Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Story: The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Ilipoishia...


mtuhumiwa atakuwa amekufa kifo cha kusababishwa na majeraha yake tu.” Aliongea Salimu. Mawazo yalionekana kuwa mazuri wote wakaanza kupiga makofi kumpongeza Salimu.

Tuendelee...

SEHEMU 11A: MCHAFUKO
Dondoo.
“Salimu na Karimu wanaamua kumfatilia msamalia mwema dereva wa taxi anayejiita Kidevu, Mzee huyo anawaeleza kuwa aliwahi kuwa mfanyakazi wa Muheshimiwa Richard na alishuhudia mauji yote yakitokea mbele ya macho yake na kutoroshwa kwa kijana Pius kisha anajitambulisha kwa jina la Jumaa Salimu anashtuka, Je! amemkumbuka Jumaa? Nini kitatokea?!!”

Kawe, Kinondoni-Dar es Salam
“Aisee sijasikia habari za Shalon siku kazaa sasa vipi unampango gani au mnawasiliana?” aliongea Karimu na kumkazia macho Salimu, Salimu akajikuta akiuziba mdomo na kuegemea sofa kama mtu aliyechoshwa na habari hiyo “…duuh! kumbe hatuja ifanya ile kazi eehh mambo yamekuwa mengi yakiungana kila kukicha, sijawasiliana nae muda kweli ngoja tutayajenga ila nafikiri kesho tufanye mpango wa kukutana nae asubuhi kabla ya kufanya mawasiliano na Dereva wa taxi” Salimu aliongea “…ni sawa tutafanya hivyo ngoja nikaitazame simu yangu kwanza huwenda alinitafuta. Karimu alinyanyuka na kuelekea upande wa vyumba na kumuacha Salimu akiwa amejishika tama akiwaza. Baada ya amuda wa takribani dakika ishirini Karimu alirudi huku akitabasamu

“Mzee nimeongea na yule mzee dereva wa taxi amenielekeza kwa kumpata na amesema itabidi iwe jioni maana anataka aingie mtaani kutafuta riziki kisha atamaliza mapema kwaa jili ya mazungumzo na sisi” Karimu alikaa na kutabasamu. Salimu akamgeukia “…kwa hiyo sisi tumseti Shalon tukutane naye kabla ya jioni”

aliongea tena Karimu “…yaani katika watu wanaonisumbua kichwa mmoja wapo ni Shalon hata sielewi kuna wakati natamani hata nisimkumbuke maana najua pigo nitakalo kutana nalo” Salimu aliongea kwa huzuni sana. “Najua kaka tutaongea namna ya kukabiliana naye lakini kwanza saizi mtumie ujumbe haraka kuwa unahitaji mkutane kesho mapema alafu asubuhi tutaongea kipi muhimu na kipi sio muhimu basi, najua kuna mambo yatakayotufaa sana” Karimu aliongea huku akitingisha kichwa kukubaliana na kauli yake. Salimu akaamua kuandika kitu na kutuma kwa Shalon “Mzee kwa kuwa umenilazimisha naomba tujadiliane sasa hivi kesho tukiamka tunaamka na mengine tu” aliongea Salimu na Majadiliano yakaanza.

Bunju, Kinondini -Dar es Salam
Mlango wa bafu ulifunguliwa na binti mrembo Shalon akatokeza huku akiendelea kusugua nywele zake ndefu kwa kitaulo kidogo kifuani tauro likiwa limeshikizwa kusitiri maungo yake, akasimama mbele ya dressing table yake kuubwa ya rangi ya dhahabu kisha taratibu akalifungua tauro kwa juu nalo bila hiyana likaanza kuteremka kwa kupanda milima na kufata maporomoko likiacha sehemu moja na kufata nyinginemwisho ukomo ukawa sakafuni akatabasamu kwa kujitazama maungo yake

“Very beuty full, sasa naonekana ni mwanamke sio kasichana” akajigeuza gezua akijitazama sehemu zake huku akijishika hapa na pale kujihakiki alipolizika akainama na kufungua droo na kutoa bahasha moja na kutazama picha ya mwanaume alimtazama kwa dakika kisha machozi ya kaaanza kumtoka “Baba…nitalipa kila kitu kwa ajili yako” akarejesha picha kwenye bahasha na kutoa picha nyingine ikimuonesha pandekizi la mwanamke mrembo mwenye hasili ya kiarabu na mwenye kufanana sana na yeye “Mama sasa usijali lazima nimfanya alipe aliyekutendea unyama”

akaisogeza mdomoni na kuibusu kwa midomo yake mizuri ya mfano wa kopa dogo kisha akarejesha mtoto wa droo pahala pake na kufunga vizuri akajitupa kitandani akiwa mtupu. Akapeleka mkono wake wa kuume kichovu chovu hadi katika simu yake iliyochomekwa waya wa kupitisha chaji toka katika circuit ukutani karibu zaidi na kitanda chake na kutoa password. Akiwa amejilaza chali akagundua jumbe za maneno zilizoingia akiwa anabofya hapa na pale mshangao mkubwa ulimuingia na kubadili muonekano wa sura yake kisha tabasamu likajitokeza surani macho yakamtoka akashindwa kujizuia

“Yes ….Yes thanks God” alinyanyuka na kuruka kwa furaha kitanda nacho kilimpokea na kumrusha juu kama alivyotaka tena tena na tena huku mlio wa swing swing ukisikika aliporizika akatulizana kitandani na kuanza kuandika “Ohh mambo Salimu, habari njema sana kwangu nimefurahi sana nilikuwa nimeacha simu chumbani, usiwe na hofu naisubiri kwa hamu sana hiyo siku” aliusoma kwa sauti kisha akautuma ‘Nitakupata tu safari hii sikuachii’ Shalon alijisemea huku mikono yake akiwa na ngozi isiyo na doa akipitisha mikono katika kifua chake na kubinya binya chuchu zake huku akitabasamu. “Kumbe nimerudi nyumbani wakati muafaka sasa sina haja ya kurudi Morrocco nitawatumia barua ya kuacha kazi mara nikikutana na Salimu wangu” alijisemea kwa sauti.


Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Ilipoishia...


akipitisha mikono katika kifua chake na kubinya binya chuchu zake huku akitabasamu. “Kumbe nimerudi nyumbani wakati muafaka sasa sina haja ya kurudi Morrocco nitawatumia barua ya kuacha kazi mara nikikutana na Salimu wangu” alijisemea kwa sauti.

Tuendelee...
Sehemu 11B: Mchafuko

Samil Resataurant, Kigamboni -Dar es Salam
Kesho ikawa leo Salimu na Karimu walikuwa wamo ndani ya mgahawa pendwa teyali meza ikiwa na vyakula mbalimbali. Wakiwa katikati ya mlo wakifaidi vinono nje kupitia dirisha la kioo gari moja maridhawa lilionekana likiegeshwa na mara mrembo Shalon akaonekana kutoka katika gari akiwa anang’ara kweli kweli kiasi cha kutumbuliwa macho na watu walioingia na kutoka mgahawani hapo gauni lake refu la rangi ya samawati lenye kumeta meta huku akiwa na kipochi cha rangi ya silva miwani yake kubwa nyeusi huku akiwa na viatu virefu vya rangi nyeusi kichwani kishungi cha uongo na kweli kikiwa kimeegeshwa kiushahidi, alivutia haswa. Taratibu mguu mosi mguu pili safarini akiufata mlango wa kuingilia. Akiwa mbele akiangaza angaza nyuma yake kukasikika sauti ya mtu mzee akilalama “Ni saidie mwanagu…” Shalon alisikia sauti hiyo hatua kama tatu tu toka langoni na kumfanya kugeuka,

akamuona Mzee aliyevalia gloves za baridi mikononi na koti la mikono mirefu na kofia anina ya pama kichwani. Hakuitaji maelezo akajisogeza na kumshika mkono akimuongoza njia “Asante mwanangu huu mguu huwa unakataa na kukubali” Mzee kwa uchangamfu aliongea huku akiketi “Usijali we ni kama baba yangu tu” akamuitia muhudumu na kumuaga akapiga hatua akitazama huku na kule kutafuta kitu katika ukumbi huo wa chakula. “Ohh nimewaona” Shalon alijisemea akatabasamu na kuharakisha kuelekea upande mwengine.

“Habari zenu nimechelewa sana ee?” alivuta kiti akakaa, “Waoo shemeji ni wewee” aliongea Karimu kwa bashasha akiendelea kumtazama kwa makini “Leo nimebadilika eehh kiostadhat kidogo” aliongea Shalon kwa aibu akijichekesha macho akiyachimbia sakafuni “Wala hauja chelewa wasiwasi wako tu” Salimu aliongea na kutabsamu, Macho ya Shalon hayakubanduka katika mwili wa Salimu yakienda huku na kule huku mdomo ukiwa wazi kwa uduanzi “Shalon nakielewa unachokifikiria tutayaongea yote, ehh nambie habari za miaka kazaa na vipi wazazi hawajambo?” Salimu aliongea

“Jamani ngojeni niwaache najua mnamengi ya kuongea na msiwe na shaka name” Karimu aliongea huku akinyanyua sahani yake na glass ya kinywaji na kuhamia meza nyingine hatua nne mbele. “Ohh asante mwaya shem” aliongea Shalon akimsindikiza Karimu kwa macho “Shalon…nimefurahi kukuona upo na afya huku urembo wako ukizidi maradufu, pili nakuomba unisamee kwa kukuacha mpweke kwa kipindi kirefu sana” aliongea Salimu na kumfanya Shalon kutabasamu “Unajua nini Honey nilikumisi sana na leo namna ninavyokuona wa tofauti yani umekuwa handsome umejazia jazia umetanuka yani unavutia mpaka nasisimka ndani yani najikaza tu naona aibu kukutazama unajua umebadilika sana umekuwa Jentlemen”

aliongea Shalon huku akikwepesha macho yake yasikutane na Salimu, Salimu akatabsamu “Nikweli shalon wewe pia umebadilika nafkiri usingetutambua kwa namna ulivyo basi ingetupa shida, umekuwa lady mwanamke haswa na sijui niseme nini zaidi ya kusema baada ya mama yangu msichana mrembo pekee anayetawala moyo wangu ni wewe” aliongea Salimu huku akimkazia macho Shalon “Hahaha asante Salimu wangu ohh jamani nimefurahi sana umekuwa na maneno siku hizi” aliongea Shalon huku macho yakianza kuwa na mawingu ya machozi na aibu ikimtawala “Shalon nimekuita leo nataka nikupe sehemu ya maisha yangu usiyoijua”

aliongea Salimu “Samahani dada nikuhudumie nini’’ Muhudumu aliongea na kuwafanya wote kumtazama “Ohh niletee kama hivi” aliongea Shalon huku akichukua kitambaa chake na kujifuta machozi yanayomlenga lenga kisha kayarudisha macho kwa Salimu aliyekuwa amesimamisha zoezi la kula “Ni mambo mazito yanayo kabiri maisha yangu kitu ambacho kilinifanya niwe mgumu kutoa maamuzi...” Salimu alijikuta akishika kichwa chake kwa mikono yote miwili “Shalon nina kazi ambayo ni hatari sana na sio jambo rahisi kumuamini mtu wa kawaida kama wewe” aliongea Salimu na kumfanya Shalon kukunja sura na kumtazama kwa makini kwa macho ya kuonesha kuwa hajaelewa kitu au anataka kuelewa zaidi.

Salimu akavuta pumzi akamtazama Karimu aliyekuwa mbali kidogo akiwatazama huku naye akichukulia kama sehemu ya kujilinda. Salimu akaanza masimulizi kwa kadri alivyoweza mwisho akahema kwa nguvu na kumtazama Shalon ambaye alikuwa anatirikwa machozi akijifuta na kujifuta tena “Shalon naweza kukukaribisha katika maisha yangu lakini awali ya yote naomba nikwambie kuwa chukulia hayo niliyo kukwambia kuwa ni ukweli lakini siku moja utaweza kuupata ukweli ulio kamilika ila kwa sasa ridhikaka kwa haya.” Salimu aliongea “Ninachoweza kusema siku utakapo jua ukweli mwingi usije ukanichukia, tafadhari kula chakula chako kinapoa” Salimu aliongea na kuonekana


Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu 11C: Mchafuko

Tuendelee...

Ninachoweza kusema siku utakapo jua ukweli mwingi usije ukanichukia, tafadhari kula chakula chako kinapoa” Salimu aliongea na kuonekana kunyongeka sana “Salimu Sikiliza, nataka kukutoa hofu na kukuhakikishia usalama wako na usalama wa penzi lako, binafsi najitambua ni msichana wa aina gani naomba usijutie kunichagua”

Shalon alinyoosha mkono wake na kushika kiganja cha mkono wa Salimu juu ya meza kiasi kilichomfanya Salimu kunyanyua uso kumtazama Shalon “Usijali nipo nyuma yako nipo tayari kusubiri hata miaka kumi lakini tu moyo wangu ukiwa katika amani” aliongea Shalon huku akitoa tabasamu zito la mapenzi “Shalon nimekubari kuwa mume wako wakati muwafaka ukifika lakini naomba siku moja nikutambue vizuri kuhusiana na familia yako” Shalon akatoa tabasamu pana kiasi cha kung’arisha uso wake na kuufanya uzuri wa uso kuzidi kwa macho yake ya golori

“Salimu unakaribishwa muda wowote mpenzi ahh naomba nikuche ili uendelee na majukumu mengine ukinihitaji usisite kwa kweli najisikia faraja na amani sana kuwa na wewe, mambo yangu binafsi hivi sasa nitayafanya kwa ufanisi zaidi, yote hayo utayajua muda si mrefu na wewe ukiwa umekwama katika biashara zako usisite kuniambia na sio hivyo mara machimboni mara huku unanisikitisha sana” Shalon safari hii alikuwa ameshika mikono yote miwili ya Salimu huku akiisugua sugua kwa mahaba mazito macho yakiwa machoni mwake. “Sawa Shaloni safari njema”.

Shalon akasimama akajipinda kidogo na kumbusu Salimu aliyekuwa bado kitini na kuachia tabasamu kisha akaondoka zake kwa mwendo wake ule ule wa madaha huku akiziacha sehemu zake za nyuma zikiyumbishwa kama mawimbi kutokana na vishindo vya miguu kiasi cha kumfanya Salimu atabasamu na kukitingisha kichwa juu chini kukubali.
“Vipi ndugu yangu mambo yalikuwaje?” Karimu aliongea huku akikaa kitini karibu na Salimu, “Mambo yalikuwa kama tulivyo panga ila moyo unanidunda sijui hata kwanini!” “Hapana hata mimi ningekuwa hivyo hivyo, ila la msingi ili tusiwe katika mazingira magumu inatubidi tuwemakini hawa mabinti wasijuane kabisa”

Karimu alimaliza na kumtazama mwenzake Salimu akageuka kumtazma Karimu pia wakatizamana kwa sekunde kazaa kisha Salimu akatingisha kichwa huku akitabasamu kukubaliana na wazo la Karimu. “Sawa tutalifatilia hilo…Enhee nambie plan ni ipi ile ile au ” Salimu akajikalisha vizuri akifikiria jibu la kumpatia Karimu, “Yeah” Karimu akatabasamu “…nakupa heko mzee” “…sasa hivi twende town imebaki appoint ment moja” Salimu sasa akasimama Karimu akautoa mkono kumpa tano Salimu kuonesha yupo pamoja nae kisha hao wakanyanyuka kuondoka.

Nyakati Salimu na Karimu wanaondoka, yule mzee wa makamo ambaye kwa muda huo alificha uso wake kwa kuwa bize na gazeti akipekuwa karatasi na kusoma hili na lile lililo mvutia walipopita Salimu na Karimu tu na yeye akanyanyuka akiongoza njia macho yakiwa kwa kina Salimu bira kubainika.


“Habari mkuu nimefanikiwa kumfatilia mwanao na kubaini kuwa alikutana na vijana wale wale wawili na mmoja wake alikuwa ndiye muhusika maana walikuwa wakizungumza muda mrefu” mzee yule aliyekuwa pamoja na kina Salimu katika Mgahawa ule aliongea akiwa siti ya nyuma ya gari moja ya kawaida sana huku akibandua ndevu zake bandia zenye mvi “….ahh inavyonekana ni kitu cha kuhamasisha mapenzi na pia ni kama watu ambao hawakuonana muda mrefu…ndio Mkuu…sawa” alimaliza na kuitia simu yake katika mfuko wa koti lake “Twende zetu” mara moja gari ikaanza kujitoa eneo la maegesho hayo kiivivu vivu na kuondoka kusikojulikana.


Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Ilipoishia...


mapenzi na pia ni kama watu ambao hawakuonana muda mrefu…ndio Mkuu…sawa” alimaliza na kuitia simu yake katika mfuko wa koti lake “Twende zetu” mara moja gari ikaanza kujitoa eneo la maegesho hayo kiivivu vivu na kuondoka kusikojulikana.

Tuendelee...

Sehemu D: Wizi wa Benk
Tandika, Temeke-Dar es Salam
Nyakati za jioni gari moja nyeusi ya bei kali ilionekana kupaki katika maegesho katika mtaa wa Mabatini, na kisha Salimu na Karimu wakateremka wakiwa na miwani zao usoni, hao wakatoka na kuingia katika mikusanyiko ya watu wakikata kona mara kazaa mwisho wakatokea katika maeneo yaliyona taxi nyingi zilizoegeshwa bila mpangilio. “Aisee jamaa anakaa uswahilini kweli” Karimu aliongea na kuruka mfereji wa maji machafu wenye harufu mbaya iliyopelekea kukunjwa kwa sura zao. “Ndio hapa mzee”, Bira shaka ndio hapa kwa maelekezo niliyoyapata sasa ngoja tujaribu bahati yetu maana mpaka sasa hapatikani kwenye simu yake” Karimu aliongea na kuongoza njia kuelekea katika mti mmoja mdogo uliokusanya watu kazaa walika tofauti waliojikalia katika benchi la mbao wakipiga zogo na kubishana. Zogo lao lilisimamishwa kwa salamu iliyotolewa na Karimu. “Ohh salama karibuni mnahitaji Taxi”, Mzee mmoja wa makamo aliongea huku akinyanyuka mkono mmoja ukizungusha funguo zake kwa kidole. “Hapana mzee wangu”,

Karimu akaiweka sawa kola yake kisha akaendelea “…shida yetu hasa ni Mzee kidevu taxi draver yupo maeneo haya au ametoka?”, watu wote kwa pamoja wakaonekana kujawa na hofu wakatizamana kila mmoja akitegea kuongea ndipo mzee yule haraka akaanza kuongea “…jamani kwani nyinyi ni polisi…mana jamaa tuna muona mana leo kaletwa na polisi kesho wanakuja watu wengine wanamchukua na sasa nyinyi…” kabla hajamaliza Salimu akaingilia “…ni hivi mzee ni watu ambao tunafahamiana naye tafadhari tuitie”aliongea Karimu “Hahahaha” yule mzee alicheka kwa dharau akawatizama na kucheka tena “Mme chukka mipaka sasa kwa uwongo ondokeni hajawahi kuwa na jamaa matajiri kama nyinyi hebu ondokeni huko mnataka kumdhuru hata ningejua alipo nisinge waambia” Mzee alifoka kwa jazba.

Kabla ya mmoja wao hajatia neno ikaonekana taxi iiingia kijiweni na kupaki kila mmoja macho yakiwa kwenye taxi ile na mara Mzee kidevu akatoka garini na kukutana macho kwa macho na kina Salimu akaachia tabasamu na kuwafata “Oooh karibuni sana jamani” Mzee kidevu akaasogea na kupena mikono na wageni wake kitendo kilicho staajabishwa na watu waliokuwepo pale. “Kidevu Sasa mbona hatuamabiani mambo haya?” aliongea yule mzee “ Tutaongea mzee bakari usijari…” Mzee kidevu taxi dreva aliwashika mikono kwa pamoja na kuelekea nao katika taxi yake wakaingia wote. “…haya tuongelee kwenye gari” aliongea Mzee kidevu na kufungua mlango “Sawa” wote wakaitika, Sasa tusipoteze muda, sisi kweli ni maaskali kivuli, naomba ushirikiano wako Kidevu” “Sawa”

Taxi dreva alitika na kukaa sawa sawa akiwatazama “Mzee tueleze sababu hasa wewe kumvamia yule bwana na kumpiga ile siku ya tukio la ujambazi” Mzee Kidevu Taxi dreva alionekana kuswajika moyo “Nitawaamini vipi? Na vipi usalama wangu” Salimu na Karimu wakatizamana. “Sawa mtaniambia nini kuniridhishia nami niwaambie msije kuwa mnanizungusha tu hapa” Salimu na Karimu wakatizamana na kupeana ishara. “Hatuja elewa unachokimaanisha mzee” aliongea Karimu na kumfanya Mzee Kidevu kucheka “Sikilizeni mimi namtaka yule bwana nina shida naye kwa sababu alihusika na mauaji ya boss wangu na familia yake yote miaka mingi iliyopita” aliongea kwa ufupi na kuwatazama kina Salimu kwa nyuma kisha akaendelea “Yeye na wenzake waliua kila mmoja lakini walimtorosha mtoto wa boss wangu anaitwa Pius na mimi niliwahi kutoloka maana nilihofia uhai wangu” aliongea Mzee Kidevu na kujifuta machozi. Salimu na Karimu kwa pamoja walitahamaki na kutoa macho.

“Ndio mnashangaa nini mimi nilikuwa mfanyanya kazi wa ile familia naitwa Jumaa, mnadhani ni masighara acheni kabisa vijana nikukumbuka huwa nalia sanaa” Habari hiyo iliwashtua sana wakajikuta wakijizuia lakini Salimu ilimgusa mno mpaka kujishika sehemu zake za kifua karibu na pahala pa moyo akijitahidi kuuzuia na kuusishi upunguze mapigo maana kijasho kilianza kumtoka kutokana na mwili kupanda joto. kwa kuwa Mzee kidevu alikuwa kwa mbele haikuwa rahisi kuona mabadiriko hayo kirahisi yeye akaendelea “…marehemu boss wangu kilichomuuua ni mali zake na walio muua ninachokiamini ni wivu wa jamaa zake wa karibu masikini na kingine ni kama alikuwa na siri Fulani ambayo alikuwa akiishikilia muda mrefu” kwa uchungu Mzee Kidevu alikivuta kitambaa katika mfuko wake wa Suruali ya kitambaa na kujifuta machozi yalianza kumtirika kwa uchungu. Kisha akaendelea

“…Marehemu boss wangu alikuwa na marafiki wakubwa wane alikuwepo Mchungaji Johnson huyu tayari ni marehemu kifo chake mpaka leo hakijafahamika, milionea Samuel na rafiki yake Pater Mwakaza hawa hawa mnao wajua” Mzee kidevu akaanza kuzivuta ndevu zake taratibu huku akiupendisha midomo yake kulia na kushoto kwa ghadhabu huku akiwa ameikazia macho usukani wa gari. “…mmeona Richard Samuel na Pater hawa wote walikuwa wafanya bishara wakubwa tu ila baadae marehemu boss wangu aliamua kujitoa, mi pia sikuona ubaya wake hapo alijitoa na kuanzisha kampuni yake mwenyewe na kwa bahati nzuri ikawa yake akajikuta akipata mafanikio makubwa na kuwazidi hata wenzake na hapo ndipo tatizio lilipo anza mahusiano yakafa” Mzee Kidevu akagonganisha viganja vyake vya mikono na kutingisha kichwa akisikitika.

Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu E: Mchafuko

Tuendelee....


