The Hidden Truth (Ukweli Uliofichika)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email
akidasiri@gmail.com
MSIMU 4
Sehemu 12E: Ahadi ILIYOTIMIA
Ilipoishia...
...nilivyokuwa mdogo…sijasahau kitu na nina uwakika huyu baba ndiye aliyemuua mama yangu baada ya kumtambua alihusika kumuuwa baba yangu” “…baba yako? Inamaana Samuel sio baba yako?” aliongea Salimu “Ndio mpenzi baba yangu sio Samuel” aliongea Shalon kwa masikitiko sana na kutilia huruma “Pole sana mpenzi pole sana, baba yako alikuwa nani kwani na…au mama yako alikimbia kwa baba yako nakukimbilia kwa Samuel?” Shalon aligeuka na kumtazama Salimu “…sina majibu ya maswali yako ninachokumbuka sikuwahi kumuona mama akiwa nafuraha na hata siku Moja....
.
Tuendelee
..... anakufa nilikuwa nimeshikilia simu yake kwa nia ya kumpiga picha tulikuwa tuna cheza lakini wakati wanazozana mama akaniambia niondoke niliposikia kelele zimezidi nilirudi nikiwa nimeshikilia simu kwa mtindo wa kupiga picha nilipofungua mlango ndipo mama yangu alikuwa anaongea kwa uchungu akimlaumu Samuel alivunja ahadi walioiweka kwanini alimuua akamshambulia huku akimuita mama Malaya akijisifu na kumkaba huku akimgongesha ukutani kisha akamtupa na kuondoka alipokuja mlangoni nikajificha alipotoka nikamfata mama nikilia simu nikiwa bado nimeshikilia ndipo alipo niambia kuwa Samuel sio baba yangu mzazi bali baba yangu ni Richard Edward kisha akafariki mbele yangu”
aliongea Shalon kwa uchungu wakati huo Salimu alikuwa kajishika kichwa machozi yakimtoka “Na wewe ni Richard Edward…haiwezekani iwe hivi Nooo” aliongea kwa uchungu kiasi cha kumshangaza Shalon ambaye alibaki akimshangaa “Mbona Au huamini au wewe umeelewa nini mpenzi” Shalon aliongea “Hebu nambie mbona unanichanganya Shalon inawezekana vipi hilo lakini” aliongea Salimu huku akimshika mabega akimtikisa hadi Shalon kuogopa “Salimu kwanini isiwezekane inamaana ulikuwa unanidanganya sio hunipendi au vipi unaelewa ninachoongelea lakini mbona na wewe sikuelewi? Sijafika pakunisaidia hata sijakwambia umeanza kunikwepa kumbe hunipendi”
Sahlon aliongea huku akiitoa mikono ya Salimu mabegani mwake. Kila mmoja alibaki kumshangaa mwezie. “Sikia Salimu ningekuwa na uwezo basi ningemtafuta kaka yangu Pius na kushirikiana nae katika hili kumbe wewe ni wale wale” Shalon aliongea kwa uchungu na sauti ya kilio. Salimu alijikuta akiishiwa pozi machozi yakimlenga lenga “Ina maana wewe ni dada yangu” Salimu bila kujielewa alijikuta ameyasema maneno hayo na kumshitua Shalon “Dada yako hivi sijakusikia au Eehhh hebu sema kitu hebu rudia” Shalon alimvamia Salimu na kumkwida akimtingisha tingisha Salimu hakuwa na lingine bali kutokwa na machozi pekee mwisho akajikuta akimkumbatia Shalon kumbatio zito.
Walibembelezana na kuongelea mambo baadhi yaliyopita. “…nimeshafika kwa bibi yupo hai na nimeshaonana na shangazi zangu na hivi ninavyo kwambia tunawasiliana kila wakati nimeyafanya mengi tutaongea kaka” aliongea Shalon “ Unajua nini dada Shalon kiukweli mungu ni mkubwa katika siku zote hizi nilihisi kitu tofauti kabisa juu yako sikuwa na hisia za mapenzi kabisa juu yako na sikujua kwanini kumbe nilikutanishwa na dada yangu siku ile ohh mungu wangu asante sana” aliongea Salimu na kutabasamu “Mi pia kaka lakini sikutafakari zaidi hayo, lakini nashukuru kwakuwa ni kaka yangu basi inatosha sina nafasi ya mtu mwengine wewe tu kaka”
aliongea Shalon “Ni sawa na muda umeenda sana naomba uniache niende nikapange mambo vizuri naomba usije kumuonesha hisia zozote za mashaka bwana Samuel badae nitakupigia simu nitakuelekeza pahala tukutane hatuna muda kabisa” Salimu aliongea na Shalon akatingisha kichwa kukubali wakashikana mikono na kutoka eneo hilo.
HOT spot club, Ubungo -Dar es Salam
Mziki wa taratibu ulisikika kwa mbali, katika meza ya peke “Aisee ni jambo la kushtukiza na kushangaza sana kwa kweli nimefurahia sana na tumshukuru mungu kwa kusimama upande wetu, maana nilikuwa muoga” Meroda aliongea na kutabasamu. “Jambo la msingi ni kujikaza tu Shalon kwa sababu timu yetu ipo makini na tumejipanga hatukufanyi chambo lakini najua kwa upande wako ni sehemu ya ndoto zako katika maisha ambazo unaenda kuzikamilisha” Salimu aliongea,
“Jamani kaka,wala msijali kuhusu hilo hamjui tu namna ninavyofurahi kufahamiana na nyinyi nyote nina amani sana” Shalon aliongea “… nitajitahidi kufata maelekezo na mazoezi mliyo nipa bila makosa” aliongea Shalon kwa furahs “…Vizuri dada Shalon kila kitu kitaenda sawa, kuna watu maalumu watakaoshughulikia usalama wako bila wasiwasi, maaskali watakuja kwa wakati na hata pia taarifa ya kukamatwa itakuwa tayari katika mitandao ya kijamii pindi tu tukipata signal toka kwako kwa kukibonyeza kifaa maalumu utakachokiwasha ukiwa tayari tu na si vinginivyo baada ya kuanza majibizano na Samuel ambaye kwa muda huo atakuwa ni mtu mwenye jazba hatoweza kukaa kimya akikusikiliza pindi tu ukipita mule tulipo kwambia na hapo mchezo utakuwa umekwisha maskari wataingia na kumuweka chini ya ulinzi na kumchukua”
Salimu aliongea na kumfanya Shalon kutabasamu na kutingisha kichwa “Nipo tayari kwa kazi kaka natamani siku iishe haraka haraka naamini nitafanya” “Vipi kuhusu Karimu mliwasiliana” Meroda alidakia “Yeah japo mtandao unasumbua sana lakini anaendelea vizuri na mchakato nafikiri mpaka leo jioni kesho atakuwa amefanikisha upelelezi kwa kiwango kikubwa”, Salimu aliongea na kumuacha Meroda akitabasamu “Inaonekana nyinyi wawili mlijuana muda mrefu eeh” Shalon aliongea na kutabasamu Salimu na Meroda wakatazamana “Sijui ingekuaje kama isingekuwa udugu?”
Shalon aliongea tena “Huenda tusingefahamiana, Waislamu dunia nzima wanaamini kuwa hakuna jambo linalofanywa bila idhini ya Allah Subhanahu wataala tofauti na hapo haiwezekani, na kila jambo hutokea kwa sababu na wala sio bahati mbaya” aliongea Salimu Shalon akanyanyua uso kumtazama kaka yake na kutabasamu “Ahh tuache hii mada tafadhari” aliongea Meroda” wote wakatabasamu. “Basi tufanye umpeleke mapema dada ako siunajua kesho sio mbali na jioni hii anahitaji muda wa mazoezi” meroda aliongea “Nikweli Kwa ajili ya familia na mafanikio” wote wakagongeshana glass zao.
Itaendeleaa...