye simu yake na kuhamisha file kisha akaitoa USB na kuichomeka kwenye computer haraka haraka alifungua faili “Mhhh” alisikika akiguna na macho kuyatoa Meroda akiwa nyuma ya kiti alichokalia akiwa na kikombe cha kahawa alibaki kutabasamu tu

“Ebwana ee haiwezekani Samuel na Pater wawe na nguvu ya kiasi hiki mbona kama wanajiandaa na Uasi hawa watu” Macho yalimtoka akizitazama picha alizotumiwa na Karimu toka katika kambi ndani ya msitu wa Magamba Lushoto, picha hizo ziliwaonesha wanaume wakiwa mazoezini, majengo, ulinzi mkali, na shamba la bangi na cocain. “Yeah ni kweli mpenzi ile kambi inatisha ina kila kitu ndani na idadi kubwa ya watu kama nilivyo watarifu siku za nyuma isitoshe ina watalamu wa kila namna lakini mpaka hivi leo sio mimi wala kina Samira wanaojua kuwa nyuma ya Samuel na Pater kuna nani na nani japo hilo tunaliamini” aliongea Meroda na kumfanya Salimu (Pius) kutingisha kichwa kukubali

“Nahisi wanataka kuipindua serikari hawa jamaa mbona wana nguvu ya kijeshi kiasi hiki” waziwazi Salimu (Pius) alionekana kuchanganyikiwa wasiwasi ukimuingia ‘Tutaweza kweli’ “Hilo linawezekana mpenzi tunapaswa kuchukua hatua kabla hawajatuwahi naamini huko waliko wana taarifa ya kukamatwa kwa mshirika wao mkubwa sijajua wamejipangaje na Pater na yeye kwa taarifa za haraka hayupo nchini” Salimu (Pius) akakusanya mikono yake na kutafakari kwa muda “Kama kuna watu nyuma ya Samuel na Pater basi Samuel yupo kwenye matatizo lazima watamuwinda aidha wamtoroshe au wamuuwe kuna haja ya kukutana na Samuel leo leo” aliongea Salimu “Yea itakuwa vizuri najua hilo unalimudu sina shaka na wewe mpenzi basi jiandae na uende” aliongea Meroda sasa akimshika begani macho yake regevu yenye kusema

“Nataka” yakimdondokea Salimu aliye baki kujichekea “Teyali nina maradhi twende ukanitibu kwanza” Salimu aliongea akimaanisha maana ulijali ulimsukuma kengere ya ushabiki na kiu ya penzi ilimjaa na kupelekea bukta yake kutuna na kucheza cheza Meroda akabaini akatabasamu akasogea zaidi na kukaa juu ya mapaja ya Salimu “Nitakutibu hapa hapa unataka dozi au nusu dozi” aliongea kwa kunong’ona teyali midomo ikiwa masikioni mwa Salimu mikono ikizunguka mgongoni huku akizungusha kiuno na miguno ya huba ikimuelemea “Nipe vyote mpaka nisahau shida zangu, sita kwenda leo nimeghairi huba nataka unipe vyote” aliongea Salimu kwa sauti ya mtetemo mikono teyali ikiwa kwenye matuta akipalaza kufatisha maporomoko hadi katika mfereji akitafuta kisima cha asali Loo! Wakaingia kwenye sayari ya huba wakishereheka.

Central Polis Station, Kinondoni-Dar es Salam.
Salimu akiwa kasimama mlangoni akimtazama Samuel ambaye na yeye alikuwa kamkazia macho ya uchu na hasira ya wazi wazi, akaanza kupiga hatua fupi fupi kisha akakaa katika kiti kilichokaribu na kitanda. “Shikamoo” aliongea Salimu “Itabadilisha kitu gani kaa nayo mwenyewe” Samuel alijibu, Salimu akaiuma midomo yake kisha akatoa pumzi nzito

“…nimekuja kama mwanao nataka tuzungumze kuhusu sakata la jana na kama tutaelewana basi wewe utabaki salama na heshima yako na mimi nitakuwa nimefanikisha kazi yangu ya miaka mingi mimi ndiye muamuzi wa wewe kudhibitiwa au laa” aliongea Salimu (Pius) Samuel alibaki kimya tu “Baada ya uchungunzi tumeitambua kambi yenu ya uharifu kule Lushoto na cha zaidi sio wewe wala Pater wala ushirikiano wenu unaoweza kumiliki watu wote wale na kambi kubwa ile bila mkono toka sehemu yenye nguvu” aliongea tena Salimu akitembea taratibu chumbani humo.

Samuel ambaye muda mwingi alikuwakimya akitazama pembeni kuepuka macho ya Salimu alijikuta akigeuka na kumtazama kwa mshangao na uso ukiwa na viulizo vingi “…yea tangu nimeligundua hilo…nimejikuta nikibadili maamuzi yangu na hata kukuonea huruma hasa wewe” Samuel akiwa bado anamtazama Salimu, “Najua ni vita ya mapenzi ambayo sikupaswa kuingilia wacha niiache kama ilivyo ila na naomba umsamehe baba angu huko alipo ili aishi kwa amani japo sijui ilikuwaje” Samuel alimeza mate na wazi uso ukionesha kuelewa kinacho maanishwa “…Pius…unachokitaka kwangu ni nini?”

Mzee Samuel alijikuta akiongea “Mzee ninacho kitaka kwako kwanza umsamehe baba yangu pia umsamee Shalon mtu yeyote asiye jua undani wa mambo haya angeweza kureact kama alivyoreact Shalon…” Salimu aliongea na kukaa kitandani karibu na Samuel “Unajua nini Pius mapenzi ni kitu cha ajabu sana unapo kuwa unapenda ni rahisi kufanya kitu chochote kile” kwa masikitiko aliongea Samuel na kunyanyua mkono wake na kuanza kufuta mchozi yaliyo anza kumtoka machoni “…nilipaswa kumuacha Sabrina afanye anachokitaka na nilikuwa na uwezo wa kuwa na mwanamke mwengine mzuri na tajiri lakini nilikuwa pofu sikuona wala sikusikiliza shauri za watu, kwa ujinga wangu tulipoteza maisha ya mtu ambaye hakuwa na hatia kabisa Mchungaji Johnson loo! Nafsi inanisuta sikuwahi kupata maumivu kama hivi sasa” aliongea Samuel na kuanza kulia na kushindwa kuendelea kuongea kabisa,

Salimu alimeza mate na kutingisha kichwa kusikitika “…pole baba bado una nafasi mimi nitakuwa mwanao na Shalon atabaki kuwa mwano pia vipo ulivyovipoteza lakini sisi wawili hujatupoteza unaweza usiamini lakini nilikaa na ndugu yangu tukayaongea yote” aliongea Samuel. Zikapita dakika kama kumi na tano hivi Samuel akiwa anaugulia maumivu ya moyo na mara aka akkokhoa na kuongea “Pius kuna bwana mmoja anaitwa Komandoo Swai huyu bwana ndiye konkod wa ile kambi kule Lushoto historia yake imekuwa ngumu kidogo kuifahamu labda kwa sababu sikuwa na muda huo lakini ni mwanajeshi aliye simamishwa kazi miaka hiyo naweza pata hisia kuwa huenda anakisa na baba yako na alinitumia mimi kulipa kisasi chake kwa udhaifu wa mapenzi yangu kwa Sabrina” Salimu (Pius) akatingisha kichwa akionekana kukubali na kuelewa “ Yea naelewa naelewa sasa nimeelewa vizuri” aliongea Salimu

“Alitupatia kila tulochokihitaji na kutushawishi kuingia katika biashara haramu na kwakuwa tulikuwa vijana tuliopoteza dira ya biashara na heshima kama mimi niliwahi kuingia kwenye siasa kwa lengo la kuongeza kipatp juu ya hasara nilizozipata baada ya kutelekezwa na Richard lakini sikuijua Siasa inataka nini nilijiuta nikipotelea huko mazima baada ya Richard na yeye kuingia kwenye hilo kila nilipojifananisha nae sikumfikia bwana yule nikapoteza jimbo” alijisikitikia Mzee Samuel kwa kutingisha kichwa baada ya kuongea

“Lakini mpaka leo hatuja wahi kuiona sura ya Huyo aliyejiita kuwa ni Komandoo Swai alikuwa ni mtu wa kuvaa kinyago kila tulipokutana naye pia hatujui, sijajua bwana yule ananguvu gani mana kila alilolitaka lilikuwa tena kwa wakati lakini alitusisitiza tusije mwambia mtu yeyote kuwa Komandoo Swai ni boss wetu yani mpaka leo kila mtu anaamini sisi ndio kila kitu” aliongea Samuel safari hii macho yakiwa makavu kabisa “Komandoo Swai aliwahi kukwambia kwanini aliamua kufanya hivo” Salimu aliongea na kukaa vizuri akimakinika “Yea ni kama sisi tu, ni mtu aliyepoteza familia yake na alisalitiwa na jeshi akituhumiwa na kesi ya ugaidi, Uasi na biashara ya madawa ya kulevya” aliongea Samuel akiwa ni mwenye kujiamini sana

“Basi Mzee Samuel hakunashida baba nashukuru kwa kuelewana kama nilivyotamani japo haikuwa rahisi, ni hivi utaupata ulinzi mkubwa tu na pia usiwe na shaka ya kusimama kizimbani na kujibu kile unachokijua naamini utakuwa sehemu salama na pale ulipo kosea basi ukubali kuadhibiwa kwa moyo mmoja tafadhari, naomba nikuache nitakutembelea badae kidogo na ujiandae kunipa address ya Komandoo Swai” Salimu (Pius) akaondoka. “Amerithi mambo mengi toka kwa baba yake like farther like son” alijisemea Mzee Samuel akimuangalia Salimu (Pius) akiishilia mlangoni katika rumande hiyo.

Itaendeleaa...
 
Simulizi: The Hidden Truth ( Ukweli uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU 4

Sehemu 12 H: Ahadi Iliyotimia


Tulipoishia...
....nikuache nitakutembelea badae kidogo na ujiandae kunipa address ya Komandoo Swai” Salimu (Pius) akaondoka. “Amerithi mambo mengi toka kwa baba yake like farther like son” alijisemea Mzee Samuel akimuangalia Salimu (Pius) akiishilia mlangoni katika rumande hiyo.

Tuendelee...

Fish zone Hotel, New York City-United State of America
Sauti ya mziki wa taratibu ulikuwa ukilindima ndani ya sebure kubwa ya kifahari sana iliyopambwa kwa namna ya kipekee sana. Sauti za mihemko na miguno ya mapenzi iliyokuwa chini kwa chini ikaanza kupaa na kushamiri ikidhihirisha wazi watu waliokuwa wakishereheka kwa makutano ya viungo vya miili yao mambo yaliiva haswa. Sauti ya kike ilianza taratibu kupiga kelelee za raha ikaanza kupanda na kuongezeka “Oghh yeaa…comon baby comon” na ya kiume nayo ikafatia “Ohh okay…Okay” kelelee za pamoja zikaungana zikishereheka maungano yao kila mmoja akijitahidi kuonesha anachokijua na mara kimya kikaingia.

Mara mlio wa simu ikiita toka mezani ulisikika mkono ukaogezwa ukipapasa na ikanyakuliwa toka mezani. “Hallow…Mogisha vipi? Sina ratiba ya kuongea na wewe kunatatizo gani wakati huu?” Mzee Pater aliongea Kwa jazba akijinyanyua sofani na kumuacha mwanamama wa kizungu akiwa mtupu puu akitabasamu “….hivi umeshindwa kumtafuta Samuel mpaka Mimi eeh hivi unajua sijapata mapumziko vizuri teyari unanipigia nini shida” Safari hii akiwa amekaa kitako katika sofa akiwa mtupu bila nguo mikono milaini ya mwanamke wakizungu ikionekana kupapasa kifuwa kilichochafuka kwa vinyweleo virefu tokea mgongoni mwake.

“….What!! Sijakuelewa, inawezekanaje?” Pater alijikuta akitetemeka na kuishiwa nguvu huku macho yamemtoka kiasi chakumfanya mwanamama wa kizungu aliyekuwa amemganda akimpiga mabusu ya huba kumuachia kwa woga na kusimama kando ya sofa. “Shiiit Pius nae ni mzima inamaana ndiye aliyesuka mpango wote huo?...ohh my God… sina muda wakuvumilia inanibidi nirudi mapema haraka iwezekanavyo” Pater akakata simu yake teyali amesimama mikono kiunoni machozi yakimlenga lenga ‘Linawezekanaje hili’ akachukua tena simu yake ya samart phone aliyoiweka kando yake na kuanza kuperuzi katika mitandao ya kijamii wakati huo mwanamama wakizungu akiwa anamuangalia kwa wasiwasi tu “Ohh my God its true every thing now is open ohhh” zilikuwa picha mbalimbali akizishuhudia katika mtandao wa Istagram na maelezo mbalimbali juu ya tukio la kukamatwa kwa rafiki yake kipenzi bwana Samuel.

“Hallow wajina…uko wapi muda huuu?” Pater simu ikiwa sikioni macho yamemtoka aliongea “…yeaah nimepata taarifa muda si mrefu kuhusu tukio zima tafadhari naomba panda ndege na uwende Tanzania mara moja tutaongea ukifika ”. Pater akajiziba mdomo na kuyafumba macho akisikilizia mapigo ya moyo yakienda kwa mshindo mkubwa mara akaanza chutuma taratibu “My husbund whats wrong ith you ehh?” aliongea mwanamama wakizungu mwenye umbile la kuvutia na sura yake yakitoto akichutama karibu na Pater akimshika kwa tahadhari “ “Please take me to the bed” aliongea Pater “Okay” Mkokoto ukaanza te te kama mtoto anaenza kutembea miguu ikiwa mizito kwa shambulio la mwili. Kichwani mwa Pater mlijawa na hofu wasiwasi na mashaka kwa pamoja asijue namna ya kujiuzuia na hali hiyo.

Central Polis Station, Kinondoni- Dar es Salam
Samuel alionekana akiwa peke yake katika chumba maalumu ambacho kilikuwa na huduma zote muhimu, huenda ni kwa heshima yake. Akiwa kajiinamia tuli akitazama sakafu kwa muda mrefu bila kupepesa macho mawazo yakamchukua na kuhama kihisia mpaka miaka kazaa nyuma.

Mawazoni, Sauti ya mziki iliendelea kunogesha radha ya bia aliyokuwa akinywa Samuel ambaye chwee alijawa na hasira nyingi usoni macho akiwa kayakaza kwa muda mrefu kwenye kona iliyokuwa mita hamsini toka alipo kuwa ilikuwa kama sinema kwa namna ilivyopita kumbukumbu hiyo kichwani . Alikunywa kwa fujo wakati mwengine akipunguza kasi huku akiendelea kuongeza chupa za bia huku bado akikazia upande ule ambao hakutaka kupitwa na tukio lolote.

Baada ya masaa mawili kiti cha pembeni yake kilivutwa na mwanaume mweusi mrefu ambaye hakuonekana vizuri sura yake kutokana na kiza na eneo alipofikia, alikaa na kuungana naye kutazama upende ule ule. “Samuel ni wazi unampenda sana Sabrina lakini unashindwa kabisa kujua utampataje sio” Samuel akageuza shingo kumtazama mtu anaye mzungumzisha wakati huo, kisha akarudi kuendelea kutazama. “Bado unayofulsa ya kuwa na naye kama ukitaka” Samuel akageuka kumtazama “…rahisi tishia kuchukua maisha ya Richard kwa kumpata mtu unaye mpenda, tishia hata kunyakua roho za watu anaowapenda, tumia pesa upate unachokitaka” Bwana yule akanyanyuka na kuondoka

“…subiri…” aliongea Samuel na kumfanya bwana yule aliyekuwa hatua tatu mbele kusimama na kugeuka, “…nimekubali azimio lako”. Samuel akiwa bado mawazoni ikapita sauti laini ya mwanamke aliyewahi kumpenda sana.

“Samuel tafadhari usitumie udhaifu wangu kunitesa sio kitu kizuri, yea ni fact kuwa sina hisia zozote na wewe, nakubali unanijali unanisaidia hata nisipo taka msaada wako lakini haimaanishi kuna siku nitakulipa kwakukupa penzi la dhati hapana mimi sikupendi wewe” Samuel akiwa katulia alipata kumbukumbu ya mazingira yote ya sentensi hiyo iliotokea na kila kitu akakiona kama sinema. Pembeni ya kitanda Samuel akiendelea kuvuta sigara akaishia kutabasamu. “…nina pesa Sabrina nina uwezo wa kufanya lolote lakini nataka kukwambia kuwa hata Richard hakupendi kimapenzi” aliongea Samuel “ ….najua na hata sijawahi jisikia vibaya kwahilo kwa sababu nimeridhika kwa kulikosa penzi lake natosheka anapo nijali tu na kunipa muda wake anapoupata” “Nyamazaaa” Samuel alfoka kwa hasira “…usiongelee ujinga huo mbona mimi hunipi mhuo muda wako, kwa nini unapoteza muda wangu na wa kwako pia sasa nisikize kama nilivyosema nina uwezo wa kutoa roho ya Richard ni kitaka muda wowote na ukakosa hata kusikia sauti yake au aidha nikuoe na ubaki ukimuona hai” Samuel aliongea macho akiwa kayatoa akimtazama bila kubwenza , Sabrina wa watu akiwa anatetemeka tu macho yamekuwa mekundu kwa kulia akakurupuka kutoka kitandani na kushika miguu ya Samuel akilia “…mimi nimeshakupa muda wangu mara nyingi na kukujali lakini wewe unataka niwe wako ahh… ni tofauti, tafadhari nitafanya utakacho yaache maisha ya Richard tafadhari nakuomba muache aaishi nimekubali nimeshindwa”.

Samuel akatabasamu “Nitafanya mipango ya harusi haraka iwezekanvyo” Samuel akajinyanyua na kuelekea mlangoni huku akimuacha Sabrina akiendelea kulia kwa kwikwi. Kabla hajataka hata kuvuta hewa nyingine sauti ya mwanamke ikapita akilini
“Umeona mke wako alivyokuwa Malaya amethubutu kumtafuta mume wangu na kungonoka naye bila aibu, we mwanaume vipi mkeo umeshindwa mzibiti mkeo anaye tishia amani ya mume wangu kwa kuivuruga heshima yake kisa penzi pokea picha hizo ukijionea ufuska wa mkeo na kama hutomkanya zitasambaa mtandaoni na wewe utaisha mazima” ‘Nilidharaulika sana mpaka kufikia hatua ya Winifrida kujua udhaifu wangu na kunitusi alivyopenda kama mumewe akijinadi kwa picha za utupu za mke wangu Sabrina ningefanyaje kama si kuwaangamiza?’ alijiwazia huku akitingisha kichwa kuondoa kumbukumbu mbaya akilini. ‘Hivi ile sura ni ya nani ni nani yule bwana mbona nashindwa kuelewa huyu Komandoo Swai a yule bwana ni mtu mmoja au tofauti, na kama tofauti kwanini yule hajawahi kurudi tena’ Samuel akafumba macho akijifikirisha ‘Swai alikuja na dhamira ya kumdondosha Richard lakini hakuzungumzia mahusiano yangu, Ohh kichwa kina niuma sasa’ Samuel alijiongelea mwenyewe na kukishika kichwa ‘Inamaana Shalon ni mtoto halali wa Richard Ohh my god kwanini nilichelewa kumuua tangu mwanzo, nimebaki sina mbele wala sina nyuma, nimemuua mke wangu mwenyewe nimejichoma kisu cha tumbo mwenyewe Ohh mungu wangu nisamee na unisaidie’alijiongelea nafsini akaanza kulia kama mtoto mdogo ikaingia kumbukumbu ya mfano wa sinema alijiona akibishana na Sabrina chumbani bila maelewano Sabrina akilia kwa sauti “Si bora ungeniua tu Samuel kwanini umeyaangamiza maisha ya Richard ukwachoma kama mishikaki why wewee mbaya nitakufunga nakwambiaaa nitakufunga”

aliongea Sabrina ndipo Samuel kwa hasira alimkwida na kumgongesha ukutani mara tatu na kumuacha akitwetwa uchogo damu zikimtoka akiita jina la Shalon kisha Samuel akageuka na kutazama mlangoni na kumuona Shalon akiwa mdogo wa miaka mitatu kasoro akimtazama kwa hasira akaondoka na kuwaacha, “Ehh mungu wanguuu nifute hizi kumbu kumbu mbaya inamaana Shalon alielewa na kujua kilicho tokea ndomana hakuwahi kunipendaaa alihefadhi kila kitu” aliongea Samuel na kujilaza kitandani na kuanza kulia kama mtoto.

Itaendeleaa...
 
The hidden Truth ( Ukweli uliofichika)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 4

Sehemu 12 I : Ahadi Iliyotimia.

Ilipoishia....

....inamaana Shalon alielewa na kujua kilicho tokea ndomana hakuwahi kunipendaaa alihefadhi kila kitu” aliongea Samuel na kujilaza kitandani na kuanza kulia kama mtoto.

Tuendelee...

*****
Watu mbalimbali maarufu walionekana kuendelea kuja katika kituo kikuu cha polisi baadhi yao wakijenga vikundi vidogo vidogo wakijadiri tukio zima lililotokea asubuhi ya siku hiyo, kila mmoja kwa nafasi yake alitamani kukukutana na Muheshimiwa Samuel na kupata kujua |kulikoni maana zilikuwa ni taarifa za kushtusha na kushangaza sana.

Waandishi wa habari hawakukosekana eneo hilo wakijaribu kuwa hoji baadhi ya watu maarufu waliotokea kushangazwa na kumuelezea namna wanavyo mjua mzee wao huyo kwa upande wa mazuri sana na sio vinginevyo huku wakimtuhumu huyo mtu aliyeizusha na kuamsha kesi hiyo ya miaka mingi. Bahati haikuwa kwao hawakuipta ruhusa hiyo.

Jullius Nyerere International Airport, Dar es Salam
Msururu wa watu wakiwa katika foleni ya ukaguzi uliendelea kupungua taratibu, hatimaye bwana mmoja mnene na mfupi wa wastani alichukua mzigo wake na kuanza kuburuta akielekea katika upande wa kutokea mara ghafla alijikuta akipepesuka na kupoteza muelekeo wa utembeaji hakuanguka akakaa sawa kwa mshangao akimtazama mtu aliye mgonga ambaye wala hakuonekana kujali juu ya tukio lake na kuendelea na safari huku mdomo wake ukiwa bize kutafuna, “…watu wachache ndio wastaarabu katika umati wa watu inastaajabisha” alimuangalia kwa akimsitikia kijana yule huku mkono mmoja ukiwa umeshikilia msukumo wa begi la matairi huyo akaendelea na safari baada hatua kazaa alinyanyua mkono wake na kutazama saa yake ya mkononi kisha akapeneyza mkono hadi katika suruali yake na kutoa simu ya mkononi. “…nimeshawasiri nakaribia kutoka nje kabisa”. Alikata simu na kurejesha simu mfukoni. Akiwa amesimama nje kabisa ya uwanja wa ndege akitazama huku na kule hali ya hewa ikiwa tulivu gari moja ndogo ilionekana kusogea maeneo hayo kisha mwanaume mmoja aliye jaa kwa misuri alitoka na kufungua mlango kwa ishara ya karibu uingie.

Bwana huyo mara moja aliiingia na gari ikatokomea. “Karibu muheshimiwa wakili nchini nikajua utaingia usiku sana” aliongea bwana aliyemfata nakumfungulia gari “Hapana niliamua kubadili ndege, poleni kwa masahibu yaliyo wakuta… msiwe na shaka kila kitu kitakuwa sawa” akaingia garini “…ni kweli inasikitisha lakini inatupa somo pia kwetu” “ Unamaanisha nini” aliikunja midomo kwa muda “Hakuna, usiwe na shaka nafikiria kuna mambo unayahitaji kumuhusu Muheshimiwa au hakuna unachokihitaji toka kwetu” Wakili akamuangalia kwa muda kisha akatabasamu, “Nashukuru nimepata ushirikiano wa kutosha toka kwa bwana Pater hakuna nisichokijua sasa na nitafanya kwa juhudi zangu zote japo lazima tutazame upande wa pili imekuwa ghafla sana hakuna aliyewahi fikiria itakuwa hivi, hivyo naamini wamejipanga sana upande wa mashtaka”.

Taratibu gari hiyo ikatoka maeneo hayo na kuondoka. Katika lango la kutokea katika Uwanja wa ndege alionekana yule kijana ambaye haukutambulika utambulisho wake kutokana na namna alivyovaa na utembeaji wa kijana wa kisasa sharobaro haswa alionekana kutembea kawaida na sasa alivua miwani yake na kofia ya jacket iliyofunika kichwa chake, alikuwa Karimu taratibu alitoa tabasamu na kuchukua simu yake aliyoiweka nyuma ya suruali ya jinsi iliyokuwa chini ya kiuno katikati ya makalio simu ikiwa sikioni “…hallow bro mambo yameenda vizuri tumepata maelezo yote kupitia kinasa sauti nilichomuwekea, muda huu anakuja huko Fahari Hotel…poa” alitulia kidogo na kufungua mlango wa gari simu bado ikiwa sikioni, “…Haina shida kiongozi nitafanya kama tulivyo panga…sawa”

Baada ya siku tano

Central Polis Sation- Dar es Salam
“Naitwa Pater Sambano nahitaji kukutana na mteja wangu Muheshimiwa Samuel tafadhari” wakili Sambano aliongea huku akionesha kitambulisho chake kilichokuwa kikining’inia shingoni akiwa amevalia suti nyeusi “…ni sawa naomba usubiri kidogo” Wakili Sambano alishusha pumzi na kukaa kitini akimuacha askari wa zamu mapokezi akinyanyua simu ya mkonga baada ya kubonyeza namba Fulani “…habari mkuu wakili wa Muheshimiwa Samuel yupo hapa…ndio…sawa mkuu” alikata simu na kupiga simu sehemu nyingine “…jambo afande….teyari wakili yupo hapa” akarudisha simu pahala pake na kutabasamu. “…sasa hivi utafika sehemu usika” “Hakuna shida afande” Wakili Sambano aliongea.

Hazikupita hata dakika tano teyari Salimu pamoja na kijana mmoja wakawasili na kumchukua wakili Sambano ambaye alibaki akishangaa kuona ulinzi ukiwa umekithiri eneo hilo, walikatiza koldo kazaa na kuingia katika chumba kimoja ambacho kilionekana kuwa cha tofauti kwa nmna kilivyokuwa. “Karibu bwana wakili unaweza anza kazi yako unalisaa limoja pekee” aliongea Salimu akiwa na mavazi ya kipolisi , kwa dharau bwana Sambano alimtazama Salimu “Naona, naona sasa jeshi la polisi mme amka, makinika kijana unaweza poteza uhai wako bure” aliongea kwa sauti ya chini akitabasamu na kunyonga kitasa chamlango kuingia chumbani.

“Muheshimiwa habari yako na pole kwa matatizo” aliongea Wakili Sambano “…sizani kama ni muhimu sana, ni nani aliyekuagiza kuja hapa”aliongea Samuel, Wakili Sambano akiwa anaweka sawa mkoba wake uliobeba nyaraka juu ya meza alitulia kwa muda akimuangali Samuel kwa mashangao “…muheshimiwa inamaana huna habari ya ujio wangu kweli?” Sambano aliongea akimtazama kwa mshangao Samuel akauma meno na kutazama katika ukuta ambao uliwekwa kiooo ambacho mtu wa nje pakee ndiye alikuwa na uwezo wa kuona vya ndani.

“…Sambano nisikie kwa makini naomba umwambie Pater awe makini sana asimuamini mtu yeyote yule kuanzia sasa” aliongea Samuel akisisitiza kwa macho yake aliyo yatoa kama mjusi “Okay ni sawa ni sawa Muheshimiwa lakini nimekuja hapa kwa mengine hebu nipe ushirikiano kwanza hayo mengine tufanye badae” aliongea Sambano huku akichambua makarablasha Samuel akaigonga meza kwa hasira “…unasemaje wewe hilo ndilo la muhimu zaidi unaelewa?” Sambano alishtuka na kumkodolea macho Samuel aliyekuwa kasimima akihema kwa hasira “ Sawa sawa naomba ukae nimelelewa nitafanya hivyo…”Sambano aliongea “Vizuri, kingine fanya kazi yako usiingize kitu cha tofauti hivi sasa” Samuel aliongea,

Sambano waziwazi alionekana kuwa na sintofahamu kwa muonekano aliouonesha mteja wake “…naelewa…naelewa naelewa Sambano nimekushambulia elewa tu wee elewa, najua dhamana yangu imekataliwa lakini usijali nipo sehemu salama na nina lindwa pia mwambie Pater hivyo na wewe ufanye kazi yako, sitaki uingie kwenye matatizo…nitakusikiliza niahidi utabaki kwenye mipaka yako” Samuel alimaliza na kumtazama Sambano ambaye wakati huo alibaki akimuangalia tu Samuel kisha akatingisha kichwa kukubali kishingo upande “…okay nitaanza”. Majadiliano yakaanza.

Itaendeleaa.....
IMG_20210528_122353_600.jpg
 
The hidden Truth (Ukweli uliofichika)

Nani Anahusika??!!

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU 4
Sehemu 12 J: Ahadi Iliyotimia

Ilipoishia....
.....pia mwambie Pater hivyo na wewe ufanye kazi yako, sitaki uingie kwenye matatizo…nitakusikiliza niahidi utabaki kwenye mipaka yako” Samuel alimaliza na kumtazama Sambano ambaye wakati huo alibaki akimuangalia tu Samuel kisha akatingisha kichwa kukubali kishingo upande “…okay nitaanza”. Majadiliano yakaanza.

Tuendelee...

Usiku wa manane

Sauti za funguo zikifungua lango zilisikika na mlango ukafunguka mwanaume kwa mbali ilisikika minong’ono kwa nje. Samuel waziwazi alionekana kutambua uwepo wa watu upande wa pili wa mlango alimeza fundo la mate lililopita kwa shida kohoni nywele zikimsimama na mwili kusisimka. Taratibu mlango ukafunguka na mwanaume mmoja mrefu aliingia kwa mwendo wa taratibu bila kuonekana sura yake. “Swai…!” Samuel aliongea kwa kunong’ona macho yakiwa yamemtoka.

“Samuel unashangaa kuniona hahahahaaa” alicheka bwana huyo na kukaa kitandani “…niliwahi kukwambia siku moja usiwe mjinga kiasi hicho lakini hukunielewa nafikiri umeona matunda yake kila mtu huko nje anaongea stori yako na yule mwanao wa laaana niliwahi kukwambia hukunisikiliza” Samuel akiwa kajiinamia akasema “…ni kipi kilichokuleta hapa muda huu” “Samuel hujapenda kutembelewa na mimi…usinitanie!” alihamaki aligeuza shingo kumtazama Samuel kwa muda “…tuachane nayo hayo ni hivi nataka kukuhamisha nchi maana naona utaenda kuozea jela na kila kitu kitaharibika na bado unadeni langu hujalilipa” Samuel akamtazama

“…wala sijali kwa hilo naona ni sawa kwa sababu nastahili huenda ningekuwa na maisha mazuri zaidi kuliko hivi sasa nimekuwa mpofu miaka yote lakini sio sasa niache na maisha yangu” “…unasemaje wewe!? nikuache alafu…sio rahisi hivyo namba ya watu wangu haija isha” akasimama kwa hasira “…ndio chaguo lako sio? Basi tutaona kama utaimaliza kesho ukiwa hai” kwa hasira alinyanyuka bwana yule na kukasikika sauti ya spray ikipulizwa mara tatu kisha sauti za viatu zikasikika zikipotelea kufata mlango. “Ohhhhh mungu wangu amekuwa mpenda anasa mpaka kutembea na pafyumu usiku huu”

Samuel aliongea na kushika kichwa chake kwa mikono miwili “…mtu pekee aliyekuwa ananipa nguvu ya kuishi ni Shalon lakini sasa hakuna tena” kwa uchungu wa wazi toka moyoni ulipelekea kububujikwa kwa machozi. “…yeah hii ni adhabu ninayo stahili kuipata na sitajisamee kabisa” aliongea tena kwa masikitiko, na kuachia uchungu aliokuwa nao kwa kuanza kulia kama mtoto ndani ya usiku mzito ndani ya chumba maalumu.

*******

Mlango chumba cha mahabusu alichokuwa amehefadhiwa Muheshimiwa Samuel ulifunguliwa na maaskari wawili waliingia na kumfunga pingu mikononi, “…kuna nini kwani vijana” aliongea kwa sauti ya unyong’onyo macho yakiwa yamezidiwa na usingizi mzito mwili ukimlegea “Mzee hujui kama leo ni siku ya kusikilizwa kesi yako?” “…kwani leo ni lini jamani” aliongea huku akifumbua macho tabu sana “Naomba mniitie Pius nataka kumwambia kitu tafadhari niacheni” aliongea Samuel akienedelea kubuluzwa “Mzee usituletee aigizo hapa “Jamani kichwa kina niuma nazidiwa na kiza siwezi kuona vizuri na mwili unanissha nguvu” Samuel aliongea tena kwa shida, lakini alipuuzwa.

Nje ya kabisa msururu wa wawatu tofauti ikiwemo jamaa wa karibu na muheshimiwa huyo wapambe, watu wa wakawaida, viongozi wa kiserikari na wandishi wa habari walikuwa wakionekana kuzagaaa zagaa huku askari maalumu wakiwa tayari kukabiriana na jaribio lolote la kuvunjwa kwa amani eneo hilo macho mbele siraha mkononi.

Watu waliendelea kusukumizana wakiminyana mikono ikiwa juu juu imeshikilia simu na vinasa sauti mfano wa watu wanaokufa maji wakitaka msaaada wa uokozi “sogea kidogo… nipishe… unanikanyaga…unanisukuma” sauti hizo zilisikika katika kundi la watu wakiwa nje ya uzio wa kituo kikuu cha Polisi jijini Dar es salam muda huo huo Samuel alionekana akitolewa kila mtu vurumai ikazidi kila mmoja akijitahidi kushuhudia namna alivyoonekana akitilia huruma, baadhi ya watu walisikika wakinong’ona kumuombea akashinde kesi wengine wakilaani shtaka hilo kwa mtu wa hadhi kama yeye.

Wenye simu za Kamera wakajitahidi kuelekeza walau kupata picha mbili tatu. “…ndio kama tarifa zilivyotolewa jana toka ofisini mwa kamanda mkuu wa jeshi la Polisi kuwa leo Muheshimiwa Samuel atafikishwa katika ofisi za Hakim mkazi Kisutu kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi yake…mlikuwa na mi mtangazaji wenu Rehema Shukuru Bwakila wa Channel 2” alimaliza kuongea moja ya watangazaji waliokusanyika nje ya uzio wa Kituo kikuu cha Polisi Dar es salam.

Itaendeleaa...
 
The hidden Truth (Ukweli Uliofichika)
Nani Anahusika!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596

MSIMU 4

Ilipoishia...

....Channel 2” alimaliza kuongea moja ya watangazaji waliokusanyika nje ya uzio wa Kituo kikuu cha Polisi Dar es salam.

Tuendelee...
SEHEMU 13A: MSIBA
“Samuel anashikwa na umauti huku akinuia kusema ukweli kuhusu yale yaliyojificha, anaongea ukweli anaoujua mbele ya kila mtu, mbele ya Pater ambaye hakuwa akiyajua mambo ya nyuma ya pazia huku akimtaja muhusika mkuu wa yote yalitokea na kuzidisha hasira za kila mmoja wao na mwishowe anaaga dunia huku akiacha vumbi likitimka. Je! Marehemu Samuel ameuacha ukweli upi na ni nani anayehusika?”

MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL, Dar es Salam
Manesi hawakuwa na muda wa kusubiri zaidi ya kunusuru sehemu ya maisha ya mtu mahututi huku drip zikiwa juu juu zikining’inia. Mzobe mzobe hao hao wakakata kona na mlango ukafunguliwa na mara ukafungwa mbaa “ICU…dah itakuwaje” Salimu akiwa kaelekeza macho yake juu ya kibao cha mlango huku mikono ikiwa kiunoni. Kabla hajapata jibu la swali lake teyari Mzee Ochola na vijana watatu pamoja na Kamanda Mkuu wakawasili eneo hilo nyuso zikiwa na amshaka makuu.

“…vipi hali ya Muheshimiwa ilikuwaje maana nimeshangaa imekuwaje” Salimu (Pius) aligeuza macho kumtazama Kamanda mkuu kisha kwa ghadhabu aliruka na kumvamia akamkunja shati tayari ngumi ikiwa hewani kumjeruhi kiongozi huyo “…achaa mara moja” Ochola aliongea kwa ukali ikawa ni nusra yake. Kamanda mkuu macho yakiwa yamemtoka moyo ukimdunda alimeza mate na kujiweka sawa kisha akaangalia huku na kule kuangalia usalama kwabahati hapakuwa na watu zaidi yao ikawa ni bahati alishusha pumzi nzito kama mtu anae puliza moto

“…nikosa langu” aliongea huku macho yakiwa chini wakati huo Salim (Pius) aligeuka na kuwapa mgongo mkono mmoja kichwani hasira zikiwa zimemjaaa “…Salimu teyari yametokea hebu tutazame shida iko wapi taaarifa kama alikuwa analalamika kuishiwa nguvu na kupoteza nuru ya macho na mala damu zikaanza kumtoka puani, masikioni na mdomoni huku akibadilika rangi kuwa mweusi na mala aliwazidi nguvu askali na kuanguka inawezekana sio wewe wala Kamanda mkuu ambaye analijua hilo” aliongea Ochola

“Tatizo lenu nyinyi polisi wa kawaida hampo makini” Pius aliongea kwa ghadhabu, Kamanda mkuu akajisogeza taratibu hadi katika benchi na kukaa akionekana kujitahidi kufikiria kitu. “Mbona kila kitu kilikuwa sawa tangu jana hadi asubuhi ya leo…mhh kuna mtu kanichezea mchezo” Kamanda Mkuu aliongea pasina kujielewa kisha akajishika kichwa na kumfanya Salimu (Pius) na Ochola kumtazama kwa mshangao na kutazamana mara Daktari alitoka haraka katika chumba cha ICU “Dokta vipi hali ya mgonjwa” aliongea Salimu (Pius) akiwa na uso wa kutamani kujua “Nasikitika sana sumu imeshambulia eneo kubwa la mwili wake tumejaribu kumpatia aina tofauti za anti dote, anatia moyo tumuachie Mungu hili, mnaweza kumuona sasa” aliondoka zake daktari

“Rafiki yangu yupo wapi” aliongea Peter Sambano na vijana wake wa Ulinzi punde Meroda pamoja na Karimu nao wakaingia eneo hilo. “Mzee kwa kuwa tumeruhusiwa kumuona mgonjwa ni bora tukamsabahi kwanza” aliongea Salimu, Pater alimuangalia kwa jicho la hasira na kuingia chumbani kina Salimu wakamfata
“Nakufa rafiki yangu kipenzi lakini sita kufa bila kukwambia mambo muhimu ili iwe muhimu kwako”

Samuel akiwa hoi aliongea kwa kutweta kwa tabu sana kutokana na uso kuonesha hali hiyo. Pater machozi yalikuwa yakiendelea kumtoka kwa wingi huku mkono mmoja umeshikila kiganja cha rafiki yake kipenzi Samuel “…nikweli naomba unisamee sikuwa rafiki mzuri kwako nilikuwa mbinafsi” Pater mdomo ukiwa unacheza cheza kwa machungu huku kamasi zikichuruzika akanyanyua uso kwa mshangao “…mimi na Sabrina hatukuwahi kufurahia penzi hatukuwa wa wapenzi…nilimjua Sabrina kupitia Richard siku alipokuja naye ofisini, na nikamnyima furaha yake kwa kuamini siku moja moyo wake utakuja kwangu kwa kumtishia kumuua Richard lakini siku aliponitishia kuhusu kumuua Richard nilimuua”

Samuel mchozi wa uchungu ukamtoka machoni na kutiririka kushukia upande wa sikio baada ya kuzidiwa na wingu la machozi “…Swai hakuwa tu anatusaidia bali ilikuwa ni sehemu ya kiasasi chake dhidi ya watu walio mkosea kama Richard hata Muheshimiwa Emanuel Godfley Meza aliuwawa kwa msaada wetu wewe ukiwa Italy Kibiashara” Samuel aliongea akitazama mlango “Naomba unisamee mwanangu Pius Ni hasira tu hatukupanga kuiua familia yako kwa namna ile hasira za baba yako kuihujumu kampuni yetu na kisha kuendeleza mahusiano na mke wangu zaidi mama yako kunitusi ndivyo vilipelekea yale yaliyotokea mnisamee wewe na Shalon na wengine wote mnao nisikiliza”

Pater macho yalimtoka muda huo akiwa kapiga magoti” wajina wake wakili Sambano akiwa kamshika bega mara alam ya hatari ilianza kulia na kila mmoja alitupia macho Respirator ventilator kila mmoja aliogopa maana tena hakukuonekana mawimbi mawimbi bali mstari ulio nyoofu ukipita “Samuel hapana usife rafiki yangu Samuel” Pater aliita kwa majonzi manesi na madokta walijitahidi kumtoa huku wengine wakipambana na hali ya Samuel ambaye alibaki akitweta macho yamemtoka akipambana na hali ya umauti iliyokuwa ikimkabiri wakati huo.

“Haraka unganisha Defibrillator machine” aliongea Daktari na kushika kifaa hicho chenye mfanano wa pasi ya umeme na kumgusanisha katika kifua cha Samuel mara moja, mwili ukatikisika jicho likaelekea katika Respirator ventilator “Ongeza joto tafadhari” aliongea tena huku watu wakitazama hali ya uokoaji ikiendelea Daktari akaweka tena katika kifua cha Samuel lakini ikawa hola, akatulia kwa sekunde “Ohh my god ametutoka” ilikuwa sauti ya dokta Jamali Adan huku mikono ikiwa juu ya kifua cha Samuel akisikitika, kimya kikatawala huku Pater na wengine wakiwa hawaamini macho yao.

Ochola akatoka katika chumba cha ICU “Sheenzi, Swai nitakupata wapi we mpumbavu” aliongea Komandoo Ochola huku akiwaacha maaskari walio tapakaa eneo hilo wakiweka ulinzi wakimkodolea tu. Ochola kaanza kuukuna upara wake akiendna kurudi wazi kuchanganyikiwa kuliinza kumtawala ‘Kitu gani kipo katikati mbona nashindwa kuelewa hapa’ mara akatazama upande wa koldo ya kutokea na kumuona mwanaume akijificha.

Haraka akatoka kwa kukuzana kumfata mtu huyo aliyemfananisha huku koti lake la suti likipepea “Yuko wapi?” alijiuliza akikodoa macho huku na kule upande huo wenye uelekezo wa kutoka Hospitalini hapo. Mara akakurupuka safari hii akikimbia kadri alivyoweza huyoo huyoo mpaka nje ya geti alipotazama kulia aliona gari ikitoka katika maegesho ya nje ya hospitali “Sina muda wa kusubiri” “Mzee unahitaji taxi” bwana mmoja aliongea na gari teyari ikiwa karibu na miguu ya Ochola “Ifate ile gari” Ochola aliongea na kuingia garini.

Itaendeleaa....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom