Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Comments mbaya na nzuri zinamaana kubwa Sana kwa mtunzi
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Tuendelee....

Sehemu. 9...: VIJANA KAZINI


..... “…siwezi isahau hii sentensi ipo akili miaka mingi sana sentensi hiyo, Mnainonaje hiyo snetensi vijana mnafikiri Joka na Muheshimiwa Richard ni watu wawili tofauti?” Salimu na Karimu wakatazamana tena bila kuongea kitu lakini wakiwa na nyuso zenye kuhisi kitu “…Kiongozi na nafiri ni vema ukatueleza hisia zako kwanza maana sentensi yenyewe inaonekana ni tata sana inaitaji utulivu sana” alioongea Karimu Komandoo Ochola akatabasamu

“Vizuri Kalimu basi hiyo kauli niliambiwa na Muheshimiwa Fanuel Mkwasi wakati ule alikuwa waziri wa mambo ya ndani kipindi kile na nikakubali kurudi lakini kwa ajili ya Muheshimiwa Richard Edward baba ako na Joka ikiwa kama zawadi ya taifa iliyopotea kwa kuwafanya muwe walithi wa Joka ambaye binafsi sikuwahi hata kumuona wala kuongea naye bali kazi zake zote nazijua alikuwa Interpol wa kundi maalumu la kijasusi mara nyingi amefanya kazi nje ya nchi” Komandoo Ochola aliongea kwa huzuni kisha akatulia kwa muda bila kutia neno kisha akaendelea “Muheshimiwa Richard Edward na Joka ni mtu mmoja haya nimeyatambua hivi karibuni baaada ya kuchunguza mimi mwenyewe na nilipokuwa nimemuuliza Muheshimiwa Waziri Mkuu Fanuel Mkwasi alicheka tu” kwa pumzi nzito alihema Komandoo Ochola akaendelea

“…katika maisha yangu sijawahi kumuona mtu wa ajabu na makini sana kama Muheshimiwa Richard kwanza alikuwa mwanahabari wa kujitegemea tena alifanya kazi yake kisiri sana akiwa na taaluma hiyo kabla hajaingia katika siasa na kuacha ilikuwa siri sana kumbe alikuwa Informer wa siri wa TISS miaka ile na alitumia jina la Joka kama nick name yake hata mimi siku fahamu hilo nimelijua hivi karibuni inastaajabisha sana” aliuma meno yake, habari ilikuwa ya vuuup na yenye kushtusha katika masikio ya Salimu na Karimu. “…haiwezekani” Salimu alijikuta akionge kwa sauti ya taratibu sana. “Kumbe ni yeye aliyekuwa anaenda nje na kufanya pelelezi za siri na kutoa taarifa katika kamati maalumu na sisi ndipo tulikuwa tunatumwa kwenda kukamilisha mission kumbe mzizi wa habari alikuwa ni yeye.” Ochola machozi yakimlenga lenga na kuendelea “…alikuwa na uwezo wa kipekee sana…alifanya yote hayo kwa mgongo wa Biashara na umaarufu wake, alikuwa msiri sana kwakweli na mtu mwenye kujiamini kupita kawaida” Sasa machozi yalikuwa mashavuni yakitoka tu hovyo hovyo na kwa haraka akajifuta kwa kutumia kitambaa alichokuwa amekiweka begani. Kilipita kimya kila mmoja akiugulia maumivu moyoni vijana wote sasa wakiwa wakitokwa na machozi hasa Salimu aliyekuwa akilia kimya kimya kimya Ochola akauvunja ukimya


“…vijana tusidanganyike kifo cha Richard ni lazima kuta kuwa na watu wengine na sio Samuel na Pater peke yao tu tena watu hatari sana waliomtega Muheshimiwa na bila kupepesa ni watu wa usalama” kauli hiyo ilinyanyua vichwa vya vijana vilivyoinamishwa vikifikirishwa sasa wakawa wanamtazama Ochola maneno yakiwa yamewaingia vizuri. “Kiongozi hata Mzee Habibu pia naamini hajui kama Joka ni baba Muheshimiwa Richard na hakika ilo lakini mara kazaa alikuwa akitupa sifa zake sana bwana huyo si atajiskiaje akijua alikuwa ni Muheshimiwa Richard Edward” wote walibaki kimya wakiyapima maneno ya Karimu. “Sasa Mission inayofata ni ya moja kwa moja dhidi yao, mnasemaje?” Ochola aliongea huku macho akiwa kayatoa akiwatazama. Wote walikubalina nae na wakaanza kuongea mambo kazaa juu ya hatua watakazo zichukua iliwachukua dakika ishirini nzima na ndipo Salimu akadokeza kitu. “Nafikiri kumtumia Shalon itakuwanjia salama sana kwetu” kauli hiyo ilifungua njia za mawazo ya Ochola na kumfanya atabasamu “good idea” wote wakatabasamu na kuendelea na mazungumzo yao.

“Samahani Kiongozi kuna kitu napenda kushare hapa lakini kipo nje ya mada kidogo” aliongea Salimu huku akimkazia macho Ochola “Ongea tu” aliongea ochola “Unajua siku nyingi kidogo na habari hii ya leo inaendelea kunipa hisia ya jambo Fulani naona wazi kuwa kuna sehemu kuna taarifa tunazo zihitaji kama baba yangu kweli ndiye mwenye sifa hizo basi kuna ofisi ya siri mahali, hisia zinanipa kwenda kupachunguza nyumbani alipokuwa anaishi mzee” aliongea Salimu kwa kujiamini Ochola alimtazama kwa makini Salimu akiyanyambua maneno hayo akajikuta akisema “…like father like son, yes good idea” haraka haraka alitoka alipokuwepo na kumkumbatia Salimu “…nahisi naona amefufuka Joka, haraka sana muifanye hii kazi leoleo bila kusubiri hatuna muda”

Baada ya masaa mawili na nusu

Msasani, Kinondoni-Dar es Salam
Gari aina ya MAZDA CX-9 nyeusi kwa maringo ilionekana ikisimama umbali wa mita kumi toka katika jengo kubwa lililotelekezwa, kuta zilizo zeeka na kubanduka kwa kukosa matunzo zilionekana wazi, palikuwa ziii kiza tiii tuli nyumba jirani pekee zikiwa na miale ya mwanga kwa mbali maana ukuta huo ulichukua eneo kubwa sana huku ukitazamana na msitu mdogo ulio karibia na bahari ya Hindi. Salimu alitokea mkono wa kushoto wa gari akifatiwa na Karimu. Baada ya chunguzi ya muda mchache hao wakaelekea katika mwambao wa ukuta na kuambaa nao kwa tahadhari na mara mmoja akajampu na kujitupia upande wa pili wa ukuta na mwengine akafata. Kwa utulivu kwa mwendo ule ule wa tahadhari walisogea hadi katika jengo lililoaathiriwa lilloonekana kuathiriwa na moto. Salimu alijikuta akiishiwa nguvu na mwili kuanza kumsisimka akikumbuka kumbukumbu zilizokuwa zikiishi kichwani mwake kwa muda mrefu


“Ndugu najua unavyojisikia, jikaze na tufanye kilichotuleta kwanza jikaze”, Salimu akamtazama Karimu kwa hisia katika kiza kile “Ni sawa”, Hao wakaingia zaidi katika jengo hilo na kuanza chunguzi yao, ya hapa na pale huku waki mulika mulika kwa kurunzi katika vyumba. Iliwachukua takribani masaa matatu wakiwa hawajapata kituchochote kile na kufikia kukata tama kabosa kuwa hakuna kitu chochote. “Karimu unajua nini? mimi bado hisia za kunionesha kuwa hapa pana kitu ninazo aliyakuwa hakuna dalili zinazo onesha kuwa pana chumba hapa isitoshe …” aliokota kitu kizito kilichokuwa karibu yake na kukitupa mbele kwa nguvu kwa hasira kuu pakalia mlio uliofanana na bati gumu kiasi cha wote kushtuka na kutazamana na kumulikia mwanga upande ule huku wakifata kwa tahadhari katika chumba hicho cha hifadhio la magari lililotumika kama gereji ndogo enzi hizo. Kwa pamoja walichutama na kuanza kupagonga gonga kwa ngumi huku masikio yakiwa tayari kusikia mlio, “Mhh hii mbona sio sakafu” Salimu alihoji nakumtazama Karimu ambaye nay eye alithibitisha kwa ugongaji wake kupitia mshikio wa kuruzi. Salimu akaanza kupangusa akitumia mikono yake miwili


Itaendeleaa...
 
Kitu tamu sana hii japo inakuja polepole.ila ni bonge la story. Pamoja sana kiongozi
 
Kitu kizuri sana ila unatupimia sana mkuu fungulia kwa fujo mkuu
 
Kitu kizuri sana ila unatupimia sana mkuu fungulia kwa fujo mkuu
Unajua Bora what's up unaona wangapi wamefungua uzi inatia moyo

Huku Ni kimya kimya unaweza hisi upo mwenyewe tu.

Unajikuta ganzi

Lakn Sasa nimepata moyo wa kuleta za kutosha
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com
0658328596


MSIMU 3

Sehemu 9

Ilipoishiaa...
...cha wote kushtuka na kutazamana na kumulikia mwanga upande ule huku wakifata kwa tahadhari katika chumba hicho cha hifadhio la magari lililotumika kama gereji ndogo enzi hizo. Kwa pamoja walichutama na kuanza kupagonga gonga kwa ngumi huku masikio yakiwa tayari kusikia mlio, “Mhh hii mbona sio sakafu” Salimu alihoji nakumtazama Karimu ambaye nay eye alithibitisha kwa ugongaji wake kupitia mshikio wa kuruzi.

Tuendelee....

Salimu akaanza kupangusa akitumia mikono yake miwili Karimu naye alifata. “Mhhh aisee hebu nipatie kurunzi hapo Salimu aliongea na kuingiza mkono pamoja na kichwa kuchungulia yaliyomo ndani ya shimo baada ya kuliweka bati la chuma la urefu wa mita moja kwa upana wa nusu mita. Salimu alionekana akiwa ametoa macho wazi akiwahaamini alichokuwa akikiona nyakati hizo “Ndugu tumefauru hili sio shimo la kawaida ni chumba cha siri mzee” Salimu aliongea na kujigeuza mwili na kaunza kushuka kupitia ngazi. Iliyokuwemo humo karibu kabisa na sehemu ya uwazi ambao ni mlango kwa wakati huo. “Unasema kweli?!” Karimu na yeye akafuata kuingia.


“Ebwana wee duhh aisee Mzee alikuwa bonge la Jasusi” Mdomo ukiwa wazi macho yamemtoka Karimu aliongea huku akigeuka huku na kule kwa kusaidiwa kuona kupitia kurunzi yake. Palikuwa ni chumba cha siri tena kilicho kuwa kimekamilika kweli kweli. “Hii kweli ni ikulu ya jasusi khaa…mzee mbona kunaonekana kuna harufu ya pafyumu humu” Salimu aliongea akihakikisha kwa kuiweka sawa pua yake “Yeaa ni kweli, inaonekana kuna mtu ametuwahi kaka.” Salimu akaanza kuangaza angaza kurunzi kila mahala “…Umeona atazama hapa hivi si ni vidole kabisa kuna kitu kimetolewa hapa sio ma hardisk?”

Karimu akasogea kuhakiki “Nikweli mzee sasa atakuwa nani?” aliongea Karimu huku akIchukua moja ya saa iliyokuwa juu ya meza na kuitazama vizuri akatabasamu baada ya kuitambua. “…hii si saaa ya kawaida inatumika kama, kinasa sauti na ina kamera vile vile pia inakuonesha sehemu ulipo dahh” alimpatia SaLimu na kumuacha akiichunguza

“Naona sasa tuna msaada mkubwa sana na tuna kila sababu ya kushinda”, Salimu akiwa anashika shika vitu akitazama hiki na kile akafungua droo moja ndipo akakutana na picha iliyomuonesha Muheshimiwa Richard akiwa na bwana mmoja mwenye asili ya kisomali wakiwa wameshikana mabega wakiwa katika sehemu iliyoashiria kuwa pana baridi kutokana na mavazi waliyovaa. “Kuna haja ya kuondoka nayo hii picha” akaitia mfukoni, “…nafkiri tuondoke sasa tumefauru jaribio letu.” Karimu alionekana kukubaliana na wazo hilo. Hao wakatoka.

Kitonga, Ilala- Dar es Salam.
Ochola alionekana akisogea akiwa ameshikilia vikombe viwili “Shikeni vijana” Ochola akakaa na kuchukua bahasha iliyopo mezani na kuifungua akatoa picha kaitazama kwa muda na kuwatzama kina Salimu “Anaitwa Ferdric Shaka Dodo, huyu sio msomali bali kabila lake ni Mtusi aliyelowea Tanzania mwisho wa siku akawa Mtanzania huru, alioa na kupata watoto, alikuwa mfanya kazi serikalini akiwa Wakili binafsi lakini baadae aliteuliwa kuwa Wakili Mkuu wa serikali familia yake ipo Arusha lakini sija jua mahusiano yake na Joka yalikuwa ya namna gani, ninachokikumbuka aliweza kuokoa pesa takribani tirioni 22 baada ya ushindi katika mahakama mbalimbali lakini alipokufa tu Richard na yeye hakuchukua hata mwaka akaomba kustaafu, taarifa za chinichini ni kuwa alilazimishwa na kutishiwa baada ya kunuia kuifatilia kesi ya Mauji ya Richard”

Ochola akaanza kufikiri huku akiitazama tena vizuri picha iliyokuwa kiganjani mwake “…tatizo ni muda mrefu sana umepita, na sijawahi kufikiria kamaa…hebu ngoja mhhh Yes huyu kuna kitu anaweza kutupatia” aliongea Ochola huku akitingisha kichwa kukubali maneno yake.

Salimu kwa makini akamuangalia Ochola “Kiongozi vipi kuhusu taaluma nyingine maana hii haitoshi kuonesha uhusiano wa karibu” Ochola akageuza shingo kumtazama Salimu “Eeehh inawezekana ahhh okay….swali zuri huyu alikuwa ni mmoja ya watu waliopata Shahada ya Computer science kwa watu maalumu aliienda Uiengereza alikuwa peke yake Tanzania nzima, lakini ngoja inamaaana hii ndio sababu urafiki wao na Richard Mhh inawezekana ndiye aliyemtengenezea Richard Web ya Mzalendo!?”

Ochola aliongea na kubinya jicho lake la kushoto akiyatafakari mawazo yake na taratibu akaanza kutyatumbua akitafakari, “Vijana kuna sentensi moja aliiacha ambayo ilileta kizaa zaa kwa watu tunaomjua lakini naamini jamii haikujua aliandika ukurasa wake wa mwisho hivi Ukweli ulionyuma ya mgongo ni sawa na kiza mbele ya macho hata kwa kupapasa huwezi ujua mpaka iwashwe taa, nikipona basi nitaiwasha mshumaa nikishindwa nitaushika utambi” “Mhh mbona maneno hayo mazito sana kiongozi” Salimu aliongea akitafakri “Kwakweli mbona hapo pana mabano nikipona nitauwasha mshumaa nikishindwa nitaushika utambi mhh” aliongea Karimu na kushika kiuno “Mzalendo Web” Salimu alidakia akimkodolea macho Ochola

“Yes, Web ya Mzalendo ni ya Richard na ni siri, ahh hebu liacheni kwanza tutaweza kuchanganyana hapa kichwa kinaniuma” Ochola aliongea akimaanisha kwa kunyanyua mikono yake juu kiasi cha kuwashangaza vijana wake“Inapaswa kufikiria ni nani aliyefika katika yale maficho lakini mimi jawabu ninanalo ninaamini ni Komandoo Swai tu ndio mwenye jeuri hiyo mshenzi yule Richard tulisha mzika au aidha kuwe kuna mtu mwengine tusiyemjua ndiye aliyeingia” aliongea Ochola kwa hasira Tutapanga namna ya kumpata Dodo lakini hamtaenda nyinyi kuna mtu nitampa hiyo kazi” aliongea Ochola na kutoka kwa hasira huku akiwaacha vijana wake midomo wazi.


Itaendeleaa...
IMG-20220103-WA0024.jpg
 
Unajua Bora what's up unaona wangapi wamefungua uzi inatia moyo

Huku Ni kimya kimya unaweza hisi upo mwenyewe tu.

Unajikuta ganzi

Lakn Sasa nimepata moyo wa kuleta za kutosha
Ucjali tupo mkuu
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Tuendelee...

SEHEMU 10: UVAMIZI WA BENK

Dondoo;
“Salimu anapokea taarifa ya uvamizi wa benk kuu ya Tanzania, katika hatua za kukamilisha majukumu anatokea dereva wa tax na kumjeruhi moja ya majambazi na kuwashangaza watu yeye ni nani hasa?! Kabla ya kuamua la kufanya wanapanga mpango wa kukutana na dereva wa tax huku wakipanga mpango wa kumtorosha jambazi lillokamatwa na kufanya mahojiano. Je! mipango yao itafanikiwa?”

Ngome Msitu wa Magamba, Lushoto- Tanga.
Meroda na rafiki zake wakiwa wamejibanza katika mwisho wa jengo wakichungulia kwa tahadhari, mara kundi likaonekana kundi likikatika. Meroda na wenzake wakatoka kulifata huku wakilindana, ghafla wote wakabonyea baada ya kusikika kwa vishindo vya watu upande mwengine, lilikuwa kundi lingine wakielekea upande ule uliokwenda kundi lililotangulia.

Baada ya utulivu kukolea Meroda akajitosa kwa mwendo wa mbonyeo akiwafata nyuma nyuma hadi katika jengo moja refu akatulia akageuka na kutoa ishara kwa wenzake. Baada ya kufika wenzake Meroda kwa ustadi akabetua dirisha la mbao ukapatikana upenyo akaliweka jicho lake na kuchungulia.

Samuel na Pater wakiwa katikati ya nusu duara la kundi la watu. Upande wa nje akaonekana msichana matata ndani ya mavazi meusi ya mterezo yakiwaka waka chini akiwa na viatu virefu akiwa na haraka kubwa akiufata mlango wa jengo. “Hee Jane!” Meroda aliongea kwa mshtuko kwa sauti ya kunong’ona wazi akiwa na wasiwasi. Hofu ikiwa imempanda Meroda aliendelea kutegesha sikio kunasa habari kwa kadri alivyoweza, alipotosheka akang’atuka na kutoka zake kwa staili ile ile aliyoingilia pahala hapo ya nyatu nyatu. Meroda baada ya kuingia katika chumba ambacho wanaishi yeye na wenzake

“Jamani habari mbaya kundi B na kundi F la Jane Dume yalikuwa na kikao cha uteuzi chini ya usimamizi wa Meja Mogisha na Alfani Mashu kwaa ajili ya uvamizi wa Benk Kuu ya BOT kesho kutwa naogopa itakuwaje”

aliongea akiwatazama wenzake mikono ikiwa kiunoni akiibana midomo yake “Mhh hapo wanaenda kwenye vita au maana hao watu sio watu wa mchezo ni vichaaaa wa bunduki” Monica aliongea akiuwacha wazi mdomo wake na kuwatazama wenzake zamu zamu “Sasa tunafanyaje shemeji zangu…. ehhh mungu wangu” aliongea tena na kujishika tama akiwa bado amekaa kitandani “Sijui kwa kweli lakini naona la msingi ni kuwatumia ujumbe mfupi muda huu”

aliongea Meroda huku akichukua simu yake mezani na kuanza kuandika ujumbe na kuutuma. “Vipi umeshamtumia na imefunguliwa tayari?” Samira aliuliza “Yeah nimeshafanya” Meroda akasogeza uso kutazama kioo cha simu “Amejibu tayari…anasema asante kwa taarifa mapema kukikucha atafanya mipango ya kuzuia tukio” mara Meroda akaonekana kuwa na mawazo

“… lakini nina wasiwasi sana jamani sijajua uwezo wao sijawahi kuwaona kwa macho uwezo wao kiasi cha kuwalinganisha na kina Jane wanaofanya mazoezi magumu kila kukicha” aliongea Meroda, Samira akamuangalia Meroda huku akiwa kasimama “Dada wala usijali ni kazi yao binafsi nina imani watafanikiwa” Samira akajitupa kitandani. “Jamani sijui nimwambie na lile lingine” Meroda aliazisha mazungumzo kiasi cha kuwafanya wenzake wamtazame kwa mshangao

“Dada kwani huja mwambia? kama umeamua kumsaidia mtu basi msaidie bila kujali hainahaja ya kuwaza mambo katika negative mind siku akija jua ulijua au unajua utamuu ni taarifa anapaswa kuwa nazo ili wajipange wataanzia wapi” Monica aliongea huku akimtolea macho Meroda,

“Dada sio siri nakuona ujasiri wako umeanza kupotea kwa sababu ya mapenzi na sizani kama utafanikiwa kwa stairi hiyo acha wivu” Meroda aligeuka na kumtazama Monica akionekana kuumizwa na maneno hayo kaisi cha kuandika ujumbe mwengine na kuutuma na kuaambatanisha na picha kisha akajilaza.

Kawe, Kinondoni-Dar es Salam
Muda wote Salimu alikuwa bado kajiinamia tu huku mkono ukiwa umeshikilia simu shingo kaipinda ikitazama pembeni macho yakiwa mekundu na michirizi ya machozi yaliyo kauka kuchola ramani toka machoni hadi mashavuni akiwa sofani, huku sauti ya hodi ikifatana na mlio wa mlango unaogongwa ukiendelea kusikika chumbani humo lakini wala hakuonekana kushtuka wala kujali. Ndipo mlango ukafunguliwa na Karimu akaingia “Kaka kuna nini?”


Karimu aliduwaa kuona hali ya unyong’onyo ikiwa imemtawala ndugu yake wa hiyari hakusubiri akakurupuka hadi alipo. Kinyonge Salimu akanyanyua mkono na kumnyooshea simu. Karimu akaipokea na kutoa password alichokutana nacho kilimfanya ashtuke macho yakamtoka akamtazama Salimu na kujikalisha kitini kama mtu aliyetembea muda mrefu bila kupumzika. Simuni kulikuwa na mtiririko wa picha za Shalon akiwa na Mzee Samuel na maelezo chini yake yakithibitisha hilo, kikapita kimya “…kaka unapaswa kuwa na nguvu Shalon kuwa mtoto wa Samuel haimaanishi kuwa tumeshafeli, ni hatua nyingine na tunapaswa kukubaliana na ukweli uliopo” Karimu aliongea kisha akamshika bega “Kaka kila kitu kitakuwa sawa jiandae tukakutane na Ochola kwanza hata ofisini leo tusiende kwanza” Salimu mara akajikuta akishindwa kujizuia hali ya ubinadamu ikamtawala


Itaendeleaa....

Mambo yameiva huku
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom