Mr Acky
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 234
- 313
- Thread starter
- #81
The Hidden Truth (Ukweli uliofichika)
Nani Anahusika??
MSIMU WA PILI
SEHEMU YA 7A- MUUNGANO
“Kwa kisingizio cha kuitwa na Mkuu wa shule Salimu na Karimu wanatekwa na watu wasio julikana na kupelekwa Kando ya mji, wanashtuka wakiwa kizuizini katika jengo kubwa hofu na wasiwasi unawajaa anasimama mtu wasiye mjua na kuwauliza wao ni akina nani na wanafanya kazi yao ya upelelezi na nani? Je! Ni nini kitawakuata vijana hao?”
Mpiji, Kibaha –Mkoa wa Pwani
Katika nyumba ya ghrorofa iliyokaa peke katika msitu mdogo wa miti iliyoshikana na kuleta hewa nzuri na utulivu Bwana yule anaefata nyendo za kina Salimu akiwa juu ya ghorofa mkononi darubini akiwa amevalia kaptula aligeuka kusogelea meza iliyokuwa mbele yake na akazitawanya picha tano ambazo zilikuwa zimekusanywa pahala pamoja. Baada ya kuzitawanya akachukua picha mbili tu ambazo zilikuwa zikimuonesha Salimu na Karimu wakiwa katika miuonekano ya mazigira tofauti kisha akaanza kutingisha kichwa kukubariana na mawazo yake. Akiwa kazishikilia akapiga hatua fupi fupi hadi katika moja ya vyumba “Vijana nimesha amua sasa chukuaeni majina haya na muyatume kabla ya jua halijazama hawa wanatutosha na kikubwa wameshamaliza mitihani yao ya form six jana wacha tuone”. Aliongea bwana huyo mtu mzima akiwatazama vijana wawili waliokuwa bize na kompyuta zao.
Akaziweka picha mbili mezani na mmoja wao akachukua picha hizo zilizo wekwa karibu kabisa katika meza yake “Sawa mkuu” akaitika “Mziscan hizo picha na kuzituma kwa email yake binafsi ndiyo tutakayo itumia kwa sasa sawa zungu”, “Sawa mkuu” Zungu aliitika tena.
Kibaha High School, Kibaha - Mkoa wa Pwani
“Mzee, Mkuu wa shule anasemaje hapo mbona umebung’aaa mdomo wazi” Karimu alishusha pumzi na kumtazama Karimu kwa muda, “Ndugu Mkuu wa shule anahitaji kutuona nyumbani kwake ameagiza gari nje ya uzio ni dharura” aliongea Salimu “Mhh! Mbona ghafla hivyo ahh sasa…” aliongea Karimu na kukatisghwa na Salimu “Karimu ni hivi haina shida lakini lazima tulifikirie hili vema ni yale yale mambo ya siasa tena kama siku zote au ni kuhusu mambo ya shule” Walijaribu kudodosa walau kutambua ni jambo gani. Hazikupita hata dakika sita tayari walisikia majina yao yakiitwa nje ya bweni wakaitika nakupata habari ya ugeni unaowasubiri nje ya uzio. Walitazamana Salimu na Karimu mioyo iliwabadirika wasiwasi ukawapanda “Kaka mbona imekuwa harakaharaka sana leo amemaliza tu hata…mara tunauliziwa mhh!” Salimu alihoji akimtazma Karimu. “Kaka sikia mi pia nimeshangaa lakini hebu tuvae fasta twende huenda huyo mtu aliagizwa muda ila mzee alisahau hivyo amechelewa kutoa taarifa”.
Salimu akayapima maelezo ya Karimu akayapa uzito Fulani yalimuingia kiasi Fulani lakini bado hakuridhika alichofanya ni kupotezea. Haraka haraka walivaa viwaro kisha wakatoka nje kabisa Salimu alimsimamisha Karimu kisha akatoa simu yake ya smartphone na kuipiga namba ya Mkuu wa Shule na akaiweka simu sikioni akisikilizia simu ambayo ilikuwa ikiita tu bira kupokelewa wakiwa mbele ya gari moja ndogo aina ya nissan murano rangi ya kahawia. “Shit mbona hapokei simu huyu mzee” Salimu alikunja ndita kisha akaitazama gari hiyo ambapo Dereva alionekana nje akiwaoneshea ishara ya muda unaenda. “Kaka vipi?” “hivi hii gari ulishawahi iona kabla?” Karimu aliitazama akagutuka kidogo “Mhh hapana mzee” sura ikiwa yenye wasiwasi na viulizo. “Nataka kumuuliza mkuu gari gani iliyokuja kutuchukua maana hapa naiona hii tu na sio ile gari yake tuliyoizoea wee huoni ni tatizo”. Wakati huo kwa mbali ilionekana gari ikiwa imesimama ikitazama upande ambao vijana hao walikuwepo.
Dereva sasa alionekana kupiga kelele akiwataka wafanye haraka. “Basi tufanye hivi...mtumie meseji kuwa nimekupigia na wewe hukupokea kunagari hapa inaonekana ndiyo uliyoituma sisi hatujawahi iona sasa sisi tunapanda lolote likitokea utahusika”. Salimu alionekana kufurahia wazo hilo la Karimu na yeye akafanya kama alivyoshauriwa kisha akasogea hadi kwa mlinzi na kuanza mazungumzo kisha akampa simu huyo akasogea pahala alipo karimu. “Twende zetu” hao wakaondoka na kuingia katika gari na safari ikaanza. Dereva akiwa anaendesha mwendo wa kawaida alichukua simu yake ambayo ilikuwa ikiwaka na kuzima ikionesha maneno ya 1 NEW MESSAGE iliyokuwa upande wa kushoto karibu na sehemu ya chupa ndogo ya maji ya kunywa akaichukua akaifungua kuusoma ujumbe huo. “Unaweza kuanza kazi mara moja”. Bwana huyo baada ya kuusoma ujumbe huo wa maneno na yeye akaandika wake chapu chapu “Sawa Mkuu” na akautuma kwa namba ile ile iliyotumika kutuma ujumbe wa mwanzo. Kisha akaongeza kidogo spidi na kuupandisha vioo vyote vya gari hiyo
Itaendelea .....
Mambo yanazidi kuwakaa


Nani Anahusika??
MSIMU WA PILI
SEHEMU YA 7A- MUUNGANO
“Kwa kisingizio cha kuitwa na Mkuu wa shule Salimu na Karimu wanatekwa na watu wasio julikana na kupelekwa Kando ya mji, wanashtuka wakiwa kizuizini katika jengo kubwa hofu na wasiwasi unawajaa anasimama mtu wasiye mjua na kuwauliza wao ni akina nani na wanafanya kazi yao ya upelelezi na nani? Je! Ni nini kitawakuata vijana hao?”
Mpiji, Kibaha –Mkoa wa Pwani
Katika nyumba ya ghrorofa iliyokaa peke katika msitu mdogo wa miti iliyoshikana na kuleta hewa nzuri na utulivu Bwana yule anaefata nyendo za kina Salimu akiwa juu ya ghorofa mkononi darubini akiwa amevalia kaptula aligeuka kusogelea meza iliyokuwa mbele yake na akazitawanya picha tano ambazo zilikuwa zimekusanywa pahala pamoja. Baada ya kuzitawanya akachukua picha mbili tu ambazo zilikuwa zikimuonesha Salimu na Karimu wakiwa katika miuonekano ya mazigira tofauti kisha akaanza kutingisha kichwa kukubariana na mawazo yake. Akiwa kazishikilia akapiga hatua fupi fupi hadi katika moja ya vyumba “Vijana nimesha amua sasa chukuaeni majina haya na muyatume kabla ya jua halijazama hawa wanatutosha na kikubwa wameshamaliza mitihani yao ya form six jana wacha tuone”. Aliongea bwana huyo mtu mzima akiwatazama vijana wawili waliokuwa bize na kompyuta zao.
Akaziweka picha mbili mezani na mmoja wao akachukua picha hizo zilizo wekwa karibu kabisa katika meza yake “Sawa mkuu” akaitika “Mziscan hizo picha na kuzituma kwa email yake binafsi ndiyo tutakayo itumia kwa sasa sawa zungu”, “Sawa mkuu” Zungu aliitika tena.
Kibaha High School, Kibaha - Mkoa wa Pwani
“Mzee, Mkuu wa shule anasemaje hapo mbona umebung’aaa mdomo wazi” Karimu alishusha pumzi na kumtazama Karimu kwa muda, “Ndugu Mkuu wa shule anahitaji kutuona nyumbani kwake ameagiza gari nje ya uzio ni dharura” aliongea Salimu “Mhh! Mbona ghafla hivyo ahh sasa…” aliongea Karimu na kukatisghwa na Salimu “Karimu ni hivi haina shida lakini lazima tulifikirie hili vema ni yale yale mambo ya siasa tena kama siku zote au ni kuhusu mambo ya shule” Walijaribu kudodosa walau kutambua ni jambo gani. Hazikupita hata dakika sita tayari walisikia majina yao yakiitwa nje ya bweni wakaitika nakupata habari ya ugeni unaowasubiri nje ya uzio. Walitazamana Salimu na Karimu mioyo iliwabadirika wasiwasi ukawapanda “Kaka mbona imekuwa harakaharaka sana leo amemaliza tu hata…mara tunauliziwa mhh!” Salimu alihoji akimtazma Karimu. “Kaka sikia mi pia nimeshangaa lakini hebu tuvae fasta twende huenda huyo mtu aliagizwa muda ila mzee alisahau hivyo amechelewa kutoa taarifa”.
Salimu akayapima maelezo ya Karimu akayapa uzito Fulani yalimuingia kiasi Fulani lakini bado hakuridhika alichofanya ni kupotezea. Haraka haraka walivaa viwaro kisha wakatoka nje kabisa Salimu alimsimamisha Karimu kisha akatoa simu yake ya smartphone na kuipiga namba ya Mkuu wa Shule na akaiweka simu sikioni akisikilizia simu ambayo ilikuwa ikiita tu bira kupokelewa wakiwa mbele ya gari moja ndogo aina ya nissan murano rangi ya kahawia. “Shit mbona hapokei simu huyu mzee” Salimu alikunja ndita kisha akaitazama gari hiyo ambapo Dereva alionekana nje akiwaoneshea ishara ya muda unaenda. “Kaka vipi?” “hivi hii gari ulishawahi iona kabla?” Karimu aliitazama akagutuka kidogo “Mhh hapana mzee” sura ikiwa yenye wasiwasi na viulizo. “Nataka kumuuliza mkuu gari gani iliyokuja kutuchukua maana hapa naiona hii tu na sio ile gari yake tuliyoizoea wee huoni ni tatizo”. Wakati huo kwa mbali ilionekana gari ikiwa imesimama ikitazama upande ambao vijana hao walikuwepo.
Dereva sasa alionekana kupiga kelele akiwataka wafanye haraka. “Basi tufanye hivi...mtumie meseji kuwa nimekupigia na wewe hukupokea kunagari hapa inaonekana ndiyo uliyoituma sisi hatujawahi iona sasa sisi tunapanda lolote likitokea utahusika”. Salimu alionekana kufurahia wazo hilo la Karimu na yeye akafanya kama alivyoshauriwa kisha akasogea hadi kwa mlinzi na kuanza mazungumzo kisha akampa simu huyo akasogea pahala alipo karimu. “Twende zetu” hao wakaondoka na kuingia katika gari na safari ikaanza. Dereva akiwa anaendesha mwendo wa kawaida alichukua simu yake ambayo ilikuwa ikiwaka na kuzima ikionesha maneno ya 1 NEW MESSAGE iliyokuwa upande wa kushoto karibu na sehemu ya chupa ndogo ya maji ya kunywa akaichukua akaifungua kuusoma ujumbe huo. “Unaweza kuanza kazi mara moja”. Bwana huyo baada ya kuusoma ujumbe huo wa maneno na yeye akaandika wake chapu chapu “Sawa Mkuu” na akautuma kwa namba ile ile iliyotumika kutuma ujumbe wa mwanzo. Kisha akaongeza kidogo spidi na kuupandisha vioo vyote vya gari hiyo
Itaendelea .....
Mambo yanazidi kuwakaa