"....mmeona Richard Samuel na Pater hawa wote walikuwa wafanya bishara wakubwa tu ila baadae marehemu boss wangu aliamua kujitoa, mi pia sikuona ubaya wake hapo alijitoa na kuanzisha kampuni yake mwenyewe na kwa bahati nzuri ikawa yake akajikuta akipata mafanikio makubwa na kuwazidi hata wenzake na hapo ndipo tatizio lilipo anza mahusiano yakafa” Mzee Kidevu akagonganisha viganja vyake vya mikono na kutingisha a akisikitika. Salimu na Karimu tuli walikuwa wametulia wakimsikiliza kwa makini

“…mwisho wa siku dahhh sitaweza isahau ile siku jamani…” safari hii alishindwa kujizuia na kuanza kulia kama mtoto kiasi cha kuwatoa machozi kina Salimu “…vijana ni lazima muifanye kazi kwa ajiri yangu tafadhari…achaneni kuwaamini hao boss zenu na maaskali wengine itakuja kuwa kosti” Masikini Mzee kidevu sasa alitonesha kidondaa alianza kuliaa kwa uchungu aliliaa kimya kimya Salimu na Karimu kaanazakazi ya kumbembeleza mpaka akatulia na kuendelea “…nilishindwa vumilia kutazama watu wakiuwawa mbele ya macho yangu kupitia dirisha la kioo najilaamu kwa ubinafsi wangu nilijikuta nikitamani kunusuru nafsi yangu na…” Mzee Kidevu aligeuka kuwatazama kina Salimu ambao nao macho yalikuwa mekundu kwa maaumivu wanayo yajua wenyewe Mzee kidevu hakushngazwa alichokiona ni kuwa nihuzuni ya masimulizi tu akaendelea

“…nilikuwa na akili zangu timamu nikamuona Samuel ameegemea gari lake usiku ule akivuta sigara nikaaambaa ambaa na ukuta na kutimka kwenda kusimamia mbali nikiwaza cha kufanya na ndipo…” alijikuta kitulia kwa muda na kukazia macho usukani wa gari akajifuta uso na kusikitika kwa kutingisha kichwa akaendelea “…na ndipo nikaona nyumba ya boss wangu ikiteketea kwa moto hapo nilikuwa kama zuzu Fulani sikuamini nilichokiona machoni mwangu vijana, eeehh fikirieni kwa ubaya gani mpaka kuwachoma watu kama mishikaki kwa moto jamani” aliongea Mzee Kidevu “…vijana naomba tufanye kazi pamoja kwa siri” aliongea tena Mzee kidevu kwa macho ya ombi “Sawa pole sana Mzee tunaomba tukuache naona muda umekwenda sana na nitakupigia simu tukutane pahala tuyajenge vizuri juu ya kesi hii sawa” aliongea Salimu na kumpa mkono Karimu na yeye akafanya kisha hao wakaondoka zao na kumuacha Mzee Kidevu akitabasamu huku akifuta machozi yake kwa mikono


Bunju, Kinondini -Dar es Salam
Makaribisho ya usiku yalianza kutwala kijua kikiwa kimezidiwa na giza linalotawanyika kwa mbali manyunyu ya hapa na pale yakishuka Shalon alionekana akishuka katika tax mkononi kashika vifuko, alipomalizana na dereva akalipa mgongo gari na kutembea hatua zenye haraka akiielekea nyumba moja yenye muonekano wa kifahari sana huku sura yake ikiwa imeshiba furaha ya kutosha “Jamani mvua” alijisemea huku akijikunyata akijikwepesha na manyunyu lakini haikuwa msaada. Juu ya ghorofa dirishani Mzee Samuel katika moja ya vyumba alionekana akitazama nje mkononi akiwa na glass ya maji, akanyanyua mkono wake na kutazama saa kisha akatabasamu kidogo na kutoka eneo lile. Mlango ulifungwa na Shalon akaingia sebureni akijiweka sawa huku akijikagua mara alipatwa na mshtuko Mzee Samuel alikuwa anashuka ngazini akiwa kanawiri akatabasamu akikuna kipara chake. “Ohh dady….shikamoo” Shalon aliongea wasiwasi umemjaa macho ya kiwa ya kipepesa hayatulii. “Ohh surprise to you my doughter welcome” mzee Samuel mikono akitanua akimaanisha kumbatio kwa mwanawe wakati huo ameshamaliza kushuka ngazi, Shalon akasogea kukumbatiwa na baba yake kisha pamoja wakasogea kukaa katika sofa.

“Mwanangu mbona unaishi kama mtoto wa masikini Fulani hivi…” Mzee Samuel aliongea baada ya kujikokholesha, binti mmoja akiwa na mavazi ya upishi alionekana kusogea pahala hapo “Habari dada Shalon…nikuletee kinywaji gani”, “Salama nitachukua mwenyewe tu usijali dada” Shalon kwa tabasamu aliongea “Haya asante” Binti huyo akashika njia. Mzee Samuel sura ikakunjamana sana kiasi cha kuchukizwa sana Shalon akatulia “Mwanangu hivi unataka maisha ya namna gani, unanishangaza sana” akajikuna upande wa shavu la kulia “…nimekupa gari mbili za kifahari huzitaki zimekaa tu hapo nje, nimekwambia kaa tu ufurahie maisha lakini umeng’ang’ania kazi ukaenda fanya kazi Morroco na ukakataa kusimamia baishara za baba yako…nimetaka uishi kama malkia hapa lakini hutaki na ulinzi nao hautaki ahhh…” Mzee Samuel alitulia sura ikabadirika na kuwa na huzuni, “Haya tuachane na hayo…nambie unampenda yule kijana sio?” ilikuwa ni taarifa ya kumshtua sana Shalon moyo ukamfanya paaa! “Nambie mwanangu unampenda sana” Shalon akiwa bado anajiuliza uliza akatwangwa swali lingine

“Anaitwa nani?” Shalon akatafakari la kumjibu “Baba nampenda, yeye pia ananipenda lakini kwa sasa kukwambia jina lake ni mapema sana” macho ya Shalon yakiwa na aibu na wasiwasi yakaelekezwa chini kutazama mifuko yake aliyoongozana nayo toka safari iliyokuwa sakafuni. Mzee Samuel taratibu akaanza kutabasamu Mwanangu nimefurahi kusikia hivyo, lakini sio kwamba nakufatilia kwa ubaya laa , nakulinda na watu wabaya” “Baba napenda kuwa huru sana na maisha yangu lakini bado unanifatilia kila siku” Mzee Samuel alitulia kwa muda “Ni kweli nimekufatilia sana siku nyingi hii ni baada ya kukuona hauna furaha, wewe ni mtoto wa mtu maarufu sana sasa ulinzi ni muhimu sana kwako kwa kifupi kila siku unalindwa nakufatiliwa” Shalon ilionekana kumsikitisha sana habari hiyo alionekana kuchukia akanyanyuka huyo na kuondoka zake.

“Mwanangu mwambie huyo kijana aje ajitambulishe mara moja nitakuoza sitajali chochote zaidi akupende kweli” aliongea Mzee Samuel Shalon akiwa na hatua tatu tu toka pale alipo kuwa kakaa akatabasamu kiasi cha kuthibitisha kufurahishwa huyo akaenda zake kuelekea upande wa ngazi. “Unafanana sana na mama yako binti yangu” alijiongelea kwa sauti wakati huo Shalon akiendelea kupanda ngazi “Nimefurahi sana kusikia upo katika mahusiano na mtu unaempenda s” aliongea Mzee Samuel huku akitabasamu machoni machozi yakimlenga . Shalon kwa furaha alipanda ngazi haraka haraka na kukimbilia chumbani akafungua na kujitupa kitandani akipiga kelele za furaha.

Itaendeleaa...
 
Zote hapo just Ni sehemu ya 11 Mchafuko, nimesagau kuweka na sijui namna ya kuedit
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika???

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu 11F: Mchafuko

Ilipoishia...

mahusiano na mtu unaempenda s” aliongea Mzee Samuel huku akitabasamu machoni machozi yakimlenga . Shalon kwa furaha alipanda ngazi haraka haraka na kukimbilia chumbani akafungua na kujitupa kitandani akipiga kelele za furaha.

Tuendelee....

Muhimbili National Hospital, Kinondoni- Dar es Salam
Karibu kabisa na saa kumi na moja asubuhi kigiza kikiwa kina randa randa Komandoo Ochola, Salimu na Karimu walikuwa wamo Hospitalini. Kwa tahadhari Komandoo Ochola akiwa na vijana wake wakaingia katika moja ya chumba na kufunga mlango. Mara taa ikawashwa macho kwa macho wote wakayakutanisha kwa Jambazi, “Haaa Mgaya imekuwaje? Kimetokea nini mbona sielewi!?” Komandoo Ochola macho yamemtoka akipiga hatua za kuchoka na kumshika bega Mgaya “Mgaya ni wewe?” Mgaya kwa tabu alijitahidi kunyanyuka baada ya kuisikia sauti anayoifahamu huku macho yakimtoka “Ocholaaa, Ochola we ni mzimaaaa hujafa Ocholaa” aliongea kwa tabu na yeye akiwa haamini macho yake


“…acha tu ndugu yangu sijui hata pakuanzi…ulipokuwa umepotea tulipata mission ya kwenda DRC yaliyotukuta huko tuliyofanyiwa ni mabaya sana na baadhi ya wenzetu tuliuana kama kuku baada ya kugawanyika makundi mawili, sababu kuu ni uchu wa madaraka kwa kweli jeshi liligawanyika na kuchafuka watu tukawa hatuaminiani tulibaki kukukumbuka tu Ochola mi nilinusurika katika msitu wa kongo nikatokea Rwanda nikiwa sina hili wala hili dahh”. Alimaliza Mgaya kwa uchungu “Aisee mi nipo na vijana hapa tuna kazi maalumu ya kusafisha nchi na kumtafuta Komandoo Swai kwa udi na uvumba najua ndiye tatizo na mtu mbaya zaidi” aliongea Ochola Mgaya akatabasamu

“Nimefurahia sana maamuzi yako Ochola mi pia nilitamani sana kuyafanya hayo lakini sikuwa na wakumuamini na tena nilipokuja kugundua nimewekwa katika watu marehemu na mafao yangu yote kuliwa nilijikuta nakuwa masikini wa kutupwa mmoja mbaya wa kukaba na kuibia watu usiku ndipo nikajikuta nikiingia katika njia hii ndugu yangu” aliongea Mgaya na kujifuta machozi yaliyokuwa yamejaa machoni mwake. Salimu na Karimu walijikuta wakijiinamia tu sura zikiwa zimewashuka “Vijana tuna weza anza kazi yetu tafadhari anzeni mhojiano” aliongea Ochola huku akirudi nyuma taratibu

“Ndio mnaweza kunihoji kuweni huru mnataka habari gani ya maboss zangu majina ya viongozi wala rushwa mafisadi, majambazi au mnataka majina ya watu wanaofanya biashara ya siraha na madawa ya kulevya mnataka nini?...” aliongea Mgaya huku akitabasamu kisha akaendelea “…nitaongea kila kitu na kutubu kwa mola wangu hata mkiniua pia nipo radhi” alimaliza na kuendelea kuwatazama kina Salimu,

“ Ni sawa naomba kujua tu majina kamili ya mabosi zako bishara wanazozifanya washirika wao ni kina nani, maskani yenu ipo wapi idadi yenu, na ni watu wanamna gani na mnafanyaje shughuli zenu zote kwa ujumla” aliongea Karimu. Maohojiano ya pande mbili yakachukua nafasi kadri walivyopanga ikawa bandika swali bandua weka lingine toa. “Ni saa kumi na mbili kamili sasa muda hauna rafiki, asante Mzee Mgaya kwa ushirikiano wako nina mambo ya nyongeza tafadhari” aliongea Salimu akimtazama Ochola kisha Karimu kwa utulivu kisha akayarudisha macho kwa Mzee Mgaya “Ndio endelea...” aliongea Mgaya “Asante, hivi unakumbuka kifo cha Muheshimiwa Richard Edward pamoja na familia yake?..unakumbuka ubaya mlio mfanyia” Machozi yakiwa yana mlenga lenga,

Hamadi Salimu akatoka kwa nguvu na kumsogelea Mgaya lakini hakuwa wahi Karimu Alisha mzuia na kumuweka kando akimpiga piga mgongoni “Tulia kaka punguza jazba kidogo” aliongea Karimu wakati huo Salimu hasira zikiwa machoni akijaribu kujizuia kifua kikipanda na kushuka kwa hasira “Bira shaka wewe utakuwa ni mtoto wa Richard…wewe ni Pius, pole kijana nimefurahi kukutana na wewe hapa ni stori ndefu kijana” aliongea Mgaya na kumfanya Salimu aliyekuwa kajiegemeza ukutani akituliza hasira kugeuka taratibu na kumtazama “ Dunia ina mambo ya ajabu sana ni hivi mimi niliye okoa maisha yako siku ile sikujua kisa cha mauaji ya familia yako mpaka sasa sikuwahi kujua sababu hasa ya kuuliwa kwa familia yako lakini ninachokihsi ni mambo ya kimapenzi,wivu,chuki,kisasi ndivyo vilivyochukua uhai wa baba yako ila kwa sasa naomba unisamee sana kwa jambo hilo”

Salimu akamtazama sana Mzee Mgaya akatizama chini akajifuta chozi kwa tabu akaongea “…ni sawa na pole kwa majeraha yako, inamaana hakuna unachokikumbuka siku hiyo?”. “Shukran kijana wangu najua sina maisha marefu tangu sasa najua nitakufa nashukuru imekuwa sababu ya kufumbuka macho leo wewe niliye okoa maisha yako umekuwa sababu ya kunirudisha kule nilipo kuwa awali asante…lakini kuna kauli aliongea siku ile baba yako ilimaanisha kuwa kuna mtu mwengine pia aliyekuwa anahitaji maisha yake tofauti na rafiki zake kwa sababu…” Mgaya akashusha pumzi kidogo na kuwatazama kisha akaongea “…sijui lakini sisi hatukumuua baba yako aliuwawa na kijana ambaye mpaka hivi leo sikumjua na wala sikupata mtu wa kunipa jawabu zaidi ya kusisitizwa ninyamaze tu”

Kila mmoja chumbani hapo alionekana kushangazwa na kutoa macho yanayosema “KIVIPI” Mgaya akaendelea “Siku ile kijana tukiwa garini kwa ajili ya mauaji nilipokea ujumbe mfupi ulio sema “Hakikisha mtoto Pius hafi” lakin niliona na wenzangu wakitazama simu zao kana kwamba wajumbe walizotumiwa kwa kweli sikujua ujumbe ule ulitoka wapi na wala sikuwa na jeuri ya kumuuliza mtu yeyote mpaka leo, lakini siku ile…” Mgaya akajiweka sawa na kuendelea “…ilikuwa tuuwawe wote na baba yako lakini alitokea mtu...

Nani alitokeaaa usikoseee kufatilia.....
 
The Hidden Truth Ukweli Uliofichika

Nani Anahusika!

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu 11G: Mchafuko

Ilipoishia....
kushangazwa na kutoa macho yanayosema “KIVIPI” Mgaya akaendelea “Siku ile kijana tukiwa garini kwa ajili ya mauaji nilipokea ujumbe mfupi ulio sema “Hakikisha mtoto Pius hafi” lakin niliona na wenzangu wakitazama simu zao kana kwamba wajumbe walizotumiwa kwa kweli sikujua ujumbe ule ulitoka wapi na wala sikuwa na jeuri ya kumuuliza mtu yeyote mpaka leo, lakini siku ile…”


Tuendelee...
Mgaya akajiweka sawa na kuendelea “…ilikuwa tuuwawe wote na baba yako lakini alitokea mtu ambaye hatukumuona kabla na kummiminia risasi za mgongoni nyingi kisha alipanda ghorofani akashuka na bahasha akaondoka zake wazi alionekana kama mtu aliye tumwa kusimamia zoezi pindi tukishindwa kulifanya na alikuwa jasiri sana kama mtu aliye wahi kuua kabla lakini macho yake yalionekana kama ni mtu mwenye kufanya kitu kwa shinikizo Fulani sijui alionekana kuwa mwana familia yule jina lake silikumbuki” aliongea na kuonekna kuwaza kitu “Mzee lakini siku ile uliyo kamatwa kuna mzee alikuwa anakusurubu je unaweza kutuambia kwanini” Karimu aliuliza “Ohh vizuri sana kijana hapa nilikuwa nawaza lile tukio, yule mzee alikuwa akinipiga na kuniuliza yupo wapi Mtoto Pius, nakumbuka alisema tumesababisha maisha yake kuwa magumu alafu akasema tena nimtazame usoni je namkumbuka”

Salimu akameza mate na kutafakari , muda huohuo mlango ukaonekana kufungwa kwa nje kila mmoja akashtuka “Jamani kuna mtu anatupeleleza” Salimu aliongea na kumshtua Karimu kwa ishara amfuate, wakatoka nje ya chumba na kumuona mtu aliyevalia koti jeupe akitembea kwa haraka mara akakata kushoto “Shenzi kuna spy hapa” akaanza kumkimbilia huku Karimu akimfata kwa nyuma upande mwengine walionekana watu waliovalia nguo nyeusi wanaume watatu wakikimbia kuelekea lango kuu la Hospitali “Karimu harakisha kuna matatizo” Salimu akaongeza kasi ya kukimbia na kuwaacha watu wakibaki midomo wazi. Mara milio ya risasi ikasikika kwa nje “Mamaaa tuna kufaa mamaaa” kelele zilisikika watu wakitawanyika kunusuru maisha yao.

Salimu na Karimu kwa tahadhari wakaharakisha hadi nje kabisa walichokikuta kiliwaacha midomo wazi “Jumaaaaaa” Salimu aliishia kutamka kwa mshangao akiwa kasimama na kumtizama Jumaaa akitapa tapa kunusuru maisha lakini wapi aliaga dunia huku Salimu akiwa kasimama asijue la kufanya uso ukiwa umempwaya kwa mshangao Karimu akiwa nyuma yake. Mara akagutuka nakuchukua simu yake mfukoni akapiga na kuiweka sikioni “…Hi…Meroda hivi tofauti na nyinyi kuna mtu mwengine anaye mfatilia Mgaya…Shit Karimu hapa kuna HIDDEN TRUTH mzee wakina Meroda hawahusiki na haya mauaji hebu tumtafute Meroda haraka”. Salimu aliongea macho ya hasira yakiwa yamemtoka. “Tuondoke haraka hapa turudi wodini”. Nyakati Salimu wakiwa wanatembea katika koldo wakipishana na watu waliochachawa na milio ya risasi wakikimbizana wao vichwa vilikuwa juu juu vikitafuta wakumshuku wakakutana uso kwa uso na Meroda akiwa amevalia mavazi ya nesi huku akiwa ameambatana na Monica tu Samira naye akafika “Dada kila kitu kipo sawa sasa tuharakishe kabla mambo hayaja haribika” Samira aliongea huku macho yakiwa na wasiwasi, Salimu alibaki kumkazia macho akiwaza kitu akimtazama

“Mpenzi tutawasiliana badae” Meroda aliaga na kuondoka na wenzake, Salimu alibaki kumtazama tu Samira “Kaka…” Karimu aliongea na kumtoa Salimu mawazoni “Una nini nimekuona ukimtazama sana Samira” “Yesss” aliongea Salimu huku macho yamemtoka akiwatazama kina Meroda wakienda “Kuna kitu mzee inatupasa tukijue kuhusu Jumaa hiki sio kifo cha kawaida” Salimu akamshika mkono Karimu na kuanza kundoka “Sisi pia tupo katika hali mbaya tuwe makini” aliongea tena Salimu kisha wakaondoka.

Baada ya Lisaa kupita

Ikonga, Kinondoni-Dar es Salam.
“…Ni mambo ya kuogopesha sana kwa raia na jeshi la polisi kutia aibu kwa kushindwa kuhakikisha usalama wa raia hospitalini hapa naomba radhi kwa wagonjwa na wauguzi wote na watanzania kiujumla kwa tukio hili, ni kweli asubuhi hii kumetokea kwa majibizano ya risasi ya watu wasiojulikana wenyewe kwa wenyewe na kupelekea kusababisha kifo kwa mtu aliyetambulika kwa jina la Jumaa aliyetembelea Hospilini hapa asubuhi hii na baada ya dakika kumi na tano tu mtuhumiwa Mgaya aliyekamatwa kwa kesi ya wizi wa fedha za benk na yeye aliripotiwa kuaga dunia, jeshi la polisi limechukua kesi zote mbili na kuzifanyia kazi na uzembe wote ukibainika wahusika watachukuliwa hatua mara moja” aliongea ASP Kamandaa Watito kupitia kituo cha Habari cha Taifa wanahabari wakiwa wamemzunguka

“Kiongozi” salimu aliita na kuizima luninga Ochola akiwakajiinamia akanyanyua kichwa “Amini maneno yangu tuna kazi ngumu sana kama nilivyokwambia awali mpaka sasa simuamini Mgaya wala maneno ya Jumaa Mzee Kidevu tuliyekuwa tuna mtegemea kama shahidi na yeye inawezekana ni muongo vilevile au asiwe Jumaa tuliyemzania maana kule anapoishi hana familia ni yeye tu watu anaoishi nao sio familia yake alafu Jumaa mwenyewe kweli aishi kiholela holela tu kilichomfanya aje kutupeleleza na kutukimbia ni nini yeye ni nani lazima tujue alikuwa nani? isitoshe kile alichotuhadithia kinaweza kuwa kweli au sio kweli sasa nani mkweli?...shit” Kwa hasira Salimu akaigonga meza kwa nguvu “Kiongzi naomba tukapumzike vijana wako” Salimu akakusanya mikono ya ombi Ochola akatingisha kichwa kukubali hao wakanyanyuka na kuanza kuondoka.

Itaendeleaa...

Taadhari usikoseeee
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Nani Anahusika!!!??

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu 11H: Mchafuko

Ilipoishia..

...sasa nani mkweli?...shit” Kwa hasira Salimu akaigonga meza kwa nguvu “Kiongzi naomba tukapumzike vijana wako” Salimu akakusanya mikono ya ombi Ochola akatingisha kichwa kukubali hao wakanyanyuka na kuanza kuondoka.

Tuendelee...

Kawe, Kinondoni-Dar es Salam
Mlio wa ujumbe wa maneno ulimtoa katika dimbwi la mawazo dhahiri alionekana kukasirika kiuchovu akanyanyua mkono wake wa kuume hadi katika simu na kuinyakua huku sura ikiwa na makunyazi, “Kesho watatoka mafichoni safari ni kurudi Morogoro na barabara ni hiyo ya Morogoro Dar majira ya saa tano asubuhi, mengine tutawasiliana” Salimu aliousoma kwa sauti “Saa mbili usiku, sijachelewa” aliongea tena akitazama saa yake mkononi. “lazima niwapate” aliongea tena akakurupuka sofani na kuelekea upande wa vyumba akaingia kimoja wapo na muda mfupi akatoka na kuingia chumba kingine dakika tano tu pekee alitoka akiwa na Karimu huku wakiweka sawa suti zao.

HOT spot club, Ubungo- Dar es Salam
Mziki laini ulisikika ukirindima tokea upande wa mbele ambapo watu kazaa walionekana wakiwa wameshikana viuno wakienda taratibu na kurudi wakifatisha midundo ya ala za muziki zilizoshereheshwa na muimbaji wa nyimbo za laivu akiiga sauti Fulani Fulani za wasanii wakubwa toka pande za dunia. Ilikuwa ni DDC Mlimani Park Orchestra band ikiwa imealikwa katika ukumbi tulivu wa Hot spot. Sehemu za mbele zaidi toka katika upande wa stage Komandoo Ochola alikuwa akitingisha kichwa kukipeleka huku na huku akiiimba “…tena bila kinyongo moyoni mwangu…ahh Neema” akatabasamu akitingisha kichwa chake kufatisha midundo.

Pembeni yake kulikuwa na bwana Jeff ambaye na yeye alikuwa na ya kwake akimtazama mwanadada mrembo aliyeingia na kuelekea upande wa vinywaji akiliaacha gauni lake refu jekundu lenye mpasuo wa haja lililoishia kifuani huku likiachia sehemu kubwa ya maziwa yake kuonekana na sehemu zake za nyuma kubwa zikitikisika kwa kila hatua aliyoipiga, alibaki kujilamba na kujichekea lakini haikusababishwa na pombe aliyokuwa anakunywa. Ochola alimuona na kutamani kutazama kinachomfurahisha kijana wake “…ni watamu lakini wakati mwengine ni siraha kubwa zaidi ya nuclear be careful” aliongea Ochola “Habari za usiku huu tumechelewa sana ee?” Salimu akavuta kiti na kukaa, “Sio tatizo kubwa…” Ochola aliongea. “Mara zote tunafurahia vinywaji laini kuburudiisha nyoyo” Salimu alimimina juisi glasini “Ndio maana tukawaagizia kabisa asali zenu” aliongea Ochola na kutabasamu kisha akendelea “…ndio vijana bila kupoteza muda tuanze,

kwanza kabisa tujipongeze kwa kazi kubwa tuliyoifanya siku nzima yenye maumivu sana, kingine ni kuwa teyali nimepata jina kamili la mtu mliye mfahamu kwa jina la Jumaa Zabibu hilo sio jina lake halisi” aliongea Ochola na kumfanya kila mtu kuacha anachokifanya na kumsikiliza Ochola akachukua glass yake na kupiga fundo moja kisha akaendelea “Ndio, anaitwa Jacob Silvester Mkuyu yeye mwanajeshi toka katika kundi la jeshi la anga na cheo chake ni Luteni, kwa hiyo inamaanisha alikuwa spy ndani ya nyumba ya Muheshimiwa Richard lakini haija bainika alikuwa akimfanyia kazi nani kama ingekuwa ni Richard mwenyewe basi isingeishia kumuua” aliongea Ochola “Aisee nilikuwa na hisia za namna hiyo lakini Kiongozi kwani Mzee alikuwa akimfanyia kazi nani”

Salimu aliongea nakuuliza mara mlio wa simu ukasikika na kukatisha mawazo ya kila mmoja, Ochola akachukua simu yake na kupokea “Hallow…ndio…” aliongea Ochola na sura ikaanza kubadilika taratibu akakata simu na kuiweka mezani kinyonge akawatazama vijana wake “Vjana tuna bahati mbaya nimepokea taarifa kuwa Wakili Dodo jioni hii alipotoka kwa ajili ya mazoezi na mbwa wake hakurudi na alipo fatiliwa ulikutwa mwili wake kwenye korongo kichwa kikiwa kimepasuka vibaya wanasema ni ajali ya gari, tumewahiwa hatuna bahati” Ochola akakishika kichwa chake na kukitingisha akitazama chini

“Kikweli alipewa kazi na marehemu Muheshimiwa Meza aliyekuwa Raisi wa Jamuhuri ya Tanzania na akakabidhiwa kwa Fanuel Mkwasi ambaye ni Waziri Mkuu wa hivi sasa kipindi hicho Raisi wa sasa bwana Mkuchu alikuwa ndiye mtu wa siri na mshauri aliyewahi kuaminiwa na Raisi Meza na Fanuel Mkwasi najua mnajua ndiye aliye uunda umoja huu tulio nao, tunapaswa kuwa makini sana maadui zetu wanatuzidi hatua moja mbele na kupita katika akili zetu” alimaliza Ochola na kumfanya kila mtu kujiwazia lake “Samahani hivi tofauti na sisi ni nani anayejua taarifa za kufatiliwa kwa Bwana Dodo” aliuliza Samuel “Fanuel Mkwasi anajua na ndiye aliye mtuma kijana wake amfatilie Dodo, Muheshiwa Raisi halijui hili” aliongea Ochola akiwa na wasiwasi wa wazi “Je na kuhusu mimi ni Pius na tulikutana na Jumaa nalo nani anajua kati yao”

aliuliza tena Salimu akimtazama Ochola machoni “Hili la kuwa wewe ni Pius tulishakubaliana kuwa hatutakiwi kulisema lakini la Jumaa kukutana na nyinyi hili analijua Mkwasi maana yupo nyuma pia kulifatilia” aliongea Ochola huku akimtazama Salimu kwa macho ya viulizo “Sawa, kwa upande wetu taarifa tuliyo nayo ni kuwa majambazi waliohusika na wizi wa benki kesho wataanza safari ya kwenda Lushoto nyakati za saa tano asubuhi kesho” Salimu aliongea na kurudisha mgongo nyuma kuegemea kiti cha plastic huku mkono wake wa kuume ukiwa umeshikiria glass. “Okay timu mnamawazo gani ya kurahisisha kazi, maana hapo piga ua kutakuwa na mabishano ya risasi hivyo ni kuchagua njia ambayo ni salama” Ochola aliongea na Majadiliano yakaanza “…minaona hamna jinsi hii kazi tufanye na jeshi la polisi” aliodokeza Karimu “Kivipi?” Jeff aliiiuliza na kumtazama machoni Karimu.


“…rahisi, ni hivi tuombe watu makini toka jeshi la polisi wakiwemo wale wa barabarani na kuunda kikosi kitakacho kuwa chini yake Kamanda Mkuu tukipata aina ya gari na namba zake za usajili hapo itakuwa rahisi tu” Karimu akatoa macho na kuendelea “…lakini kunahitajika maboresho kidogo…lengo likiwa ni kuwa weka mtu kati wengine wakitokea barabara ya moro gogoro na wengine Huku Dar kabla ya Chalinze hivyo tutatengeneza ajali ya makusudi na kuwakamata wakiwa kati” Karimu alimaliza na kuwafanya watu wote watabasamu “Yaaah iko poa sana…Sasa tuiboreshe kwa kuijaza nyama inenepe” . Mjadiliano yakaanza wakibishana na kuendelea kuwekana sawa kadri walivyo weza mwisho wakaafikiana na kuagana.

Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 3

Sehemu 12A: Mchafuko

....watabasamu “Yaaah iko poa sana…Sasa tuiboreshe kwa kuijaza nyama inenepe” . Mjadiliano yakaanza wakibishana na kuendelea kuwekana sawa kadri walivyo weza mwisho wakaafikiana na kuagana

Tuendelee..
High Way, Ubungo, Dar es Salam
Kwa muda wa dakika mbili nzima wanaume wawili walibaki wakitazamana kila mmoja akimsubiri mwenzake kuongea, mmoja wao akakata shauri “Samahani Ochola naomba uniambie ni kipi nisichokijua mpaka sasa unanifanya nitoke nyumbani usiku kama huu mzito eeh na hata kunimegea siri ndugu yangu maana muda mrefu sasa nimekuwa nikifanya kazi na watu nisio waona na hata kupitisha maagizo bila kuyatambua vizuri” alilalamika IGP Lugole Mateasi “Najua ni mtu muungwana sana ndomana ukapewa cheo hicho na Raisi”

Ochola akajikuna kichwa chake “kikubwa fata maelekezo ikifikia hatua ya kujua utajua…nahitaji timu iongozwe na Kamanda Mkuu wa mkoa ASP Japhet Mokiwa mataharisho yawe asubuhi saa tatu mission inaanza bila kukosa” Ochola akanyanyuka na kuweka nyaraka juu ya meza “ Maelezo mengine muhim yapo hapo” Ochola huyo akanyanyuka na kuondoka zake akimuacha IGP Lugole Mdomo wazi.

Morogoro Road, Ubungo-Dar es salam
Asubuhi tulivu ilipambwa na kajua kalichokuwa kakichomoza kwa maringo na kuwaburudisha watu wote walio kuwa wakienda na kurudi wakikwea magari wengine wakitembea kwa miguu na wale wakiendesha baiskeli, kila mtu alikuwa bize akiwa na lake kichwani kama ilivyokuwa kwa Salimu na Timu yake iliyobana kando ya barabara ikifatilia gari zote zinazopita wakiwa garini “…okay tumeshawapata hawa mbwaa”. Salimu alijiongelea akiwa ndani ya gari pemebezoni mwa barabara. Mara moja aka forward kwa Komando ochola na Karimu, Salimu akiwa katulia eneo la mbezi ya Kimara macho makini yakiwa upande wa ng’ambo ya barabara ambpo kulikuwa na barabara ya vumbi, dakika chache mbele gari ndogo nyeupe aina ya Mazda yenye vioo vya tinted likangia barabarani na kufata njia ya morogoro. Haraka haraka akaanza kuandika ujumbe wa maneno kisha safari ya kuifatilia gari nyuma nyuma ikaanza.

Msafara wa kimya kimya huku kila askali akiwa na hamu ya kushambuliana na majambazi ulikuwa upo juu juu kihemu hemu kiliamsha hisia zao na hasa Kamanda mkuu wa Jiji aliyekuwa amechoka kupewa maagizo. Mazungumzo ya simu bado yaliendelea maaskali wa trafik road waliendelea kuwatambulisha wenzao juu ya kupita kwa gari hilo. cha karibu kabisa na Chalinze “Hallow Mkuu nafikiri kuna zaidi ya makundi mawili na kundi moja ni chambo ….yea hapa naliona gari moja nina mashaka nalo...ndio watu nimewaona wanaonekana sio watu wakawaida kabisa…yea hatuna muda”

Salimu aliongea huku macho yake makini yakiwa kwenye plat number za gari yenye bodi iliyofunikiwa na turubai jeusi Haraka haraka aliongeza spid na kukatiza kwa mbele na kulikata mtindo wa kuzuia njia mita kumi na ushee. Paap Salimu akatoka na kukaa imara akioneshea bastola yake ndogo. Magari mengine yaliyokuwa katika msafara wa kulekea kule walipokuwa wanatoka yalisimama na watu wakaficha sura zao wasijuue nini kinaendelea asubuhi hiyo idadi ya polisi ilionekana kuwa kubwa kutokana na wengi kujitokeza wakioneshea siraha gari dogo na lile lenye bodi nyuma kwa mbali. Kamanda mkuu wa jiji hakuwa mbali teyari alikuwa na mike ya kipolisi mkononi akielekezea katika gari lile lilotulia. “hallow ni polisi wapo mbele yako na wapo na siraha kali sana unachotakiwa ni kutoka kwa hiyari yenu wenyewe bila kutumia nguvu za kuwatoa garini”

gari yao ikitazama upande kkuelekea Dar es salam alimaliza Kamanda na kutulia akitazama upande ule wa gari. Macho ya asakri yakiwa garini kila mmoja akiwa na hamu ya kuona nyuso za hao waliosemekana ni majambazi, mlango huo ukaonekana kufunguka na mguu uliovalia kiatu kirefu cha kike ukachomoza na kutua katika sakafu ya rami kisha mwili nao ukafata. Looh! alikuwa binti aliyevalia vazi lake jeusi lenye kupendeza akiwa na uso wa mshanago uliochanganyika na wasiwasi akiwa kama asiyejua kinachoendelea. “Lisa” Kamanda alijikuta akilitaja jina hilo kana kwamba limemponyoka mdomoni na kuwatazama watu wake wa karibu kama wamemsikia akilitaja.

Itaendeleaa...
 
The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com
Contact 065832859

MSIMU 3

Sehemu 12B: Mchafuko

Ilipoishia


Lisa” Kamanda alijikuta akilitaja jina hilo kana kwamba limemponyoka mdomoni na kuwatazama watu wake wa karibu kama wamemsikia akilitaja.

Tuendelee...

Uchomozaji wake katika gari na wingi wa mashaka ulipelekea kuwaduwazwa watu maana si walichokuwa wakikitegemea kukiona, Salimu alionesha ishara ya kumtaka atoke upande ule lakini binti Lisa akaonekana akiwa ni mwenye kujishauri shauri akigeuka nyuma kutazama gari ile yeney bodi. Salimu akiwa anamfatilia kwa makini aliweza patwa hisia ambazo kwake aliziona ni chanya kwa kile alichokuwa anakifikiria kutokana na namna ya utazamaji wa msichana Lisa katika gari iliyokuwa nyuma yake Haraka akamtupia macho Karimu aliyekuwa upande wa pili wa magari yanayorudi Dar akimuoneshea ishara za kikomandoo kisha.

Kupitia redio call aliyoifunga sikioni akaongea “Tujihadhari sio muda mrefu tunashambuliwa maana sasa kuna gari tatu zipo upande wetu na zote hazitaki kuondoka kila mmoja ashike vizuri siraha yake” maongezi hayo yalimfikia kila mmoja aliyepewa fulsa ya kusikia. Ghafla binvuu pindi binti akiwa anataka kuthubutu kupiga hatua kusogea upande wa askali ulisikika mlio wa bunduki na mara binti akaanguka chini “Puuhh” Salimu hakuuliza alijigeuza haraka na kuachia risasi iliyotoka na kupenya katika kioo chagari cha mbele na damu zikaruka katika kioo. Sasa ikawa ni piga ni kupige.

Lisa akiwa chini akigugumia maumivu ya kifua ambacho sasa kilichakaa kwa kutoka damu maskali wawili walijitoa na kuhawi kumbuluza kumuweka pembeni ya gari huku wakilindwa na wenzao. Haikuchukua muda mrefu teyari majambazi walikuwa wamezungukwa na polisi wakawa hawana la kufanya zaidi ya kutii amri tu huku wanaume wawili wakiwa teyari wamepoteza maisha na mmoja akiwa na jeraha sehemu za tumboni. Chini ya usimamizi wa Salimu na Karimu waarifu wakatiwa pingu na kuwekwa katika karandinga ambalo lilikuwa limeandaliwa kwa ajili yao muda mrefu.

Watu wote waliendelea kuwashangaa watu hao walioitwa majambazi maana walikuwa ni watu wenye umri mkubwa lakini hawakuonekana kuchoka kimwili. Lisa fahamu zilimpotea akachukuliwa na kupewa huduma ya kwanza kabla ya kuwahishwa Hospitali. “Kiongozi nilikusikia ukilitaja jina la Lisa unamjuaje yule binti” aliuliza Karimu akimtazama Kamanda “Ndio namjua Lisa ni mtoto wa waziri wa Nishati na madini nchini bwana George Mkesa ni binti yake wa pekee aliyetokea kupendwa sana na baba yake lakini katika asili yake ni binti aliyekuwa anapenda sana starehe na kusafiri mara kwa mara nchi za nje kwa ajiri ya shoping mabalimbali npia isitoshe kijana wangu ametokea kumpenda sana na walikuwa katika mahusiano lakini waliachana kutokana na binti kuwa wa gharama sana aking’ang’ania watu maarufu hapo ana miaka thelathini tu bado haikubainika ni mwanaume gani atakae kujafunga nae pingu za maisha na leo yupo hatiyani vijana wa siku hizi” alimaliza kuongea Kamanda Japhet Mokiwa na kumfanya Karimu kugeuza shingo kulisindikiza gari ya Ambulance. “Ni mrembo ana kwakweli” Karimu alijisemea.

Ngome Msitu wa Magamba, Lushoto-Tanga
Sauti za wadudu na milio ya vyura iliendelea kusikika ikishindana huku giza likiwa totoro nje kwa mbali taa kazaa za umeme na taa kubwa la usalama linalozungushwa likipelekwa huku na kurudishwa kule ndio lillo saidia kuongeza nuru fifii “Jamani naona mambo yapo sawa…”. Monica kwa tahadhari akaufunga mlango na kutazamana na wenzake. “…viongozi wote wamekusanyi kakatika chumba cha mikutano kujadiliana juu ya kukamatwa kwakina J4 na Jnae Dume” Meroda akatabasamu “…vizuri sana basi ni wasaa wetu kuondoka haraka iwezekanavyo pindi muda wetu ukifika lakini ngojakwanza ni mtaarifu Salimu” “…habari za jioni mpenzi, pole na kazi, leo ndio siku ambayo tumeamua kutoroka na wenzangu naomba uniombee tutoke salama humu” alipomaliza tu kuandika akutuma moja kwa moja
Timu ya Meroda haikuwa ikiwaza na kupanga mipango ya kutoka kambini bali walikuwa teyari wamo ndani ya zoezi la utorokaji macho yao yalikaza yakitazama nyakati katika saa zao zitimie watoke mara moja.

Muda muafaka uliwadia alarm katika saa zao maalumu ilisikika ikilia mara moja Samira akatoka chumbani, na dakika moja pekee ilitosha alirudi chumban na kuwaonesha dole kuwa mambo yako shwari wanaweza kutoka mara moja. Kwa namna ya kulindana muda huo wa saa sita usiku walitumia mlango wa nyuma ya nyumba waliokuwa wakishi na hatimaye wakawa wapo nje umbali wa mita thelathini hivi toka katika nyumba. Huku makelele ya kushangilia yakiwa yapo juu yakisikika.

Watu “Oyooo heeee ohhh woyooo”. Ulikuwa ni usiku wa mapambano ambayo hufanyika kila ijumaa usiku nyakati kama hizo ambapo mkusanyiko mkubwa wa watu huundwa katika uwanja wa mapambano wakipigana kwa kushindania pesa, kupitia mapigano ya ngumi na shabaha ni jambo ambalo limo katika taratibu na ratiba ya kambi. Kwamacho makini ya kujihami wakiwa wamechutama masikio yakiwa juu macho yakizunguka wakitazama huku na kule na kusikiliza hatua na mazungumzo ya wale walio kuwa wakipita eneo la karibu na walipo fichama muda huo wakiimarisha ulinzi wa kambi.

Mfano wa nyoka Meroda akaanza kutambaa taratibu na wenzake nyuma wakifata mtindo wake. Walizifata njia zile zile walizoziandaa na hatua zile zile japo palikuwa na changamoto za hapa na pale ikiwemo michubuko katika sehemu badhi ya ngozi zao. Usiku ukiendelea kutembea ukikazana kuitafuta alfajiri ukiwa wakaingia katika hatua ya pili ya kukatiza katikati ya shamba la bhangi lililochukua takribani heka khamsini na usheee ambalo muda huo lilikuwa kimya wadudu tu pekee wakisikika wakilia lia bila mpangilio lakini wakinyamaza na kuanza tena baada ya vishindo na makele ya nyasi kuisha. Sauti hizo zilipelekea kuupamba usiku huo uliokosa mbalamwezi na kuwa na giza totoro kuwatoa upweke na wasiwasi na kuwa fanya wasichana hao kuendelea kupamba moto na tumaini la kutoka salama.

Itaendeleaa....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom